Kiswahili Questions and Answers - Form 2 Mid-term Exams Term 1 2022

Share via Whatsapp

MASWALI

Maagizo: Jibu maswali yote katika nafasi zilizoachwa baada ya kila swali.
Sehemu A (Alama 20)

  1. Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya maneno yafuatayo: (alama 2)
    1. bali
    2. mbali
  2. Taja aina mbili za mofimu na utolee mfano kwa kila moja. (alama 2)
  3. Andika kwa wingi: (alama 1)
    Gaidi alipigwa risasi na askari aliyekuwa akilinda doria.
  4. Taja aina nne za nomino. (alama 2)
  5. Ni nomino gani isiyochukuana na nyingine? (alama 1)
    Kumbi, paa, kubeta, kuta, mlango.
  6. Tegua vitendawili vifuatavyo: (alama 2)
    1. Abeba mishale kila anapoenda.
    2. Ana meno lakini hayaumi.
  7. Tumia kivumishi cha sifa katika mabano kukamilisha sentensi ifuatayo. (alama 1)
    Bei ya meli ni ………… mno (ghali).
  8. Jaza pengo kwa kiulizi mwafaka: (alama 1)
    Ni muundo ………………… uliotumiwa?
  9. Ziandike upya sentensi zifuatazo ukitumia kiwakilishi cha pekee –ote. (alama 2)
    1. ……………………. Kilivunjika kilipoanguka.
    2. …………………….. ulipasuliwa.
  10. Geuza sentensi hii iwe katika wingi: (alama 2)
    Mwanzi alioupanda karibu na mto umeshikana ukawa msitu mkubwa.
  11. Tumia vitenzi vishirikishi vipungufu kukamilisha sentensi zifuatazo: (alama 2)
    1. Kipya kinyemi …………… kidonda.
    2. Mungu …………. wa kuabudiwa milele.
  12. Taja aina mbili za vielezi namna. (alama 2)

SEHEMU B
ISIMUJAMII

  1. Fafanua sifa tano za rejista ya kituo cha polisi. (alama 5) 
    FASIHI SIMULIZI
  2. Taja njia tano za kumalizia hadithi. (alama 5)

MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA

Maagizo: Jibu maswali yote katika nafasi zilizoachwa baada ya kila swali.
Sehemu A (Alama 20)

  1. Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya maneno yafuatayo: (alama 2)
    1. bali
    2. mbali
      Wasafiri walinyeshewa bali waliendelea na safari hiyo ya mbali.
      (mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi)
  2. Taja aina mbili za mofimu na utolee mfano kwa kila moja. (alama 2)
    • Mofimu huru- baba
    • Mofimu tegemezi- mtoto
      (mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi)
  3. Andika kwa wingi: (alama 1)
    • Gaidi alipigwa risasi na askari aliyekuwa akilinda doria.
      Magaidi walipigwa risasi na askari waliokuwa wakilinda doria.
  4. Taja aina nne za nomino. (alama 2)
    • Nomino za kawaida
    • Nomino za pekee
    • Nomino za wingi
    • Nomino dhahania
    • Nomino za wingi
    • Nomino za vitenzi jina.
  5. Ni nomino gani isiyochukuana na nyingine? (alama 1)
    • Kumbi, paa, kubeta, kuta, mlango.
      Kubeta
  6. Tegua kitendawili vifuatavyo: (alama 2)
    1. Abeba mishale kila anapoenda- nungunungu
    2. Ana meno lakini hayaumi- kitana
  7. Tumia kivumishi cha sifa katika mabano kukamilisha sentensi ifuatayo. (alama 1)
    • Bei ya meli ni ghali mno.
  8. Jaza pengo kwa kiulizi mwafaka: (alama 1)
    • Ni muundo …gani/ upi……………… uliotumiwa?
  9. Ziandike upya sentensi zifuatazo ukitumia kiwakilishi cha pekee –ote. (alama 2)
    1. …………chote…………. kilivunjika kilipoanguka.
    2. ……………wote……….. ulipasuliwa.
  10. Geuza sentensi hii iwe katika wingi: (alama 2)
    • Mwanzi alioupanda karibu na mto umeshikana ukawa msitu mkubwa.
      Mianzi waliyoipanda karibu na mito imeshikana ikawa misitu mikubwa.
  11. Tumia vitenzi vishirikishi vipungufu kukamilisha sentensi zifuatazo: (alama 2)
    1. Kipya kinyemi ……ki……… kidonda.
    2. Mungu ……yu/ni……. wa kuabudiwa milele.
  12. Taja aina mbili za vielezi namna.
    • Vielezi namna hali
    • Vielezi namna halisi
    • Vielezi namna vikariri
    • Vielezi namna viigizi
    • Vielezi ala/ vitumizi (alama 2)

SEHEMU B
ISIMUJAMII

Fafanua sifa tano za rejista ya kituo cha polisi. (alama 5)

  • Msamiati maalumu- afisa
  • Lugha legevu- hii kijana
  • Lugha ya unyenyekevu- samahani
  • Lugha ya kuamuru- njoo hapa
  • Lugha ya kudadisi- ulikuwa wapi?
    (mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi)

FASIHI SIMULIZI
Taja njia tano za kumalizia hadithi. (alama 5)

  • Hadithi yangu imeisha hapo.na wakaisha raha mustarehe.
  • Na huo ndio mwisho wa hadithi yangu.
  • Na hiyo ndiyo hadithi yangu.
  • Hadithi yangu ni hiyo.
  • Na wakaishi raha ustarehe.
    (mwalimu atathmini majibu ya wanafunzi)
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Form 2 Mid-term Exams Term 1 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest