Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Kakamega Evaluation Mock Exams 2022

Share via Whatsapp

MASWALI

  1. Lazima
    Wewe ni Mwenyekiti wa Tume ya kupigana na ufisadi nchini. Umealikwa kuhutubia magavana kuhusu athari za ufisadi huku ukipendekeza hatua za kukabiliana na jinamizi hili. Andika hotuba utakayoiwasilisha.
  2. Mitandao ya kijamii ina madhara mengi kuliko faida. Jadili.
  3. Andika kisa kitakachodhihirisha maana ya methali: Achezeaye tope humrukia.
  4. Andika insha itakayoanza kwa maneno yafuatayo:
    Mara nilisikia ukemi mkali kutoka nje. Majibwa yalibweka kwa mfululizo kana kwamba yanasemezana…


MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. Hii ni insha ya hotuba. Muundo ufuatao uzingatiwe.
    1. Kichwa/Mada/Anwani ya hotuba km. Hotuba kuhusu Athari za ufisadi na jinsi ya kukabiliana nao. (Anwani iandikwe kwa herufi kubwa na kisha ipigiwe mstari.
    2. Utangulizi 
      • Itifaki izingatiwe katika kuwatambua watu muhimu waliopo.
      • Mhutubi ajitambulishe kwa hadhira yake na lengo la hotuba yake.
      • Pawe na maamkizi.
      • Alama za mtajo zaweza kutumiwa mwanzoni mwa hotuba na mwisho mwa hotuba ama zisitumiwe.
    3. Mwili
      • Hii ni sehemu ya maudhui/hoja.
      • Athari za ufisadi zitajwe na kufafanuliwa ipasavyo na kisha mapendekezo yatolewe.
    4. Hitimisho
      • Mhutubi atoe shukrani kwa hadhira yake kwa kutenga muda wao ili kumsikiza.
      • Atilie mkazo kiini cha hotuba yake.
        Athari za ufisadi
      • Ukosefu wa dawa hospitalini.
      • Ujenzi duni wa barabara nchini.
      • Kuongezeka kwa ajali barabarani.
      • Watu kupewa ajira ambazo hawajasomea na kusababisha huduma mbovu.
      • Mijengo kuporomoka na kusababisha mauti na hasara .
      • Nchi kufifia kiuchumi.
      • Taifa kuwa na sifa hasi ughaibuni.
      • Pengo kati ya matajiri na maskini kupanuka zaidi.
      • Nchi kunyimwa msaada na mataifa/mashirika ya ufadhili (kadiria hoja za mtahiniwa
        Mapendekezo
      • Kupiga kalamu mafisadi.
      • Kufungwa gerezani.
      • Faini kubwa kwa mafisadi.
      • Kutowaruhusu mafisadi kuwania kiti chochote cha uongozi.
      • Mali iliyopatikana kifisadi itwaliwe na serikali.
      • Umma kuhamasishwa athari za ufisadi kupitia vyombo vya habari.
      • Somo kuhusu maadili lifunzwe katika shule za msingi, upili na hata vyuo vikuu. (kadiria hoja za mtahiniwa.
  2. Swali la mjadala/mdahalo.
    • Mtahiniwa aunge mkono mada kwa kutoa hoja nyingi zinazoonyesha madhara ya mitandao kisha atoe hoja chache za faida. 
    • Mtahiniwa apinge mada kwa kutoa kutoa hoja nyingi za faida na chache za hasara.
    • Mtahiniwa atakayezungumzia upande mmoja tu k.m. Faida na akose kutoa hasara, asipite C+ 10.
      Hasara za mitandao
    • Inaendeleza utapeli k.m Umeshinda katika mchezo wa bahati nasibu na kumbe ni ulaghai.
    • Inaendeleza wizi wa mitihani ya kitaifa nchini.
    • Imezorotesha utamaduni wa kiafrika k.m mavazi.
    • Unaendeleza uozo k.m. ponografia.
    • Matendo ya kihalifu hupangwa kupitia mitandao hii.
    • Watu hupoteza fedha zao zilizo katika akaunti zao kupitia mitandao hii. (kadiria hoja za mtahiniwa.)
      Faida za mitandao
    • Imerahishisha mawasiliano.
    • Imenawirisha biashara.
    • Ulipaji nauli umerahisishwa.
    • Nafasi za ajira zimebuniwa.
    • Imeendeleza utafiti wa kimasomo na kisayansi.
    • Upashaji wa habari umerahisishwa.
    • Mambo muhimu huhifadhiwa kwa mitandao hii.
    • Wanaosaka ajira hujuzwa sehemu zilizo na nafasi za kazi. 
      (kadiria hoja za mtahiniwa).
  3. Swali la methali
    • Achezeaye tope humrukia.
    • Maana: Mtu anayechezea tope huishia kuchafuliwa nalo.
    • Matumizi: Methali hii huwakanya watu dhidi ya kuandamana au kuhusiana na watu wenye sifa mbaya. Anayehusiana na mtu mbaya huishia kuambukizwa ubaya huo.
    • Mtahiniwa atunge kisa kinachodhihirisha matumizi haya.
  4. Insha ya mdokezo.
    • Mtahiniwa aonyeshe mtu/watu waliokuwa taabani nje na hatua aliyoichukua kuwanusuru.
    • Mtahiniwa azingatie nafsi ya kwanza umoja.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Kakamega Evaluation Mock Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?