Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Mathioya Mock Exams 2022

Share via Whatsapp
Maswali
 
Maagizo
  • Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
  • Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400.
  • Kila insha ina alama 20.
  • Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
  • Insha zote sharti ziandikwe katika nafasi ulizoachiwa katika kijitabu hiki cha maswali.
  • Kurasa zote zimepigwa chapa.
 
  1. Wewe ni katibu wa jopokazi lililoteuliwa kuchunguza athari za mikopo ya kifedha inayochukuliwa na serekali kutoka mataifa ya kigeni. Andika kumbukumbu za uchunguzi huo.        Alama 20
  2. Andika insha kuhusu umuhimu wa hazina ya ustawishaji wa maeneo bunge.     Alama 20
  3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo :         alama 20
    Pang’okapo jino pana pengo
  4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa
    ...... milio ya manusura wenzangu ilihanikiza ukumbi wa shule na kuyaziba masikio ya waombolezaji.         Alama 20

Mwongozo wa Kusahihisha

  1. Wewe ni katibu wa jopokazi lililoteuliwa kuchunguza athari za mikopo ya kifedha inayochukuliwa na serekali kutoka mataifa ya kigeni. Andika kumbukumbu za uchunguzi huo. Alama 20
    1. Inasababisha uoga mionkgoniu mwa wananchi kuwa watakuwa watumwa wa mataifa na mashirika haya.
    2. Mikopo huja na masharti ambayo yanaumiza kwa vile hayafaidi taifa letu. Kwa mfano kuwaajiri wafanyakazi kutoka nje kama China.
    3. Huenda mikopo hii ikailemea taifa letu.
    4. Biashara zetu na mataifa haya zitaathirika – zikakosa faida. Kwa vile mataifa haya , huenda yakawa yananunua bidhaa zetu kwa bei watakayo – hivyo sisi ndio tutawahitaji zaidi
    5. Kutawaliwa na mataifa au mashirika ya kifedha. Kwa mfano, masharti tutakayowekewakama kupunguzaidadi ya wafanyakazi wa serekali ilhali idadi ya watu inaendelea kuongezeka.
    6. Kuingilia uhuru wetu wa kibiashara pale ambapo wananchi wa mataifa hayo na mashirika yao ya kifedha wataanza kufanya biashara zinazotakikana kufanywa na wenyeji.
    7. Asilimia kubwa ya mapato yetu itagharamia ulipaji wa mikopo na kutuacha tukiwa wategemezi wa mashirika na mataifa hayo.
    8. Inachangia ukoloni mambo leo
    9. Inaleta utegemezi mkubwa wa taifa.
    10. Kupandisha gharama ya maisha kwa wananchi
    11. Kudunisha dhamana ya shilingi
    12. Uhamiaji wa wasomi na wawekezaji katika nchi zingine zilizo na sera nzuri za kibiashara na utendakazi
    13. Kuanguka kwa mashirika ya kibinafsi na ya kiserikali kutikana na bidhaa zinazotoka nje ya nchi kwa bei nafuu
  2. Andika insha kuhusu umuhimu wa hazina ya ustawishaji wa maeneo bunge.  Alama 20
    1. Hazina hii inatumika kuimarisha na kustawisha miradi na miundo msingi katika nchi nzima - mathalani maji ya mabomba
    2. Kustawisha elimu – inatumika kulipia karok w awatoto mayatima na kuwasaidia wanafunzi hawa kuhitimisha masomo yao
    3. Wazazi wamepungukiwa na mzigo wa ujenzi wa shule. Wanaweza kushughhulikia watoto wao ipasavyo katika mahitaji mengine kama malazi na makazi.
    4. Uchukuzi kulahisishwa kwa vile barabara zimeboreshwa hivyo kupunguza hasara kutokana na barabara mbovu
    5. Kuleta maendeleo kwa wanajamii- kama vile kufadhili mradi wa kusabazwa kwa umeme
    6. Kuanzisha nafasi za kazi hasa katika sekta ya juakali
    7. Kuinua na kuboresha kiwango cha maisha ya wananchi kwa kuwaletea huduma karibu na wanakoishi kama vile ofisi za chifu
    8. Imeimarisha afya kwa kujenga vituo vipya vya afya kote nchini.
  3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo : alama 20
    Pang’okapo jino pana pengo.
    Methali hii ilenge kisa kitakachoonyesha umuhimu wa:
    1. Mzazi baada ya kuondoka mfano kufa
    2. Umuhimu wa serikali iliyojishughulisha na wananchi inapoondoka na nyingine kuchaguliwa isiyoshughulika
    3. Kupoteza kazi na baadaye kuteseka
    4. Kupatwa na ajali napengine kupoteza kiungo cha mwili kama vile uwezo wakutembea
  4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa
    ..... milio ya manusura wenzangu ilihanikiza ukumbi wa shule na kuyaziba masikio ya waombolezaji. Alama 20
    Kisa hiki kifanyike katika mazingira ya shuleni
    1. Visa vinaweza kutokana na :
    2. Kisa cha moto uliotokea bwenini na kuwaumiza wanafunzi
    3. Kisa cha mjengo ulioporomokla shuleni
    4. Kisa cha shambulizi la kigaidi lililotokea shuleni
    5. Choo ambacho kilichozama wanafunzi wakiwa ndani.
    6. Tukio la ambukizo la ugonjwa hatari wa Korona uliosambaa na kuwaumiza wengi
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Mathioya Mock Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?