Print this page

KISWAHILI KARATASI YA 3 - 2019 KCSE Prediction Maswali Set 1

Share via Whatsapp

MAAGIZO

  • Jibu maswali manne.
  • Swali la kwanza ni la lazima
  • Chagua maswali mengine matatu kutoka kwa sehemu zilizosalia:

Riwaya, Tamthilia, Hadithi fupi na Ushairi.

  • Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.

SEHEMU YA  A

  1. SWALI LA LAZIMA
    1.  
      1. Semi nini? (alama 1)
      2. Fafanua sifa nne za misimu (alama 4)
    2. Soma wimbo ufuatao kisha ujibu maswali

      Ewe kilizi
      Ulozowea kujificha
      Nyuma ya mama kujikinga, dhidi ya milio
      Yanadi ilo juu mbinguni
      Jua kesho ni siku ya siku
      Siku ya kujua mbivu na mbichi
      Kutofautisha jogoo na vipora
      Na riba takaposhika, chake kisu
      Ndipo utakapojua bayana
      Ukoo wetu si wa kunguru
      ikiwa hutayari
      kisu kukidhihaki
      sithubutu kamwe, wanjani kuingia
      sije kuniaibisha miye, amiyo na akraba nzima!

      Maswali

      1. Huu wimbo huitwaje? (alama 1)
      2. Eleza majukumu yoyote manne yanayotekelezwa na wimbo huu katika jamii (alama 4)
    3.  
      1. Mivigha ni nini? (alama 2)
      2. Eleza sifa tatu za mivigha (alama 3)
    4. Fafanua matatizo matano ambayo yanaikumba fasihi simulizi duniani (alama 5)

SEHEMU YA  B

RIWARA: CHOZI LA HERI: ASUMPTA MATEI

  1. “…haifai kucheza na uwezo wavijana, wao ni kama nanga. Huwezi kuzamisha na kuiongea merikebu.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
    2. Bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumika katika dondoo (alama 4)
    3. Kwa kurejelea riwaya hii, onyesha jinsi vijana wamezamisha merikebu ya wahafidhina. (alama 12)
  2. Baada ya dhiki faraja. Onyesha vile ukweli wa methali hii unavyodhihirika kwenye riwaya. (alama 20)

SEHEMU YA  C

TAMTHILIA: KIGOGO: PAULINE KEA

  1. “Sitaki kuaibishwa na mwanamke mimi, siwezi.”
    1. Yaweke maneno haya katika muktadha wake. (alama 4)
    2. Fafanua kwa hoja nane kuwa msemaji wa maneno haya anafaa kuaibishwa     (alama 16)
  2.  
    1. Jadili jinsi kumi ambazo kwazo maudhui ya ukatili yanajitokeza katika tamthilia ya Kigogo (alama 10)
    2. Eleza mifano mitano ya matumizi ya kinaya katika tamthilia ya Kigogo (alama 10)

SEHEMU YA D : HADITHI FUPI

TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI NYINGINE

  1. Eleza nafasi ya vijana katika jamii ukirejelea hadithi fupi zifuatazo.
    1. Mapenzi ya kifaurongo (alama 5)
    2. Shogake Dada ana ndevu (alama 5)
    3. Mame Bakari (alama 10)
  2. Ndoto ya mashaka: Ali Abdalla Ali
    “Sasa nimechoka mja. Nimechoka hata naradua kufa kuliko kuishi. Hadi lini haya mashaka ya kutengenezwa? Mashaka ya mashaka!
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
    2. Tambua mbinu mbili za lugha zilizotumika (alama 4)
    3. Fafanua mambo sita yanayomfanya mrejelewa aradue kufa. (alama 12)

SEHEMU YA E: USHAIRI

  1. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

    Barabaraba do ni ndefu
    Nami tayari nimecho katiki
    Natama ni kuketi
    Ni’nyooshe misuli
    Nitulize akili

    Lakini

    Azma ya nisukuma
    Mbele ikinihimiza kuendelea
    Baada ya miinuko na kuruba
    Sasa naona unyoofu wake
    Unyoofu ambao unatisha zaidi

    Punde natumbukia katika shimo
    Nahitaji siha zaidi ili kupanda tena
    Ghafla nakumbuka ilivyosema
    Ile sauti zamani kidogo
    “Kuwa tayari kupanda na kushuka”.

    Ingawa nimechoka
    Jambo moja dhahiri
    Lazima hufuate barabara
    Ingawa machweo yaingia
    Nizame na kuibuka
    Nipandenakushuka

    Jambo moja na kumbuka; Mungu
    Je nimwombe tena? Hadi lini?
    Labda amechoshwa na ombaomba zangu
    Nashangaa tena!
    Kitu kimoja na kiamini
    Lazima niendelee kujitahidi kwa kila hatua mpya
    Nijikokote kuiandama hii barabara yenye ukungu
    Nikinaswa na kujinasua
    Yumkini nitafika mwisho wake
    Ikiwa wangu mwisho haitauwahi kabla.

    Maswali

    1. Taja naueleze aina ya shairi hili (alama 2)
    2. Eleza toni ya shairi hili (alama 2)
    3. Huku ukitoa mifano mwafaka eleza tamathali tatu za usemi ambazo zinajitokeza katika shairi (alama 3)
    4. Mshairi ametumia uhuru wake wa utunzi. Eleza mifano mitatu huku ukitolea mifano. (alama 3)
    5. Fafanua dhamira ya mtunzi wa shairi hili (alama 2)
    6. Andika kifungu cha mwisho katika lugha ya nathari. (alama 4)
    7. Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi (alama 4)
      1. Kuruba
      2. Siha
      3. Machweo
      4. Kujinasua
Join our whatsapp group for latest updates

Download KISWAHILI KARATASI YA 3 - 2019 KCSE Prediction Maswali Set 1.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Read 29988 times Last modified on Tuesday, 21 May 2019 07:36

Related items

Get on WhatsApp Download as PDF