Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Joint Pre-Mock Exams 2021/2022

Share via Whatsapp

INSTRUCTIONS TO CANDIDATES

  • Andika insha mbili.
  • Insha ya kwanza ni ya lazima kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia
  • Kila insha isipungue maneno 400
  • Kila insha ni alama 20
  • Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili
  1. Wewe ni mwandishi wa habari. Umemwalika mwenyekiti wa tume ya utangamano na uwiano wa kitaifa nchini studioni ili kuangazia kwa kina swala la ukabila ambalo limekita mizizi katika taifa. Andika dayolojia kati yenu.
  2. Nchi imekumbwa na mizozo mingi ya kijamii hivi karibini. Huku ukipendekeza suluhisho, jadili vyanzo vya mizozo hiyo.
  3. Andika kisa kitakachodhihirisha maana ya methali: Nyumba njema sio mlango, ingia ndani uone.
  4. Tunga kisa kitakachoanza kwa maneno yafuatayo: Giza lilikuwa limechukua milki ya viumbe wote duniani. Nyota zilitoa mwanga hafifu na mwezi ulikuwa ushatua. Katika giza hilo la kaniki.


MARKING SCHEME

  1. Hii ni insha ya dayolojia, sura ya dayolojia izingatiwe
    Kuwe na kichwa na kitaje neno dayolojia mf
    Dayolojia kati ya mwandishi na waziri kuhusu…
    Kichwa kiandikwe kwa herufi kubwa, kipigiwe mstari
    Kuwe na utangulizi mfupi kuhusu mada mabanoni
    Mtindo wa kitamthlia ufuatwe
    Koloni zitumiwe kutenga majina ya wahusika na maneno wasemayo
    Wahusika wote wawili wachangie hoja
    Kwa kila hoja kuwe na suluhu mwishoni mwa aya
    Maelezo katika mabano yawe kwa uchache sana

    Baadhi ya hoja;
    Mapendeleo kazini kwa misingi ya kikabila
    Kuchagua viongozi kufuatia misingi ya kikabila
    Kuchukia wasio wa kabila lako
    Kudharau mila na desturi za kabila jingine
    Kuzuka kwa makundi haramu ya kikabila
    Matumizi ya lugha za kienyeji katika taasisi za umma
    Kufurusha watu kutoka katika maeneo yanayoaminika kuwa ngome ya kabila fulani
    Ukatili dhidi ya watu wa kabila jingine n.k

    Suluhu
    Kuhubiri Amani hasa katika maeneo ya kazi
    Watu waajiriwe bila kuzingatia misingi ya kikabila
    Kuchagua viongozi kulingana na utendakazi sio ukabila
    Wanaochochea watu kufurushwa makwao kuchukuliwa hatua za kisheria
    Kuheshimu mila, desturi za jamii nyingine n.k
  2. Mizozo ya kijamii
    Umiliki wa rasilimali muhimu kama maji, mashamba nk
    Imani potovu zinazodunisha baadhi ya jamii
    Uchochezi wa kisiasa
    Mila kinzani
    Mipaka ya kihistoria iliyowekwa na wakoloni
    Mfumo wa elimu unaotweza baadhi ya mila na kulemeza nyingine
    Migao ya nyadhifa na kazi isiyo sawa
    Kutweza matumiza ya lugha za makabila mbalimbali katika vyombo vya habari

    Suluhu
    Ugavi sawa wa rasilimali
    Utangamano wa jamii kupitia asasi mbalimbali kv dini
    Kudhibiti kampeni za kisiasa
    Kuchochea mwingiliano wa jamii kupitia ndoa
    Kuwa na mipaka mipya ya maeneo mbalimbali isiyotenganisha jamii kikabila
    Migao ya nyadhifa na kazi iwe sawa
    Tumia lugha rasmi nay a taifa katika vyombo vya habari
  3. Methali
    Mwanafunzi atunge kisa kimoja kitakachoafiki maana ya matumizi ya methali hii
    Kisa kiwe cha kuvutia
    Mapambo ya lugha yaonekane
    Makossa ya sarufi na hijai yaepukwe
    Mtahiniwa aeleze pande zote mbili za methali
    Uzuri wa nyumba huwezi kuujua kwa kuangalia tu ukiwa nje. Lazima uingie ndani.
    Tabia za mtu si mavazi au umbo lake la nje ila ni matendo yake.
    Huwezi kueleza uzuri wa kitu au mtu kwa kumwangalia umbo au mavazi. Lazima utangamane naye ujue tabia yake
  4. Hii ni insha ya mdokezo
    Mtahiniwa sharti aanze kwa maneno hayo
    Asipoanza kwa maneno hayo, ataadhibiwa kimtindo
    Mtahiniwa atunge kisa kitakachooana na maneno hayo
    Kisa kiwe cha kushtua, kuhuzunisha na kudhihirisha hali fulani ya hofu
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Joint Pre-Mock Exams 2021/2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest