Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Kapsabet Pre Mock Exams 2021/2022

Share via Whatsapp

KISWAHILI
KARATASI YA 1: INSHA

MAAGIZO

  • Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
  • Kisha chagua insha moja nyingine kutoka kwa hizo tatu zilizobakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400.
  • Kila insha ina alama 20.
  1. Siku za hivi karibuni umesoma riwaya mpya iliyoandikwa na Msanifu Kombo inayoitwa : Afrika imelaaniwa. Andika tahakiki ya riwaya hii.
  2. Hatua ya serikali kuu kumpa kila mwanafunzi wa darasa la kwanza tarakilishi ni manufaa sana. Jadili
  3. Andika kisa kitakachodihirisha ukweli wa methali ifuatayo:
    Ukiona cha mwenzako kikinyolewa na chako tia maji
  4. Andika insha itakayomalizikia kwa kauli hii: Ama kweli sikufikiria wala kutegemea kuwa aushi yangu ingebadilika jinsi hiyo.

MAAKIZO

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. Hii ni insha ya tahakiki. Insha hii ni lazima ionyeshe sehemu zifuatazo: kichwa, utangulizi, mwili , na hitimisho.
    1. Kichwa/ anwani
      • Anwani itaje jina halisi la kitabu au inaweza kuhusu jambo muhimu ambalo linatawala kitabu
      • Anwani iandikwe kwa herufi kubwa na kupigiwa mstari.
    2. Utangulizi
      Hii ni sehemu ya kwanza ambayo ni lazima iwe na sehemu hizi:
      1. Mada ya kitabu : Afrika Imelaaniwa
      2. Jina la mwandishi
      3. Wachapishaji
      4. Mwaka wa kuchapishwa
      5. Mhakiki
      6. Kurasa
      7. Bei
    3. Yaliyomo
      1. Mtindo- mwanafunzi aeleze jinsi mwandishi alivyotumia lugha ili kunata hadhira yake na kuwasilisha maudhui yake.
      2. Katika aya ya kwanza, mtahiniwa aeleze kwa kifupi dhamira ya yaliyomo kwenye riwaya
      3. Mtahiniwa aeleze maudhui machache na jinsi yameifanya Afrika kulaaniwa.
      4. Wahusika –awataje na tabia zao na pengine umuhimu wao
      5. Maoni yake-hapa mtahiniwa anaweza kuonyesha kufaulu au kutofaulu kwake kimtindo, maudhui au uundaji wa wahusika wake.
    4. Tamati- atoe maoni yake ya jumla kuhusu kitabu

utunzaji

  • Atakayekosa sehemu zote za kichwa na utangulizi atakuwa amekosa sura na aondolewe alama 4 baada ya kutunzwa.
  • Sura- idhihirishe sura ya tahakiki
  • Mtahini akadirie utangulizi na vipengele vya kichwa na yaliyomo
  • Hoja za mtahiniwa zitakuwa bora ikiwa zitafungamanishwa na kichwa.
  • Atakayekosa kufanya haya ana upungufu wa maudhui na asipate alama c 8/20
  • Mtahini atie mikwaju pembezoni kuonyesha mtahiniwa amezingatia utangulizi, maudhui, wahusika, mtindo , udhaifu na tamati
  • Insha inayozingatia vipengele vyote imekamilika. Akikosa baadhi ya vipengele akadirie vilivyo.

Urefu

  • Lazima insha itimize urefu kamili wa maneno 400
  • Insha yenye urefu wa robo asipite kiwango cha D+ 05
  • Insha yenye urefu wa nusu isipite kiwango cha C+ 10 wakati wa utunzaji hata kama amezingatia vipengele vyote.
  • Insha yenye urefu wa robo tatu asipate kiwango cha B+ 15 wakati wa utunzaji hata kama amezingatia vipengele vyote.
  • Atakayekosa kurejelea mwandishi Msanifu Kombo, au anwani Afrika Imelaaniwa, achukuliwe kuwa na upungufu wa kimtindo

manufaa

  • tarakilishi zitarahisisha ufunzaji wa masomo mbalimbali kwa upande wa mwalimu
  • zitakuza na kuimarisha ubunifu miongoni mwa wanafunzi
  • hatua hii itamtanguliza mapema mwanafunzi katika ulimwengu wa tarakilishi na teknohama
  • hurahisisha kuelewa haraka kwa masomo kwa kurahisisha mada ngumu katika silabasi kwa mwanafunzi
  • itaboresha matokeo ya mtihani kwa wanafunzi husika
  • itaimarisha uchumi wa watengenezaji wa tarakilishi na program
  • zitatumika katika utafiti
  • zitapunguza mzigo kwa wanafunzi wa kubeba vitabu vingi.

Hasara

  • ni ghali kutekeleza-inahitaji fadha nyingi
  • bila kuwepo kwa walimu walio na umilisi wa kutosha wa kompyuta, hatua hiyo haitakuwa na manufaa
  • kutakuwa na tatizo la usalama wa wanafunzi na tarakilishi zenyewe
  • baadhi ya shule hazina miundo-msingi ya kutekeleza masomo ya tarakikilishi kama vile kawi na madarasa.
  • zisipodhibitiwa, tarakilishi zitaweza kusababisha utovu wa maadili kwa wanafunzi kupitia mitandao

hili ni swali la methali

  • mtahiniwa sharti atunge kisa kinachoafikiana na methali yenyewe
  • mtahiniwa ashughulikie pande zote mbili za methali husika
  • ukiona cha mwenzako kikinyolewa-huu ni upande wa kwanza
  • na chako tia maji- huu ni upande wa pili
  • mtahiniwa awe na hoja toshelezi katika pande zote mbili
  • amalize kwa kutoa funzo kutokana na methali

andika insha itakayomalizikia kwa kauli hii;ama kweli sikufikiria wala kutegemea kuwa aushi yangu ingebadilika jinsi hiyo.

  • Maneno kiini katika kauli hii ni; sikufikiria, aushi yangu na ingebadilika, .hali inayodhihirika katika mdokezo huu ni mabadiliko yanayotokea katika maisha ya mhusika. Kisa kidhihirishe:
  • Mabadiliko yanayotokea katika maisha ya mhusika
  • Mhusika anaweza kuwa aliishi kimaskini kisha akabahatika kumpata mfadhili
  • Mhusika ambaye alitelekezwa na familia yake amepata mhisani
  • Mhusika ambaye alizoea kuishi maisha ya juu anaipoteza kazi yake na maisha yanakuwa magumu
  • Mhusika ambaye anawapoteza wazazi wake akiwa na umri mdogo analazimika kujitegemea
  • Mhusika anagunduliwa kuugua ugonjwa hatari usio na tiba
  • Mhusika ambaye anaachana na mumewe au mkewe kwa hiari au sharuti kisha maisha yanamharibikia.

Tanbihi

  • mtahiniwa atakuwa amepotoka kimaudhui pale tu hakumaliza kwa kauli aliyopewa, hivyo kuandika yasiyohusiana na swali
  • mtahiniwa akikosa kumaliza kwa kauli aliyopewa lakini kisa chake kioane na kauli ya swali, atakuwa hajapotoka kimaudhui bali atakuwa amepungukiwa kimtindo tu
  • akikosa kumaliza kwa kauli hii na kisa kisioane na kauli ya swali, atakuwa amejitungia swali
  • mtahiniwa asimulie kisa kinachodhihirisha hali yoyote: chanya au hasi.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Kapsabet Pre Mock Exams 2021/2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest