Ushairi - Kiswahili Notes

Share via Whatsapp


Istilahi za Kishairi

1. Arudhi

  • Sheria za jadi zinazofuatwa na watunzi wa mashairi:
    • kugawa shairi katika beti
    • beti kugawika katika mishororo inayolingana kiidadi
    • mishororo kugawika katika vipande
    • mishororo kuwa na mizani zinazolingana kiidadi (urari wa mizani)
    • kuwa na vina vya kati na vya mwisho vinavyotamkika kwa namna sawa (urari wa vina)
    • mtoshelezo wa beti au beti kutoa wazo kamili

2. Bahari

  • Aina tofauti tofauti za mashairi k.m. ukara

3. Ubeti/beti

  • Kifungu katika shairi kinachojitosheleza kimaaa

4. Mshororo

  • Mstari katika ubeti

5. Mwanzo

  • Mshororo katika ubeti

6. Mloto

  • Mshororo wa pili katika ubeti

7. Mleo

  • mshororo wa tatu katika ubeti

8. Kimalizio

  • Mshororo wa mwisho ambao haurudiwi katika kila ubeti

9. Kibwagizo/mkarara/kipokeo/kiitikio

  • Mshororo wa mwisho ambao hurudiwarudiwa katika kila ubeti na hubeba maudhui au kiini cha shairi.

10. Kipande/mgao

  • Sehemu katika mshororo ambayo huonyeshwa na koma na huwa na kina

11. Ukwapi

  • Kipande cha kwanza katika mshororo

12. Utao

  • Kipande cha pili katika mshororo

13. Mwandamizi

  • Kipande cha tatu katika mshororo

14. Mizani

  • Silabi zinazotamkika katika mishororo

15. Urari wa mizani

  • Kuwepo kwa idadi sawa ya mizani katika mishororo

16. Kina/vina

  • Silabi zinazotamkika kwa namna sawa zinazopatikana katikati na mwishoni mwa sentensi.

17. Urari wa vina/vue

  • Kuwepo kwa silabi zinazotamkika kwa namna sawa


Aina za Mashairi

  1. Mashairi ya arudhi/Ushairi wa kijadi
    • Ambayo huzingatia sheria za jadi za utunzi wa mashairi.
  2. Mashairi huru
    • Ambayo hayazingatii sheria za jadi za utunzi wa mashairi.

Mashairi ya Arudhi

  1. Aina 
    • tathmina (mshororo mmoja katika kila ubeti)
    • tathnia (miwili)
    • tathlitha (mitatu)
    • tarbia (minne)
    • takhmisa (mitano)
    • tasdisa (sita)
    • ushuri (kumi)
  2. Bahari
    • mtiririko (mfanano wa vina vya kati na vya mwisho katika shairi zima)
    • ukara (vina vya mwisho kufanana na vya kati kutofautiana)
    • ukaraguni (vina vya kati na vya mwisho kutofautiana katika shairi zima)
    • kikwamba (mishororo kuanza kwa neno fulani katika shairi zima)
    • pindu (neno au maneno mawili ya mwisho ya kila mshororo kutumiwa kuanzia mshororo unaofuata) k.m. kicha changu wachezea. Wachezea kichwa changu.
    • Tenzi/tendi (mgao mmoja, kina kimoja)
    • Mathnawi (migao miwili, vina viwili)
    • Ukawafi (migao mitatu, tumbuizo 8,8,8)
    • Ngonjera (majibizano)
    • Malumbano (kujinaki/kuonyesha ugwiji akimdunisha mshairi mpinzani ili kutaniana)
    • Msuko (mshororo wa mwisho mfupi kuliko inayotangulia)
    • Sakarani (mchanganyiko wa bahari)
    • Dura mandhuma (kauli/swali katika ukwapi na mjalizo/jibu katika utao k.m. shida zikishinda, hazishindiki. Unalolipenda, halipendeki. Unapopaenda, hapaendeki)
    • Gungu (mizani 12, kina kimoja cha mwisho)
    • Upeo (mishororo inayozidiana ki mizani)
    • Kikai (mizani 12, 4:8 au 8:4, hakuna ulinganifu wa mizani katika ukwapi na utao)
    • Zivindo (hutoa maana tofauti za neno k.m.
    • Sumbila (kila ubeti una kimalizio tofauti na beti nyingine)
  3. Muundo/Umbo/Sura ya Nje
    • Kutaja idadi ya beti
    • Mishororo mingapi katika kila ubeti
    • Vipande vingapi katika kila mshororo-aina
    • Mpangilio wa mizani na jumla k.m. ukwapi 8, utao 8, jumla 16.
      8 8
      8 8
      8 8
      8 8
    • Mpangilio wa vina au kufanana, kutofanana katika shairi zima au vina vya mwisho kufanana na vya kati kutofautiana-bahari

      na ma
      na ma
      na ma
      ka ba

      Vina na Mizani
      8a 8b
      8a 8b
      8a 8b
      8c 8b
    • Kibwagizo(linacho au halina. Kinakili kama kipo)
    • Majibizano (ngonjera)
    • Malumbano (majinaki)
  4. Uhuru/Idhini za Kishairi
    • kibali mshairi alichonacho kukiuka sheria fulani.
      1. Inkisari (kufupisha ili kuwe na urari wa mizani na vina. Aghalabu huonyeshwa kwa matumizi ya ritifaa k.m. ‘sikate-usikate)
      2. Mazda/mazida (kurefusha neno ili kuwa na urari wa mizani na vina)
      3. Tabdila (kubadilisha tahajia ya neno bila kuzidisha au kupunguza mizani k.m. siachi-siati)
      4. Utohozi - kuswahilisha maneno kutoka lugha nyingine k.m bratha, sekretari, kompyuta
      5. Kuboronga/kufinyanga sarufi (kubadili mpangilio wa maneno katika sentensi k.m. upesi jielimishe)
      6. Kiswahili cha kikale/ujadi (mtima, ngeu, insi, mja, ,maozi)
      7. Lahaja k.m. ficha-fita
      8. Matumizi ya ritifaa
  5. Lugha ya Nathari
    • lugha ya kawaida na kimtiririko
    • Kutotumia koma au vipande
    • Kutumia maumbo ya kawaida ya maneno
    • Ubeti kutengewa aya moja
    • Kuondoa uhuru na kusanifisha lahaja na kikale
  6. matumizi ya lugha/fani
  7. matumizi ya maneno (kama yalivyotumiwa)
  8. ujumbe
  9. maudhui
  10. dhamira
    • kusimanga, kusuta, kudharau, kusifu, kufunza, n.k.

Mashairi Huru

Sifa/Mbinu

  1. urudiaji
    • wa neno (takriri neno)
    • wa kifungu (usambamba)

      Umuhimu
    • kusisitiza ujumbe
    • kutia ridhimu/mapigo fulani katika usomaji
  2. mishata
    • mishtari ambayo haikamiliki. Mistari toshelezi ni mistari iliyokamilika.
  3. sehemu za beti kuingizwa ndani

    Umuhimu
    • ili kusisitiza
    • kuzifanya zionekane wazi


Ulinganishaji wa Shairi la Arudhi na Shairi Huru

Kufananisha

  1. yote mawili ni sanaa ya ushairi
  2. mishororo kupangwa katika beti
  3. yametumia mbinu za lugha za namna moja
  4. alama za kuakifisha zinazofanana
  5. kufanana kimuundo
  6. uhuru wa kishairi

Kutofautisha

  1. moja ni la arudhi jingine ni huru
  2. mishata
  3. sehemu za beti kuingizwa ndani
  4. kuwa au kutokuwa na urari wa mizani
  5. kuwa au kutokuwa na urari wa vina
  6. tofauti kimaudhui
  7. idadi ya beti
  8. idadi ya mishororo katika beti
  9. vipande
  10. kutumia alama za uakifishi tofauti
  11. uhuru wa kishairi
Join our whatsapp group for latest updates

Download Ushairi - Kiswahili Notes.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Read 13213 times Last modified on Monday, 16 November 2020 07:17
Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest