Kiswahili Paper 3 Questions with No Answers - Maseno Mock Exams 2020/2021

Share via Whatsapp

Kenya Certificate of Secondary Education
102/3- KISWAHILI -Karatasi ya 3
(FASIHI)
Muda: Saa - 2 ½

Maagizo

  1. Jibu maswali manne pekee.
  2. Swali la kwanza ni la lazima.
  3. Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki; yaani: Riwaya, Hadithi Fupi, Ushairi na Fasihi Simulizi..
  4. Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
  5. Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
  6. Majibu yote sharti yaandikwe kwenye nafasi ulizoachiwa kwenye kijitabu hiki cha maswali.

SEHEMU A: TAMTHILIA

P. Kea: Kigogo

  1. Lazima
    “Ama ale hizo falsafa zake! Udongo haubishani na mfinyazi...Kigogo hachezewi; watafuta maangamizi!”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Bainisha mbinu nne za kimtindo kwenye dondoo hili. (alama 4)
    3. Huku ukitoa hoja kumi na mbili, thibitisha kuwa kumchezea kigogo ni kutafuta maangamizi. (alama 12)

SEHEMU B: RIWAYA

A. Matei: Chozi la Heri

Jibu swali 2 au 3

  1. “… kile ambacho raia wanahitaji ni mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi na sera zenyewe za uongozi. Na naona awamu hii,…wingu la mabadiliko limetanda.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Eleza sifa sita za msemaji wa maneno haya. (alama 6)
    3. Huku ukitoa hoja kumi, dhihirisha kuwa wingu la mabadiliko limetanda katika jamii ya Wahafidhina. (alama 10)
  2.  
    1. Wanawake katika riwaya ya Chozi la Heri ni vyombo vikuu vya ukiukaji wa haki za kibinadamu. Thibitisha. (alama 10)
    2. Huku ukitoa mifano kumi, onyesha namna mwandishi wa riwaya ya Chozi
      La Heri ametumia mbinu rejeshi kuendeleza maudhui. (alama 10)

SEHEMU C: HADITHI FUPI

Jibu swali 4 au 5

A. Chokocho na D. Kayanda (Wah): Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine

  1.  
    1. Salma Omar Hamad: Shibe Inatumaliza.
      “Ndugu yangu kula kunatumaliza.’’
      “Kunatumaliza au tunakumaliza?’’
      1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 5)
      2. Eleza namna “kula” kunaimaliza jamii ya hadithi hii . (alama 5)
    2. Ali Abdulla Ali: Ndoto Ya Mashaka
      “Nimechoka hata naradua kufa kuliko kuishi. Hadi lini mashaka haya ya kutengenezwa?”
      1. Fafanua umuhimu wa msemaji wa kauli hii katika kuendeleza hadithi hii. (alama 5)
      2. Fafanua kwa hoja tano mambo yanayopelekea msemaji kuradua kufa kuliko kuishi. (alama 5)
  2. Mohammed Khelef Ghassany : Mame Bakari
    “Aliendelea kububujikwa na machozi kila alipoyafikiri yaliyompata na yatakayompata miezi si mingi ijayo.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Fafanua mambo ambayo mrejelewa alifikiri yangempata miezi si mingi ijayo. (alama 6)
    3. Eleza namna maudhui ya elimu yanajitokeza katika hadithi zifuatazo
      1. Mwalimu Mstaafu (alama 5)
      2. Mtihani wa Maisha (alama 5)

SEHEMU D: USHAIRI

Jibu swali 6 au 7

  1. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

    Jicho, tavumiliaje, kwa hayo uyaonayo?
    Kicho, utasubirije, maonevu yapitayo?
    Kwacho, lijalo nalije, nimechoka vumiliyo
    Naandika!

    Moyo, unao timbuko, maudhi tusikiayo
    Nayo, visa na mauko, wanyonge yawakutayo
    Kwayo, sina zuiliko, natoa niyahisiyo
    Naandika!

    Hawa, wanotulimiya, dhiki wavumiliayo
    Hawa, mamiya mamiya, na mali wazalishayo
    Hawa, ndo wanoumiya, na maafa wakutayo
    Naandika!

    Hawa, sioni wengine, kwao liko angamiyo
    Hawa, huwapa unene, watukufu wenye nayo
    Hawa, bado ni wavune, Kwa shida waikutayo
    Naandika!

    Bado, wawapo mabwana, wenye pupa na kamiyo
    Bado, tofauti sana, kwa pato na mengineyo
    Bado, tuling’owe shina, ulaji pia na choyo
    Naandika!
    1. Huku ukitoa hoja sita, eleza mambo ambayo yanamsukuma mshairi kuandika shairi hili. (alama 6)
    2. Eleza bahari zinazojitokeza katika shairi hili ukizingatia vigezo vifuatavyo; (alama 3)
      1. Idadi ya vipande katika mishororo
      2. Idadi ya mizani katika mishororo
      3. Mpangilio wa vina katika beti
    3. Changanua muundo wa shairi hili. (alama 4)
    4. Eleza toni katika shairi hili (alama 2)
    5. Fafanua kwa kutoa mifano mitatu mbinu ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika shairi hili. (alama 3)
    6. Andika ubeti wa pili kwa lugha ya nathari. (alama 2)
  2. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

    Jua la mashariki limezibwa
    Na mchweo ya magharibi
    Tukabaki kUhesabu siku
    Na kila sekunde inayopita
    Ikilifyatua shaka jipya
    Ambalo bado kidogo
    Litakuwa limeliua tumaini
    Na sumu yake kulipuka hadharani
    Ulimwengu ushuhudie.

    Ni upeo wa sayansi:
    Waundapo silaha
    Mabomu ya masafa ya mbali
    Yanayomwaya yake mimweso
    Na kutudonoa
    Kama yule jogoo
    Wa radi.

    Ni upeo wa uhayawani:
    Tuundapo silaha
    Mabomu ya masafa ya karibu
    Au zana za kukingia wao jogoo
    Asitudonoe na kututia mautuni
    Katika yetu ardhi
    Walipoishi na kuzikwa wetu wahenga.

    Ni udikteta sisi kuongozana bibaya
    Ni udikteta viongozi kuwauwa wapinzani
    Ni unyama watu kupigwa watu risasi
    Ni unyama wananchi kuteswa
          Lakini
    Ni demokrasia wao kutuvamia
    Na yetu ardhi kukalia
    Ni demokrasia kuwaua viongozi wetu
    Pamoja na wananchi kwa yao makombora
    Yenye kiu ya damu yetu.

    Ni haki kutukatia mifereji ya maji
    Tukanyauka na kujifia kama vipando
    Katika majira magumu ya ukame?
    Ni utu kuwatesa watoto wetu
    Waliojisabilia kuipigania nchi katika ushinde
    Katika ardhi hii tulopawa
    Naye Mola Moliwa?

    Lakini fahamuni:
    Tofauti kati ya hadithi fupi na ndefu
    Ni kuwa ndefu huchukua mrefu wakati kuisha
    Na ile fupi huchukua muda mfupi
    Zote lakini zina miisho
    Na hii nayo ipo siku
    Ukingoni itafika
    Hatimaye watoto wetu wapate tena
    Jioni kuitamani
    Jioni isiyo na mimweso
    Mimweso ya kutishia wao uhai
    Na mingurumo na mirindimo
    Ya kutangaza yao maangamizo!

    Najua sitakuwepo hili kulishuhudia
    Lakini kwangu itakuwa si kitu
    Muhimu ni wajukuu wafahamishwe
    Kuwa hapa nilipita na kushuhudia
    Binadamu akiutekeleza unyama
    Alipoupindua juu chini, nje ndani
    Kama funzo la demokrasia
    Kwa ulimwengu kipofu!

    Maswali
    1. Huku ukitoa hoja sita, dhihirisha kuwa jamii ya nafsineni imekandamizwa. (alama 6)
    2. Toa mfano mmoja mmoja wa mitindo ifuatayo kwenye shairi. (alama 4)
      1. Usambamba
      2. Taswira
      3. Tashibihi
      4. tashihisi
    3. Toa mifano ya idhini zifuatazo za kishairi. (alama 2)
      1. Kuboronga sarufi
      2. Tabdila
    4. Tambua nafsineni katika shairi hili. (alama 1)
    5. Andika ubeti wa tano katika lugha tutumbi. (alama 4)
    6. Eleza toni ya mshairi katika shairi hili. (alama 1)
    7. Eleza matumaini ya mshairi katika shairi hili. (alama 2)

SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI

  1.  
    1. Eleza maana ya miviga katika Fasihi Simulizi. (alama 2)
    2. Fafanua sifa tano za miviga. (alama 5)
    3. Wewe ni mwigizaji wa michezo ya jukwaani. Eleza mambo matano ambayo utazingatia ili kufanikisha uigizaji wako. (alama 5)
    4. Unanuia kutumia mbinu ya maandishi kukusanya na kuhifadhi habari kuhusu miviga ya tohara.
      1. Eleza manufaa ya kutumia mbinu hii. (alama 4)
      2. Eleza udhaifu wa kutumia mbinu hii. (alama 4)
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 3 Questions with No Answers - Maseno Mock Exams 2020/2021.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest