Maneno Maalum
Ila
- isipokuwa
- Watu wote ila yeye wameenda. - kasoro
- Hakuna kizuri kisicho na ila.
Labda (pengine/shaka)
- Haonekani siku hizi labda amepata uhamisho.
Ikiwa
- (kama/shaka)
- Tutamkuta nyumbani ikiwa amepewa likizo. - masharti
- Mgonjwa atapona ikiwa atakunywa dawa ipasavyo.
Walakini
- Dosari
- Ghorofa limebomolewa kwa sababu lilikuwa na walakini. - lakini/bali
- Nimekula walakini sijashiba.
Ingawa/ingawaje (hata kama)
- Nilijilaza kitandani ingawa sikuwa na usingizi.
Ijapokuwa/japo (hata kama)
- Usicheze na nyoka ijapokuwa ni mdogo.
Jinsi
- njia/utaratibu wa kufanyia jambo
- Sijui jinsi ugali unavyopikwa. - aina/namna/sampuli
- Siwezi kula chakula jinsi hii. - kulingana na/kama
- Alikuja jinsi alivyoniahidi.
Kwa
- Kuonyesha umiliki wa mahali
- Sheila amekwenda kwa Bi Mashaka.
- Kwa akina Kawia ni mbali kutoka Vikwazoni. - Kutolea sababu au nia na Kuulizia Sababu
- Umeadhibiwa kwa kukosa nidhamu.
- Kali amelala mapema kwa kuwa anaenda shule mapema kesho.
- Ni kwa nini binadamu hawamheshimu Mungu - Kuonyesha sehemu ya kitu kizima (akisami)
- Katika mtihani walioufanya, Jabu alipata kumi na tatu kwa ishirini (13/20).
- Sehemu ya nne kwa tano (4/5) ya ndizi hizi imeoza. - Kulinganisha
- Timu yao ilishindwa mabao mawili kwa sufuri.
- Rita na Anita wanafanana kama shilingi kwa ya pili - Kuonyesha muda uliochukuliwa na kitendo
- Tulimsubiri kwa masaa mawili kisha tukaondoka.
- Yeye huoga kwa muda mfupi sana. - Kuelezea Ala au kitumizi
- Alikuwa akilima kwa jembe kuukuu.
- Walikuja kwa basi. - Kuelezea Mbinu, Jinsi au Namna
- Kaombi alipata pesa kwa kuandaa harambee.
- Mgonjwa aliongea kwa uchungu mwingi sana - Hutumika katika misemo
- Kesha na Nuru waliketi sako kwa bako.
- Mshindi alibebwa juu kwa juu
na
- kiunganishi
- Mama na baba wanalima. - umilikaji
- Kamau ana kitabu kizuri. - wakati uliopo
- Anaandika barua. - kauli/mnyambuliko
- Kamau na Juma wanapigana. - kuonyesha tofauti
- Kiatu hiki ni tofauti na kile. - mtenzi
- Alipigwa na mwalimu. - kuonyesha ufupisho wa nafsi
- Alisaidiwa nao.
Wala (kukanusha)
- Sikumtusi wala kumpiga.
Viambishi Maalum
- Tutaangazia viambishi au maneno ya silabi moja yanayotumika sana kwa Kiswahili kuwakilisha dhana mbalimbali. Viambishi hivi huitwa viambishi maalum.
Matumizi ya KI
- Kiambishi Kiwakilishi cha ngeli ya KI-VI
- Kiatu kilichochomeka kilikuwa kimeharibika.
- Kisiwa hiki kilichohamwa hakikaliki.
- KI ya Masharti
- Ukitaka kufua dafu, lazima utie bidii.
- Ukicheka sana utavunjika mbavu.
- Nitazichukua zikianguka.
- KI ya Mfanano - Kulinganisha(Vivumishi na vielezi vya Ki-Mfanano)
- Watu wa Mizukani wanaabudu kishetani.
- Amevalia mavazi ya kifalme.
- Msichana huyo huongea kimalaika.
- KI ya Udogo
- Kijiji chao ni mahame.
- Kitabu kile kimejifunga.
- Kuonyesha kinatendeka wakati mmoja na kitendo kingine
- Kesha alipobisha, Mganga Kuzimu alikuwa akila nzi.
- Tulimkuta akichoma mhindi.
- Mama alicheka mtoto akilia.
- Kukanusha kauli ya kutendeka
- Wasichana warembo huoleka - Wasichana warembo hawaoleki.
- Sauti nzuri zinasikika - Sauti nzuri hazisikiki.
- Kiambishi Kiwakilishi cha ngeli ya KI-VI
- Ukiona vyalea vyaundwa.
- Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni.
- Kutangulia majina ya lugha mbalimbali
- Ali Kiba huimba kwa Kiswahili.
- Kiingereza ndiyo lugha ya Wazungu kutoka Uingereza.
Matumizi ya KU
- Kiambishi Kiwakilishi cha Ngeli ya mahali KU-KU
- Shuleni hakuna usalama.
- Huku kumekauka sana.
- Kuanzisha vitenzi vya silabi moja au hali kamilifu ya kitendo.
- Ninataka kula.
- Walikuja jana asubuhi.
- Kuanzisha nomino za kitenzi jina.
- Kuchekacheka kwake kulimsaliti.
- Kuimba kwenu hakunipendezi.
- Kuanzisha vitenzi katika hali ya kawaida au kitenzi cha pili katika vitenzi sambamba.
- Kisu hutumika kukatia vitu.
- Wamekwenda kupiga ngoma.
- Kiambishi cha Kukanusha Wakati Uliopita
- Maji yako yalimwagika - Maji yako hayakumwagika.
- Niliingia kwenye chumba kile - Sikuingia kwenye chumba kile.
- Kiambishi kiwakilishi cha mtendwa/mtendewa nafsi ya pili.
- Watoto watakuchekelea ukivalia viatu vya manjano.
- Sijakueleza jinsi nilivyopambana na simba mwenye njaa.
Matumizi ya NI
- Kiambishi kiwakilishi cha Nafsi ya Kwanza umoja
- Nitakapokasirika watanitambua.
- Nitayainua macho yangu nitazame milima.
- Kiunganishi cha wakati uliopo kuonyesha hali au sifa ya kitu.
- Katosha ni msichana mpole sana.
- Tegemeo letu ni kufika Mbinguni.
- Kiambishi kiwakilishi cha kielezi cha mahali
- Nyuki wamefukuza wavulana uwanjani.
- Shimoni humu hamna nuru.
- Kukanusha kauli ya kutendana, kutendeana
- Maji na mafuta hayatoshani uzani.
- Giza na nuru hazishirikiani.
- Kiishio katika hali ya kuagiza, kuamuru au kuhimiza nafsi ya pili wingi
- Wahubirini watu wote.
- Ondokeni enyi msioijua njia.
- Pokeeni baraka tele.
- Kiambishi kiwakilishi cha vivumishi viulizi - nini na kwa nini
- Pilipili usiyoila ya kuwashiani?
- Mama amenipigia simu mara sita leo, sijui ananitakiani.
Matumizi ya KA
- Kiambishi kiwakilishi cha Wakati Usiodhihirika
- Mama akamtuma mwanawe aende kuchota maji.
- Nikamwuliza anionyeshe sanduku lake.
- Katika vitenzi sambamba - kitendo kimoja kinapofanyika baada ya kingine
- Alikula akashiba kisha akalala.
- Tulifika nyumbani, baba akatuuliza tumewaacha wapi fahali.
- Kuagiza au Kuamuru
- 'Kalaleni!' Mama akawaamuru watoto.
- Kamwambie asirudi hapa tena.
- Kiishio cha kauli ya kutendeka
- Kijana mtundu alipigwa akapigika.
- Tulijaribu kufungua mlango lakini haukufunguka.
Matumizi ya PO
- PO ya Mahali
- Mahali alipoanguka paliacha kuota nyasi.
- Hapo ndipo tulipoketi. Jumapili ifikapo tutakwenda Kisetoni.
- PO ya Wakati
- Nilipomlilia aliisikia sauti ya dua langu.
- Kitumbua kilipikwa mayai yalipoletwa.
- Zitakaporudishwa tutazificha mbali.
- PO ya Hisia(Hasira)
- Umenikosea sana! Po! Utakiona cha mtema kuni.
Matumizi ya JI
- Kuunda nomino kutokana na kitenzi.
- sema - msemaji.
- kimbia - mkimbiaji
- Kuonyesha Ukubwa
- Jikapu lile lina jitunda kubwa.
- Jito lile limemeza watu wengi.
- Kuonyesha mtendaji anapokuwa mtendewa (kujitenda, kujitendea)
- Amejikwaa kidole cha kati.
- Kitabu kimejifungua chenyewe
Matumizi ya a
- Hali isiyodhihirika ya wakati uliopo
- Watoto wacheza uwanjani. - vichwa vya habari
- Waziri aaibishwa na wananchi. - kitendo kinaendelea
Twaenda sokoni. - nafsi ya tatu umoja
- Yeye aliudhika sana. - ngeli
- Mbuzi yule atachinjwa kesho. - kiishio
- Mtoto amekula vizuri
Matumizi ya Nge
- Nge hutumika kuonyesha kwamba kitendo fulani hakijafanyika na kwa hivyo jambo fulani halijatokea lakini kuna uwezekano wa kufanya kitendo hicho na jambo hilo litokee.
k.m
- Ningekuwa na pesa ningenunua simu - Sina pesa wala sikununua simu, lakini nikipata pesa saa hii, ninaweza kununua simu
- Ningejua nyumbani mwake ningemtembelea - Sijui nyumbani kwao wala sijamtembelea, lakini nikijua nitamtembelea.
Matumizi ya Ngali (au Ngeli)
- Ngali hutumika kuonyesha kwamba kitendo fulani hakijafanyika na kwa hivyo jambo fulani halijatokea wala hakuna uwezekano wa kufanya kitendo hicho. Hutumika hasa kuonyesha majuto.
k.m
- Ningalifika mapema ningalimpata kabla aondoke - Sikufika mapema, hivyo basi sikumpata, wala siwezi kumpata kwa sababu nishachelewa naye ashaondoka
- Ungalimsikiza mwalimu, ungalipita mtihani - Hukumsikiza mwalimu na hivyo basi hukupita mtihani, wala hakuna uwezekano wa kumsikiza wala kupita mtihani.
Matumizi ya ndi- (kitenzi kishirikishi kipungufu)
- Yeye ndiye aliniibia pesa
Download Matumizi ya Maneno na Viambishi Maalum - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students