Watch Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34
  • Home
  • Past Papers
  • High School Term Past Papers
  • Form 4 Past Papers
  • 2020 Form 4 Term 1 Past Papers Revision
  • BIOLOGY PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020

KISWAHILI PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - KISWAHILI PAPER 1 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020 BIOLOGY PAPER 1 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020 - Next »
Download PDF for future reference Install our android app for easier access
  1. UFAHAMU
    1. Ni dalili ipi inayoonyesha mwanzo wa mageuzi? (al.1)
    2. Mtaala mpya unalenga nini? (al.4)
    3. Eleza lawama zinazoelekezewa kikosi cha polisi (al.2)
    4. Kwa mujibu wa taarifa eleza mageuzi matatu yaliyofanywa katika kikosi cha polisi (al.3)
    5.  Taja makundi mawili yaliyohusika katika kuandaa mtalaa mpya (al.2)
    6. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu (al.3)
      1. Kubisha hodi
      2. Kukolewa
      3. Makurutu
  1. UFUPISHO
    1. Kwa maneno yasiyozidi 70, fupishsa aya za kwanza nne. (al.9)  Mtiririko alama 1
    2. Kwa nini serikali haitaweza kulipa madeni yake. (maneno 40-50) (al.6) Mtiririko alama 1
  1. SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (alama 40)
    1. Tambua sauti.
      Kipasuo ghuna cha kaakaa laini (al.1)
    2. Unda neno lenye muundo ufuatao wa sauti (al.1)
      KKKKI
    3. Eleza maana ya istilahi zifuatazo za sauti (al.4)
      1. Kiimbo
      2. Konsonanti mwambatano
    4. Tunga sentensi moja ukitumia neno –zuri kama kiwakilishi, kivumishi na kielezi (al.3)
    5. Eleza tofauti kati ya sentensi hizi (al.2)
      Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani.
      Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani
    6. Tunga sentensi moja sahihi itakayotumia vitenzi vifuatavyo (al.3)
      -wahi, -enda, -ona
    7. Huku ukitumia mifano mwafaka, tofautisha silabi wazi na silabi funge (al.2)
    8. Andika sentensi ifuatayo katika hali ya yakinishi (al.2)
      Wanafunzi wasiposoma kwa bidii hawatapita mtihani
    9. Bainisha vishazi katika sentensi ifuatayo (al.2)
      Gaidi aliyelipua guruneti ile ametiwa mbaroni
    10. Andika katika msemo wa taarifa: (al.2)
      “Wakazi wa eneo hili ni wafugaji stadi wa sungura” kakangu aliniambia.
    11. Bainisha aina za virai katika sentensi ifuatayo (al.3)
      Sheria hizo mpya zilitundikwa juu ya ukuta usiku wa manane.
    12. Unda nomino kutokana na vitenzi vifuatavyo (al.2)
      1. Sali
      2. La
    13. Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi (al.4)
      Jengo lijengwalo kwenye msingi thabiti hudumu sana.
    14. Andika katika kauli ya kutendesha (al.2)
      Amani alikunywa pombe mpaka akalewa sana
    15. Andika kwa udogo (al.2)
      Njia iendayo mbinguni ni nyembamba
    16. Neno changa lina maana ya kutoa kitu au fedha ili kukusanya kwa makusudi Fulani. Eleza maana zingine mbili (al.2)
    17. Taja nahau zingine mbili sawa na “Enda ahera” (al.2)
    18. Andika kwa wingi (al.1)
      Zigo la kuliwa halilemei
  1. ISIMU JAMII (alama 10)

    Soma kifungu kifuatacho halafu ujibu maswali.

    “Naona “Horsepower” mwenyewe ndiye atakayepiga, atakayecheza foul hiyo. Wachezaji wa……”

    1. Tambua sajili inayorejelewa (al.2)
    2.  Tambua sifa zinazobainisha sajili yenyewe (al.8)

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. UFAHAMU
    1. Ni dalili ipi inayoonyesha mwanzo wa mageuzi? (al.1)
      • Kuzinduliwa kwa mtaala mpya wa kutoa mafunzo kwa maafisa wa polisi 1x1=1
    2. Mtaala mpya unalenga nini? (al.4)
      • Kuimarisha utendakazi katika kikosi ambacho kwa muda mrefu kimelaumiwa kwa kulowa ufisadi na uvunjaji wa haki za kimsingi
      • Unaashiria mwanzo wa mageuzi makubwa yanayonuiwa kukipatia kikosi hicho sura mpya
      • Kuwapa maafisa wa polisi mafunzo mapya
      • Kuunda kikosi imara chenye nidhamu na kinachoheshimu haki za kibinadamu 4x1 = 4
    3. Eleza lawama zinazoelekezewa kikosi cha polisi (al.2)
      • Ukosefu wa nidhamu
      • Kutoheshimu haki za binadamu/kimsingi
      • Kukolea kwa ufisadi
    4. Kwa mujibu wa taarifa eleza mageuzi matatu yaliyofanywa katika kikosi cha polisi (al.3)
      • Maafisa wa polisi kupokea mafunzo kwa kipindi cha kati ya miezi 15 na 21 kinyume na awali ilipochukua miezi 9
      • Alama za kujiunga na kikosi hicho zimeongezewa kutoka D hadi C
      • Asilimia 10 ya makurutu wawe na digrii kutoka chuo kikuu ili kuhitimu naibu wa inspekta wa polisi
      • Usawa wa jinsia kuzingatiwa katika uajiri wa maafisa wa polisi 3x1 = 3
    5.  Taja makundi mawili yaliyohusika katika kuandaa mtalaa mpya (al.2)
      • Jopo iliyoteuliwa na Rais mwaka wa 2003
      • Taasisi ya elimu
      • Wakufunzi kutokea chuo cha mafunzo cha Kiganjo
      • Wataalam wa maswala ya usalama kutoka Uswizi 2x1 =2
    6. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu (al.3)
      1. Kubisha hodi
        • Kuingia/kutukia
      2. Kukolewa
        • Kuendeleza/kushamirisha
      3. Makurutu
        • Wanafunzi wanaojiunga na kikosi cha polisi
  1. UFUPISHO
    1. Kwa maneno yasiyozidi 70, fupishsa aya za kwanza nne. (al.9)
      • Serikali kuwasilisha bajeti
      • Kueleza jinsi mabilioni yalivyotumiwa
      • Serikali ya Kenyatta kusema itatumia shilingi 1.6 trilioni kwa maendeleo.
      • Makadirio kuwasilishwa na kiongozi wa walio wengi bungeni
      • Kukosa kueleza jinsi ya kupata kitifa hicho
      • Habari hizi kunipa wasiwasi
      • Kenya kudaiwa shilingi 1.8 trilioni na wafadhili
      • Kutolaumu wale wasiolewa ukubwa wa deni hili
      • Kugawanya deni hili kwa Wakenya wote
      • Kila Mkenya kadaiwa shilingi 45,000
      • Kenyatta kurithi deni kutoka kwa Kibaki
      • Deni kumkosesha usingizi Rais
      • Kutafuta njia ya kulipa bila kuathiri uchumi
        9x1 = 9
        Mtiririko alama 1
    2. Kwa nini serikali haitaweza kulipa madeni yake. (maneno 40-50) (al.6)
      • Serikali kutenga fedha nyingi kuwalipa wafanyikazi
      • KRA kutokusanya kiwango kinachohitajika
      • Ukusanyaji wa ushuru kutatizwa na hofu wakati wa uchaguzi
      • Serikali za kaunti kupendekeza kutumia mabilioni ambayo hawana
        4x1 = 4
        Mtiririko alama 1
  1. SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (alama 40)
    1. Tambua sauti.
      Kipasuo ghuna cha kaakaa laini (al.1)
      • /g/
    2. Unda neno lenye muundo ufuatao wa sauti (al.1)
      KKKKI
      • Mchwa
    3. Eleza maana ya istilahi zifuatazo za sauti (al.4)
      1. Kiimbo
        • Kupanda na kushuka kwa sauti mtu anapozungumza
      2. Konsonanti mwambatano
        • Mfuatano wa konsonanti mbili au zaidi katika silabi unapotamka
    4. Tunga sentensi moja ukitumia neno –zuri kama kiwakilishi, kivumishi na kielezi (al.3)
      • Vizuri vile ni vya watu wazuri walioandikiwa vibaya
    5. Eleza tofauti kati ya sentensi hizi (al.2)
      Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani.
      • Kuna uwezekano wa kitendo kutendeka/wakati uliopo

      Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani
      • Hakuna uwezekano/wakati uliopita
    6. Tunga sentensi moja sahihi itakayotumia vitenzi vifuatavyo (al.3)
      -wahi, -enda, -ona
      • Aliwahi kwenda kumuona afisini mwake (1x3=3)
    7. Huku ukitumia mifano mwafaka, tofautisha silabi wazi na silabi funge (al.2)
      • Silabi wazi ni zile zinazoishia kwa irabu k.m. ru + ka ba + ba
      • Funge ni zile zinazoishia kwa konsonanti k.m. m + t u Da - k - ta - ri
    8. Andika sentensi ifuatayo katika hali ya yakinishi (al.2)
      Wanafunzi wasiposoma kwa bidii hawatapita mtihani
      • Wanafunzi wakisoma kwa bidii watapita mtihani
    9. Bainisha vishazi katika sentensi ifuatayo (al.2)
      Gaidi aliyelipua guruneti ile ametiwa mbaroni
      • Gaidi aliyelipua guruneti – k – huru ametiwa baroni – Kishazi tegemezi
    10. Andika katika msemo wa taarifa: (al.2)
      “Wakazi wa eneo hili ni wafugaji stadi wa sungura” kakangu aliniambia.
      • Kakangu aliniambia kuwa wakazi wa eneo hilo ni wafugaji stadi wa sungura.
    11. Bainisha aina za virai katika sentensi ifuatayo (al.3)
      Sheria hizo mpya zilitundikwa juu ya ukuta usiku wa manane.
      • Sheria mpya – Kikundi nomino
      • Zilitundikwa juu ya – Kikundi tenzi
      • Juu ya ukuta – Kikundi kihusishi
      • Usiku wa manane – Kikundi kielezi
        1x4 = 4
    12. Unda nomino kutokana na vitenzi vifuatavyo (al.2)
      1. Sali
        • Sala, msala, msalihina,
      2. La
        • Chakula, mlo, mlaji, ulaji
    13. Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi (al.4)
      Sentensi changamano.PNG
    14. Andika katika kauli ya kutendesha (al.2)
      Amani alikunywa pombe mpaka akalewa sana
      • Pombe ilimlevya Amani
    15. Andika kwa udogo (al.2)
      Njia iendayo mbinguni ni nyembamba
      • Kijia kiendacho mbinguni ni chembamba 1x2 = 2
    16. Neno changa lina maana ya kutoa kitu au fedha ili kukusanya kwa makusudi Fulani. Eleza maana zingine mbili (al.2)
      • Umwa viungoni au mishiopani kama ugonjwa wa biridi ya bisi
      • Siyokomaa/siyopevuka
    17. Taja nahau zingine mbili sawa na “Enda ahera” (al.2)
      • Kata kamba
      • Aga dunia
      • Ipa dunia kisogo
      • Enda jongomeo
    18. Andika kwa wingi (al.1)
      Zigo la kuliwa halilemei
      • Mizigo ya kuliwa hayalemei
  1. ISIMU JAMII (alama 10)

    Soma kifungu kifuatacho halafu ujibu maswali.

    “Naona “Horsepower” mwenyewe ndiye atakayepiga, atakayecheza foul hiyo. Wachezaji wa……”
    1. Tambua sajili inayorejelewa (al.2)
      • Sajili ya michezo/kandanda/kambumbu
    2.  Tambua sifa zinazobainisha sajili yenyewe (al.8)
      • Lugha changamfu/cheshi/porojo
      • Kupiga chuku/kutiwa chumvi
      • Lugha shawishi
      • Utohozi/mf. Foul, Horse power
      • Lugha mseto/kuchanganya ndimi/msimbo
      • Matumizi ya tamathali za usemi
      • Lugha nyepesi inayoeleweka
      • Kuhamisha ndimi
      • Huchanganywa na nyimbo
      • Matumizi ya msamiati teule wa kambukambu
      • Kauli/sentensi fupi fupi
      • Sentensi zisizokamilika
      • Uradidi/takriri/urudiaji
      • Matumizi ya lakabu
      • Sifa kemkem kwa wachezaji
        Zozote nane 1x8=8
        Adhabu
        Makosa ya sarufi ya kwanza manne yaondolewe alama 2 4x1/2 =2
        Makosa ya hijai hadi manne 4x1/2 =2
        Jumla alama 4

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "KISWAHILI PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "KISWAHILI PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020" on Whatsapp

OR




Read 9421 times Last modified on Monday, 10 February 2020 12:24
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - KISWAHILI PAPER 1 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020 BIOLOGY PAPER 1 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020 - Next »
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in FORM 4 END TERM 1 EXAM 2020
Tagged under
  • Kiswahili
  • KCSE
  • 2020
  • Form 4
  • TERM 1

Related items

  • Kiswahili Paper 3 Questions and Answers - Maranda Post Mocks 2020/2021
  • Kiswahili Paper 2 Questions and Answers - Maranda Post Mocks 2020/2021
  • Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Maranda Post Mocks 2020/2021
  • Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Murang'a County Mocks 2020/2021
  • Physics Paper 2 Questions and Answers - Kassu Jet Joint Exams 2020/2021
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
2020 Form 4 Term 1 Past Papers Revision