Ukubwa na Udogo
- Maneno huwekwa katika ukubwa au udogo yanapozidi kiasi cha wastani kinachotarajiwa. Hali ya ukubwa na udogo hutumika hasa unaposifia au kudharau kitu
Ukubwa
- Nomino zote katika hali ya ukubwa huwa katika ngeli ya LI-YA. Tunaweka maneno katika ukubwa kwa kuongeza kiungo JI na/au kutoa kiwakilishi cha ngeli
Udogo
- Maneno huwekwa katika udogo ili kusifia udogo wao au kudharau kiasi chake. Nomino zote katika hali ya udogo huwa katika ngeli ya KI-VI. Maneno huwekwa katika udogo kwa kuongeza kiungo ki- au kiji-.
- Katika baadhi ya maneno, kiambishi kiwakilishi cha ngeli huachwa nje tunapoweka maneno katika udogo.
Wastani
- Hii ni hali ya kawaida/katikati ya nomino. Si kubwa si ndogo.
WASTANI | UDOGO | UKUBWA | |
1. | mtu | kijitu | jitu |
2. | mto | kijito | jito |
3. | kitu | kijikitu | jikitu |
4. | mtoto | kitoto/kijitoto | toto/jitoto |
5. | mlango | kijilango | lango |
6. | mwiko | kijimwiko/kijiko | jimwiko |
7. | chungu | kijichungu | jungu |
8. | nyumba | chumba/kijumba | jumba |
9. | kikapu | kijikapu | kapu/jikapu |
10. | miji | kijiji | jiji |
Umoja na Wingi
- Sentensi za Kiswahili zinaweza kubadilishwa kutoka kwa umoja hadi wingi, kulingana na ngeli yake.
- Baadhi ya ngeli hubaki sawia katika umoja na wingi.
Mifano ifuatayo itakuonyesha umoja na wingi wa sentensi katika ngeli mbalimbali.
Ngeli ya A-WA | ||
1. | Mtoto huyu ni mvivu sana. | Watoto hawa ni wavuvi sana. |
2. | Mwizi aliyeiba ng'ombe wa mzee mkongwe amekamatwa na mwananchi. | Wezi walioiba ng'ombe wa wazee wakongwe wamekamatwa na wananchi |
Ngeli ya KI-VI | ||
1. | Kitabu chako kiko juu ya kitanda | Vitabu vyenu viko juu ya vitanda |
2. | Chumba kile kidogo kimeangukia chungu | Vyumba vile vidogo vimeangukia vyungu. |
Ngeli ya LI-YA | ||
1. | Jani lile linaficha tunda kubwa ambalo limeiva | Majani yale yanaficha matunda makubwa ambayo yameiva. |
2. | Jiko lolote lenye kaa moto litolewe nje | Meko yoyote yenye makaa moto yatolewe nje. |
Ngeli ya U-I | ||
1. | Mtaa huo hauna mti wowote | Mitaa hiyo haina miti yoyote. |
2. | Huu ndio mto uletao maji katika mji wetu | Hii ndiyo mito iletayo maji katika mito yetu. |
Ngeli ya U-ZI | ||
1. | Ukuta mwingine umepigwa kwa upembe | Kuta nyingine zimevunjwa kwa pembe. |
2. | Ubao mrefu uliokuwa kwenye ua wetu ulikatwa kwa upanga mweusi | Ndefu ndefu zilizokuwa kwenye nyua zetu zilikatwa kwa panga nyeusi. |
Ngeli ya I-ZI | ||
1. | Nyumba iliyo karibu na barabara ile imefungwa | Nyumba zilizo karibu na barabara zile zimefungwa. |
2. | Ndoo yenye maji imewekwa juu ya mbao kubwa | Ndoo zenye maji zimewekwa juu ya mbao kubwa. |
Ngeli ya U-YA | ||
1. | Uyoga uliokuwa hapa umeoza. | Mayoga yaliyokuwa hapa yameoza. |
2. | Mhindi wa kuchoma umeibiwa. | Mahindi ya kuchoma yameibiwa. |
Ngeli ya YA-YA | ||
1. | Mafuta na maji hayawezi kuchanganyika | Mafuta na maji hayawezi kuchanganyika. |
2. | Marashi haya yananukia vizuri | Marashi haya yananaukia vizuri |
Ngeli ya I-I | ||
1. | Sukari imemwagika kwenye changarawe hii. | Sukari imemwagika kwenye changarawe hii. |
2. | Damu ni nzito kuliko maji | Damu ni nzito kuliko maji. |
Ngeli ya U-U | ||
1. | Uji uliopikwa kwa unga wa wimbi ni mtamu kuliko ule wa mtama. | Uji uliopikwa kwa unga wa wimbi ni mtamu kuliko ule wa mtama. |
2 | Ugali ni tamu lakini mboga haina chumvi. | Ugali ni tamu lakini mboga haina chumvi. |
Ngeli ya PA | ||
1. | Mahali ambapo palipandwa maua panapendeza sana | Mahali ambapo palipandwa maua panapendeza sana. |
Ngeli ya KU | ||
1. | Huku niliko hakuvutii kama kwangu | Huku tuliko hakuvutii kama kwetu |
2. | Kukimbia huku kunachosha. | Kukimbia huku kunachosha. |
Ngeli ya MU | ||
1 | Nyumbani humu mna giza totoro | Nyumbani humu mna giza totoro |
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Ukubwa na Udogo; Umoja na Wingi - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students