Watch Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34
  • Home
  • High School Notes
  • Kiswahili
  • Tumbo Lililoshiba na Hadithi Nyingine
  • SHIBE INATUMALIZA - Salma Omar Hamad - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA

Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba MASHARTI YA KISASA - Alifa Chokocho - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA - Next »
Download PDF for future reference Install our android app for easier access

Click the button below to download the full Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA pdf document, with all the topics.

Download Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA PDF to Print or Offline Reading

CLICK HERE to get "Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA" on Whatsapp for offline reading/ printing.

Tumbo Lisiloshiba Insha Questions and Answers

Maswali ya Insha

Haya ni maswali ambayo hutoa kauli inayohitaji kujibiwa kwa kirefu na kwa kina. Swali linaweza kuwa la jumla yaani linalohusu Hadithi nzima. Pia, swali laweza kulenga sehemu ya kazi husika katika nyanja na maudhui, wahusika na hulka zao, mafunzo na fani. Maswali haya huhitaji zaidi uwezo wa kukumbuka wa mtu, kupanga hoja na kuelezea msimamo au maoni yake kuhusiana nayo. Mtahiniwa anahitajika kutoa hoja na kuziteteta kwa mifano dhabiti. Mtahiniwa asitumie vistari vistari, afafanue hoja kikamilifu akiandamisha mifano mingi kutoka kwa Hadithi.

Swali la Insha 1

  1. Eleza namna maudhui ya ndoa yalivyosawiriwa katika hadithi ya Masharti ya Kisasa (alama 13)
  2. Kwa kurejelea hadithi ya Shibe inatumaliza,eleza namna maudhui ya ufisadi yanavyojitokeza (alama 7)

Eleza namna maudhui ya ndoa yalivyosawiriwa katika hadithi ya Masharti ya Kisasa (alama 13)

  • Mwanaume humposa wanamke. Dadi alienda nyumbani kwa Kidawa kumposa
  • Mwanamke ndiye huamua wakati wa kuolewa na nani wa kumwoa. Kidawa alimchagua Dadi baada ya muda refu
  • Ndoa huandamana na masharti. Dadi alipewa masharti na Kidawa ili akubali kuolewa naye.
  • Wanandoa hufanya kazi pamoja ili kukithi mahitaji ya nyumbani. Dadi anachunza samaki na kidawa ni metroni
  • Wanaume hawafurahi wake wao wanapotangamana na wanaume wengine. Kidawa anaposimama kuongea na wanaume,Dadi anadhika sana.
  • Wanandoa husaidia kazi za nyumbani, Dadi anasaidia kidawa kazi za nyumbani kama vile kuosha vyombo na kufagia.
  • Wanandoa wanapanga uzazi,Dadi na Kidawa wanapanga kuwa na mtoto mmoja pekee
  • Mwanamke anaajiriwa. Kidawa aliajiriwa shuleni kama metroni.
  • Mwanamke anajinunulia nguo na fashoni nyingine. Kidawa ananunua viatu na kanzu anayaovalia kwenda kazini.
  • Ndoa imekosa uaminifu. Dadi anashuku kuwa Kidawa ana mapenzi na mwalimu mkuu.
  • Kiwango cha elimu si kikwazo katika ndoa. Kidawa anaolewa na Dadi licha ya kuwa ana kisomo cha juu kuliko Dadi.
  • Mwanamke amekengeuka. Kidawa anapenda fashoni
  • Wote wawili. Mwanamke na mwanaume wanachangizana nyumbani
  • Kuna makubaliano ya kufanya mambo kwa pamoja (13x1=13)

Kwa kurejelea hadithi ya Shibe inatumaliza,eleza namna maudhui ya ufisadi yanavyojitokeza (alama 7)

  • Mzee Mambo hafanyi kazi wizarani ilhali analipwa mshahara mkubwa kuliko Sasa na Mbura wanaofanya kazi wizarani
  • Mambo anatumia runinga ya taifa inayofaa kuufahamisha umma masuala yataifa lao kwa maslahi yake. Anaitumia kupeperusha sherehe inauofahamika nyumbani kwao.
  • Mambo anaifilisi serikali kwa kutumia pesa za serikali kugharamia sherehe zake binafsi. DJ na wenzake wanalipwa mabilioni ya pesa za serikali kwa kusimamia sherehe hii.
  • DJ anaipunja serikali kwa kutumia mtaji wa bohari kuu ya dawa za serikali kufungua duka lake la dawa.
  • Dj anaifilisi serikali kwa kupokea huduma za maji,umeme na matibabu bure ilhali wananchi maskini wanazilipia.
  • Wafanyakazi wa umma wanaibia serikali saa za kazi. Sasa na Mbura wanahudhuria shere zilizofanyika kwa Mambo siku nzima ilhali walipaswa kuwa kazini.
  • Mzee Mambo anatumia magari ya serikali kwa maslahi yake binafsi. Kwa mfano, anayatumia kusomba maji, chakula, kuwaleta jamaa wa Mambo shereheni na mapambo. (7x1=7)

Swali la Insha 2

Ukirejelea hadithi zifuatazo, eleza jinsi maudhui ya mapenzi na asasi ya ndoa yanavyojitokeza.   (alama 20)

  1. Mapenzi ya kifaurongo
  2. Masharti ya kisasa
  3. Ndoto ya Mashaka
  4. Mtihani wa maisha

Mapenzi ya kifaurongo

  • Ndoa iliyotarajiwa ya Dennis na Penina ilitawaliwa na unafiki. Penina anamjia Dennis na wazo la kuwa wapenzi bila kuzingatia hali duni ya familia yake. Dennis anapokosa ajira anamfukuza
  • Inatawaliwa na kuhimiliana
  • Imetawaliwa na kukata tamaa - Penina anakata tamaa baada ya Dennis kukosa kazi
  • Imezingirwa na utabaka wa kiasili
  • Mapenzi hukua, huugua na hufa 5 x 1 = 5

Masharti ya kisasa

  • Ndoa ya Dadi na Kidawa
  • Ndoa inayodhibitiwa na masharti
  • Ndoa ya kugawana majukumu
  • Ndoa ya kupanga uzazi
  • Ndoa inayoruhusu mwanamke kufanya kazi. Kidawa anafanya kazi ya umetroni usiku na kuuza bidhaa mtaani
  • Baadhi ya watu huingilia ndoa za wenzao kama njia ya kuona mapenzi yamevunjika baina ya wanandoa husika 5 x 1 = 5

Mtihani wa maisha

  • wazazi wa Samueli ni wenye mapenzi wanaonyesha mapenzi kwa mtoto huyu wao kwa kumpeleka shuleni akajipatie elimu
  • Samuel anaonyesha mapenzi kwa Nina. Kwa muda amekuwa mpenziwe
  • Nina anaamini kuwa mwanaume huyu ni bingwa kutokana na kudanganywa alikodanganywa na mwanaume huyu
  • mamake Samueli ana mapenzi ya dhati kwake, baada ya Samuel kujaribu kujitoa uhai mamake anamsihi waende nyumbani “Twende zetu nyumbani mwanangu.”  zozote 4 x 1 = 4

Ndoto ya Mashaka

  • Kuna ndoa ya Mashaka na Waridi
  • Kuna ndoa ya mtumwa na mumewe mzee Rubeya
  • Tatizo la kwanza ni ndoa ya kulazimishwa. Mashaka na Waridi walitoka kwenye matabaka mawili tofauti
  • Waridi - tabaka la kitajiri
  • Mashaka - tabaka la maskini
  • Kuna kutohusisha wanawake katika ndoa. Mamake Waridi hakuhusishwa katika harusi
  • Ndoa inakumbwa na tatizo la malazi bora - upendo, kujikubali, ukosefu wa taasubi ya kiume
  • Kuna changamoto zinazojitokeza baada ya kifo cha mmoja. Mashaka anawachwa yatima
  • Kuna utengano katika ndoa. Waridi anatengana na mumewe kutokana na hali ngumu ya kiuchumi

Swali la Insha 3

  1. Eleza ufaafu wa anwani mapenzi ya kifuaurongo kwa kurejelea mhusika Penina. Al.10
  2. Eleza nafasi ya elimu katika maisha ya wanajamii ukirejelea hadithi: Mtihani wa maisha.

Eleza ufaafu wa anwani mapenzi ya kifuaurongo kwa kurejelea mhusika Penina. Al.10

Kifaurongo ni mmea wenye sifa ya kujifisha mara unapoguswa. Mwandishi akejeli mahusiano yaliyojengwa katika msingi wa unafiki.

  • Penina anajifanya kumjali Dennis katika hali yake ya kunywa uji na kuonyesha huzuni. Anamtia Dennis mshawasha wa mapenzi ila si mapenzi kamili.
  • Msimulizi anadai wavulana wengi wameangamia katika utandabui wa mapenzi baada ya kufanyiwa makuruhu na wasichana wenye tabia ya kifaurongo.
  • Penina anadai atakuwa na Dennis kwa mazuri na mabaya lakini alimwacha alipokosa ajira.
  • Penina asema kuwa hafanyi mzaha na kuwa hawezi kumchagua mpenzi kwa msingi wowote kama si mapenzi. Mwishowe alivunja ndoa yake kwa sababu Dennis alikuwa fukara. Hii ni tabia ya kifaurongo.
  • Penina hataki kuitwa mpenzi wa Dennis na amtaka atafute msichana wa kufu yake akidai mgomba changaraweni haupandwi ukamea.
  • Penina amfukuza Dennis nyumbani alipokosa kazi ilhali alikuwa ameapa hangemsaliti kwa vyovyote vile. Hoja 5 x 2 = 10

Eleza nafasi ya elimu katika maisha ya wanajamii ukirejelea hadithi: Mtihani wa maisha.

  • Wanafunzi wanatarajiwa kufanya mtihani wa kidato cha nne ili kubaini hatima yao. Samueli awaza kuwa matokeao ya mthihani yangekuwa daraja ya ufanisi.
  • Elimu ina daraja/viwango – Samueli anatarajia kuingia chuo kikuu anapokamilisha kidato cha nne.
  • Katika masomo kuna kufeli.
  • Wanafunzi wanahofia matokeo ya mtihani wa kidato cha nne k.m Samueli.
  • Wanafunzi wanaojiamini kupindukia huathiriwa kisaikolojia wanapofeli.
  • Wanakunzi lazima watimize matakwa Fulani kabla ya kupatiwa matokeo yao.
  • Wanafunzi wengine wanaonea aibu matokeo yao.
  • Jinsia ya kike inapiku jinsia ya kiume masomoni k.m Dada zake Samueli.
  • Jinsia ya kike inabaguliwa masomoni. Babake Samueli ameweka matumaini yake kwa Samueli.
  • Watoto wanatarajiwa kupita mtihani wanusuru familia zao.
  • Wanafunzi wanaichukulia elimul na masomo kwa mzaha na kejeli.
  • Samueli aliona shule kama jela. 10 x 1 = 10

Swali la Insha 4

Safari ya elimu ni kama ua la waridi ambalo licha ya upendezaji wake, huzingirwa na miiba. Jadili adha za safari hii kwa hoja tano tano kutoka kwa kila mojawapo wa hadithi fupi zifuatazo: Mapenzi ya Kifaurongo, Mame Bakari, Mwalimu Mstaafu na Mtihani wa Maisha.

Tanbihi: swali hili linamhitaji mtahiniwa kuonyesha changamoto zinazoikumba elimu.

Mapenzi ya Kifaurongo

  • Ugumu wa kuelewa mambo shuleni – Dennis Machora na wenzake wanapata kugumiwa na mambo wanayofunzwa katika mhadahara chuoni. Kauli za Daktari Mabonga hazieleweki upesi.
  • Utabaka shuleni – Dennis mwenye jadi ya kimaskini anatatizwa na maisha chuoni anakojipata akitagusana na wenzake kutoka familia za kitajiri.
  • Kejeli za walimu – Daktari Mabonga anawajekeli wanafunzi wake kwenye mhadhara kila wanapomwuliza maswali.
  • Kuchekwa na wanafunzi wengine – Wanafunzi wanamcheka sana Dennis anapomwomba Daktari Mabonga kutumia lugha nyepesi katika mhadhara.
  • Kutamauka shuleni – Dennis anakatizwa tamaa na masomo anapoyaona kama madubwana ambayo hakujua yalitoka wapi.
  • Utashi /Umaskini huwakumba baadhi ya wanafunzi – Dennis anajipata na uhitaji wa vitu muhimu vikiwemo malazi bora, chakula n.k. Analazimika kulalia shuka zilizozeeka na kuchanikachanika na pia kunywa uji anapokosa chakula.
  • Upweke/Ubaguzi shuleni – Wanafunzi wa familia za kitajiri huona haya hujinasibisha na wenzao wasio na chochote. Dennis anajipata katika upweke kutokana na hili.
  • Anasa/ Mapenzi shuleni – Wanafunzi katika Chuo cha Kivukoni wanatumbukia kwenye anasa na masuala ya mapenzi , Dennis anawaona wenzake wakitembea huku wameshikana wawili wawili.
  • Kukosa kazi baada ya kusoma – Dennis anatafuta kazi bila ya mafanikio licha ya kuhitimu na shahada ya uanahabari kutoka kutoka chuoni.

Mame Bakari

  • Mimba za mapema kwa wasichana – Sara anajipata na ujauzito unaomtatiza kimawazo akiwa mwanafunzi.
  • Kubakwa kwa wanafunzi wa kike – Sara anabakwa na janadume asilolijua majira ya saa tatu unusu akitoka ‘twisheni’.
  • Kutengwa kwa wanafunzi wajawazito – Sara anawazia kutengwa na watu wote wa kando na wa karibu.
  • Wanafunzi kukosa wa kuwasikiliza wanapopatwa na balaaa mishani - Sara anawaza jinsi ambavyo hakuna mtu ambaye angemwelewa baada ya kubakwa.
  • Kufukuzwa shuleni kwa wasichana wajawazito/ kukatiziwa masomo – Sara anawazia jinsi ambavyo mwalimu mkuu angemfukuza kwa kusema shule ni ya wanafunzi sio wamama.
  • Msongo wa mawazo/ Shinikizo za akilini – Sara anajiwa na wazo la kujitoa uhai, hata hivyo nalikomesha wazo hilo.
  • Uavyaji mimba – Wanafunzi wa kike huweza kulazimika kuavya mimba ili wafiche hali zao. Wazo hili liliwahi kumjia Sara na akalitupilia mbali.
  • Kuaibishwa – Sara anawazia ambavyo mwalimu mkuu angemwita mama hadharani.

Mwalimu Mstaafu

  • Ubaguanaji kwa misingi wa wepesi wa kupata mambo darasani – Jairo alibaguliwa katika sherehe ya kustaafau kwa mwalimu Mosi kwa kuwa hakuwa hodari masomoni hivyo hakutajirika baada ya shule.
  • Dhana potovu ya baadhi ya wanafunzi – Jairo alikuwa na dhana ya kwamba mwalimu Mosi kwa kuendelea kumpa matumaini shuleni alikuwa anamharibia wakati.
  • Mtazamo hasi dhidi ya masomo – Jairo hakupenda masomo. Kwake waliosoma na kufanikiwa ni wakora.
  • Baadhi ya wanafunzi huwa na uwezo wa chini wa kuelewa mambo darasani – Jairo alipata sufuri ambazo mwalimu Mosi alimpa matumaini kwamba zingepisha mia mia.
  • Walimu kupata lawama kutokana na upungufu wa wanafunzi – Jairo anamlaumu Mwalimu Mosi kwa mapungufu yake shuleni.
  • Baadhi ya wanafunzi huzipuuza nasaha za walimu – Jairo alipuuza kabisa ushauri alioupata kutoka kwa Mwalimu Mosi kuhusu kuepuka ufuska, ulevi n.k.

Mtihani wa Maisha

  • Wasi wasi utokanao na matokeo ya mtihani – Samueli anajipata moyo ukimtuta anapokwenda kuyapokea matokeo ya mtihani wake wa kidato cha nne.
  • Walimu kuwadunisha wanafunzi – Samueli anasema vile ambavyo Mwalimu mkuu hakuwahi kumwamini.
  • Dharau kutoka kwa walimu – Mwalimu mkuu anamwonyesha dharau Samueli anapoingia ofisini kuyapokea matokeo yake. Anamtupia matokeo yake badala ya kumpa kwa njia nzuri.
  • Wanafunzi kupumbazwa na sifa wanazopaliwa na wenzao – Samueli alipokuwa akisoma, alipumbazika na umaarufu kutoka kwa wanafunzi wengine akasahau kutia bidi. Wenzake walimtambua kama ‘rasta’ shuleni.
  • Kuvunjwa moyo na matokeo duni ya mtihani – Samueli anavunjika moyo anapopata matokeo duni ya mtihani.
  • Mapenzi ya mapema – Samueli anaingilia uhusiano wa kimapenzi na msichana kwa jina Nina.
  • Udanganyifu wa wanafunzi kwa wazazi wao – Samueli anamdanganya babake kuwa hakupata matokeo ya mtihani kwa kuwa hakukamilisha kulipa karo.
  • Baadhi ya wanafunzi huwakosea heshima walimu- Samueli anamrejelea mwalimu mkuu kama ‘hambe’.
  • Wanafunzi kwenda mbali kupata elimu – Samueli alilazimika kusomea shule iliyokuwa mbali na nyumbani.
  • Kusalitika kwa wazazi – Wazazi wa Samueli wanahisi kusalitika baada ya mtoto wao mvulana, waliyemtegemea sana kufeli mtihani wa kidato cha nne.
  • Elimu ya msichana kutodhaminiwa sana – Babake Samueli aliona fahari kumwona mtoto wa kiume akifanikiwa, licha ya kuwa binti zake wawili Bilha na Mwajuma walifaulu katika mtihani ya sekondari na walikuwa vyuoni.

Tanbihi: Mwanafunzi anaweza kupendekeza hoja nje ya zilizotolewa kwenye mwongozo huu. Hivyo, mtahini atathmini hoja za mwanafunzi.

Hoja tano kutoka kwa kila hadithi ( 5 × 4 = 20)

Swali la Insha 5

``Wahusika katika hadithi shibe inatumaliza wanatumia uhuru wao vibaya.’’ Onyesha ukweli wa kauli hii kwa kutoa mifano.  alama 20

  • Mzee mambo anatumia uhuru wa cheo chake serikalini vibaya kwa kupokea misharaha kutoka wizara mbalimbali ilhali hafanyi kazi yoyote.
  • Sasa na mbura wanatumia uhuru wao vibaya kwa kupanga na kupangilia wapi kwa kudoea badala ya kushiriki katika shughuli ya ujenzi wa jamii.
  • Wananchi wa taifa la Mzee Mambo wanatumia uhuru wao vibaya kwa kuzingatia kirenda kazini bila kujali kama wanfanya kazi yoyote. Muhimu si kwenda/ kazini ila kufanya kazi.
  • Mzee mambo anatumia uhuru wake vibaya kwa kutumia mali na wakati wa taifa kuandaa sehere zisizo na msingi wowote. Anaandaa sherehe kubwa kwa madai ya kusheherekea kuingizwa kwa mtoto wake ``nasari’’.
  • Mambo anatumia magari ya serikali kuhudumu katika sherehe yake.
  • Walaji katika sherehe ya kuingizwa kwa mtoto wa kwanza wa Mzee mambo nasari wanatumia uhuru wao wa kula vibaya kwa vile hawachunguzi kile wanachokula
  • Vyombo vya habari vinatumia uhuru wao vibaya kwa kupeperusha sherehe ya kibinafsi moja kwa moja badala ya kumulika mambo yanayoathiri taifa.
  • Dj na wengine wenye nafasi katika taifa wanatumia uhuru kupokea mabilioni ya pesa za serikali kutumbuiza katika sherehe za mtu binafsi.
  • DJ na wenzake wanatumia uhuru wao kupata huduma za maji, umame, matibabu miongoni mwa huduma nyingine bila malipo huku wananchi wakalazimika kulipia huduma hizi kwa dhiki na ufukara.
  • Sasa na mbura wanatumia uhuru wao wa kula kila kitu kibaya na kizuri, wanachokijua na wasichokijua,vyao na vya wenzao hata vya kuokotwa. Hili linawaweka katika hatari ya kupatwa na maradhi kama kisukari na saratani.    Hoja ( 1x 2 = 2)    ( 10 x 2= 20)

Swali la Insha 6

Kwa kurejelea hadithi ya Mapenzi ya Kifaurongo, Mame Bakari, Nizikeni Papa Hapa , Mtihani wa Maisha na Mkubwa, eleza changamoto zinazowakumba vijana. (al.20)

Mapenzi ya Kifaurongo.

  • Ukosefu wa karo -wazazi wa Dennis kufanya kazi kwa majirani kudunduiza karo yake.
  • Ukosefu wa hela za matunzo – Dennis hana cha kupika ila uji mweupe bila sukari.
  • Mapenzi shuleni – wanafunzi wa Chuo kikuu cha Kivukoni wanahusiana kimapenzi.
  • Masomo magumu – wanafunzi hawaelewi anayofunza Dkt. Mabonga.

Mame Bakari

  • Ubakaji – Sara anabakwa na jana dume.
  • Kuavya mimba – Sara anatupilia mbali wazo la kuavya.
  • Kujitia kitanzi – Sara alilikataza wazo la hili likome hata kumpitikia.
  • Kutengwa –Alijiona akitengwa na jamii kwa jumla.

Nizikeni Papa Hapa

  • Mapenzi ya kiholela - Otii kuhusiana na Rehema bila kujali ushauri wa mwendani wake.
  • Ukimwi – Otii anaugua gonjwa lenye dalili zote za UKIMWI.
  • Kuumia kazini – Otii anaumia mguu akiichezea timu yake ya Bandari.
  • Kutelekezwa na waajiri wao – anapoumia timu yake haikumjali wala kumfidia.

Mtihani wa Maisha

  • Kutembea kwenda shule – Samueli anatembea kilomita sita kila siku kwenda shuleni.
  • Ukosefu wa karo – babake Samueli analazimika kuuza ng`ombe ili kulipa karo.
  • Mapenzi shuleni – Samueli anahusiana na Nina.
  • Kufeli mtihani wa kitaifa – Samueli anafeli mtihani wake.

Mkubwa

  • Umaskini- Mwavuli wa Mubwa umetoka mistari mitatu.
  • Matumizi ya dawa za kulevya – vijana wengi vichochoroni anakopitia Mkubwa wanatumia dawa hizi.
  • Ufisadi – wanafunzi wa profesa wanahongwa kumpigia Mkubwa kura.
  • Kufungwa – vijana wanaotumiwa kulangua dawa na wanaozitumia wanapokamatwa hutiwa kizuizini.

Swali la Insha 7

  1. “Mame Bakari”
    Kwa mujibu wa hadithi hii, ubahaimu anaotendewa mwanamke unakuwa na athari mbaya kwake. Onyesha kwa mifano mwafaka. (alama 10)
  2. “Masharti ya Kisasa”
    “…mapenzi ni mateso, ni utumwa, ni ukandamizaji, ni ushabiki usio na maana.”
    Thibitisha ukweli wa kauli hii kama unavyojitokeza kwenye hadithi. (alama 10)

“Mame Bakari”
Kwa mujibu wa hadithi hii, ubahaimu anaotendewa mwanamke unakuwa na athari mbaya kwake. Onyesha kwa mifano mwafaka. (alama 10)

  • Tukio la kubakwa linampotesea fahamu na anaaibika sana anapozinduka na
    kujipata akiwa uchi uk 47
  • Mwanamke kujeruhiwa - Baada ya Sara kubakwa na janadume lile,
    anaharibiwa na kuvuja damu.
  • Mwanamke kuvunjiwa ujanajike na utu wake.
  • Maisha ya mwanamke kuingiliwa na kuharibiwa.
  • Masomo yake yanakatizwa - mwalimu mkuu alimkabidhii Sara barua ya
    kumfukuza shuleni (uk 49)
  • Mwalimu mkuu hamsikilizi wala kumhurumia - badala yake aliongoza
    kumkejeli na kumweleza ile haikuwa shuke ya wazazi bali wa wasichana.
    Anasema hawafundishi wanawake hapo.
  • Mwanamke anateseka kiakili - Sara anaingiwa na mawazo mengi jinsi
    atakvyoukabili ule ujauzito. Anafikiria hata kuitoa ile mimba, kuhama kwao na hata kujiua.
  • Mwanamke katika umri mdogo anabebeshwa mimba jinsi Sara alivyofanysihwa. Mzigo huo ungekuwa na changamoto nyingi kutokana na umri wake mdogo.
  • Kuishi adhabu ya wazazi - Sara anahofia babake angemchinja kwa ujauzito
    wake.
  • Kuogopa kutoa taarifa ya kubakwa kwa wazazi kwa sababu wazazi hawangemwamini.
  • Kuishi maisha ya kimaskini - msimulizi anaeleza kuwa Sara angekunjiwakunjiwa matambatra yake na kurushiwa nje. Kila mara mwanamke anapobakwa, anayelaumiwa ni mwanamke na hata huonwa kama shetani. Uk 48 (hoja 10 x 1 = 10)

“Masharti ya Kisasa”
“…mapenzi ni mateso, ni utumwa, ni ukandamizaji, ni ushabiki usio na maana.”
Thibitisha ukweli wa kauli hii kama unavyojitokeza kwenye hadithi. (alama 10)

  • Mtahiniwa azingatie masharti ambayo mwanamume anafaa ayazingatie pamoja na athari zake katika maisha y andoa.)
  • Dadi ndiye mchuma riziki-yeye ni muuza samaki na apatacho kinatumiwa kuilisha jamaa yake. Pesa za mkewe ni za kununua mavazi ya fasheni mpya mpya na mapambo.
  • Dadi anasaidia kazi za nyumbani lakini mkewe Kidawa hatosheki na hayo. Kidawa hakubali kuwa mwanamume kazi ni za nje si za ndani na kuwa Dadi kufanya kazi za ndani ni hisani tu. Uk 60.
  • Dadi analazimika kushika shughuli za upishi kama vile kukuna nazi na kutia mboga tui.
  • Dadi anaosha nyumba, kufagia, kufua na hata kupiga nguo pasi. Wanandoa kujiwekea masharti ya uzazi. Wanahiari kumzaa mtoto mmoja tu kutokana na athari za usasa.
  • Dadi hataki mkewe atembeze bidhaa za kuwauzia wateja. Kila mara mkewe anapofanya hivyo, anaumia sana. Anaiona hiyo kama fursa ya mkewe kuhusiana na wanaume wengine. Uk 61.
  • Dadi anaona ugumu wa masharti ya mkewe katika maisha ya ndoa lakini anashinda kumweleza. Licha ya kuwa Dadi aliona ugumu wa kuzingatia masharti aliyowekewa na mkewe, hangeyavunja. Angefanya hivyo  ndoa yao ingevunjika na huko kungekuwa ni kumvunja yeye pia.
  • Dadi kushuku mkewe ana uhusiano wa kimapenzi na mwalimu mkuu. Hali hiyo inampa wasiwasi sana hata anashindwa kula.
  • Kila mara Dadi alitarajiwa kuwa baada ya kula angeviondoa vyombo mezani na hata kuvisafisha.
  • Dadi anapoamua kuzua mpango wa kupeleleza uhusiano wa mkewe na mwalimu mkuu, anafumaniwa na watu akiwa amepanda paipu na anaaguka na kuumia vibaya sana jambo linalomshutua sana mkewe pamoja na mwalimu mkuu anayelazimika kumwitia ambulensi impeleka hospitalini

Swali la Insha 8

  1. Tulipokutana Tena – Alfa Chokocho
    Jadili jinsi maudhui ya umaskini yalivyoshughulikiwa katika hadithi ya ‘Tulipokutana Tena’. (al.10)
  2. Mame Bakari
    Kina dada wanaobakwa wanakabiliwa na changamoto nyingi. Tetea. (al. 10)

Tulipokutana Tena – Alfa Chokocho
Jadili jinsi maudhui ya umaskini yalivyoshughulikiwa katika hadithi ya ‘Tulipokutana Tena’. (al.10)

  • Watoto kukosa elimu
  • wazazi wa Bogoa walishindwa kuelimisha
  • Wazazi kushindwa kuwalea watoto wao
  • Kudharauliwa kwa watoto maskini
  • Watoto wa maskini kufanyishwa kazi za sulubu
  • Maskini kukosa mavazi
  • Kukosa nauli
  • Watoto wa maskini kudhulumiwa
  • Maskini kubaguliwa (Pogogo ni ya watu wa chini)
  • Watoto kuwalaumu wazazi wao - Bogoa hapendi wazazi
  • Maskini wanalaumiwa bila hatia - waliokosa kuenda shule walidhaniwa watoto -
  • Ukosefu wa upangaji uzazi unazidisha umaskini.

Mame Bakari
Kina dada wanaobakwa wanakabiliwa na changamoto nyingi. Tetea. (al. 10)

  • Tukio la kubakwa linampotozea fahamu na anaaibika anapozinduka na kujipata
    akiwa uchi
  • Mwananmke kujeruhiwa - Sara anavuja damu nyingi
  • Mwananmke kuvunjiwa ujanajike na utu wake
  • Maisha ya mwanamke kuingiliwa na kuharibiwa
  • Kukatizwa masomo
  • Kukejeliwa - mwalimu mkuu
  • Mwanamke anateseka kiakili
  • Sara ana mawazo mengi
  • Mwanamke kubebeshwa mimba katika umri mdogo
  • Kuishi adhabu ya wazazi
  • Sara anahofia babake
  • Kuogopa kutoa habari ya kubakwa kwa wazazi kwa sababu hawangemwamini
  • kuishi maisha ya kimaskini
  • Kulaumiwa hata kama ni yeye aliyebakwa 

Swali la Insha 9

Onyesha jinsi wahusika wafuatao wanavyochangia katika kufanikisha maudhui kwenye hadithi Masharti ya kisasa:

  1. Kidawa
  2. Dadi

Kidawa

  • Ndoa;anakubali kuolewa na Dida hata baada ya kutoa masharti ya kisasi ambayo anatarajia kuwa Dida angezingatia.
  • Mapenzi,anampenda Dida kwa hivyo anakubali kuacha kazi yake shuleni ili mapenzi yao yasimbaratike kutokana na wivu wa Dida.
  • Bidii,anafanya kazi mbalimbali kwa wakati moja ili aweze kuyakidhi mahitaji ya familia yake licha ya kuwa Dadi hapendezwi na hali hii
  • Nafasi ya mwanamke,ameonyesha mwanamke kama mwenye mapenzi kwa mumewe na pia mwenye bidii. Anaonyesha bidii kwa kufanya kazi kadhaa na kukubali kuacha kazi hizo ili kulinda ndoa yake.
  • Usasa anaamini kuwa katika ndoa za kisasi mwanamke na mwanaume wana nafasi na majukumu sawa kwenye familia zao.
  • Elimu; amesoma madarasa kumi na mawili;pia pia anafanya kazi ya umetroni shuleni.
  • Ajira; kidawa anafanya kazi ya umetroni shuleni ambapo anawalinda wanafunzi wa kike bwenini, pia anauza nguo na viatu.
  • Uaminifu,yeye ni mwaminifu katika ndoa yake licha ya kuwamumewe anashuku kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwalimu mkuu.
  • Mabadiliko;annamini katika mtindo tofauti wa maisha kati ya mke na mume tofauti na ilivyokuwa kitambo,mwanamke na mwanaume wanafaa kushirikiana katika ndoa.
  • Utamaduni,anamwarifu Dadi kuwa aende ampose kwao ili amwoe ,haya ni kuwa mujibu wa utamaduni.

Dadi

  • Wivu;kutokana na hisia za wivu,Dadi anafikiria kuwa mkewe kidawa ana mahusiano ya mapenzi na mwalimu mkuu,anafanya uchunguzi kuhusu jambo hili.
  • Taasabi ya kiume ;Dadi anaamini kuwa nyumbani kuna kazi za mwanaume na zile za wanawake,mwanaume hafai kufanya kazi za jikoni.
  • Mapenzi;Dadi alimtafuta kidawa kuwa mkewe wa ndoa ingawa kidawa alikuwa amewakataa wanaume wengine kadhaa.
  • Ndoa;anafaulu kumshawishi kidawa kuwa mkewe wa ndoa ingawa kidawa alikuwa amewakataa wanaume wengine kadhaa.
  • Elimu;Dadi anaamini kuwa ingawa hakusoma sana shuleni yeye si mjinga hivyo ana uwezo wa kutambua mambo mbalimbali.
  • Ajira;Dadi anafanya kazi ya uchuuzi wa samaki kwa vile hakusoma sana.
  • Ujanja,anapoelekea shuleni,anafanya ujanja wa kupitia kwa mwalimu mkuu
    abainishe iwapo yupo nyumbani au la.
  • Utamaduni,anaamini kuwa kuna kazi za wanawake na wanume nyumbani kwa mujibu wa utamaduni wa kiafrika.
  • Uasherati anashuku kuwa kidawa ana mahusiano ya kimapenzi na mwalimu mkuu hili ni tendo la kiusherati.
  • Nafasi ya mwanamke;Dadi anaamini kuwa majukumu ya mwanamke ni kutekeleza kazi ya jikoni.

Swali la Insha 10

  1. Huku ukirejelea hadithi ya Tumbo Lisiloshiba, fafanua maudhui ya ukiukaji wa haki. (alama 10)
  2. Shibe inatumaliza; Salma Omar
    Jazanda ni mbinu mojawapo ya mbinu za lugha zilizo tumiwa kwa ukamilifu. Ukirejelea hadithi shibe inatumaliza fafanua mifano kumi. (alama 10)

Huku ukirejelea hadithi ya Tumbo Lisiloshiba, fafanua maudhui ya ukiukaji wa haki. (alama 10)

  • Viongozi kuweka vitego na vikwazo vya sheria ili watu wadogo wasiweze kutetea mali zao.
  • Kutowahusisha maskini katika maamuzi muhimu yanayoathiri maisha yao.
  • Kunyakua ardhi ya madongoporomoka ambapo watu maskini waliishi.
  • Kupanga njama za kuwapatia wanyonge visenti vichache ili waondoke madongoporomoka.
  • Jitu la miraba mine kula chakula chote bila kubakishia wateja.
  • Wanamadongoporomoka kubomolewa vibanda vyao na mabuldoza.
  • Askari wa baraza kutimua watu waliokuwa wanabomolewa.
  • Jeshi la polisi kulinda askari wa baraza wakibomoa vibanda vya wanamadongoporomoka.
  • Askari kuwapiga virungu watu.
  • Kueneza zisizo za ukweli
  • Mawakili kuwalaghai watu wanaodai haki

Mifano kumi ya Jazanda katika 'shibe inatumaliza'

  • 'sasa' na 'mbura' - kusasambura (kumaliza kila kitu kuto kila kitu, kupora mali yote.
  • sherehe - mipango isiyo na maana ya kufilisi mali ya umma
  • mchele wa mbeya - Bidhaa za kigeni na zenye manufaa makubwa
  • mchele wa mbeya - Bidhaa za humu nchini na zenye manufaa makubwa
  • Njaa uroho/uchi wa kupora mali ya umma serikalini
  • Kupakua vyakula - kupora mali ya umma
  • Shibe - unyakuzi wa mali kwa wingi zaidi
  • Kivuli (Mzee mambo) - mtu asiye na maana kama kivuli chake
  • Vyetu vyao - mali ya umma mali ya wananchi
  • Kioo cha taifa wasapu fesibuku, kalamu na karatasi = Hadharani (uporaji wa mali ya umma unafanywa kila mtu akijua lakini hakuna hatua inachukuliwa)
  • ( wimbo wa sijali lawama = Hii ni tabia yatakriban viongozi watu. Tabia ya kutojali wanayofanya au lawama kutoka kwa wananchi.
  • Ni kana kwamba wao wanaoimba wimbo moja.
  • Mtahini ahakik majibi yoyote (10 x 1=10)

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "Maswali na Majibu ya Insha katika Tumbo Lisiloshiba" on Whatsapp

OR

This is the most affordable option. You get all topics/full set papers at a lesser price than if you bought per paper/ per topic.

Click here to download the full document with all topics

OR




Read 337 times Last modified on Tuesday, 26 January 2021 12:49
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba MASHARTI YA KISASA - Alifa Chokocho - Mwongozo wa TUMBO LISILOSHIBA - Next »
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine
Tagged under
  • Kiswahili
  • tumbo

Related items

  • Kiswahili Karatasi ya Pili Maswali na Majibu - Kassu Jet Joint Exams 2020/2021
  • Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tumbo Lisiloshiba
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Riwaya ya Chozi la Heri
  • Maswali na Majibu ya Insha katika Tamthilia ya Kigogo
  • Maswali na Majibu ya Dondoo katika Tamthilia ya Kigogo
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
Tumbo Lililoshiba na Hadithi Nyingine