Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Londiani Joint Mock Exams 2022

Share via Whatsapp
MAAGIZO:
  1. Andika jina lako na nambari yako ya usajili wa mtihani.
  2. Andika Insha mbili, Insha ya kwanza ni ya lazima.
  3. Chagua Insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
  4. Kila Insha isipungue maneno 400.
  5. Kila Insha ina alama 20.
  6. Kila Insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
  7. Karatasi hii ina kurasa mbili zilizopigwa chapa. 
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE.

SWALI

UPEO

ALAMA

1

20

 
 

20

 

JUMLA

40

 

MASWALI

  1. LAZIMA
    Wewe ni kiranja mkuu wa shule ya Fahamuni. Umealikwa katika hafla ya kustaafu kwa Mwalimu wako; mlezi wa kidato chako. Andika wasifu utakaotoa kuhusu mwalimu huyu. (alama 20)
  2. Magari ya matatu yameleta faida nyingi hapa nchini kuliko hasara. Jadili. (alama 20)
  3. Tunga kisa kinachodhihirisha maana ya methali ifuatayo: (alama 20)
    Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.
  4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa maneno  yafuatayo: (alama 20)
    Sikutarajia hayo kutoka kwa mwandani wangu. Niliamua kuufungua ukurasa mpya wa maisha yangu.

MWONGOZO WA INSHA

  1. LAZIMA
    Sura ya wasifu
    1. Kichwa – kitaje wasifu ni wa nani kwa mfano, Wasifu wa Mwalimu wangu mlezi wa kidato au utaje jina, wasifu wa Mwalimu Juma na kadhalika.
    2. Sehemu ya mwili
      • Tambulisha msifiwa kwa majina yote.
      • Mwaka wa kuzaliwa, umri wake.
      • Mahali pa kuzaliwa.
      • Wazazi wake, familia yake n.k.
      • Maelezo haya ya kimsingi yawe katika aya moja.
      • Masomo yake.
        • Shule ya chekechea, msingi na upili.
        • Chuo kikuu (iwapo alienda)
        • Ndoa yake.
        • Kazi na tajiriba ya kazi.
        • Mchango wake katika jamii.
        • Ushirika au uanachama.
    3. Hitimisho
      Aya ya mwisho ndiyo huhitimisha wasifu.
      Mwandishi/mtahini aeleze umaarufu wa anayeandikiwa wasifu na sababu za mtu huyo, kuhitaji utambulisho au sifa alizopewa.

Tanbihi

  1. Mtahiniwa arejelee nafsi ya tatu (umoja) kama vile Darwesh alizaliwa mnamo….
  2. Hutaja tu sifa chanya za mrejelewa.
  3.  Huweze kuandikiwa aliye hai au aliyekufa.
  4. Mtu huyu lazima awe ametoa mchango fulani wa kupigiwa mfano.
  5. Ajaze urefu wa maneno 400.
  6. Sarufi bora izingatiwe.
  7. Atakayeandika wasifu kazi au tawasifu aondolewe alama 4S (sura)

II). SWALI LA PILI
Mjadala/mdahalo

Arejelee sehemu mbili za swali.
Faida

  • Usafiri wa haraka.
  • Nauli yake ni nafuu ikilinganishwa na ndege.
  • Husaidia kubeba mizigo.
  • Ni nyingi hivyo basi rahisi kupatikana.

Hasara.

  • Ajali nyingi hutokea na kusababisha majereha na mauti.
  • Madereva na makanga wenye matusi.
  • Abiria kurundikana pamoja ni chanzo cha kusambaza magonjwa kama vile korona, homa kali, kikohozi n.k.
  • Kuongeza nauli ovyo ovyo.
  • Maadam ni nyingi husababisha misongamano hususan katika miji mikubwa.
    (kadiria hoja nyingine za mwanafunzi)

Tanbihi
Sehemu moja iwe na hoja nyingi kuliko nyingine anaweza kutoa msimamo wake kutokana na idadi ya hoja.

III) METHALI – MGAAGAA NA UPWA HALI WALI MKAVU.

  • Kichwa ni methali yenyewe.
  • Mtahiniwa arejelee sehemu mbili za methali, asipofanya hivyo asipate zaidi ya alama kumi.
  • Atunge kisa kinacholenga maana na matumizi ya methali hii.

Maana na matumizi.

  • Mtu anayejishughulisha na jambo fulani lazima mwishowe atafanikiwa au ataambulia kitu/mapato/mavuno.
  • Methali hii inahimiza bidii ya kutenda jambo.
  • Utungo huu uwe na mvuto.
  • Azingatie sarufi na hijai bora.
  • Ajaze maneno mia nne.
  • Atakayepinga maana atuzwe D03.
  • Atakayetoa maelezo bila utungo atakuwa amepotoka kimaudhui.

4. MDOKEZO WA KUMALIZIA.

  • Abuni kichwa mwafaka.
  • Pawe na tukio linalomhusu yeye na rafiki (mwandani wake)
  • Tukio hilo liwe baya la kumsaliti rafiki (kinyume na matarajio)
  • Mhusika (Nafsi ya kwanza) aathirike na tendo la mwandani
  • Tukio hilo liwatenganisha marafiki ndipo mmoja (nafsi ya kwanza) aamue kuanza maisha mapya bila msaada wa rafiki huyo msaliti.
  • Amalize mtungo wake kwa maneno haya.

Hatua

  1. Kichwa.
  2. Wahusika wawili – Mwandishi (mimi) na rafiki.
  3. Aonyehse urafiki huu na ushirikiano wao.
  4. Tukio (tendo la usaliti)
  5. Utengano.
  6. Mwandishi kuufungua ukurasa mpya.

Tukio hili linaweza kuwa:

  • Kumsengenya/kumsingizia.
  • Kumshtaki kwa mkuu.
  • Kumsaliti kwa watu wengine.
  • Kumnyima nafasi fulani/kataa kumsaidia.
  • Kumuibia mali
  • Kumbaka n.k.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Londiani Joint Mock Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?