Pata mwongozo wote ama sehemu unayotaka kama PDF hapa!!
WhatsApp ama piga numbari hii uweze kupata kitabu hiki leo +254 703 165 909
Kuhusu kitabu
Bembea ya Maisha ni kitabu kinachotahiniwa katika shule za upili chini ya karatasi ya Kiswahili 3- 102/3.
Pia ni kitabu kilichowekwa cha lazima kwa shule za Sekondari za Kenya chini ya Kiswahili Fasihi.
Uchambuzi wa Bembea ya Maisha
Kitabu hiki kinazungumzia jinsi maisha yanavyoendelea kusonga mbele na kurudi nyuma kama bembea.
Kwa wale wasiofahamu, tafsiri ya neno bembea kwa kingereza ni 'swing'
Unakumbuka, kile kichezeo ulichozoea kukalia ulipokuwa mdogo na kuomba familia yako au rafiki akusukume ili uweze kuruka juu?
Ulipokuwa juu ulihisi kama unaweza kugusa anga.
Ulipokuwa nyuma ulilazimika kusukumwa mbele.
Hiyo ni angalau hadi ujifunze kujisukuma mbele kwa miguu yako unapokua.
Ahh, sasa umeifahamu?
Kama bado jua kuwa 'bembea' ni kifaa kama vile ubao, kamba au chuma inayoning'inia baina ya chuma au mti ambacho hutumiwa kuchezea aghalabu na watoto.
Kupitia wahusika mbalimbali kama Sara, Yona, Bunju, Neema na wengineo, mwandishi anatuonyesha na kutueleza jinsi wakati mwingine maisha yanavyoweza kujaa furaha na mara nyingine kujaa matatizo yanayosababisha maumivu na huzuni.
Kimsingi, maisha yana panda shuka zake. Wakati mwingine tuko juu na tunahisi kama tunaweza kugusa anga na wakati mwingine tuko chini.
Direct translation -> Basically, life has ups and downs. Sometimes we are up and we feel like we can touch the sky and other times we are back (down).
Mwandishi kwa kutumia sitiari ya bembea pia anatuambia jinsi wakati mwingine kama tu wakati wa kubembea tunahitaji msaada.
Msaada kwa namna ya mtu wa kutusukuma mbele ili bembea letu lisikae palepale.
Dhamira huelezwa kama lengo au shabaha ya mwandishi wa kazi ya fasihi.
Mwandishi wa tamthilia ya Bembea ya Maisha anadhamiria:
Kuonyesha masaibu ya pombe katika maisha ya familia
Kuonyesha kuwa ili kujenga jamii mpya, mapinduzi ni muhimu na ni lazima wanajamii wajitolee kupinga tamaduni zisizo na umuhimu wowote katika maisha ya wanajamii
Kutuonyesha kuwa watoto wa jinsia zote ni sawa na hawafai
Kutenganishwa kwa mila na tamaduni za jamii
Kutuonyesha kuwa hakuna lililo na mwanzo lisilokuwa na mwisho.
Maswali ambayo unaweza kujibu kwa kutumia mwongozo wa Bembe ya Maisha uliotayarishwa na Easy Elimu:
Nafasi ya mwanamke katika Bembea ya Maisha
Eleza ufaafu wa anwani Bembea ya Maisha
Sifa za Yona katika Bembea ya Maisha
Sifa za Neema katika Bembea ya Maisha
Sifa za sara katika Bembea ya Maisha
Sifa za dina katika Bembea ya Maisha
Kinaya katika Bembea ya Maisha
Haya ni baadhi tu ya maswali ya Bembea ya Maisha ambayo unaweza kupata majibu yake
Hitimisho
Mwongozo huu unatoa uchambuzi kamili wa riwaya ya Bembea ya Maisha ambayo hakika itawasaidia wanafunzi kupata alama nzuri linapokuja suala la maswali ya mitihani inayohusu riwaya hiyo.