Click the link below to download as a full set with all the subjects.
https://downloads.easyelimu.com/details/32-Maranda_High_School_2018_Form_1_End_Term_1_Past_Papers
KISWAHILI
KARATASI MSETO
SAA 2

SHULE YA UPILI YA MARANDA
KISWAHILI KIDATO CHA KWANZA
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA 1, 2018
Maagizo
- Jibu maswali yote katika nafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia Kiswahili sanifu
- Makosa ya tahajia na sarufi yataadhibiwa
1. MATUMIZI YA LUGHA (alama 40)
- Tambua sauti zifuatazo: (alama 3)
- Irabu ya nyuma wastani.
- Irabu ya kati tandazwa.
- Kikwamizo sighuna cha ufizi.
-
- Huku ukitoa mfano mwafaka, eleza dhana silabi wazi. (alama 2)
- Eleza muundo wa silabi katika neno tafrija. (alama 2)
- Kanusha:
Mtoto anaimba na kucheza -
- Eleza maana ya shadda. (alama 2)
- Wekea shadda maneno yafuatayo: (alama 2)
Karatasi............
Nzi...................
- Geuza kwa udogo: (alama 2)
Mti ule ulianguka baada ya mvua kubwa. - Andika sentensi ifuatayo katika hali ya wingi: (alama 2)
Popo aliruka akatua mgombani. - Sahihisha: (alama 2)
Tulipofika nyumbani tulimkuta hayuko. - Andika maana mbili tofauti za neno: panda. (alama 2)
- Tunga sentensi kudhihirisha matumizi ya ngeli U-I (alama 2)
- Bainisha maneno katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
Msichana mrembo ataleta machache - Sabalkheri ni salamu za asubuhi. Jibu lake ni... (alama 1)
-
- Eleza maana ya mzizi. .(alama 2)
- Onyesha mizizi ya maneno yafuatayo:
Mdharaulifu..
Kuombea..
- Eleza maana ya methali: mgaagaa na upwa, hali wali mkavu. (alama 2)
- Bainisha viambishi katika neno: atampikia. (alama 3)
- Tambua aina za sentensi zifuatazo kutokana na kiimbo: (alama 3)
- Watu wanakula nyoka.
- Watu wanakula nyoka?
- Watu wanakula nyoka!
- Kamilisha tanakali zifuatazo. (alama 2)
Shillingi huanguka mchangani......................na Tom amejifunika...........
2. FASIHI SIMULIZI (ALAMA 20)
