Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Sukellemo Joint Mock 2020/2021

Share via Whatsapp

MTIHANI WA PAMOJA WA SUKELLEMO
KISWAHILI
KARATASI YA 1
INSHA
Muda: Saa 1 ¾

MAAGIZO

  • Andika insha mbili. Swali la kwanza ni la lazima.
  • Kisha chagua insha nyingine moja kutoka kwa hizo tatu zilizobakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400.
  • Kila insha ina alama 20.
  • Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili
  1. Andika wasifu utakaosoma katika sherehe ya kuadhimishwa kwa siku ya mashujaa katika jimbo lenu kuhusu shujaa unayemuenzi.
  2. Mchakato wa kisiasa umeleta madhara mengi nchini. Jadili kauli hii.
  3. Andika kisa kitakacho dhihirisha maana ya methali ifuatayo: Dudu liumalo silipe kidole.
  4. Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo: ...Nilimtazama kwa muda punde tu aliponikaribia. Nikajisemea kimoyomoyo, Hili haliwezi kukubalika.

MAAKIZO

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. Mwanafunzi azingatie muundo wa wasifu;
    1. Kichwa
      • Kitaje wasifu ni wa nani, iandikwe kwa herufi kubwa na kupigiwa mstari
    2. Mwili
      • Maelezo ya kibinafsi kuhusu anayesifiwa mfano majina yake kamili, alikozaliwa, alikosomea, wazazi au familia yake n.k
        Mambo mengine kumhusu ,matendo aliyotenda, ushindi wake n.k
    3. Hitimisho
      • Mwanafunzi ahitimishe kwa kutoa kauli ya mwisho kuhusu umaarufu wa anayeandikiwa wasifu na sababu za kuhitaji utambulisho.
      • Maudhui katika mwili wa insha yatiririke kiwakati
      • Wasifu uandikwe kwa wakati uliopita kwa sababu yanayosimuliwa huwa yamefanyika tayari.
      • Mwanafunzi atumie nafsi yan tatu umoja.
      • Wasifu uwe wa kuvutia kwa KUZINGATIA SABABU ZA MHUSIKA KUWA SHUJAA na kutoa mifano ya mambo maarufu yaliyotendwa na mhusika.
      • Mambo hasi ambayo yanaweza kumwathiri au kumwaibisha mhusika yaachwe.
    4. TANBIHI
      • Akitumia nafsi ya kwanza amepotoka apewe 03
      • Akitumia hotuba kama sura atuzwe maudhui na atolewe maki nne za sura
      • Maudhui yake yazingatie kwa nini mhusika ni shujaa

  2. Mchakato wa kisiasa umeleta madhara mengi nchini. Jadili kauli hii.
    1. Kiuchumi - umezorota
    2. ukabila–mauaji
    3. ukoloni mamboleo – wale wanaotawala wananyanyasa watu
    4. ukosefu wa miundomsingi
    5. utabaka – jamii kugawika
    6. uchochezi kupitia kwa wafuasi wa viogozi hasa vijana
    7. ufisadi – umekithiri kwa vile wezi wanafichwa
    8. uhalifu
    9. maendeleo kuegemea sehemu fulani za nchi na kusahau wengine
    10. ubadhinifu wa mali – hela nyingi kutumika kwa siasa badala ya kusaidia wananchi
    11. sera potovu

  3. Hii ni insha ya methali; ukiona mahali kuna hatari /jambo linaloweza kukudhuru usikaribie
    Insha hii ina sehemu mbili;
    1. Dudu liumalo - hatari ya aina yoyote ile
    2. Silipe kidole – tahadhari

  4.    
    1. Kisa kioane na mdokezo uliopewa.
    2. Kisa kisimuliwe katika nafsi yoyote
    3. Lazima kisa kisimulie tendo / tukio ambalo msemaji aliliona na halikubaliki katika jamii yake kama vilemitindo ya mavazi, ulevi/dawa za kulevya, mahusiano yasiyokubalikahali ya anayerejelewa n.k.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Sukellemo Joint Mock 2020/2021.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest