Sauti za Kiswahili - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes

Share via Whatsapp


Utangulizi

  • Kuna makundi mawili ya sauti za kiswahili:
    • Irabu (Vokali);
    • Konsonanti; 


Irabu (Vokali)

a, e, i, o, u

  • Sauti ambazo hutamkwa kwa ulaini bila hewa kuzuiliwa katika ala za sauti.

Matamshi/Uainishaji wa Irabu

ulimi irabu

  • a ni ya katikati na chini kinywani na midomo ikiwa imeviringa.
  • e ni ya mbele na kati kinywani na midomo ikiwa imetandazwa.
  • i ni ya mbele na juu kinywani na midomo ikiwa imetandazwa.
  • o ni ya nyuma na kati kinywani na midomo ikiwa imeviringa.
  • u ni ya nyuma na juu kinywani na midomo ikiwa imeviringa.


Konsonanti

b, ch, d, f, g, h, j, k, l, m, n, p, r, s, t, v,w, y, z

  • Sauti ambazo wakati wa kutamkwa hewa huzuiliwa katika ala za sauti.
  • Kuna aina mbili kuu za sauti za konsonanti:
    1. Sauti Ghunakonsonanti hizi zinapotamkwa, hewa hutikisa nyuzi za sauti
    2. Sauti Sighunakonsonanti hizi zinapotamkwa, hewa haitikisi nyuzi za sauti

Aina za Ala za Sauti

Ala Tuli

  • Ambazo hazisogei mtu akitamka k.m. meno, ufizi, kaa kaa gumu, kaa kaa laini na koo/koromeo.

Ala sogezi

  • Ambazo husogea mtu akitamka k.m. midomo na ulimi.

Matamshi/Uainishaji wa Konsonanti

  • Huainishwa kulingana na inapotamkiwa, kuwepo au kutokuwepo kwa mtetemeko katika nyuzi za sauti na jinsi hewa inavyozuiliwa katika ala k.m. /p/ ni ya midomo, kipasuo na sighuna
  Midomo  Midomo+ Meno  Meno+Ulimi  Ufizi  Kaakaa+ufizi  Kaakaa gumu  Kaakaa laini  Koo Aina ya sauti
Vipasuo    p      t    j  k    sighuna
 d      d      g    ghuna
Vikwamizo/Vikwaruzo      f  th  s    sh  gh h  Sighuna
   v  dh  z          ghuna
 Kipasuo - Kwamizo          ch        sighuna
 Nazali/Ving'ong'o  m      n    ny  ng'    ghuna
 Kitambaza        l          ghuna
 Kimadende       r          ghuna
 Viyeyusho/Nusu Irabu            y  w    ghuna

Vipasuo

  • Konsonanti ambazo wakati wa kutamkwa hewa husukumwa, huzuiliwa kabisa na kuachiliwa kwa ghafla na mpasuko mdogo kutokea.

Vikwamizo/Vikwaruzo

  • Konsonanti ambazo wakati wa kutamkwa hewa hupitishwa katikati ya ala kwa kukwamizwa.

Kipasuo kwamizo/kwaruzo

  • Konsonanti ambayo wakati wa kutamkwa hewa husukumwa nje kwa nguvu, huzuiliwa kabisa halafu mwanya mdogo huachwa hewa ipite kwa kukwamizwa.

Nazali/Ving’ong’o

  • Konsonanti ambazo wakati wa kutamkwa kuna kiasi cha hewa huachiliwa na kupitia puani

Kitambaza

  • Konsonanti ambayo wakati wa kutamkwa hewa husukumwa kwa nguvu, kuzuiliwa na kuachiliwa ipite kando ya ulimi

Kimadende

  • Konsonanti ambayo wakati wa kutamkwa hewa husukumwa, kuzuiliwa na kuachiliwa na kusababisha ncha ya ulimi kupigapiga ufizi mfululizo.

Nusu irabu/Viyeyusho

  • Konsonanti ambazo wakati wa kutamkwa hewa hupitishwa katikati ya ala kwa ulaini kama katika utamkaji wa irabu
Join our whatsapp group for latest updates

Download Sauti za Kiswahili - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Read 9580 times Last modified on Wednesday, 11 November 2020 09:36
Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest