Kenya Certificate of Secondary Education
102/3- KISWAHILI -Karatasi ya 3
(FASIHI)
Muda: Saa - 2 ½
Maagizo
- Jibu maswali manne pekee.
- Swali la kwanza ni la lazima.
- Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki; yaani: Riwaya, Hadithi Fupi, Ushairi na Fasihi Simulizi..
- Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
- Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
- Majibu yote sharti yaandikwe kwenye nafasi ulizoachiwa kwenye kijitabu hiki cha maswali.
SEHEMU A: TAMTHILIA
P. Kea: Kigogo
- Lazima
“Ama ale hizo falsafa zake! Udongo haubishani na mfinyazi...Kigogo hachezewi; watafuta maangamizi!”- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Bainisha mbinu nne za kimtindo kwenye dondoo hili. (alama 4)
- Huku ukitoa hoja kumi na mbili, thibitisha kuwa kumchezea kigogo ni kutafuta maangamizi. (alama 12)
SEHEMU B: RIWAYA
A. Matei: Chozi la Heri
Jibu swali 2 au 3
- “… kile ambacho raia wanahitaji ni mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi na sera zenyewe za uongozi. Na naona awamu hii,…wingu la mabadiliko limetanda.”
- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Eleza sifa sita za msemaji wa maneno haya. (alama 6)
- Huku ukitoa hoja kumi, dhihirisha kuwa wingu la mabadiliko limetanda katika jamii ya Wahafidhina. (alama 10)
-
- Wanawake katika riwaya ya Chozi la Heri ni vyombo vikuu vya ukiukaji wa haki za kibinadamu. Thibitisha. (alama 10)
- Huku ukitoa mifano kumi, onyesha namna mwandishi wa riwaya ya Chozi
La Heri ametumia mbinu rejeshi kuendeleza maudhui. (alama 10)
SEHEMU C: HADITHI FUPI
Jibu swali 4 au 5
A. Chokocho na D. Kayanda (Wah): Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine
-
- Salma Omar Hamad: Shibe Inatumaliza.
“Ndugu yangu kula kunatumaliza.’’
“Kunatumaliza au tunakumaliza?’’- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 5)
- Eleza namna “kula” kunaimaliza jamii ya hadithi hii . (alama 5)
- Ali Abdulla Ali: Ndoto Ya Mashaka
“Nimechoka hata naradua kufa kuliko kuishi. Hadi lini mashaka haya ya kutengenezwa?”- Fafanua umuhimu wa msemaji wa kauli hii katika kuendeleza hadithi hii. (alama 5)
- Fafanua kwa hoja tano mambo yanayopelekea msemaji kuradua kufa kuliko kuishi. (alama 5)
- Salma Omar Hamad: Shibe Inatumaliza.
- Mohammed Khelef Ghassany : Mame Bakari
“Aliendelea kububujikwa na machozi kila alipoyafikiri yaliyompata na yatakayompata miezi si mingi ijayo.”- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Fafanua mambo ambayo mrejelewa alifikiri yangempata miezi si mingi ijayo. (alama 6)
- Eleza namna maudhui ya elimu yanajitokeza katika hadithi zifuatazo
- Mwalimu Mstaafu (alama 5)
- Mtihani wa Maisha (alama 5)
SEHEMU D: USHAIRI
Jibu swali 6 au 7
- Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Jicho, tavumiliaje, kwa hayo uyaonayo?
Kicho, utasubirije, maonevu yapitayo?
Kwacho, lijalo nalije, nimechoka vumiliyo
Naandika!
Moyo, unao timbuko, maudhi tusikiayo
Nayo, visa na mauko, wanyonge yawakutayo
Kwayo, sina zuiliko, natoa niyahisiyo
Naandika!
Hawa, wanotulimiya, dhiki wavumiliayo
Hawa, mamiya mamiya, na mali wazalishayo
Hawa, ndo wanoumiya, na maafa wakutayo
Naandika!
Hawa, sioni wengine, kwao liko angamiyo
Hawa, huwapa unene, watukufu wenye nayo
Hawa, bado ni wavune, Kwa shida waikutayo
Naandika!
Bado, wawapo mabwana, wenye pupa na kamiyo
Bado, tofauti sana, kwa pato na mengineyo
Bado, tuling’owe shina, ulaji pia na choyo
Naandika!- Huku ukitoa hoja sita, eleza mambo ambayo yanamsukuma mshairi kuandika shairi hili. (alama 6)
- Eleza bahari zinazojitokeza katika shairi hili ukizingatia vigezo vifuatavyo; (alama 3)
- Idadi ya vipande katika mishororo
- Idadi ya mizani katika mishororo
- Mpangilio wa vina katika beti
- Changanua muundo wa shairi hili. (alama 4)
- Eleza toni katika shairi hili (alama 2)
- Fafanua kwa kutoa mifano mitatu mbinu ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika shairi hili. (alama 3)
- Andika ubeti wa pili kwa lugha ya nathari. (alama 2)
- Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Jua la mashariki limezibwa
Na mchweo ya magharibi
Tukabaki kUhesabu siku
Na kila sekunde inayopita
Ikilifyatua shaka jipya
Ambalo bado kidogo
Litakuwa limeliua tumaini
Na sumu yake kulipuka hadharani
Ulimwengu ushuhudie.
Ni upeo wa sayansi:
Waundapo silaha
Mabomu ya masafa ya mbali
Yanayomwaya yake mimweso
Na kutudonoa
Kama yule jogoo
Wa radi.
Ni upeo wa uhayawani:
Tuundapo silaha
Mabomu ya masafa ya karibu
Au zana za kukingia wao jogoo
Asitudonoe na kututia mautuni
Katika yetu ardhi
Walipoishi na kuzikwa wetu wahenga.
Ni udikteta sisi kuongozana bibaya
Ni udikteta viongozi kuwauwa wapinzani
Ni unyama watu kupigwa watu risasi
Ni unyama wananchi kuteswa
Lakini
Ni demokrasia wao kutuvamia
Na yetu ardhi kukalia
Ni demokrasia kuwaua viongozi wetu
Pamoja na wananchi kwa yao makombora
Yenye kiu ya damu yetu.
Ni haki kutukatia mifereji ya maji
Tukanyauka na kujifia kama vipando
Katika majira magumu ya ukame?
Ni utu kuwatesa watoto wetu
Waliojisabilia kuipigania nchi katika ushinde
Katika ardhi hii tulopawa
Naye Mola Moliwa?
Lakini fahamuni:
Tofauti kati ya hadithi fupi na ndefu
Ni kuwa ndefu huchukua mrefu wakati kuisha
Na ile fupi huchukua muda mfupi
Zote lakini zina miisho
Na hii nayo ipo siku
Ukingoni itafika
Hatimaye watoto wetu wapate tena
Jioni kuitamani
Jioni isiyo na mimweso
Mimweso ya kutishia wao uhai
Na mingurumo na mirindimo
Ya kutangaza yao maangamizo!
Najua sitakuwepo hili kulishuhudia
Lakini kwangu itakuwa si kitu
Muhimu ni wajukuu wafahamishwe
Kuwa hapa nilipita na kushuhudia
Binadamu akiutekeleza unyama
Alipoupindua juu chini, nje ndani
Kama funzo la demokrasia
Kwa ulimwengu kipofu!
Maswali- Huku ukitoa hoja sita, dhihirisha kuwa jamii ya nafsineni imekandamizwa. (alama 6)
- Toa mfano mmoja mmoja wa mitindo ifuatayo kwenye shairi. (alama 4)
- Usambamba
- Taswira
- Tashibihi
- tashihisi
- Toa mifano ya idhini zifuatazo za kishairi. (alama 2)
- Kuboronga sarufi
- Tabdila
- Tambua nafsineni katika shairi hili. (alama 1)
- Andika ubeti wa tano katika lugha tutumbi. (alama 4)
- Eleza toni ya mshairi katika shairi hili. (alama 1)
- Eleza matumaini ya mshairi katika shairi hili. (alama 2)
SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI
-
- Eleza maana ya miviga katika Fasihi Simulizi. (alama 2)
- Fafanua sifa tano za miviga. (alama 5)
- Wewe ni mwigizaji wa michezo ya jukwaani. Eleza mambo matano ambayo utazingatia ili kufanikisha uigizaji wako. (alama 5)
- Unanuia kutumia mbinu ya maandishi kukusanya na kuhifadhi habari kuhusu miviga ya tohara.
- Eleza manufaa ya kutumia mbinu hii. (alama 4)
- Eleza udhaifu wa kutumia mbinu hii. (alama 4)
Download Kiswahili Paper 3 Questions with No Answers - Maseno Mock Exams 2020/2021.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students