Watch Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34

Alama za Uakifishaji - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - Matumizi ya Maneno na Viambishi Maalum - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes Mnyambuliko wa Vitenzi - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes - Next »
Download PDF for future reference Install our android app for easier access
  • Utangulizi
  • Alama ya Kikomo au Kituo Kikuu
  • Alama ya Kituo, Kipumuo au Koma
  • Alama ya Dukuduku
  • Alama ya Kinukuu
  • Alama ya Kiulizi
  • Alama ya Hisi
  • Alama ya Nukta-Mbili au Koloni 
  • Alama ya Nukta-Kituo au Semi Koloni
  • Alama ya Kistari Kifupi
  • Alama ya Kistari Kirefu 
  • Alama ya Mabano au Parandesi
  • Alama ya Kinyota
  • Alama ya Mlazo
  • Alama ya HERUFI KUBWA

Utangulizi

  • Kunazo alama kadhaa zinazotumika kuakifisha maneno na sentensi za Kiswahili.

Alama ya Kikomo au Kituo Kikuu (.)

  1. Kuonyesha mwisho wa sentensi.
    1. Huu ndio mwisho wa sentensi hii.
    2. Kioo kimevunjika
  2. Katika kufupisha maneno
    1. U.N, K.B.C, Y.C.S, N.Y.S
    2. Dkt. Maktaba, Bw. Msumari
  3. Kuonyesha Saa 
    1. Misa ilianza saa 4.30 za asubuhi.
    2. Hivi sasa ni saa 10.20.
  4. Katika hesabu kuonyesha sehemu isiyo nzima
    1. Ukigawa tatu mara mbili, utapata 1.5
    2. Mtoto huyo ana uzani wa kilo 8.27
  5. Kuonyesha senti katika pesa
    1. Bei yake ni shilingi 12.50.
    2. Karo ya shule mwaka huu ni 80,000.00

Alama ya Kituo, Kipumuo au Koma (,)

  1. Kuorodhesha vitu zaidi ya mbili
    1. Nimenunua simu, saa, redio na viatu.
    2. Kina mama waliimba, wakapiga ngoma na kunengua viuno vyao.
  2. Kugawanya mawazo katika sentensi.
    1. Baada ya sala za jioni, Mzee Makosa alitoka nje na kuwasha sigara yake.
    2. Nilipomwuliza kama alimjua binti yule, aliniangalia tu na kucheka
    3. Ingawa kitabu hiki ni kizito, sina budi kukibeba.
  3. Kutoa maelezo zaidi.
    1. Shabiba, mmojawapo ya wanawake wajawazito, amejifungua mtoto wa kike.
    2. Shati hili, ingawa nalichukia, nitalivalia tu.
  4. Katika tarakimu, kugawa elfu.
    1. Shilingi 209, 408, 000 ziliporwa na serikali.
    2. Dawa hiyo iliua takribani mbu 61, 247.

Alama ya Dukuduku (…)

  1. Hutumika kuonyesha kuwa maneno yameachwa ya kutangulia, kati au ya mwisho. Yaweza kuachwa kwa kuwa makali
    - Nyani haoni…
  2. kukatizwa usemi/kauli
    AMINA: Mama ni…
    MAMA: Kwanza watoka wapi usiku huu?
  3. maneno yanaendelea
    - Alimwambia ajihadhari anapovuka barabara…

Alama ya Kinukuu (' na ")

  1. Kunukuu usemi halisi
    1. "Ukitaka kufua dafu," mama akamwambia mwanawe, "lazima utie bidii."
    2. Alimtazama kisha akamwuliza, "Unadhani nimechanganyikiwa kama wewe?"
  2. Kunukuu kichwa cha kazi ya sanaa k.v kitabu, wimbo, kipindi n.k
    1. Saumu na Neema ni wahusika katika riwaya "Hamu ya Sumu Tamu".
    2. Rose Muhando ndiye aliyeimba "Mteule Uwe Macho".
  3. Kuonyesha maneno yasiyo ya Kiswahili unapochanganya ndimi katika sentensi
    1. Huyu ndiye mchezaji "number one"
    2. Amesema "keyboard" ya "computer" yake haifanyi kazi..
  4. Kuonyesha maneno yanayowakilisha maana tofauti na maana yake ya kawaida au kinaya.
    1. Lesi alipoenda kwenye 'maktaba' alipata mimba.
    2. Rais wetu 'mtukufu' amewatisha mawaziri wake.
    3. Moto ulioteketeza shule hiyo ulitokana na kusudi la wanafunzi la 'kumshtua' mwalimu wao.
  5. Kuonyesha herufi iliyoachwa nje au kufupisha maneno katika ushairi hasa kwa kusudi la kutosheleza idadi ya mizani
    1. 'takufuata popote wendapo,
    2. 'liapo ya mgambo, lazima kuna jambo
  6. Katika maendelezo ya sauti ya ung'on'g'o (ng')
    1. Ng'ombe wa Ng'ang'a wanang'ang'ania nini?
    2. King'ang'i anapenda kunung'unika ovyo ovyo.

Alama ya Kiulizi (?)

  1. Kuulizia swali
    1. Je, utamtembelea lini?
    2. Ariana anaishi wapi?
  2. Kuonyesha pengo lililoachwa wazi
    1. Ndama ni mwana wa ng'ombe ilhali ___?___ ni mtoto wa mbuzi.
    2. __?__ mpokee mke wako, __?__, siku ya leo umepata jiko.

Alama ya Hisi (!)

  1. Kuonyesha hisia kama vile hasira, mshangao, furaha n.k
    1. Lo! Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni.
    2. Pepo nyeusi! Shindwa! Chomeka! Kwenda kuzimu!
  2. Kuigiza Tanakali za Sauti
    1. Amejikwaa sasa ameanguka pu!
    2. Moyo ulidunda ndu! ndu!

Alama ya Nukta-Mbili au Koloni (:)

  1. Kutanguliza orodha
    1. Harusi hiyo ilihudhuriwa na watu wa wengi: wake kwa waume; wadogo kwa wakubwa; wazee kwa vijana.
    2. Kuna aina kadhaa za vivumishi: vivumishi vya sifa, vivumishi vya idadi, vivumishi viwakilishi na kadhalika
  2. Kuelezea sababu au kuonyesha matokeo ya kitu.
    1. Saumu a lipoingia chumbani alipigwa na butwaa: mamake alikuwa amekufa.
    2. Baba alinipatia zawadi nzuri sana: nilirukaruka kwa furaha.
  3. Kuonyesha saa
    1. Wimbo huo unachukua dakika 4:45.
    2. Aliingia saa 5:1 5
  4. Kunukuu ukurasa wa Bibilia
    1. Padre alisoma Luka 2:1-6
    2. Katika kitabu cha Mwanzo 5: 2-7, Bibilia inasema...
  5. Kuonyesha maneno ya msemaji katika tamthilia au mchezo wa kuigiza
    1. Mzee Mwanyati: Unafikiria mimi ni nyanyako?
    2. Kadogo: (akitetemeka) Tafadhali naomba unisamehe.
  6. Kuonyesha mada katika barua au kumbukumbu za mkutano
    1. KUH: Ombi Lako la Kujiuzulu.
    2. RE: Barua ya tarehe 3/2/1 999.
  7. Katika kumbukumbu za mkutano
    1. KUM: 2/321 /2000 Mbinu Mpya za Kunyamazisha Raia
    2. Ajenda 2: Kusomwa kwa kumbukumbu za mkutano uliotangulia

Alama ya Nukta-Kituo au Semi Koloni (;)

  1. Kuorodhesha vitu hasa vinapokuwa na zaidi ya neno moja
    1. Harusi hiyo ilihudhuriwa na watu wa wengi: wake kwa waume; wadogo kwa wakubwa; wazee kwa vijana.
    2. Wakati wa likizo tulitembelea sehemu kadhaa: Mombasa, Kenya; Dodoma, Tanzania; Kampala, Uganda na tukamalizia hapa Nairobi, Kenya.
  2. Kuunganisha vishazi huru viwili au kuonyesha mawazo mawili.
    1. Tuliwasili darasani tukiwa tumechelewa; mwalimu alitukaribisha kwa kiboko.
    2. Usiwe na wasiwasi; nitakuwa pamoja nawe siku zote.

Alama ya Kistari Kifupi (-)

  1. Kuunganisha maneno mawili
    1. Mbwa-koko aliuma mwana-haramu.
    2. Nawatuma kama wana-kondoo miongoni mwa mbwamwitu.
  2.  Kuonyesha hadi, au mpaka
    1. Bei imepanda kutoka shilingi 20 - 30
    2. Tutasoma kitabu cha Matendo 2: 3 - 7
  3. Kama alama ya kupunguza au kutoa katika Hesabu
    1. 9 - 7 = 2
    2. 4 - 5 = -1
  4. Kuonyesha neno ambalo halijakamilika litaendelezwa katika msitari ufuatao
    1. Ukitaka twende kwetu nyumbani nitakupeleka ukamwone mamangu.
    2. Kuna migumo kumi na mitatu katika Bustani la Kuzimu.
  5. Kuonyesha tarehe
    1. Watu wengi walikufa tarehe 07-08-1 998.
    2. Marehemu alikufa tarehe 06-06-2006

Alama ya Kistari Kirefu (‒)

  1. Kutoa maelezo zaidi
    1. Nilipokutana na Zakido ‒ ambaye aliripotiwa kupotea miaka miwili iliyopita ‒ nilimsalimia lakini hakunitambua.
    2. Hatimaye nimeshinda ‒ baada ya kujaribu kwa masaa matatu.
  2. Kuorodhesha hoja au vitu
    1. Umuhumu wa fasihi simulizi:
      ‒ kuburudisha
      ‒ kuelimisha
      ‒ kuunganisha jamii

Alama ya Mabano au Parandesi ()

  1. Kutoa maelezo zaidi
    1. Z. Anto (aliyeimba Binti Kiziwi) ametoa wimbo mpya.
    2. Shangazi yangu (ambaye ni naibu wa waziri) amenitumia zawadi.
  2. Kutoa neno jingine lenye maana sawa
    1. Dhamira (nia) ya mshairi huyu ni kutushauri tusikimbilie maisha.
    2. Mabanati (wasichana) hao hutembea uchi jijini usiku wa manane.

Alama ya Kinyota (*)

  1. Kuonyesha neno ambalo litaelezewa zaidi chini ya ukurasa(foot note)
    1. Alipopata nafasi ya kuingia shule ya upili ya Starehe*, mwanafunzi huyo alijawa na furaha tele.
                                                                                                        
      *Starehe ni mojawapo ya shule zinazofanya vizuri zaidi barani Afrika.
  2. Kuficha herufi/silabi katika neno ili kupunguza ukali wa maneno yasiyo na nidhamu.
    1. Ra is aliwaita wananchi m**i ya kuku.
    2. Aidha, alisema kwamba nyote ni wapu***vu.

Alama ya Mlazo (/)

  1. Kuonyesha 'au'
    1. Mkutano huo utahutubiwa na Rais/Waziri Mkuu.
    2. Wazungumzaji wengi wa Kiswahili wanatoka Kenya/Tanzania.
  2. Kuonyesha neno au fungu la maneno lenye maana sawa.
    1. Sheila amepewa cheo cha katibu/mwandishi.
    2. Hawa ndio wanaotapatapa ovyo/wasio na mbele wala nyuma.
  3. Katika hesabu kuonyesha kugawanya au akisami.
    1. 5/7 ya siku za juma ni siku za kazi.
    2. 12/6 = 2
  4. Katika tarehe
    1. Shule zilifunguliwa tarehe 08/01 /201 2
    2. Kamati hiyo ilikubaliana kwamba, Mwokozi alizaliwa tarehe 25/12

Alama ya HERUFI KUBWA

  1. Kuanzisha sentensi'
    1. Fisi hula mizoga.
    2. Huu ndio mwanzo wa sentensi hii.
  2. Kuonyesha Nomino za Kipekee
    1. Bi Rangile anatoka Vikwazoni.
    2. Nchi ya Tanzania imebarikiwa na Mlima Kilimanjaro unaowavutia wageni kutoka Ulaya.
  3. Kuonyesha Kichwa au Mada
    1. ALAMA ZA UAKIFISHAJI
    2. UFAHAMU
    3. Njia Tano za Kuua Mbu
  4. Kuonyesha maneno yaliyofupishwa
    1. UKIMWI ni Ukosefu wa Kinga Mwilini.
    2. TUKI ni Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "Alama za Uakifishaji - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "Alama za Uakifishaji - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes" on Whatsapp

OR




Read 1391 times Last modified on Wednesday, 11 November 2020 12:23
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - Matumizi ya Maneno na Viambishi Maalum - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes Mnyambuliko wa Vitenzi - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes - Next »
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in Sarufi na Matumizi ya Lugha
Tagged under
  • kiswahili notes

Related items

  • Barua ya Kirafiki - Kiswahili Insha Notes
  • Utangulizi - Kiswahili Insha Notes
  • Vitate, Vitawe na Visawe - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
Sarufi na Matumizi ya Lugha