Watch Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34
  • Home
  • High School Notes
  • Kiswahili
  • Mwongozo wa Chozi La Heri
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri

Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - Maswali na Majibu ya Dondoo katika Riwaya ya Chozi la Heri
Download PDF for future reference Install our android app for easier access

Click the button below to download the full Mwongozo wa Chozi la Heri pdf document, with all the topics.

Download Mwongozo wa Chozi la Heri PDF to Print or Offline Reading

CLICK HERE to get "Mwongozo wa Chozi la Heri" on Whatsapp for offline reading/ printing.

Chozi Insha Questions and Answers

Maswali ya Insha

Haya ni maswali ambayo hutoa kauli inayohitaji kujibiwa kwa kirefu na kwa kina. Swali linaweza kuwa la jumla yaani linalohusu Riwaya nzima. Pia, swali laweza kulenga sehemu ya kazi husika katika nyanja na maudhui, wahusika na hulka zao, mafunzo na fani. Maswali haya huhitaji zaidi uwezo wa kukumbuka wa mtu, kupanga hoja na kuelezea msimamo au maoni yake kuhusiana nayo. Mtahiniwa anahitajika kutoa hoja na kuziteteta kwa mifano dhabiti. Mtahiniwa asitumie vistari vistari, afafanue hoja kikamilifu akiandamisha mifano mingi kutoka kwa Riwaya.

Swali la Insha 1

Haki za watoto hazitiliwi maanani katika jamii nyingi za kiafrika. Eleza ukweli wa kauli hii kwa kurejelea Riwaya ya chozi la heri (Alama 20)

Haki ya watoto kusoma inakiukwa. Ami za Lucia na Akelo wanapinga elimu yao na kudai kuwa kuwaelimisha wasichana ni kufisidi raslimali.

Watoto wanahusishwa katika ajira. Akiwa mdogo,Sauna anaajiriwa kwenye machimbo ya mawe,kuuza maji na hata pombe baani. Vilevile Chandachema anahusishwa katika ajira ya uchunaji wa majani chai akiwa mtoto wa darasa la tano kwenye shirika la chai la Tengenea.

Kuna wizi wa watoto. Sauna anawaibia Dickson na mwaliko na kuwapeleka kwa Bi. Kangara ambaye ni Mlangunzi hodari wa watoto.

Watoto wanauawa na magari moshi kwenye mtaa wa madongoporomoa wa Sombera wanapoenda haja kwenye reli

Watoto wanahusishwa katika ulanguzi wa dawa za kulevya. Dickson anatumiwa na mzee Buda kusafirisha dawa za kulevya ughaibuni.

Baadhi ya watoto wasichana wanaolewa na vikongwe kwa lazima. Fungo anamwoa Pete kwa lazima akiwa darasa la saba kama mkewe wanne.

Kunajisiwa/kubakwa – Sauna anabakwa na babake wa kambo Bwana maya na Kutungwa mimba. Pia lime na Mwanaheri wananajisiwa na vijana wahuni.

Watoto wanapotoshwa na watu wazima. Bi. Kagara anampotosha Sauna kwa kuhadaa ajihusishe na biashara haramu ya ulanguzi wa watoto. Anapotoshwa,Sauna anahusika katika wizi wa watoto na kuwalangua

Baadhi ya watoto wanapozaliwa wanatupwa. Naomi anamwokoa mtoto aliyetupwa jalalani na kumpeleka kwenye kituo cha polisi. Matawa Cizarina anasema kwamba kuna mtoto aliyetupwa langoni mwa kituo cha watoto cha Benefactor akiwa amefungwa kijiblanketi kikuukuu.

Naomi anawahini wanawe malezi anapomtoroka mumewe. Anamtoroka Lunga baada yake kufutwa kazi na kuwa maskini jambo hili linawafanya Umu, Dickson na Mwaliko kulelewa na baba yao pekee

Sauna anapotoshwa na Bi. Kangara anapohusishwa na wizi na ulanguzi wa watoto. Bi.Kangara anamhadaa Sauna na kumwingiza katika biashara hii haramu.

Watoto wanapokea vitisho kutoka kwa watu wazima wanaopania kuwatumia vibaya. Mzee Buda anamtisha Dickson anapojaribu kukataa kujihusisha katika biashara ya ulanguzi wa dawa za kulevya. Anamwambia kwamba anamtupa nje na kumsingizia wizi. Jambo hili lingemfanya Dickson kuvamiwa na kuuawa na raia kama alivyofanywa Lemi.

Watoto wanatumiwa kama vyombo vya mapenzi. Bi.Kangara anawaiba wasichana na kuwauza kwenye mandanguro (shambiro) ili watumiwe kama vyombo vya mapenzi na wanaume katili. Fumba anajihusisha na mwanafunzi wake kimapenzi na kumringa.

Kuna ubaguzi wa watoto. Wazazi wa Pete wanamwoza kwa lazima kwa mzee Fungo kama mke wanne. Wanafanya hivi ili wapewe mahari itakaayotumiwa kuwaelimisha ndugu zake watano wa kiume.

Watoto walio mijini ya mama zao wanaavywa. Mamake Sauna anamsaidia kuavya kitoto chake. Anafanya hivi kwa kumwogopa Bwana Maya aliyemnajisi Sauna. Umulikheri kuachiwa ulezi wa Dickson na baada ya Mama yao Naomi kutoroka na baba yao kuaga.

Tuama kukumbwa na maswala ya ukeketaji wa watoto wa kike

Dick kulazimishwa kushiriki ulanguzi wa dawa za kulevya na Buda

Mwanawe Selume Sara anatengwa na mamake mzazi baada ya mumewe kumwacha Selume na kumwoa msichana wa kikwao. Anachukuliwa na babake. (Uk35)

Kairu anaeleza jinsi walipofukuzwa kwao na jinsi si kitindamimba wao anapoaga dunia kutokana na njaa.uk 91

Mwanaheri na Lime wanafanyiwa unyama-wanabakwa na vijana mbele ya baba yao. Na baadaye wanakosa penzi la Mama yao Subira anapowatoroka baada ya kupitia machungu ya kubaguliwa .Uk 97

Zohali kuhusishwa katika mapenzi mapema na kupachikwa mimba. Zohali Anadhulumiwa kimapenzi uk 98

Chandachema kutelekezwa na babake Fumba na kuachwa alelewe na Bi. Kizee ambaye anaaga akiwa darasa la kwanza. Pia hajui aliko mama yake.

Rehema, Mamake Chandachema anadhulumiwa kimapenzi kwa kuringwa mimba na Fumba mwalimu wake akiwa kidato cha tatu. Uk 103

Chandachema anaizimika kufanya kazi katika shrika la chai la Tengenea ili kujikimu akiwa darasa la pili maadamu apate nafasi ya kusoma Uk.105

Chandachema   na wanawe Tenge wanalazimika kushuhudia bwana Tenge akigeuza chumba chao Danguro japo ni watoto wachanga…na kusababishiwa dhiki ya kisaikolojia. Uk 106

Swali la insha 2

Ukabila ni tatizo sugu katika nchi nyingi za Kiafrika. Tetea kauli hii ukilejelea Chozi la Heri  ( al. 20)

Subira alitengwa na familia ya mume wake kwa kuwa wa kabila tofauti na lao.

Mwanaheri anatueleza kuwa mama yake alikuwa ametoka kwenye jamii ya mamwezi lakini babake alikuwa wa jamii tofauti. Kila mara subira aliitwa ‘muki’ au huyo wa kuja.

Kijana mmoja alimwita Ridhaa mfuata mvua jambo lilimuumiza sana Ridhaa.

Mzee kendi alimtendea udhalimu Ridhaa na kuiteketeza aila yake licha ya wao kuwa majirani kwa miaka hamsini. Ridhaa alifanyiwa hivi kwa kuwa alikuwa ametoka kwenye kabila tofauti na mzee kendi.

Ndoa ya Selume ilisabaratika baada ya vita vya kutawazwa kwa kiongozi mpya kuoa msichana wa kikwao.

Tulia alimsaidia kaizari kufunganya na kumsidikiza hadi njia panda. Alimkumbatia na kumwambia kuwa mwenyezi Mungu ndiye hupanga na nguvu na mamlaka pia hutoka kwake

Uongozi mpya umezua uhasama kati ya koo ambazo zimeishi kwa amani kwa karibu karne moja.

Subira aliweza kuvumilia kubaguliwa, kufitiniwa na kulaumiwa kwa asiyoyatenda, Mwishowe alihiari kujiondokea na kwenda mjini alikojinywea kinywaji kikali. (zozote 10 x 2)

Swali la insha 3

Jadili nafasi ya sehemu zifuatazo katika riwaya ya Chozi la Hari:

  1. Hotuba (alama 10)
  2. Uozo katika jamii (alama 10)

Hotuba

Hotuba ni maelezo maalumu yanayotolewa na mtu mmoja mbele ya watu. Pia huitwa hutuba. Mwandishi wa riwaya hii ametumia hutuba kwa ustadi mkuu kupitisha ujumbe mbalimbali.

Hotuba hizi ni:

Hotuba ya Racheal Apondi kwa maafisa waliohudhuria warsha kuhusu jukumu la vikosi vya askari katika kudumisha usalama, amani na maridhiano nchini (uk 112- 113). Katika hotuba hii, Racheal Apondi anasisitiza kuwa: Suala la usalama haliwezi tena kupuuzwa. Usalama umekuwa mojawapo ya mahitaji ya kibinadamu. Anasema kuwa bila usalama, binadamu hawezi hata kushiriki katika shughuli za kuzalisha mali, hivyo hata mahitaji yake mengine ya kimsingi kama vile chakula, malazi na makazi hayawezi kukidhiwa. Kila binadamu ana jukumu la kudumisha amani na usalama. Wafanyakazi wa umma, hasa polisi na wanajeshi wana jukumu kubwa zaidi la kudumisha usalama na amani. Kila mmoja wetu anastahili kuhakikisha kuwa ameepuka vitendo vya kihalifu. Ni vyema mtu kuwaangaza wahalifu wakati wote. Vikosi vya polisi na wanajeshi vimefunzwa maarifa ya kukabiliana na kadhia za jinai na upelelezi. (4×1= 4)

Hotuba ya Lunga Kiriri- Kangata kwa walimu na wanafunzi gwarideni (uk 68-69). Hotuba hii ilisisitiza umuhimu wa kuhifadhi mazingira. Anasisitiza kuwa: Suala la uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Misitu ilikuwa imevamiwa na viongozi wenye mate ya fisi. Baadhi ya vinara wa taasisi mbalimbali za umma wamewaacha wanyama kama mayatima kwa kuwapoka makazi yao. Maelfu ya maekari ya misitu yamefyekwa na kujengwa viwanda. Badala ya mibambakofi na miti mingine inayosafisha hewa, michai imetwaa nafasi yake. Wanaohusika na matendo haya wanapoulizwa hudai kuwa michai si adui ya mazingira! Wengine wanasema kuwa misitu haina budi kukatwa ili kupanda mimea inayotoa chakula, kwani jamii lazima ijitosheleze kwa chakula. La kuhuzunisha ni kwamba hawa hawa wanaosema hivyo ndio wanaokita majengo ya kifahari katika sehemu ambazo zinastahili kutengewa upanzi wa chakula! Wengine wamediriki kunyakua hata madhabahu kwenye Mlima wa Nasibu ili kujenga hoteli kubwa za kitalii. Wazee wetu hata hawana mahali pa kuchomea kafara! Tunakata miti bila kupanda mingine. Hata mabustani ya maua tunashindwa kuyastawisha. Tukiendelea kuharibu mazingira sehemu yetu itazidi kuwa jangwa. (2×1= 2)

Hotuba ya Umu katika hoteli ya Majaliwasiku yake ya kuzaliwa. Umu anawashuku Mwangeka na Apondi kwa kuwa wazazi wake wema. Anawashukuru kwa kumsomesha. Anawashukuru kwa kumsaidia Dick kujiendeleza kimasomo. Mwangeka na Apondi wanamshukuru Umu kwa kuwapa furaha. Apondi anamshukuru kwa kumlea mdogo wao kwa maadili bora. (2×1= 2)

Hotuba ya Dick katika hoteli ya Majaliwa siku ya kuzaliwa kwa Umu. Dick anamshukuru Umu kwa msaada wake na ahadi ya kumlea. Anamkumbusha siku walipokutana katika uwanja wa ndege na ilivyokuwa muhimu kwake. Anamshukuru Umu kwa kumwelekeza kwa wazazi wao wale. Anawashukuru Apondi, Mwangeka na wanawe kwa ushauri wanaompa. (2×1= 2)

Mtahiniwa ataje hotuba kisha aeleze masuala muhimu yanayoibuliwa na kila moja.

Uozo katika jamii (alama 10)

Uozo ni hali ya kuzorota na kutozingatiwa tena kwa maadili mema katika jamii. Ni hali ambapo milazote na desturi njema huvurugwa na wanajamii wanaofanya mambo yaliyo kinyume nahali halisi ya maisha. Mwandishi amejadili suala hili kwa undani kama ifuatavyo;

Jamii inaendeleza ubakaji. Genge la mabarobaro watano lilifululiza hadi walipokuwa maskini Lime na Mwanaheri na kuwabaka mbele ya baba yao (uk 25).

Kuna ulanguzi wa dawa za kulevya. Dick alipotoroshwa na Sauna alipelekwa kwa tajiri mmoja aliyemwingiza katika kusafirisha dawa za kulevya kutoka nchi moja hadi nyingine (uk 119- 120).

Wanajamii wanaendeleza uporaji na wizi wa mali. Vijana wanawavamia watu, kuwaua na kupora katika maduka ya kihindi, kiarabu na ya waafrika wenzao.

Jamii inaendeleza ufuska/ ukahaba. Sauna aliiba watoto na kuwapeleka kwa mama mmoja aliyewatumia kwa biashara ya nipe nikupe (uk 84).

Biashara haramu inaendelezwa. Bi. Kangara alifanya biashara ya kuwauza watoto na vijana- Safari yake ilipata mkondo mwingine baada ya polisi kupata fununu kuhusu njama ambazo yeye na Bi. Kangara walikuwa wakiendesha. Mabibi hawa walikuwa na mtandao ambao kazi yake ilikuwa kuwauza watoto na vijana (uk 84).

Kuna tatizo la mimba za mapema. Vijana wana mazoea ya kukumbatia mtafaruku wa kuhisia unaowapata na mara hujipata wameambulia ujauzito kama alivyofanya Zohali (uk 98).

Baadhi ya wanajamii wanaendeleza uavyaji mimba. Sauna alijaribu awezavyo kuavya mimba na mwishowe, baada ya kushindwa, anaamua kujiua.

Kukiuka maadili ya kikazi. Fumba (mwalimu) anakiuka maadili ya kazi na kujihusisha kwa mapenzi na mwanafunzi wake, Rehema, na hatimaye kumpachika ujauzito (uk 102).

Wazazi wanawabaka wana wao. Babake Sauna anafanya mapenzi na mwanawe kila apatapo nafasi, na mwishowe, Sauna anapata mimba.

Starehe na anasa kwa vijana. Vijana wa vyuo vikuu wameshindwa kutofautisha usiku na mchana. Tindi anasahau kumrejesha Lemi nyumbani kutokana na muziki (uk 121).

Wazazi wanakwepa malezi na kuwatupa wanao wakiwa wachanga. Neema anampeleka mtoto aliyemwokota kwa polisi (uk 162).

Vijana kuwaiga wazee. Mwangemi na Mwangeka walikuwa na tabia mbovu ya kumuiga babu yao (uk 186). (10×1= 10)

Mtahiniwa afafanue kwa mifano kutoka katika riwaya.

Swali la insha 4

  1. Fafanua namna mbinu ya majazi ilivyotumiwa katika riwaya. 10
  2. Jadili maudhui ya nafasi ya vijana katika jamii ukirejelea riwaya ya Chozi la Heri.  Al.10

Fafanua namna mbinu ya majazi ilivyotumiwa katika riwaya. 10

Ridhaa – Kukubali ama kutosheka. Mhusika Ridhaa anakubali na kutosheka na makuruhu aliyofanyiwa ya kuteketezewa mali na familia yake.

Bwana Tenge – Tenge ina maana ya fujo. Bwana Tenge anamfanyia mkewe fujo na vitimbi anamwendea kinyume mke wake, Bi. Kimai. Bwana Tenge anashiriki mapenzi na wanawake wengine.

Mzee Kedi – Neno kedi lina maana ya mambo yasiyopendeza, mambo ya hila pia ni kiburi.   Mzee Kedi anamfanyia ridhaa hila kwa kuhusika katika kuiangamiza familia yake.

Bwana Mkubwa – Mkubwa ni neno lenye maana ya cheo au hadhi kubwa. Bwana mkubwa ana cheo kikubwa serikalini.

Tetei – ina maana ya kutetea. Bi. Tetei ni mwanaharakati anayetetea haki za wanaume.

Mwalimu Dhahabu ni madini yenye thamani. Mwalimu dhahabu ni mwalimu anayekuwa wa msaada kwa Umulkheri

Hazina – Hazina ina maana mali iliyohifadhiwa. Mhusika Hazina anakuja kuwa kama hazina kwa Umukheri kwani anamfaa Umu jinsi alivyomfaa kwa kimpa noti ya shilingi mia mbili.

Zohali – Neno hili lina maana ya ajizi. Mhusika Zohali anapachikwa mimba akiwa kidato cha pili ni dalili ya uzembe na kutomakinika masomoni.

Chandachema – Chandachema ni jina lililoundwa kutokana na Chanda kidole) chema ambacho huvikwa pete. Mhusika huyu ingawa anapitia changmoto tele maishani anaishia kupewa ufadhili wa masomo(kuvishwa pete) na shirika la kidini.

Bwana Mabavu – Mabavu ni nguvu. Bwana Mabavu anatumia nguvu kumpoka babake Shamsi ardhi yake.

Mzee Maarifa- anatumia maarifa na hekima kuanzisha kituo cha kupigania hakiza kibinadamu.

Neema ni mkewe Mwangemi. Neema ina maana ya Baraka. Mhusika huyu anakuwa Baraka kwa mume   na pia kwa mwaliko.

Bwana Kimbaumbau ni mtu kigeugeu. Bwana Kimbaumbau anamsaliti Naomi kwa kutaka kufanya mapenzi naye.

Jadili maudhui ya nafasi ya vijana katika jamii ukirejelea riwaya ya Chozi la Heri.

vijana ni wasomi mf. Umu, tila.

Ni walanguzi wa dawa za kulevya mf. Dick.

Vijana wengine wa kike wakubali kukeketwa na wengine wanaaga dunia na kulazwa hospitalini mf. Tauma.

Vijana ni wapenda fujo.

Vijana hutumiwa na wanasiasa kutekeleza uovu na mauaji.

Ni dhihirisho kama wasio na huruma. K.m kuua wenzao bila huruma.

Wasio na msimamo dhabiti. Wanapotoshwa na wanasiasa bila kuwazia madhara waliosababisha.

Vijana ni wenye bidii katika kazi zao mf. Dick.

(Tanbihi: kadilia hoja za wanafunzi.) 10 x 1 = 10

Swali la insha 5

Jadili jinsi mwandishi wa riwaya hii alivyofaulu kutumia mbinu ya kinaya na sadfa. (alama 20)

Kinaya

  • Kinaya ni maelezo ya mambo kinyume na yalivyo.
  • Mwangeka anashiriki udumishaji wa amani Katika Mahariki ya kati huku familia yake ikiangamia nyumbani kutokana na ukosefu wa amani.
  • Mzee Kedi anaua familia ya Ridhaa ilhali ni yeye aliyethamini masomo ya wapwaze.
  • Ni kinaya wenye maduka kufunga milango wakati jumba la Ridhaa lilipochomeka badala ya kuyaacha wazi watu wotorokee .
  • Ni Kinaya Lunga Kirir kuachishwa kazi baada ya kutetea wanyonge wasiuziwe mahindi yaliyokuwa na sumu.
  • Ni kinaya Sauna kujifanya mzuri ilhali anawaiba watoto
  • Ni kinaya Neema kupeleka mtoto kwa makazi ya watoto na mwishowe kwenda kupanga mtoto huko
  • Ni kinaya Naomi kutoroka mmewe nawanawe ilhali hapo baadaye anajilaumu
  • Ni kinaya nchi ambayo ¡na miaka hamsini kuonekana kama mtoto wa mika hamsini
  • Ni kinaya kuwa wafrika wanakuwa wafanyikazi katika mashamba yao chini ya wakoloni
  • Ni kinaya watu walioishi na Ridhaa kwa amani wanawageukia na kuchoma nyumba yake pamoja na familia yake
  • Ni kinaya vijana kumbaka lime na Mwanaheri mbele ya wazazi wao
  • Ni kinaya mamakwe kufukuza subira kwa kuwa hawakuwa wa jamii moja
  • Ni kinaya mzee Maya kumbaka mwanawe Sauna
  • Ni kinaya wazazi wa Zohali ambao ni wasomi kumtesa Zohali kwa ajili ya ujauzito
  • Ni kinaya Tuama kusifu utamad uni wa tohara za kike iIhali ndio sababu ya kuwa hospitalini
  • Ni kinaya watu wan chi ya Wahafidhina kumkataa kiongozi wa kike na ndiye anayewafanyia kazi
  • Ni kinaya kwa pete kutaka kujia kwa kuwa na watoto watatu akiwa umri wa chini ya mia ishirini na moja   Hoja zozote 10 X1=10

Sadfa

  • Sadfa ni kuwaleta wahusika kadhaa pamoja bila kukusudiwa.
  • Selume kufikiria kustaafu katika hospitali ya uma wakati Ridhaa alikuwa anamalizia ujenzi wa hospitali ya Mwanzo Mpya
  • Umu kukutana ana Hazina alipokuwa akimtafuta.
  • Safari ya Umu kuchelewa inamfanya akutane na Dick katika uwanja wa ndege.
  • Mwangeka kukutana na Apondi katika karakana ni sadfa.
  • Ni sadfa Umu, Dick na Mwaliko kukutana katika Hoteli ya Majaaliwa.
  • Inasadifiana kuwa wakati Selume anapotaka kiacha kazi katika hospitali ya umma ndio Ridhaa anama liza kujenga hospitali ya mwanzo mpya
  • Siku ya kuzaliwa kwa Umu inasadifiana nay a Mwangemi
  • Inasadifiana wakati Neema akienda ofisini ana kiona kitoto kilichokuwa kimetupwa
  • Umu na Dick wanakitana kisadfa katika uwanja wa ndege
  • Ni sadfa Mwaliko kupangwa na binamuye mwangeka aliyempanga nduguye
  • Inasadifu kuwa Dick alipokuwa akiwaza juu ya nduguye Umu alikuwa nyuma yake
  • Kukutana kwa wana wa Lunga katika hoteli ya Majaliwa ni sadfa
  • Ni sadfa kuwa Umu anapowaza sana juu ya maisha yake wenzake wana matatizo kumliko Hoja zozote 10 X1=10

Swali la insha 6

Tathmini umuhimu wa mbinu zifuatazo katika kuijenga riwaya ya Chozi la Heri

  1. Nyimbo   (alama 10)
  2. Barua   (alama 10)

Nyimbo

Wimbo wa Shamsi unaonyesha ukengeushi,

Licha ya elimu aliyo nayo, Shamsi ameshindwa kukabiliana na changamoto za maisha. Anaingilia matumizi mabaya ya pombe.

Unabainisha ukosefu wa uwajibikaji, badala ya kutafuta mbinu ya kukabiliana na hali duni ya maisha, analalamika kwamba wenye nguvu hawakumpa kazi walizoziahidi.

Unakashifu unyakuzi wa ardhi za wanyonge. Shamba la kina Shamsi linachukuliwa na Bwana Mabavu.

Unachimuza ufisadi – Bwana Mabavu anawaonyesha hati miliki bandia na kuwafukuza shambani mwao

Unaendeleza maudhui ya ukoloni mamboleo – Mabavu anamiliki shamba la Baba ya Shamsi na kuwageuza kuwa maskwota.

Unaangazia ukiukaji wa haki za binadamu – Shamsi na wenzake wanafutwa kazi kwa kuwazia kugoma.

Inaonyesha umaskini wa familia ya Shamsi – Babake Shamsi anakufa kwa kula mizizi mwitu wenye vijaasumu

Unakashifu unyonyaji wa wafanyikazi – Shamsi na wenzake wanalipwa mishahara duni.

Unasawiri tatizo la matumizi mabaya ya vileo- Shamsi anaingilia ulevi baada ya kufutwa.

Wimbo wa Shamsi unaoghaniwa na Ridhaa

Wimbo wa majigambo unaosawiri tabia ya Shamsi – anajivunia na kusema kuwa anaogopwa kwa kutoka katika jadi tukufu.

Unamfanyia tashtiti Shamsi kwa kujisifu kwa kuzua mikakati ya kukabiliana na hali ya uhitaji na hali mwenyewe ni mlevi.

Unaonyesha uovu wa jamii – wauza pombe wanatia vijaasumu ili iwe tayari haraka bila kuwazia madhara ya watumia wayo. Zozote 10 X 1 = 10

Barua

Barua ya Lunga

Barua ya kustaafishwa kwa Lunga inaonyesha dhuluma kwa wafanyikazi. Lunga anafutwa kwa kutetea wanyonge dhidi ya kuuziwa mahindi hatari kwa afya.

Inaonyesha uadilifu wa Lunga anavyosema Afisa Mkuu Mtendaji

Inakashifu ukatili wa waajiri – Lunga anafutwa bila hali yake kuwaziwa

Inaonyesha mbinu-hasi za uongozi – Viongozi wanawaangamiza wanaowapinga njama zao za kiufisadi.

Kuonyesha uongo/ unafiki wa waajiri- kusingizia kuwa shirika linapunguza wafanyikazi kutokana na changamoto za kifedha kutokana na gharama ya uzalishaji mali ilhali Lunga anafutwa kwa kukashifu kutaka kuuza mahindi yaliyoharibika. (hoja 5)

Barua ya Subira

Inaonyesha ukosefu wa uwajibikaji wa Subira – anaondoka bila kuwazia hali ya baadaye ya watoto wake.

Inadokeza maudhui ya malezi – Subira anamuusia Mwanaheri amtunze mnuna wake na pia wamtii baba yao.

Inakashifu ubaguzi – Subira analalamikia kubaguliwa na mavyaa Inaonyesha uwajibikaji wa mzazi kwa watoto wake japo Subira anaondoka anawaachia wanawe ujumbe kwamba ameondoka na kuwashauri

Anakashifu ukiukaji wa haki za kibinadamu – anasimangwa na kuitwa mwizi.

Inajenga tabia ya wahusika – imesawiri udhaifu wa nia wa Kaizari. Hamtetei mkewe dhidi ya dhuluma ya mavyaa. Inakuza ukatili wa mavyaa kwa kumwita muuki na mwizi.  (hoja 5)

Swali la insha 7

Matatizo mengi yanayowakumba wahusika wengi katika riwaya hii ni mwiba wa kujidunga. Jadili (al.20)

Wahusika katika riwaya ya Chozi la Heri wanakumbwa na matatizo mbalimbali. matatizo hayo ni ya kiuchumi na kijamii.

Vyanzo vya matatizo yenyewe ni tofauti tofauti, kuna yale yanasababishwa na wahusika wenyewe ilhali mengine yanaletwa na watu wengine.

Tunaweza kusema kuwa matatizo mengine ni mwiba wa kujidunga huku mengine yakiwa ya kudungwa na wengine.

  • Jumba moja la Ridhaa linabomolewa kwa kuwa alilijenga katika ardhi iliyotengewa ujenzi wa barabara katika mtaa wa zari. Hakuchunguza uhalali.
  • Terry mkewe Ridhaa anapuuza maonyo na maneno ya mumewe kuhusu mkasa ambao ungetokea hivyo anateketea.
  • Ami wamwangeka anaagamia katika mkasa wa moto alipoenda kuwasaidia watu waliokuwa wanateketea.
  • Walioteketea katika moto wa lori walijiigiza matatani wenyewe kwani walikuwa wameonywa kulikuwa na hatari.
  • Uhasama, migogoro na ukosefu wa mahitaji muhimu unaoikumba familia ya Mwimo Msubili hii ni kwa sababu ya yeye kuwaoa wake wengi.
  • Kufutwa kazi kwa Lunga Kangata Kiriri baada ya kukataa kukubali mahindi ya jano kuuziwa wananchi ni mwiba wa kujidunga.
  • Mauti yanayowakumba vijana waliokuwa wakiandamana baada ya sherehe za kuapishwa kwa kiongozi mpya.
  • Tendo la Subira kuondoka nyumbani na kumwacha mumewe
  • Pete anapokubali kuolewa na Nyangumi bila kufanya uchunguzi wa kina.
  • Tukio la Zohari kupata mimba na kutumbukia katika mateso mengi.
  • Tendi la Mwangeka na Mwangemi kufanyia babu yao mzaha, kwa kuwa usiku mmoja aliamua kuwalipua viboko.
  • Mwangeka anakubaliana na Tila kuigiza maombolezi ya Dedan Kimathi ambayo yanamfanya babake kumwadhibu kwa kutowajibika.
  • Kukamatwa kwa Sauna na mwajiri wake Bi. Kangara kwa kujihusisha na Biashara ya ulanguzi wa watoto.
  • Tuama anaathirika vibaya baada ya kupaswa tohara na kulazwa hospitalini ni tendo alilolitenda kinyume na mapenzi ya baba yake.
  • Walevi wenza wa Shamsi ambao wanapoteza uwezo wa kuona au uhai wao kwa kubugia vileo.
  • Mumwewe Selume anamfukuza mkewe kwa kuwa si wa kabila lake baadaye anamlea mtoto peke yake.
  • Mandu anapouawa katika vita akiwa ughaibuni ni mwiba kwani huenda hangepoteza maisha kama hangeenda huko mapema.
  • Fujo zinazosababishwa na uhafidhina baada ya uchaguzi ambapo wanapoteza uhai na mali.
  • Wakimbizi waliohamia katika mimea na baadaye kufukuzwa ulikuwa mwiba kwani si halali kulima msituni.
  • Naomi kumwacha mumewe Lunga Kiriri na watoto na baadaye kuwatafuta baadhi ya kifo cha bwanake ulikuwa mwiba wa kujindunga. Zozote (20 x 1) = 20)

Swali la insha 8

Jadili maudhui ya 'asasi ya ndoa' kama yalivyoangaziwa riwayani (alama 20)

Ndoa ni maafikiano rasmi baina ya mwanamume na mwanamke ili waweze kuishi pamoja kama mke na mume.

Ridhaa alikuwa na mke kwa jina Terry. Walibarikiwa kuwa na watoto wafuatao: Mwangeka, Tila na marehemu Dede. Ndoa hii haikudumu kwani janga la moto iiliisambaratisha aila hii na ndipo Terry, Tila, Lily na Becky wakaiaga dunia. Ridhaa akabaki mjane.

Mwangeka alikutana Lily Nyamvula katika chuo kikuu na kumwoa. Walibarikiwa na mtoto mmoja kwa jina Becky. Ndoa hii haikudumu kwani Lily na Becky waliangamia kwenye janga la moto.

Baada ya ndoa ya mwanzo kusambaratika, Mwangeka alimwoa Apondi. Walibarikiwa na mwana wa kiume kwa jina Ridhaa.

Mwangemi alimwoa mwanamke kwa jina Neema. Hawakufaulu kupata mwana wao kindakindaki japo walipanga mwana wao kwa jina Mwaliko.

Kangata alikuwa na mke wake kwa jina Ndarine. Walibarikiwa na wana wafuatao. Lunga Kiriri, Lucia Kiriri na Akelo Kiriri.

Lucia Kiriri - Kangata - alikuwa ameolewa Kangata walishangaa mwana wao akaozwa kwa watu ambao huvaa nguo nje na pia huzaa majoka.

Kaizari alikuwa na mke kwa jina Subira. Waliborika no mabinti wawili, Lime na Mwanaheri.

Lunga alikuwa na mke kwa jina Naomi. Walikuwa wa watatu, Umu, Dick no Mwaliko. Ndoa hii haikudumu

mahari kutoka kwa buda mmoja kwa jina Fungo aliyemuoa kama bibi wa nne. Ndoa hii haikudumu kwani Pete alihiarikumwacha baba huyu.

Mwanafunzi aongezee hoja. Zozote

Swali la insha 9

Kwa kutumia hoja kumi kumi eleza jinsi maudhui ya utu na uozo wa kijamii yalivyoshughulikiwa katika Chozi la Heri (alama 20)

Maudhui ya utu katika chozi la heri

  • Dkt.Ridhaa anaonekana kujawa na utu kwa kudhamini masomo ya wapwa wawili wa mzee Kedi.
  • Ridaa alijenga kituo cha afya cha mwanzo mpya ili kunusuru maisha ya binadamu waliokuwa wakiangamia kwa kukosa huduma bora za afya
  • Mwangeka na Apondi walikubali kumchukua umu na kuwa motto wao wa kupanga.
  • Kiriri aliyekuwa mwajiri wa kangata alionyesha utu kwa kumwacha kangata afaidi ardfhi yake kiasi cha kuchukuliwa kuwa wanatoka mbari moja na kangata
  • Neema anaonyesha kujawa na utu kwa kitendo cha kumwokota mtoto Immaculata aliyekuwa ametupwa jaalani akampekeka pamoja na mwanapolisi wakampeleka katika kituo cha watoto cha Benefacto.
  • Mtawa Gizarina wa kituo cha kituo cha benefactor alikuwa na utu kwa kuwa alijitoa kuwapokea watoto mbali mbali waliohitaji msaada wa malezi.
  • Mtawa pacha aliyemhudumia zohali, baada ya kupata mimba na kuteswa na wazazi
    wake, alimtafutia shule ili aendelee na masomo aliyokuwa ameachishwa mashirika ya kidini yalitoa misaada kwa waadhiriwa wa majanga mbali mbali katika jamii. Wakristo nawaisilamu waliungana pamoja kutoa msaada katika kambi waliotimuliwa kutoka kwao.
  • Shirika la jeshi la wajana wa Kristo lilidhihirisha utu lilipoamua kujenga makao ya watoto yatima.
  • Watoto waliotupwa na wazazi wao na wenye wazazi wahitaji. Chanda chema alipata msaada kupitia kwa shirika hili.
  • Shirika la kidini la lakikisho la itaki na utulivu linadhihirisha utu kwa kuwasaidia watoto kupata elimu bora. Chanda chema anasaidika kuendelea na masomo yake kupitia shirika hili.
  • Tulia alimsaidia Kaizari kufunganya na kumsindikiza hadi njia panda. Alimkumbatia na kumwambia kuwa mwenyezi mungu ndiye hupanga na nguvu na mamlaka kutoka kwake.
  • Katika hospitali aliyofanya kazi Selume,kuna mgonjwa aliyepelekwa na wasamaria wema katika hospitali baada ya kuumizwa katika mgogoro wa kupigiana ardhi katika eneo la Tamuchungu.

Maudhui ya uozo wa maadili katika jamii ya chozi la heri.

  • Ubakaji. Lime na mwanaheri walibakwa na mabarobaro watano mbele ya macho ya wazazi wao.
  • Ulanguzi wa dawa za kulevya. Dick anaifanya kazi ya kusafirisha dawa za kulevya kutoka nchi moja hadi nyingine.
  • Uporaji na wizi-vurugu za baada ya uchaguzi alipochacha vijana walivunja maduka ya waarabu, wahindi na hata waafrika wenzao.
  • Mauaji-kendi anaichoma nyumba ya Ridhaa ambapo aila ya Righaa inachomeka.
  • Unyakuzi wa ardhi watu wamejinyakulia maelfu kwa maelfu ya ekari wakajenga Viwanda na maduka ya kibiashara kuwaacha wenyeji bila hata makazi.
  • Uendelezaji wa biashara haramu-Bi.kanagara walishirikiana na sauna Katika kutekeleza biashara ya kuwauza watoto
  • Kuavya mimba-Baada ya sauna kubakwa na baba yake wa kambo(bwana maya) mamake Sauna anamshurutisha kuavya mimba hiyo.
  • Kutupwa kwa watoto wachanga. Neema anamwokota mtoto katika jaala na kumpeleka katika Makazi ya watoto ya benefactor.
  • Mapenzi ya baba na bintiye (Sauna).
  • Ukabila-huu unajitokeza baada ya kutawazwa kwa kiongozi mpya mwanamke ambapo majirani waliwagueuka wenzao waliokuwa wametoka kwa kabila tofauti
  • Matumizi ya pombe haramu - Vijana wanasomea shahada za uzamili wanajihusisha na unywaji wa pombe haramu na kufariki.
  • Ukeketaji wa watoto wa kike - Tauma anaelezea kuwa asingepashwa tohara asingeolewa.
  • Ndoa za mapema-Pete anaozwa kwa mzee fungo kama mke wake wane
  • Ufisadi katika mtaa wa tononokeni kuna watu waliojenga majumba yao katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara
  • Uuzaji wa mahindi yaliyoharibika-Lunga alipigwa kalamu baada ya kugundua mahindi yaliyokuwa yametoka ughaibuni yalikuwa hatari kwa usalama ,hata wa panya.
  • Kuajiriwa kwa watoto wadogo ambao hata vifua havijapanuka watoto walinyakuliwa na kupelekwa sehemu mbali mbali nchini kufanya kazi.
  • Kutupwa kwa taka karibu na nyumba za watu-katika mtaa wa mabanda wa somber Anakoishi Bw.makiwa taka linamwagwa katikati mwa msongamano wa kibanda Kutoka kwa waishipo waheshimiwa. "Nimekuja kuwakombao...."

Swali la insha 10

Jadili ufaafu wa anwani Chozi la Heri.

Mwandishi anatueleza kuwa Ridhaa alipoenda shuleni siku ya kwanza alitengwa na wenzake kwani hawakutaka ashiriki michezo yao. Kijana mmoja mchokozi alimwita 'mfuata mvua' Ridhaa alikuja kuwashinda katika mitihani yote. Ridhaa alifululiza nyumbani na kujitupa mchangani na kulia kwa kite na shake.

Mamake alimliwaza na kumhakikishia kumwona mwalimu keshoye. Tangu siku hii, huu ukawa ndio mwanzo wa maisha ya heri kwa Ridhaa kwani baada ya mwalimu kuzungumza na wanafunzi umuhimu wa kuishi pamoja kwa mshikamano, Ridhaa alipaa kwenye anga ya elimu hadi kufikia kilele cha elimu na kuhitimu kama daktari.

Ridhaa alipotoka kwenye Msitu wa Mamba alijiona nafuu kwani wapwa zake Lime na Mwanaheri walikuwa wamepata matibabu. Dadake Subira alitibiwa akapona. Mwamu wake Kaizari amepona donda lililosababishwa na kuwatazama mabinti zake wakitendewa ukaini(kubakwa) na vijana wenzao. Ridhaa anajua kuwa Kaizari ni afadhali kwa sababu hakuna aliyemtenga na mmoja kati ya jamaa zake. Ridhaa anapomfikiria Kaizari anajiambia heri nusu shari kuliko shari kamili.

Ridhaa aliposikia sauti ya kike ikitangaza, tangazo lile lilimrudisha katika mandhari yake ya sasa. Alijaribu kuangaza macho yake aone anakoenda lakini macho yalijaa uzito wa machozi ambayo alikuwa ameyaacha yamchome na kutiririka yatakavyo.

Wakati Ridhaa alimkazia macho Mwangeka-waka Mwangeka alikuwa akijiuliza iwapo babake amekuwa mwehu kwa kukosa kushirikiana na majirani kuchimba kaburi kuyazika majivumatone mazito ya machozi yalitunga machoni mwake Mwangeka. Akayaacha yamdondoke na kumcharaza yatakavyo. Uvuguvugu uliotokana na mwanguko wa machozi haya uliulainisha moyo wake, ukampa amani kidogo. Moyo wake ukajaa utulivu sasa kwa kujua kuwa wino wa Mungu haufutiki.
Wakati Ridhaa_ alikuwa akimsimulia Mwangeka msiba uliyomwandama tangu siku alipoondoka kwenda kuweka amani Mashariki ya Kati Ridhaa alisita akajipagusa kijasho kilichoku- wa kimetunga kipajini mwake kisha akatoa kitambaa mfukoni na kuyafuta machozi yaliyokuwa yameanza kumpofusha. Uk 48 Mwangeka alipokuwa ameketi mkabala na kidimbwi cha kuogelea mawazo yake yalikuwa kule mbali alikoanzia.

Akawa anakumbuka changamoto za ukuaji wake. Akawakumbuka wana wake. Alipomkumbuka Annatila(Tila) mwili ulimzizima kidogo akatabasamu kisha tone moto la chozi likamdondoka. Katika Msitu wa Simba kulikuwa na maelfu watu waliogura makwao. Kati ya familia zilizoguria humu ni familia ya Bwana Kangata. Kwa Kangata na mkewe Ndarine, hapa palikuwa afadhali kwani hawakuwa na pa kwenda kwa kuwa hata kule walikokuwa wakiishi awali hakukuwa kwao. Uk 57

Wakati Dick walikutana kisadfa na Umu katika uwanja wa ndege, walikumbatiana kwa furaha. Machozi yaliwadondoka wote wawili na wakawa wanalia kimyakimya. Walijua fika kuwa jaala ilikuwa imewakutanisha na kwamba hawatawahi kutengana tena. Maisha sasa yalianza kuwa ya heri kwao. Baada ya miaka kumi ya kuuza dawa za kulevya, Dick alifaulu hatimaye kujinasua kutoka kwa kucha za mwajiri wake. Alianza biashara yake mwenyewe ya kuuza vifaa vya umeme 189 :111 P Sasa akaanza kujitegemea kwa kuwa amejiajiri. Alikuwa ameu fungua ukurasa mpya katika maisha yake. Maisha yake sasa ni ya heri.

Wakati Neema na Mwangemi walikabidhiwa mtoto wao wa kupanga na Mtawa Annastacia, Mwaliko alimkumbatia Neema na kumwita mama na kumwahidi kuwa ataenda naye. Neema alidondokwa na chozi la furaha na kumkumbatia Mwaliko kwa
mapenzi ya mama mzazi. Hili lilikuwa ni chozi la heri kwa Neema. (mwanafunzi aongezee hoja)

(Hoja zozote 20 x 1 = 20)

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri" on Whatsapp

OR

This is the most affordable option. You get all topics/full set papers at a lesser price than if you bought per paper/ per topic.

Click here to download the full document with all topics

OR




Read 386 times Last modified on Tuesday, 26 January 2021 12:49
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - Maswali na Majibu ya Dondoo katika Riwaya ya Chozi la Heri
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in Mwongozo wa Chozi La Heri
Tagged under
  • Kiswahili
  • ChoziLaHeri

Related items

  • Kiswahili Karatasi ya Pili Maswali na Majibu - Kassu Jet Joint Exams 2020/2021
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba
  • Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Tamthilia ya Kigogo
  • Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tamthilia ya Kigogo
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
Mwongozo wa Chozi La Heri