KISWAHILI 102/1
INSHA
KARATASI YA 1
KIDATO CHA TATU
MAAGIZO:
- Andika Insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
- Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobaki.
- Kila insha isipungue maneno 400.
- Kila insha ina alama 20.
MASWALI:
- Wewe ni katibu wa kamati ya maslahi ya klabu ya wasanii chipukizi mtaa wa Rehema.
Andika kumbukumbu za mkutano uliofanywa hivi karibuni kujadili suala la usalama uliozorota. - Mfumo wa elimu nchini Kenya una kasoro nyingi na unafaa kufanyiwa mabadiliko. Eleza.
- Andika kisa kinachodhihirisha maana ya methali: Ujana ni moshi ukienda haurudi.
- Tunga kisa kinachomalizika kwa maneno haya: ‘……. Hapo ndipo iliponipambazukia kuwa
nilikuwa naogelea baharini pekee, kinyume na wenzangu wote.
MAAKIZO:
- Wewe ni katibu wa kamati ya maslahi ya klabu ya wasanii chipukizi mtaa wa Rehema.
Andika kumbukumbu za mkutano uliofanywa hivi karibuni kujadili suala la usalama uliozorota.- Hii ni insha ya kiuamilifu
- Sura ya kumbukumbu izingatiwe:
- Kuwe na anwani iliyo na mahali, tarehe na saa ya kufanyika kwa mkutano
- Orodha ya waliohudhuria
- Waliotumia udhuru
- Waliokosa kutuma udhuru
- Waalikwa wengine (wageni)
- Ajenda
- Maudhui yagusie yafuatayo:-
- Visa vya kuzorota kwa usalama kama vile ujangili, utekaji nyara, ujambazi, dhuluma mbalimbali kwa umma, uhalifu mtaani, mauaji, ubakaji, wizi km wa mifugo na mali ya watu
- Ataje wahasiriwa au wahusika
- Hatua za kudhibiti usalama k.v. mpango wa nyumba kumi.
- Mfumo wa elimu nchini Kenya una kasoro nyingi na unafaa kufanyiwa mabadiliko. Eleza.
- Insha hii ina upande mmoja wa hoja. Mwanafunzi apendekeze kwa kutoa maelezo kwa nini mfumo wa elimu unafaa kufanyiwa mabadiliko.
Hoja zinazopendekezwa:-- Masomo mengi hufanyikia darasani badala ya hali halisi maishani km viwandani, shambani au biasharani.
- Wanafunzi hawana muda wa kutosha kupumzika kwa kuwa masomo ni mengi
- Karo inayolipwa ni ya juu sana na wanafunzi maskini hawawezi kuimudu.
- Elimu ya sasa haizingatii maadili ya kiafrika bali huegemea maadili ya kizungu km kazi za ofisi, mavazi, vyakula, lugha.
- Shuleni wanafunzi ni wengi na kuwafikia kila mmoja ni vigumu haswa katika shule za umma.
- Masomo ya sayansi hayafanywi vizuri na idadi kubwa ya wanafunzi.
- Watoto wengi wanfikia drasa la nane bila uwezo wa kujieleza kwa kuandika na kuzungumza.
- Elimu ya sasa haizingatii mahitaji ya jamii tofauti km wafugaji, wakulima, wavuvi, walemavu na wanaoishi vibandani.
- Wanafunzi walio na vipawa na uwezo wa kipekee hawatiliwi maanani km wakimbiaji na walio werevu zaidi au wasioelewa kwa haraka.
- Insha hii ina upande mmoja wa hoja. Mwanafunzi apendekeze kwa kutoa maelezo kwa nini mfumo wa elimu unafaa kufanyiwa mabadiliko.
- Andika kisa kinachodhihirisha maana ya methali: Ujana ni moshi ukienda haurudi.
- Methali hii inatufunza kwamba jambo likishapita halirudi tena. Ni sawa na methali isemayo maji yakimwagika hayazoleki.
- Inatufunza kuwa iwapo tutapima mambo fulani maishani ambayo tunapaswa kuyatekeleza ili tunufaike maishani, tutajuta bila lolote la kufanya.
- Mwanafunzi azingatie kisa kinachoonyesha ukweli wa methali hii.
- Kisa kinaweza kuwa cha mtu asiyezingatia mashauri.
- Kusoma kwa bidii ili afaulu mtihani
- Kujihusisha mihadarati na baadaye kujutia madhara yake.
- Kijana anayeonywa na wakubwa wake aachane na vijana wapotovu lakini anapuuza.
- Kijana anayejihusisha na mapenzi kiholela na baadaye kupata maradhi ya zinaa au mimba za mapema.
- Tanbihi
- Kisa kisichooana na methali hii apewe alama 3
- Tunga kisa kinachomalizika kwa maneno haya: ‘……. Hapo ndipo iliponipambazukia kuwa nilikuwa naogelea baharini pekee, kinyume na wenzangu wote.
- Kisa lazima kimaliziwe na maneno ‘aliyopewa bila kutoa au kuongezea neno lolote.
- Pawe na mantiki ya kisa na maneno aliyopewa.
- Mnenaji asawiriwe akingangania kufanya jambo walipopatana na wenzake.
- Wenzake hawafanyi lile
- Ndiye tu anaye endelea na jambo hilo.
- Tanbihi
- Mtahiniwa asipomalizia maneno hayo amepotoka. Atuzwe alama 2.
- Atachukuliwa kuwa alijitungia swali lake mwenyewe.
- Tanbihi
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 End Term 3 Exams 2021.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students