Jalada la tamthilia.
Kuna sura ya mwanamme ambaye ameketi akiwa na rungu mkononi.Huyu ni Majoka ambaye ni kiongozi Sagamoyo na rungu mkononi mwake inaashiria uongozi.
Mwanamme huyo anatazama jabali lenye rangi nyeusi ambalo si laini. Jabali ni Sagamoyo na kutokuwa laini ni ishara kuwa Sagamoyo kuna shida,wanasagamoyo wana matakwa mengi. Weusi wa jabali ni uongozi mbaya unaoendelezwa Sagamoyo na viongozi.
Juu ya jabali hilo kuna mwanga, ishara kuwa kuma matunaini ambayo yanatarajiwa Sagamoyo, wanamapinduzi wanapigania haki ili kujenga jamii mpya.
Ufaafu wa anwani ya tamthilia.
Kigogo ni mtu mwenye madaraka makubwa kiutawala.
Majoka anatumia madaraka yake kulaghai wananchi, anachukua vilivyo vyao.
Anatangaza kipindi cha mwezi mzima cha kusheherekea uhuru kutumia madaraka aliyonayo.
Majoka anafunga soko la Chapakazi ili sehemu hiyo ajenge hoteli ya kifahari kwa kutumia madaraka aliyonayo.
Anapandisha bei ya chakula katika kioski kwa vile ana madaraka.
Majoka anatumia mamlaka yake kumteka na kumtia ndani Ashua.Anamtendea ukatili, Ashua ana majeraha kutokana na kichapo.
Majoka anapanga kifo cha Jabali, mpinzani wake. Anampangia ajali na kuangamiza wapinzani wake pamoja na chama chake kwa kutumia mamlaka yake..
Majoka anapanga kutumia mamlaka yake kuzima uchunguzi wa Tunu kuhusu kifo cha Jabali.
Majoka anafuja pesa za kusafisha soko huku akijua hakuna wa kumhukumu kwa kuwa ndiye kiongozi.
Majoka anatumia mamlaka yake kudhibiti vyombo vya habari Sagamoyo, anasema sagamoyo kitabakia kituo kimoja tu cha habari; sauti ya mashujaa, vingine havina uhai.
Majoka kwa mamlaka yake anaamuru polisi kutawanya waandamanaji.
Majoka anafungulia biashara ya ukataji miti Sagamoyo kwa kutumia mamlaka yake bila kujali athari zake kwa wananchi.
Majoka anampa mamapima kibali cha kuuza pombe haramu kwa kutumia mamlaka yake.
Kwa mamlaka yake, Majoka anafadhili miradi isiyo muhimu, anafadhili mradi wa kuchonga vinyago kutoka nje.
Majoka anaamuru wafadhili wa wapinzani kuvunja kambi zao Sagamoyo. Anamfuta Kingi kazi kwa kutomtii apige watu risasi.
Dhamira ya mwandishi.
Mwandishi anadhamiria kuonyesha uongozi mbaya na athari zake hasa katika mataifa yanayoendea.Viongozi hutumia mbinu mbalimbali kuongoza zinazowanyanyasa wananchi huku wakijinufaisha wenyewe bila kujali.
Kuonyesha kuwa ili kijenga jamii mpya, mapinduzi ni muhimu na ni sharti wananchi wajitolee kwa uzalendo ili kupigania haki zao na usawa na kupinga viongozi wasiofaa.
Mwandishi anaonyesha kuwa licha ya changamoto zinazomkumba mwanamke katika jamii, mwanamke ana nafasi muhimu katika uongozi na kuleta maendeleo katika jamii.
Please download this document as PDF to read all it's contents.
Why PDF Download?
- You will have the content in your phone/computer to read anytime.
- Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
- Easily print the notes to hard copy.
Either
Click here to download the pdf version of "Jalada, Ufaafu wa Anwani na Dhamira ya Mwandishi - Tamthilia ya Kigogo", and read the full contents of this pageOR
OR
This is the most affordable option. You get all topics/full set papers at a lesser price than if you bought per paper/ per topic.
Click here to download the full document with all topicsOR
