Maagizo
- Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
- Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
- Kila insha isipungue maneno 400.
- Kila insha ina alama 20.
- Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
- Lazima:
Wewe ni mwakilishi wa vijana katika gatuzi lenu. Kumekuwa na tuhuma za vijana kutumia vibaya simu tamba katika jamii. Andika mahojiano yako na mwanahabari ukitetea namna simu tamba inavyowafaidi vijana. - Fafanua umuhimu wa kudumisha amani nchini wakati wa kampeni na uchaguzi wa kisiasa.
- Andika insha inayooana na methali mchuma janga hula na wa kwao.
- Andika insha itakayoisha kwa maneno yafuatayo:
….nilipogutuka niliangaza macho huku na kule. Aah! Kumbe nilikuwa nikiota!
MARKING SCHEME
- Hii ni insha ya mahojiano. Ichukue mtindo wa tamthilia.
kumb: mwanahabari ndiye anayehoji.
Baadhi ya hoja ni kama vile:- Kuleta vijana pamoja duniani na hivyo kupunguza tuhuma zinazoelekea kuleta vurugu kutokana na vijana kutofahamiana
- Usambazaji wa teknolojia inayorahisisha maisha ya vijana kote duniani kupitia kwa huduma zinazotolewa na simu.
- Kuendeleza biashara - kubadilishana bidhaa na pesa kupitia mtandao kama vile MPESA.
- Hurahisisha huduma za benki. Vijana wanaweza kufikia akaunti zao kupitia kwenye rununu.
- Huwa na vifaa kama vile vikokotoo vya kurahisisha kufanya hesabu.
- Ni chombo cha burudani - vijana hupata michezo mbalimbali.
- Huimarisha utafiti. Vijana wanaweza kufanya utafiti kupitia kwenye rununu.
- Huweza kutumiwa kupigia picha, hivyo kuokoa pesa ambazo zingenunulia kamera au video.
- Vijana wanaweza kuwasiliana na familia zao kutoka mbali, hivyo kuokoa muda na fedha ambazo wangetumia kusafiri.
- Vijana wnaweza kuhifadhi msahafu(Biblia au Korani) kwenye simu, hivyo kujikuza kiroho kila mara.
- Ni njia ya kupata habari kutoka kwenye mashirika ya usambazaji wa habari. Baadhi ya rununu zina redio na hata runinga. Vijana wanaweza kusikiliza na kutazama habari hata wakiwa safarini.
- Hufanikisha kuwanasa matapeli na magaidi wanaowadhuru vijana. Baadhi ya rununu huonyesha simuilipopigiwa hivyo kusaidia kudhibiti mitandao ya uhalifu.
- Hii ni insha ya ufafanuzi. Mwnafunzi asipinge swali.
Hoja ni kama vile:- kudumisha umoja na upendo wa wananchi
- kuwezesha wananchi kuendeleza biashara zao hivyo kujipatia mapato na kukuza uchumi wa taifa.
- kuwawezesha wanasiasa kuuza sera zao bila kutatizika
- kuhakikisha usalama wa wananchi
- kuendeleza uzalendo kwa kutii sheria na katiba
- kuwavutia wawekezaji wa kigeni
- kuzuia uharibifu wa mali
- kuwezesha masomo kuendelea shuleni
- kuwezesha usafirishaji na usambazaji wa bidhaa
- Mchuma janga hula na wa kwao
- Hii ni insha ya methali
- Chuma ni kufanya kazi na kupata faida/ tungua matunda kutoka mtini.
- Janga-balaa /baa / shida / hatari / taabu
- Ajitafutiaye shida huathirika na jamii / jamaa yake .
- Mtahiniwa asimulie kisa /visa vitakavyoafikiana na methali.
- Asipinge methali.
Ruwaza zifuatazo zinaweza kujitokeza;- Mhusika kushiriki raha za kilimwengu, akaambukizwa magonjwa yasiyotibika,hatimaye anarejea nyumbani anakougua , mzigo wa kumtunza unakuwa kwa familia yake.
- Mhusika aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni au shirika fulani, Anafutwa kazi labda kutokana na uzembe au utovu wa maadili ya kikazi,anarejea nyumbani kwa familia yake; kule hana chochote hivyo basi anaishia kutegemea jamma zake, huu unakuwa mzigo mkubwa kwa watu wake.
- Mtoto ambaye anatokea kuwa mhalifu, anafikishwa kortini na kutozwa faini kubwa.Hii inakuwa gharama kwa familia yake kwa vile ndio wanaotakiwa kulipia.
- Mwanafunzi ambaye anakosa kuwajibika masomoni shuleni , anafeli mtihani, maisha ya halafu yanakuwa magumu kwa hivyo jamaa zake wanalazimika kuingilia kati ili kumuauni kwa mahitaji ya kila siku
- na kadhalika
- Ni insha ya kubuni fikra
- Azingatie sehemu zote kv utangulizi, mwili, hitimisho.
- Mtahiniwa atunge kisa kinachomalizia kifungu kilichotolewa.
- Azingatie sehemu zote kv utangulizi, mwili, hitimisho.
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - KCSE 2022 Mock Exams Set 1.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students