KISWAHILI PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020

Share via Whatsapp
  1. UFAHAMU
    1. Ni dalili ipi inayoonyesha mwanzo wa mageuzi? (al.1)
    2. Mtaala mpya unalenga nini? (al.4)
    3. Eleza lawama zinazoelekezewa kikosi cha polisi (al.2)
    4. Kwa mujibu wa taarifa eleza mageuzi matatu yaliyofanywa katika kikosi cha polisi (al.3)
    5.  Taja makundi mawili yaliyohusika katika kuandaa mtalaa mpya (al.2)
    6. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu (al.3)
      1. Kubisha hodi
      2. Kukolewa
      3. Makurutu
  1. UFUPISHO
    1. Kwa maneno yasiyozidi 70, fupishsa aya za kwanza nne. (al.9)  Mtiririko alama 1
    2. Kwa nini serikali haitaweza kulipa madeni yake. (maneno 40-50) (al.6) Mtiririko alama 1
  1. SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (alama 40)
    1. Tambua sauti.
      Kipasuo ghuna cha kaakaa laini (al.1)
    2. Unda neno lenye muundo ufuatao wa sauti (al.1)
      KKKKI
    3. Eleza maana ya istilahi zifuatazo za sauti (al.4)
      1. Kiimbo
      2. Konsonanti mwambatano
    4. Tunga sentensi moja ukitumia neno –zuri kama kiwakilishi, kivumishi na kielezi (al.3)
    5. Eleza tofauti kati ya sentensi hizi (al.2)
      Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani.
      Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani
    6. Tunga sentensi moja sahihi itakayotumia vitenzi vifuatavyo (al.3)
      -wahi, -enda, -ona
    7. Huku ukitumia mifano mwafaka, tofautisha silabi wazi na silabi funge (al.2)
    8. Andika sentensi ifuatayo katika hali ya yakinishi (al.2)
      Wanafunzi wasiposoma kwa bidii hawatapita mtihani
    9. Bainisha vishazi katika sentensi ifuatayo (al.2)
      Gaidi aliyelipua guruneti ile ametiwa mbaroni
    10. Andika katika msemo wa taarifa: (al.2)
      “Wakazi wa eneo hili ni wafugaji stadi wa sungura” kakangu aliniambia.
    11. Bainisha aina za virai katika sentensi ifuatayo (al.3)
      Sheria hizo mpya zilitundikwa juu ya ukuta usiku wa manane.
    12. Unda nomino kutokana na vitenzi vifuatavyo (al.2)
      1. Sali
      2. La
    13. Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi (al.4)
      Jengo lijengwalo kwenye msingi thabiti hudumu sana.
    14. Andika katika kauli ya kutendesha (al.2)
      Amani alikunywa pombe mpaka akalewa sana
    15. Andika kwa udogo (al.2)
      Njia iendayo mbinguni ni nyembamba
    16. Neno changa lina maana ya kutoa kitu au fedha ili kukusanya kwa makusudi Fulani. Eleza maana zingine mbili (al.2)
    17. Taja nahau zingine mbili sawa na “Enda ahera” (al.2)
    18. Andika kwa wingi (al.1)
      Zigo la kuliwa halilemei
  1. ISIMU JAMII (alama 10)

    Soma kifungu kifuatacho halafu ujibu maswali.

    “Naona “Horsepower” mwenyewe ndiye atakayepiga, atakayecheza foul hiyo. Wachezaji wa……”

    1. Tambua sajili inayorejelewa (al.2)
    2.  Tambua sifa zinazobainisha sajili yenyewe (al.8)

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. UFAHAMU
    1. Ni dalili ipi inayoonyesha mwanzo wa mageuzi? (al.1)
      • Kuzinduliwa kwa mtaala mpya wa kutoa mafunzo kwa maafisa wa polisi 1x1=1
    2. Mtaala mpya unalenga nini? (al.4)
      • Kuimarisha utendakazi katika kikosi ambacho kwa muda mrefu kimelaumiwa kwa kulowa ufisadi na uvunjaji wa haki za kimsingi
      • Unaashiria mwanzo wa mageuzi makubwa yanayonuiwa kukipatia kikosi hicho sura mpya
      • Kuwapa maafisa wa polisi mafunzo mapya
      • Kuunda kikosi imara chenye nidhamu na kinachoheshimu haki za kibinadamu 4x1 = 4
    3. Eleza lawama zinazoelekezewa kikosi cha polisi (al.2)
      • Ukosefu wa nidhamu
      • Kutoheshimu haki za binadamu/kimsingi
      • Kukolea kwa ufisadi
    4. Kwa mujibu wa taarifa eleza mageuzi matatu yaliyofanywa katika kikosi cha polisi (al.3)
      • Maafisa wa polisi kupokea mafunzo kwa kipindi cha kati ya miezi 15 na 21 kinyume na awali ilipochukua miezi 9
      • Alama za kujiunga na kikosi hicho zimeongezewa kutoka D hadi C
      • Asilimia 10 ya makurutu wawe na digrii kutoka chuo kikuu ili kuhitimu naibu wa inspekta wa polisi
      • Usawa wa jinsia kuzingatiwa katika uajiri wa maafisa wa polisi 3x1 = 3
    5.  Taja makundi mawili yaliyohusika katika kuandaa mtalaa mpya (al.2)
      • Jopo iliyoteuliwa na Rais mwaka wa 2003
      • Taasisi ya elimu
      • Wakufunzi kutokea chuo cha mafunzo cha Kiganjo
      • Wataalam wa maswala ya usalama kutoka Uswizi 2x1 =2
    6. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumika katika kifungu (al.3)
      1. Kubisha hodi
        • Kuingia/kutukia
      2. Kukolewa
        • Kuendeleza/kushamirisha
      3. Makurutu
        • Wanafunzi wanaojiunga na kikosi cha polisi
  1. UFUPISHO
    1. Kwa maneno yasiyozidi 70, fupishsa aya za kwanza nne. (al.9)
      • Serikali kuwasilisha bajeti
      • Kueleza jinsi mabilioni yalivyotumiwa
      • Serikali ya Kenyatta kusema itatumia shilingi 1.6 trilioni kwa maendeleo.
      • Makadirio kuwasilishwa na kiongozi wa walio wengi bungeni
      • Kukosa kueleza jinsi ya kupata kitifa hicho
      • Habari hizi kunipa wasiwasi
      • Kenya kudaiwa shilingi 1.8 trilioni na wafadhili
      • Kutolaumu wale wasiolewa ukubwa wa deni hili
      • Kugawanya deni hili kwa Wakenya wote
      • Kila Mkenya kadaiwa shilingi 45,000
      • Kenyatta kurithi deni kutoka kwa Kibaki
      • Deni kumkosesha usingizi Rais
      • Kutafuta njia ya kulipa bila kuathiri uchumi
        9x1 = 9
        Mtiririko alama 1
    2. Kwa nini serikali haitaweza kulipa madeni yake. (maneno 40-50) (al.6)
      • Serikali kutenga fedha nyingi kuwalipa wafanyikazi
      • KRA kutokusanya kiwango kinachohitajika
      • Ukusanyaji wa ushuru kutatizwa na hofu wakati wa uchaguzi
      • Serikali za kaunti kupendekeza kutumia mabilioni ambayo hawana
        4x1 = 4
        Mtiririko alama 1
  1. SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (alama 40)
    1. Tambua sauti.
      Kipasuo ghuna cha kaakaa laini (al.1)
      • /g/
    2. Unda neno lenye muundo ufuatao wa sauti (al.1)
      KKKKI
      • Mchwa
    3. Eleza maana ya istilahi zifuatazo za sauti (al.4)
      1. Kiimbo
        • Kupanda na kushuka kwa sauti mtu anapozungumza
      2. Konsonanti mwambatano
        • Mfuatano wa konsonanti mbili au zaidi katika silabi unapotamka
    4. Tunga sentensi moja ukitumia neno –zuri kama kiwakilishi, kivumishi na kielezi (al.3)
      • Vizuri vile ni vya watu wazuri walioandikiwa vibaya
    5. Eleza tofauti kati ya sentensi hizi (al.2)
      Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani.
      • Kuna uwezekano wa kitendo kutendeka/wakati uliopo

      Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani
      • Hakuna uwezekano/wakati uliopita
    6. Tunga sentensi moja sahihi itakayotumia vitenzi vifuatavyo (al.3)
      -wahi, -enda, -ona
      • Aliwahi kwenda kumuona afisini mwake (1x3=3)
    7. Huku ukitumia mifano mwafaka, tofautisha silabi wazi na silabi funge (al.2)
      • Silabi wazi ni zile zinazoishia kwa irabu k.m. ru + ka ba + ba
      • Funge ni zile zinazoishia kwa konsonanti k.m. m + t u Da - k - ta - ri
    8. Andika sentensi ifuatayo katika hali ya yakinishi (al.2)
      Wanafunzi wasiposoma kwa bidii hawatapita mtihani
      • Wanafunzi wakisoma kwa bidii watapita mtihani
    9. Bainisha vishazi katika sentensi ifuatayo (al.2)
      Gaidi aliyelipua guruneti ile ametiwa mbaroni
      • Gaidi aliyelipua guruneti – k – huru ametiwa baroni – Kishazi tegemezi
    10. Andika katika msemo wa taarifa: (al.2)
      “Wakazi wa eneo hili ni wafugaji stadi wa sungura” kakangu aliniambia.
      • Kakangu aliniambia kuwa wakazi wa eneo hilo ni wafugaji stadi wa sungura.
    11. Bainisha aina za virai katika sentensi ifuatayo (al.3)
      Sheria hizo mpya zilitundikwa juu ya ukuta usiku wa manane.
      • Sheria mpya – Kikundi nomino
      • Zilitundikwa juu ya – Kikundi tenzi
      • Juu ya ukuta – Kikundi kihusishi
      • Usiku wa manane – Kikundi kielezi
        1x4 = 4
    12. Unda nomino kutokana na vitenzi vifuatavyo (al.2)
      1. Sali
        • Sala, msala, msalihina,
      2. La
        • Chakula, mlo, mlaji, ulaji
    13. Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi (al.4)
      Sentensi changamano.PNG
    14. Andika katika kauli ya kutendesha (al.2)
      Amani alikunywa pombe mpaka akalewa sana
      • Pombe ilimlevya Amani
    15. Andika kwa udogo (al.2)
      Njia iendayo mbinguni ni nyembamba
      • Kijia kiendacho mbinguni ni chembamba 1x2 = 2
    16. Neno changa lina maana ya kutoa kitu au fedha ili kukusanya kwa makusudi Fulani. Eleza maana zingine mbili (al.2)
      • Umwa viungoni au mishiopani kama ugonjwa wa biridi ya bisi
      • Siyokomaa/siyopevuka
    17. Taja nahau zingine mbili sawa na “Enda ahera” (al.2)
      • Kata kamba
      • Aga dunia
      • Ipa dunia kisogo
      • Enda jongomeo
    18. Andika kwa wingi (al.1)
      Zigo la kuliwa halilemei
      • Mizigo ya kuliwa hayalemei
  1. ISIMU JAMII (alama 10)

    Soma kifungu kifuatacho halafu ujibu maswali.

    “Naona “Horsepower” mwenyewe ndiye atakayepiga, atakayecheza foul hiyo. Wachezaji wa……”
    1. Tambua sajili inayorejelewa (al.2)
      • Sajili ya michezo/kandanda/kambumbu
    2.  Tambua sifa zinazobainisha sajili yenyewe (al.8)
      • Lugha changamfu/cheshi/porojo
      • Kupiga chuku/kutiwa chumvi
      • Lugha shawishi
      • Utohozi/mf. Foul, Horse power
      • Lugha mseto/kuchanganya ndimi/msimbo
      • Matumizi ya tamathali za usemi
      • Lugha nyepesi inayoeleweka
      • Kuhamisha ndimi
      • Huchanganywa na nyimbo
      • Matumizi ya msamiati teule wa kambukambu
      • Kauli/sentensi fupi fupi
      • Sentensi zisizokamilika
      • Uradidi/takriri/urudiaji
      • Matumizi ya lakabu
      • Sifa kemkem kwa wachezaji
        Zozote nane 1x8=8
        Adhabu
        Makosa ya sarufi ya kwanza manne yaondolewe alama 2 4x1/2 =2
        Makosa ya hijai hadi manne 4x1/2 =2
        Jumla alama 4
Join our whatsapp group for latest updates

Download KISWAHILI PAPER 2 - FORM 4 END TERM 1 EXAMS 2020.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest