Watch Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34
  • Home
  • High School Notes
  • Kiswahili
  • Tumbo Lililoshiba na Hadithi Nyingine
  • SHOGAKE DADA ANA NDEVU - Alifa Chokocho - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA

Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - MAME BAKARI - Mohammed Khelef Ghassany - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba - Next »
Download PDF for future reference Install our android app for easier access

Click the button below to download the full Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA pdf document, with all the topics.

Download Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA PDF to Print or Offline Reading

CLICK HERE to get "Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA" on Whatsapp for offline reading/ printing.

Tumbo Lisiloshiba Dondoo Questions and Answers

Maswali haya hujitokeza kwa namna ya maneno yaliyodondolewa kutoka kwenye kazi ya Fasihi. Dondoo hunukuliwa kisha maswali yanayohusiana na dondoo hilo huulizwa. Dondoo laweza kuwa maneno ya mhusika mmoja ambaye hatatajwa au maelezo katika kazi. Maswali huenda yakarejelea matukio yaliyotokea kabla au baada ya dondoo. Katika kulijibu swali la muktadha wa dondoo, mtahiniwa huhitajika kuangazia mambo yafuatayo;

  1. Kumtaja msemaji wa maneno haya
  2. Kumtaja msemewa(anayerejelewa)
  3. Kueleza mahali yalikofanyika mazungumzo haya.
  4. Kueleza kiinisababu ya mazungumzo haya kutokea.

Swali la dondoo 1

“… Ningeondoka…..mapema niende niibe au niue ili niwe mtu wa maana”

  1. Eleza muktadha wa maneno haya.  (Alama 4)
  2. Onyesha vile Kinaya kinavyojitokeza katika dondoo hili  (Alama 2)
  3. Kinaya kimetumika kwingine katika hadithi husika. Thibitisha kwa kutumia hoja tisa. (Alama 9)
  4. Eleza umuhimu wa msemaji katika hadithi hii.   (alama.5)

Majibu ya dondoo 1

  1.  
    • Haya ni maneno ya Jairo.
    • Anahutubu katika sherehe ya kumuaga mwalimu Mosi ambaye alikuwa anastaafu kutoka kazi ya ualimu.
    • Sherehe hii ilifanyika shuleni.
    • Jairo anamkosoa mwalimu Mosi kumpatia atumaini ya uongo masomoni ilhali alijua hawakuwa na uwezo wa kimasomo badala ya kumruhusu aende ajaribu mbinu nyingine ya kujikimu kimaisha ili awe mtu wa maana katika jamii
  2. Jairo anamkosoa mwalimu kwa kumfunza na kumpa atumaini maishani badala ya kumwachilia mapema aende akaibe na kuua. Jairo analodokeza hapa ni kuwa ili mtu awe wa maana ni lazima aibe na aue.
  3.  
    • Ni kinaya kwa Jairo kudai ili mtu awe wa maana, athaminiwe na kuitwa mheshimiwa na kuwa bingwa lazima aibe, apore au aue.
    • Ni kinaya kwa Jairo kuuona uelekezi na ushauri wa mwalimu wake kama upotoshi na upotezaji wa muda. Jairo anadai alipotezewa muda kwa kupatiwa matumaini ya uongo.
    • Ni kinaya pia kwa mwalimu Mosi kutaka ahutubie mtu ambaye atamkosa badala  ya kumsifu.
    • Ni kinaya kwa Jairo kumtoa bintiye na mkewe kama zawadi kwa mwalimu wake kama shukrani ya zawadi anazompa. Ni kinaya kwa mtu kubadili mkewe kama zawadi.
    • Ni kinaya kwa Jairo kudai kuwa pombe ni kiiwazo cha kimawazo kinachomsahaulisha masibu ya maisha ya kumkosoa mwalimu wake kwa kumwonya dhidi ya matumizi ya pombe.
    • Ni kinaya kwa mkewe Jairo kukubali kitendo cha mumewe Jairo kumtoa kama zawadi kwa familia nyingine. Anakubali kubadilishwa na mali.
    • Ni kinaya kwa Jairo kudai kuwa afuska ndio raha ya maisha na kuwa uaadilifu haufai. Anadai kuwa maisha ni bora bila nasaha za mwalimu.
    • Ni kinaya kwa mkewe mwalimu Mosi,Sera kukubali na kumkaribisha mwanamke mwingine na watoto wake kwenye familia yake. (Hoja Zozote 9 Alama 9)
  4.  
    • Ni kielelezo cha utovu wa nidhamu miongoni wa wanafunzi. Anakunywa pombe na hata kujihusisha katika ufuska
    • Kupitia kwake uwajibikaji wa mwalimu Mosi unajitokeza. Kama mwalimu alimkanya kunywa pombe na hata ufuska
    • Ametumiwa kudhihirisha ukweli wa methali “asante ya punda ni mateke.”

Swali la dondoo 2

Shibe inatumaliza : Salma Omar Hamad

“Hiyo ni dharau ndugu yangu. Kwa nini kila siku tunakula sisi kwa niaba ya wengine ?”

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili.    (alama 4)
  2. Eleza sifa za msemaji.     (alama 6)
  3. Eleza jinsi viongozi wanavyokuwa wabadhirifu.   (alama 10)

Majibu ya dondoo 2

  1.  
    • Maneno haya yanasemwa na Mbura
    • alikuwa anazungumza na Sasa
    • walikuwa kwenye sherehe iliyoandaliwa na mzee Mambo
    • walikuwa wanazungumza kuhusu ‘kula kwao’      4 x 1 = 4
  2.  Sifa za Mbura
    • ni mzalendo - anafanya kazi kwa bidii katika wizara yake kama njia ya kuonyesha uzalendo
    • mwenye tamaa - anajaza sahani kwa chakula na kukila chote
    • mwenye utu - anataka wananchi wale kwa niaba ya viongozi kama vile wao wamekuwa wakila kwa niaba yao
    • ni fisadi - amepokea kazi kwa afisi ya serikali kwa njia isiyo halali
    • mzembe - baada ya kula sahani tatu za vyakula kwenye sherehe analala usingizi mzito badala ya kwenda kazini
    • mtetezi wa haki
    • mvumilivu
    • mpyoro
    • msema kweli   zozote 6 x 1 = 6
  3.  
    • hulipwa mishahara mikubwa sana na serikali jambo linalochangia ubadhirifu wa mali ya umma
    • sherehe kubwa za viongozi wa kiserikali huchangia pakubwa ubadhirifu
    • viongozi hutumia raslimali za nchi kwa manufaa yao ya kibinafsi
    • magari ya serikali
    • raslimali zilizotumiwa katika kuvinunua vyakula na vinywaji vingetumika katika kuendeleza asasi tofauti za kijamii
    • DJ na wenzake wanapata mabilioni ya fedha kutokana na kuwatumbuiza wageni katikasherehe kama hizi
    • viongozi wanawachukua baadhi ya watu wao wa karibu na kufanya juu chini kuona kwamba wanajifaidi na mali na raslimali za wananchi pasipo kuzitolea jasho kamwe
    • upeperushaji wa matangazo katika vyombo vya habari ya sherehe za kiongozi binafsi ni njia ya kuendeleza ubadhirifu wa raslimali za umma
    • Mbura na Sasa wanaendeleza ubadhirifu pale wanapoamua kuchukua vyakula kupita kiasi katika sherehe za mzee Mambo
    • kuwaajiri viongozi wawili wenye nyadhifa sawa katika sekta tofauti za umma
    • vibaraka na vikaragosi kupewa mali ambayo ingewafaidi wananchi          zozote 10 x 1 = 10

Swali la dondoo 3

Ndoto ya mashaka

“Sasa nimechoka mja. Nimechoka hata naradua kufa kuliko kuishi.”

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
  2. Taja mbinu mbili za lugha katika dondoo hili. (alama 4)
  3. Mzungumzaji alikuwa na haki ya kuradua kufa. Thibitisha. (alama 12)

Majibu ya dondoo 3

  1.  
    • Haya ni mawazo ya Mashaka.
    • Yuko chumbani mwake.
    • Anakumbuka hali yake ngumu ya maisha na mashaka tele.
    • Anamkumbuke mkewe, Waridi, alivyomtoroka na wanawe.
    • Anayaona maisha kutokuwa na thamani tena kiasi kwamba anaona kifo kingemfaa. (4×1= 4)
  2.  
    • Takriri- nimechoka
    • Uzungumzi nafsi- sasa nimechoka… (2×2= 4)
  3. Mashaka alikuwa na haki ya kuradua kufa kwani alikuwa amepitia matizo mengi:
    • Mamake mzazi, Ma Mtumwa, aliiaga dunia punde tu baada ya kumkopoa.
    • Baada ya kifo cha mamake, babake alishindwa kuvumilia naye akaaga dunia.
    • Mashaka alilelewa na Biti Kidebe asiyekuwa mamake mzazi.
    • Mamake mlezi, Biti Kidebe naye alihitaji kulelewa. Daima alilalamikia miguu yake.
    • Mashaka alilazimika kufanya vijikazi ili kumsaidia mamake mlezi kupata chohcote cha kutumia.
    • Mashaka na Biti Kidebe walipanda mabokoboko ambayo wengi waliamini si ndizi.
    • Biti Kideba alienda jongomeo pindi tu Mashaka alipomaliza chumba cha nane.
    • Mzee Rubeya na Shehe Mwinyimvua wanawafungisha Mashaka na Waridi Ndoa ya Mkeka bila kupenda kwao.
    • Mzee Rubeya wanawakimbia Mashaka na Waridi na kurudi kwao Yemeni ili Mashaka wasije kuwaaibisha.
    • Kazi ya Mashaka ilikuwa ya kijungu meko- ya kupigania tumbo.
    • Mashaka na Waridi waliishi sehemu kuchafu kule Tandale, Kwatumbo, eneo la Uswahilini.
    • Walikosa vyoo wakawa wanatumia karatasi kwa haja zao zote.
    • Mashaka na Waridi walipata watoto wengi, saba, ambao wanawashinda kuwakimu.
    • Mashaka alilazimika kuomba jikoni kwa jirana yake, Chakupewa, ili wanawe wa kiume wapate mahali pa kulala.
    • Chumba chao kiliingiza maji mvua iliponyesha.
    • Mashaka alifanya kazi ya usiku katika Shirika la Zuia Wizi Security (ZWS).
    • Waridi anamtoroka Mashaka maisha yanapokuwa magumu. (12×1= 12)
                                               Kila hoja ifafanuliwe kikamilifu

Swali la dondoo 4

Mame Bakari

“Una nini? Umeshtuka mwanangu! Unaogopa? Uaogopa nini?

  1. Weka dondoo hili katika muktadha wake. al 4
  2. Eleza sifa za mrejelewa.    al  6
  3. Tambua mbinu mbili za lugha zilizotumika katika dondoo. al 2
  4. Eleza umuhimu wa msemaji. al 4
  5. Tambua maudhui yanayojitokeza katika kifungu hiki.  al 1
  6. Fafanua maudhui katika swali la (e) kwa kurejelea hadithi nzima. al 3

Majibu ya dondoo 4

  1.  
    • Msemaji ni babake Sara.
    • Akimwambia Sara.
    • Wakiwa hospitalini kwenye chumba cha daktari.
    • Sara alikuwa ameenda kufanyiwa vipimo vya ujauzito na Beluwa alipowakuta wazaziwe wakisubiri katika chumba hicho
  2.  sifa za mrejelewa.(Sara)
    • mpenda masomo
    • ni mwoga
    • mwenye busara
    • mwenye mapenzi ya dhati
    • mwenye utu hakutaka kuavya mimba
    • ni msiri
    • mwenye maadili
    • mwenye majuto
    • ni mvumilivu.
      (kila sifa itolewe maelezo. Mwanafunzi akitaja sifa tu asituzwe)
      Hoja Zozote 6 (6x 1 = 6)
  3.  
    • Swali la balagha; una nini?
    • Takriri; unaogopa, unaogopa
  4.  umuhimu wa msemaji (babake Sara)
    • Kupitia kwake tunapata habari ya ukali kupita kiasi kwa wazazi kwa wanao.
    • Ni kielelezo cha wazazi ambao hawako tayari kubadili msimamo wao mkali kwa watoto wao.
    • Anaonyesha umuhimu wa wazazi kushirikiana katika malezi.
    • Anaonyesha umuhimu wa kuweka siri katika masuala tata ya familia.
    • Ni kielelezo cha wazazi wanaouenzi utamaduni wa jamii yao.
  5.  
    • Malezi
    • mapenzi
  6.  
    • Malezi- Babake Sara anakuwa   mkali kwa sara. Babake Sara anadalika na kumwonyesha mapenzi.
    • Mapenzi - Kuna mapenzi ya dhati kati ya sarana salime. Salime anamsaidia sara anapokuwa mjamzito. Salime aidha anamsaidia sara kuweka siri ya ujauzito.

Swali la dondoo 5

“Tulipokutana Tena” (Alifa Chokocho)

Halikuwa jambo la kawaida maana maji yalikuwa hayapatikani karibu pale kijijini petu. Sharti mtu aende masafa marefu kuyatafuta. Na sabuni? Sabuni ilikuwa kitu cha anasa kwa familia yetu. Wazazi wangu hakuwa na uwezo wa kununua Sabuni. Labda mara moja moja siku za sikukuu.

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili.   (alama 4)
  2. Eleza majukumu mawili ya takriri katika dondoo hili.    (alama2)
  3. Kwa kurejelea hadithi Tulipokutana Tena jadili jinsi haki za watoto zinavyokiukwa.(alama 6)
  4. Jadili changamoto zinazokumba asasi ya ndoa ukirejelea hadithi zifuatazo:       (alama 10)
    1. Masharti ya Kisasa
    2. Ndoto ya Mashaka

Majibu ya dondoo 5

  1.  
    • Maneno haya ni ya Bogoa.
    • Anawambia msimulizi na Kazu.
    • Wako katika club Pogopogo.
    • Bogoa na msimulizi wanakutana baabaya miaka 41 baada ya kutoroka kwasababu ya kuwa mtumwa wa nyumbani kwa Bi. Sinai.
  2.  
    • Imetumika kuchimuza hali ya umasikini kwani hata sabuni hawangeweza  kununua.
    • Imetumika kuendeleza maudhui ya umasikini
    • Imetumika kusisitiza wazo. Mfano kutokuwa na uwezo wa kununua sabuni isipokuwa siku ya sikukuu.
    • Imetumika kuendeleza tamathali nyingine za semi mfano chuku. Kuthamini sabuni sana na hata kutokuwa na uwezo wa kununua sabuni.
  3.  
    • Kutengwa na familia- Bogoa alikuwa na umri mdogo wa miaka mitano na hakuta kakutengwa na baba,mama, ndugu, kaka na dada zake. Uk 114
    • Kuamrishwa kufanya vitu bila hiari ya Bogo uk. 115
    • Bogoa alitwishwa mambo yote ya nyumbani alikuwa mtoto mdogo. Uk 115
    • Watoto masikini hawapaswi kusoma shuleni. Uk 116
    • Bogoa hakuwa na uhuru wakucheza na watoto wa Bi. Sinai.
    • Kutishiwa maisha- Bi. Sinai alimtisha Bogua kuwa angemkata ulimi kama angesema chochote kuhusu maisha yake ya ndani.
    • Kuadhibiwa kwa kuchomwa- Bi. Sinai alimchoma viganja Bogoa kwa kosa la kuchoma maandazi.
    • Kutoambiwa ukweli- Bogoa anawalaumu wazazi wake kwa kumdanganya     Alama 6×1=6
  4.  

Masharti ya Kisasa

  • Masharti katika ndoa
  • Ukosefu wa uaminifu
  • uhuru
  • Taasubi ya kiume/ utamaduni
  • Wivu
  • Utabaka
  • Ukengeushi

Ndoto ya Mashaka

  • Ndoa ya lazima
  • Utabaka
  • Umaskini
  • Upangaji wa uzazi
  • Usaliti

Swali la dondoo 6

`..........Lakini shogake................. shogake.................. shogake dada nikamwona ana ndevu’.

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili.      alama 4
  2. Bainisha sifa tatu za `shoga ‘ anayezungumziwa katika dondoo hili.      alama 6
  3. Jadili umuhimu wa `dada’ anayerejelewa katika kuendeleza dhamira ya hadithi.    alama 10

Majibu ya dondoo 6

  1.  
    • Haya ni maneno ya lulua
    • Anamwambia mamake Bi. Hamida
    • Wamo nyumbani mwao wakila chomcha.
    • Lulua anamweleza jinsi alivyoingia katika chumba cha safia na kumkuta akiwa amelala kitandani na kimwana.  (4x1=4)
  2.  
    • Msiri- Wazazi wake safia hawakuwahi kuiona sura yake kwa sababu alipenda kuvaa buibui ili asijulikane kuwa ni mwanamume.
    • Mzinifu- Anazini na safia na kumpachika mimba
    • Mjanja – Anajifunika buibui na kujifanya jinsi ya kike
  3.  Dada anayerejerewa ni safia
    • Ni kiwakilishi cha uoza katika jamii. Anawahada wazazi wake kuwa kimwona ni shogake kumbe ni mpenziwe na kiume.
    • Ametumiwa kukosoa malezi ya wazazi. Wazazi wake Bwana Masudi na Bi Hamida walimwamini sana hadi wakawa wanamsifu tu badala ya kungumza naye ili kumpa mwelekeo ufaao maishaini.
    • Kuendeleza maudhui ya elimu. Alikuwa mwerevu shuleni. Kila mtihani aliofanya aliongoza katika darasa lao.
    • Ni kielelezo cha wanawake wanaoavya mimba kuuficha uovu huo. Safai anajaribu kuavya mimba ili wazazi wake wasijue lakini anakufa.
    • Suala la unafiki linajitokeza kupitia kwake. Alijifanya mzuri kwa zazazi wake hhadi wakamwamini kwa kila jambo kumbe alikuwa mwovu- anawahadaa wazaziwe kuwa kimwana ni shogaye ilhali ni mpenziwe wa kiume.
    • Ni kielezo cha athari za mapenzi kabla ya ndoa. Anafanya mapenzi na kimwana.Anapachikwa mimba na kwa sababu ya kuhofia matokeo yake anaamua kuiavya ile iwe siri lakini anakufa. ( 2x5=10) Taja       = 1, Kueleza = 1,  Jumla     = 2

Swali la dondoo 7

Ndoto ya Mashaka

"...dunia imenikunjulia mikono kunifariji baada ya kunicharaza fimbo yake aushi yangu yote."

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili (al.4)
  2. Tambua na ueleze mbinu ya lugha iliyotumiwa katika dondoo.(al.2)
  3. Eleza jinsi dunia ilimcharaza fimbo msemaji kwa kutolea hoja kumi na nne. (al.14)

Majibu ya dondoo 7

  1.  
    • Maneno ya Mashaka
    • Katika ndoto
    • Yumo chumbani mwake.
    • Anaota kuhusu kurudi kwa ua lake baada ya kupotea kwa karne moja.
  2.  
    • Tashihisi - dunia kunikunjulia mikono kunifariji baada ya kunicharaza
  3.  
    • Mamake Mashaka kufariki punde tu baada ya kumkopoa.
    • Babake pia anafariki punde tu baada ya mamake.
    • Kuambulia mama mlezi maskini.
    • Kuanza kufanya kazi za kijungu jiko kujikimu yeye na mama mlezi.
    • Licha ya bidii yao mara kwa mara walikosa ikamlazimu Kidebe kutumia akiba yake.
    • Kufiwa na mama mlezi.
    • Kufungishwa ndoa ya mkeka na Mzee Rubeya.
    • Kudharauliwa na wazazi wa Waridi kwa sababu ya umasikini wake.
    • Kuishi katika mtaa duni.
    • Chumba chake ni duni - kinavuja paa inyeshapo.
    • Alikosa samani chumbani – hana meza,viti,kitanda wala godoro.
    • Kazi ya usiku.
    • Mshahara duni.
    • Kukopoa pacha mara tatu.
    • Kulazimika kuomba nafasi ya malazi ya wana kwa jirani.
    • Mazingira yenye harufu mbaya ya chooni.
    • Mke na wana kumkimbia. Zozote 14

Swali la dondoo 8

Nizikeni papa hapa–Ken Walibora
“Ndugu yangu tahadhari na hawa.........”

  1. Eleza muktadha wa dondoo (al.4)
  2. Eleza sifa za msemewa (al.4)
  3. Taja naufafanue maudhui sita katika hadithi hii (al.12)

Majibu ya dondoo 8

  1.  
    • Maneno ya rafiki ya Otii
    • Msemewa ni Otii
    • Walikua katika klabu moja Mombasa
    • Ni baada ya Otili kuanza urafiki na Rehema Wanjiru
  2. Sifa za Otii
    • Bidii
    • Mvumilivu
    • Mchunguzi
    • Tamaa
    • Mapuuza
    • Mpenda starehe
    • Msimamo dhabiti
    • Hasira
    • Kumbulazi
  3.  
    • Ukimwi
    • Ajali Barabarani
    • Usafiri
    • Utekelezajichezaji soka
    • Ukalili/Dhuluma
    • Usaliti
    • Uanahabari
    • Teknolojia
    • uzalendo

Swali la dondoo 9

“Rasta twambie bwana!”

  1. Weka dondo katika muktadha (alama 4)
  2. Taja mbinu zilizotumiwa na mwandishi katika dondoo hili (alama 2)
  3. Nikwa vipi mzungumziwa anamchukulia mwalimu mkuu kama hambe? (alama4)
  4. Je, mtihani wa maisha niamwani faafu ya hadithi hii? (alama10)

Majibu ya dondoo 9

  1.  
    • Maneno ya wanafunzi wa shule ya Busukalala.
    • Akimwambia Rasta/ Samueli Matandiko.
    • Walipokuwa shuleni.
    • Samueli alikuwa ametoka katika afisi ya mwalimu mkuu kuchukua matoke yake ya mtihani.
    • Marafiki waliomjua wanamtaka awaelezee alama zake.
  2.  
    • Utohozi -rasta
    • nidaa-Rasta twambie bwana! c)
  3.  
    • Mwalimu mkuu wa shule ya Busukalala hakuwahi kumwamini Samueli hata siku moja kama anaweza kufaulu mtihani
    • Mwalimu mkuu hakuamini Samueli aliposema kuwa amelipa ada mpaka alipohakikisha kwa kuangalia nyaraka na kumbukumbu zake.
    • Anamwonyesha Samueli dharau kwa kumrushia karatasi kama mbwa; anarejelea kile alichokuwa akifanya na kumpuuza.
    • Mwalimu mkuu hakumpa ushauri wowote Samueli ambo unmgemsaidia kupokea matokeo yake ambayo hayakuwa mazuri hata kidogo.
    • Mwalimu mkuu alimjibu Samueli kwa karaha, alipomwita kuwa ni fidhuli.
    • Anamjibiza kwa kuuliza iwapo wanafunzi wengine wanalipa mawe au majani.
  4.  Mtihani wa Maisha ni anwani ambayo imesawiri maudhui ya hadithi hii kwa kiwango kikubwa.
    • Samueli anafanya mtihani wake wa shule ya upili na kuenda kuyachukua matokeo. Kabla ya kufikia zamu zake Samueli anajichunguza na kujipima uwapo ameufanya vizuri. Mawazo kuhusu mtihani huo yanamtawala.
    • Alianza kuwachunguza wanafunzi waliokuja kuchukua matokeo ya mtihani wanaopotoka mlangoni ili kujaribu kuona iwapo wamefaulu au la.
    • Samueli anajaribu kujiaminisha kuwa yeye atakuwa amefaulu mtihani wakati akiwa kwenye foleni ya kuchukua matokeo.
    • Samueli anajiaminisha kuwa yeye ni mjanja na angemshangaza mwalimu mkuu.
    • Anagundua kuwa amefali mtihani huo. Safu za alama ya D na ilimkodolea macho. Herufi hizo zilimfedhesha na akalemewa.
    • Nyumbani baba yake aliyengoja matokeo kwa hamu hakuyapata.
    • Samueli anadanganya kwamba ana salio la karo.
    • Baba anarauka na kutembea kilomita sita kwenda kuchukua matokeo ya mtihani.
    • Anapogundua ni uwongo anapandwa na hamaki.
    • Samueli anaamua kujitosa bwawani ili aondokane na athari za kufeli mtihani huu wa kitaaluma. Hata hivyo amaokolewa na mpita njia.
    • Mama yake anamwambia kuwa ingawa amefeli mtihani wa shule, asikate tamaa, bado ana mtihani wa maisha ambao anaweza kufaulu.
    • Anwani hii inafaa sana

Swali la dondoo 10

TUMBO LISILOSHIBA (S.AMOHAMMED)
``Hakuna aliyeweza kukitegua kitendawili chenyewe lakini…’’

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama4)
  2. Tambua tamathali ya usemi iliyotumiwa katika dondoo hili. (alama2)
  3. Fafanua chanzo na hatima ya kitendawili kinacho rejelewa katika dondoo hili.(alama10)
  4. Eleza wasifu wa warejelewa katika dondoo hili. (alama4)

Majibu ya dondoo 10

  1.  
    • Hii ni kauli ya mwandishi
    • anarejelea tukio la ulafi wa Jitu
    • mahali ni katika mkahawa mshenzi wa Mzee Mago
    • watu wamepigwa na butwaa kwa tendo la ulafi wa Jitu.(4x1=4 b)
  2.  
    • nahau- kukitegua kitendawili (alama 2)
    • jazanda - neno kitendawili kurejelea jambo fulani lililofichika (yoyote: kutaja alama 1, kutoa mfano mmoja alama 1)
  3. Chanzo
    • Kuwepo kwa uvumi na nong'ono kuhusu uwezekano wa kunyakuliwa ardhi ya Wanamadongoporomoka.
    • Mzee Mago kuwahamasisha raia kuhusu haja ya kutetea kazi zao.
    • Mikutano ya kuandaa mikakati ya kutetea haki za Wanamadongoporomoko inayofanyika katika mkahawa.
    • Jitu kuwasili mkahawa mshenzi na kuzua taharuki
    • Jitu kuamrisha kuhudumiwa na kula chakula chote kilichoandaliwa.
    • Watu kupigwa na butwaa kwa ulafi wa jitu na kuwazia tendo hili

      Hatima

    • Jitu kuahidi kurudi keshoye kula maradufu ya siku hiyo.
    • Hatimaye jitu kufika na mabuldoza
    • Askari wa baraza kuandamana na jitu
    • Jeshi la polisi kuwalinda askari wa baraza
    • Watu kupigwa virungu bila hatia
    • Vibanda kubomolewa
    • Watu kujenga upya vibanda mshezi zaidi ya hapo awali (Hoja zozote 5 za chanzo na 5 za hatima jumla ni alama 10)
  4.  
    • Wazalendo halisi wanaendeleza harakati za kupigania haki zao za kumiliki na kukomboa ardhi yao.
    • Wenye bidii: hawasiti /hawakomi kuandaa mikakati ya kupigania haki zao. mfano: mikutano yao.
    • Wenye umoja na ushirikiano : wanashirikiana kwa kukutana na kupanga utetezi wa haki zao.
    • Wakakamavu/ jasiri: wanakaidi hatua ya Jitu na kuikomboa ardhi yao iliyonyakuliwa.
    • Wenye hekima/ busara: wanabaini hila za wenye nguvu kutaka kunyakua ardhi yao na kujiandaa kukabiliana nao. (zozote 4X1-4)

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba" on Whatsapp

OR

This is the most affordable option. You get all topics/full set papers at a lesser price than if you bought per paper/ per topic.

Click here to download the full document with all topics

OR




Read 455 times Last modified on Monday, 01 February 2021 15:43
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - MAME BAKARI - Mohammed Khelef Ghassany - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba - Next »
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine
Tagged under
  • Kiswahili
  • tumbo

Related items

  • Kiswahili Karatasi ya Pili Maswali na Majibu - Kassu Jet Joint Exams 2020/2021
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Tamthilia ya Kigogo
  • Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tamthilia ya Kigogo
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
Tumbo Lililoshiba na Hadithi Nyingine