Viambishi - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes

Share via Whatsapp


Utangulizi

  • Kiambishi ni silabi inayofungamanishwa na mzizi wa neno ili kuleta maana iliyokusudiwa. Viambishi havina maana kamilifu peke yake: huhitaji kufungamanishwa na mzizi wa neno. Kwa hivyo, kiambishi ni mofimu tegemezi inayoongeza maana fulani katika neno kama vile ngeli, wakati, hali, mnyambuliko wa kitendo n.k


Aina za Viambishi

  • Kuna aina mbili kuu za viambishi:
    1. Viambishi Awali
    2. Viambishi Tamati

Viambishi Awali

  • Viambishi hivi hutokea kabla ya mzizi ya neno/shina la kitenzi. Kuna aina kadhaa za viambishi hivi kama vile viambishi viwakilishi vya nafsi, ngeli, mahali, wakati, hali n.k

Viambishi Viwakilishi vya Ngeli

  • Hizi ni silabi zinazowakilisha ngeli katika neno. Mfumo wa ngeli unaokubalika hutumia viambishi hivi kubainisha ngeli mbali mbali.
    k.m:

    a-me-avy-a => kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya A-WA(umoja)
    zi-ta-pasuk-a => kiambishi kiwakilishi cha ngeli I-ZI wingi
    ki-li-pote-a => kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya KI-VI(umoja)
    ya-na-angaz-iw-a => kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya LI-YA(wingi)

Viambishi Viwakilishi vya Nafsi

  • Hivi ni viambishi ambavyo huonyesha nafsi katika neno. Kuna aina mbili za viambishi viwakilishi vya nafsi:
    1. Viambishi Viwakilishi vya Nafsi ya Mtendaji/Mtenda
      - Hutumika kuonyesha aliyefanya kitendo katika neno.
      - Kama viambishi vya Ngeli ya Mtendaji, v
      iambishi hivi ndivyo vinavyotangulia viambishi vingine katika kitenzi.
      NAFSI UMOJA  WINGI  MFANO
      YA KWANZA  NI TU ni-na-andik-a, tu-li-shind-a
      YA PILI U M u-me-kasir-ik-a, m-na-pig-w-a
      YA TATU A WA a-li-simam-a, wa-ta-p-ew-a

    2. Viambishi Viwakilishi vya Nafsi ya Mtendewa/Mtendwa
      - Hutumika kuonyesha nafsi ya aliyeathirika na kitendo katika neno. Kama viambishi viwakilishi vya ngeli ya mtendewa, mara nyingi viambishi hivi huwekwa punde kabla ya shina la kitenzi.
      - Viambishi viwakilishi vya mtendewa ni sawa na viambishi viwakilishi vya mtendaji isipokuwa:
      NAFSI YA MTENDEWA  KIAMBISHI  MFANO
      YA PILI UMOJA KU zi-me-ku-fik-i-a
      YA PILI WINGI M, MU, WA  ni-na-wa-tum-a
      YA TATU UMOJA M ni-ta-m-tambu-a

Viambishi Viwakilishi vya Wakati/ Hali

  • Hivi ni viambishi ambavyo vinapowekwa kabla ya shina la kitenzi, vinatufahamisha wakati kitendo hicho kilipofanyika.
  • Viambishi hivi ni:
    KIAMBISHI  HUWAKILISHA: MFANO
    LI wakati uliopita ki-li-chom-ek-a
    ME wakati timilifu (uliopita muda mfupi)  zi-me-anguk-a
    NA wakati uliopo tu-na-ku-subir-i
    TA wakati ujao wa-ta-ni-ju-lish-a
    HU wakati wa mazoea hu-som-e-a
    A wakati usiodhihirika a-tu-pend-a
    KA wakati usiodhihirika zi-ka-teket-e-a
    PO PO ya wakati a-li-po-wasil-i
    KI KI ya masharti ni-ki-zi-angali-a

Viambishi Viwakilishi vya Kukanusha Wakati

  • Viambishi hivi hutumika kukanusha kitenzi katika sentensi kulingana na wakati au hali
    KIAMBISHI HUKANUSHA MFANO
    KU wakati uliopita ha-ku-ingi-a
    JA wakati timilifu (uliopita muda mfupi)  si-ja-ku-uliz-i-a
    -I* wakati uliopo na wa mazoea ha-som-i
    TA wakati ujao ha-ki-ta-maliz-ik-a
  • Tanbihi: * Tunapokanusha wakati uliopo, wakati wa mazoea na wakati usiodhihirika, tunatumia kiambishi kiishio(I) badala ya kutumia kiambishi tamati.
    k.m:si-ku-ju-i, ha-pat-ik-an-i

Viambishi Viwakilishi vya Kukanusha Nafsi

  • Tunapokanusha kitenzi, kiambishi cha kwanzwa hubadilika kulingana na nafsi.
    KIAMBISHI  MATUMIZI MFANO
    SI nafsi ya kwanza  si-ku-wa-on-a
    HU nafsi ya pili hu-ni-faham-u
    HA nafsi ya tatu ha-ta-chuku-a


Viambishi Virejeshi vya Ngeli

  • Hurejelea ngeli ya mtendewa au mtendwa na hutumika hasa katika vishazi tegemezi (vyenye o - rejeshi) k.m:
    • wa-li-cho-ni-tum-i-a => kiambishi kirejeshi cha ngeli ya KI-VI
    • ni-ta-ka-ye-m-salim-i-a => kiambishi kirejeshi cha ngeli ya A-WA
    • u-li-ko-ji-fich-a => kiambishi kirejeshi cha ngeli ya mahali KU
    • tu-li-po-pa-safish-a => kiambishi kirejeshi cha ngeli ya mahali PO

Viambishi vya ngeli

  • Ni viambishi vile ambavyo husimamia ngeli katika kitenzi ili kuonyesha mtenda au mtendwa.
    k.m: (vitabu) vilivyonunuliwa
    (vi-li-vyo-nunul-il-w-a)  => vi- na -vyo- ni viambishi vya ngeli.

Viambishi Tamati

  • Viambishi tama hutokea baada ya shina la kitenzi na hutumika kutuarifu kauli au myambuliko wa kitenzi hicho.

Viishio

  • Katika kauli ya kutenda, vitenzi vyenye asili ya Kibantu huishia kwa sauti "-a". Kwa mfano: a-na-omb-a, tu-li-zo-andik-a

    Tanbihi: Tunapokanusha vitenzi hivi vyenye asili ya Kibantu katika wakati uliopo na wakati wa mazoea, kiishio "-a" hubadilika na kuwa "-i" Kwa mfano: Ha-pat-ik-an-i, Si-ku-ju-i
  • Vitenzi vyenye asili ya kigeni huchukua viishio tofauti kama vile e, i na u katika kauli ya kutenda. Kwa mfano: ha-wa-ja-tu-jib-u, a-na-tu-subir-i, ni-me-ku-sameh-e
  • Hata hivyo katika kauli nyinginezo (isipokuwa kauli ya kutenda) vitenzi hivi vya kigeni huchukua kiishio "a". k.m harib-ik-a, tu-me-jib-iw-a

Viambishi Viwakilishi vya Kauli ya Kitenzi

  • Hubadilika kulingana na mnyambuliko wa kitenzi.
    KAULI KIAMBISHI MFANO
    KUTENDEA e, i omb-e-a, pig-i-a,
    KUTENDEANA  ean, ian omb-ean-a, pig-ian-a,
    KUTENDWA w som-w-a
    KUTENDEWA ew, iw omb-ew-a, pig-iw-a
    KUTENDEKA ek pend-ek-a
    KUTENDESHA  esh, ez, ish, iz  kom-esh-a, ing-iz-a
    KUTENDANA an finy-an-a


Uainishaji wa Neno

  • Kuainisha ni kugawa neno katika viambishi vyake mbalimbali. Tunapoainisha neno, tunaonyesha mzizi wa neno pamoja na viambishi vyote vilivyofungamanishwa kuunda neno hilo.

 

Mifano:

Ainisha maneno yafuatayo:

  1. nitasoma → ni-ta-som-a

    ni → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya kwanza umoja
    ta → kiambishi kiwakilishi cha waka= ujao
    som → shina la kitenzi cha kusoma
    a → kiishio

  2. walipozipata → wa-li-po-zi-pat-a

    wa → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili wingi
    li → kiambishi kiwakilishi cha waka= uliopita
    po → kiambishi kiwakilishi cha po ya wakati au cha ngeli ya mahali PO
    zi → kiambishi kiwakilishi cha kitendwa, ngeli ya I-ZI wingi
    pat → shina la kitenzi cha kupata
    a → kiishio

  3. vimeshikamana → vi-me-shik-aman-a

    vi → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya KI-VI wingi
    me → kiambishi kiwakilishi cha waka= uliopita muda mfupi
    shik → shina la kitenzi cha kupata
    aman→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendamana
    a → kiishio

  4. mnayemkimbilia → m-na-ye-m-kimbi-li-a

    m → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili wingi
    na → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopo
    ye → kiambishi kirejeshi cha nafsi ya tatu
    m→ kiambishi kiwakilishi cha mtendewa, nafsi ya tatu umoja
    kimbi → mzizi wa kitenzi cha kukimbia
    li → kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendea
    a → kiishio

  5. yakimwagika → ya-ki-mwag-ik-a

    ya → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya YA-YA
    ki → kiambishi kiwakilishi cha KI-ya masharti au au cha KI-ya kuendelea
    mwag → mzizi wa neno mwaga
    ik→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendeka
    a → kiishio
  6. hawakukushibisha → ha-wa-ku-ku-shib-ish-a

    ha → kiambishi kiwakilishi cha kukanusha
    wa → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya tatu wingi
    ku → kiambishi kiwakilishi cha kukanusha waka= uliopita
    ku → kiambishi kiwakilishi cha nafsi ya pili mtendewa
    shib → mzizi wa kitenzi cha kushiba
    ish→ kiambishi kiwakilishi cha kauli ya kutendesha
    a → kiishio

  7. lililolililia → li-li-lo-li-li-li-a

    li → kiambishi kiwakilishi cha ngeli ya LI-YA umoja
    li → kiambishi kiwakilishi cha wakati uliopita
    lo → kiambishi kirejeshi cha ngeli ya LI-YA umoja
    li→ kiambishi kiwakilishi cha mtendewa, ngeli ya LI-YA
    li → shina la kitenzi cha kulia
    li → kiambishi kiishio cha kauli ya kutendea
    a → kiishio
Join our whatsapp group for latest updates

Download Viambishi - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest