Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Momaliche Joint Pre Mock Exams 2022

Share via Whatsapp

MASWALI

  1. Ukiwa waziri wa Elimu nchini, umealikwa kuwazungumzia wanafunzi wa Kidato cha nne katika shule ya Ufanisi. Andika tawasifu utakayowasilisha.
  2. Wananchi ndio wakulaumiwa kutokana na kuzorota kwa usalama nchini Kenya. Jadili
  3. Andika insha itakayoafikiana na methali
    Baniani mbaya kiatu chake dawa
  4. Tunga kisa kinachomalizia maneno yafuatayo:
    .....Nilijitolea kafara na msaada wangu ukazaa natija kwa wengi.


MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA

  1. Zingatia lugha ya mririko
    1. Kujitambulisha
      • Jina
      • Kuzaliwa/Eneo/Kaunti n.k
      • Malezi yake
      • Elimu –Msingi
      • Sekondari
      • Vyuo mbalimbali alivyosoma
    2. Tajriba
      • Kazi aliyofanya/alizofanya kabla ya kuwa waziri
      • Atajika kwa jambo /mambo gani
        Mfano
      • Elimu ya juu – shahada kadhaa
      • Miradi ya maendeleo
      • Ziara alizofanya
      • Uwajibikali wake/maadili kazini
      • Falsafa yake ya maisha
      • Changamoto alizopitia
      • Ruwaza/maazimio yake
        Lugha – mtahiniwa atumie nafsi ya kwanza
        Usemi taarifa
        Lugha rasmi itumiwe
  2. Wananchi ndoo wa kulaumiwa kufuatana na kuzorota kwa usalama nchini Kenya . Jadili
    Kuunga
    • Chuki na uhasama baina ya makabila/vita vya kikabila
    • Uundaji wa kivikundi haramu vya vijana
    • Tamma ya kutajirika km; wizi wa mifugo
    • Wachochole kuingilia uhalifu kwa madai ya kujitafutia
    • Wananchi kukataa kufichua wahalifu miongoni mwano/wanawaficha
    • Umiliki wa silaha hatari na baadhi ya wananchi
    • Mitazamo hasi ya wananchi kuhusu maafisa wa usalama/hawashirikiani nao
      Kupinga
    • Usalama umekoseshwa na kutokuwepo kwa nafasi za kazi/wasio na kazi hulazimika kuingilia uhalifu ili wapate ajira
    • Uhaba wa pesa za kuendeleza uimarishaji wa usalama.
    • Idadi ndogo ya maafisa wa usalama
    • Vifaa vya kuendeleza shughuli za usalama mf. Magari , silaha havitoshi.
    • Kiwango cha chini cha mafunzo kwa walinda usalama
    • Magaidi wanaotatiza usalama nchini kutoka nchi za kigeni
      Tanbihi
    • Mtahiniwa asiwe na hoja chini ya saba
    • Hoja zote zijadiliwe kikamilifu
    • Mtahiniwa anaweza kuwa na idadi sawa na hoja katika pande zote, almuradi aonyeshe msimamo wake
    • Akishughulikia upande mmjoa tu bila kugusia upande wa pili asipite kiwango cha C+
    • Zingatia hoja zozote nyingine mwafaka
  3. Baniani mbaya kiatu chake dawa
    Maana
    Kiatu cha baniani - Kitu au watu ambao umewachukia au kudharau
    Dawa - Kitu au watu husika huenda wakawa ndio jibu au jawabu au suluhu kwa tatizo fulani maishani mwa mtu au katika jamii
    Tanbihi
    • Mtahiniwa aandike kisa kuthibitisha matumizi haya ya methali
    • Pande zote za methali zishungulikiwe. Anayeshughulikia upande mmoja asipate zaidi ya alama C – 08/20
    • Anayekosa kulenga katika kisa chake amepotoka kimaudhui alam D -03/20
  4. Mtahiniwa lazima atunge kisa kitakachoafiki mdokezo huo. Kisa lazima kionyeshe kujitolea kafara(kujitolea kwa vyovyote licha ya vikwamizo) na kuzaa natija (kufaidika) kisa cha mtahiniwa kinaweza kuafiki hali zifuatazo
    • Safarini anayejitolea kuwanusuru wengine wakati chombo au gari lilikuwa linaenda mrama.
    • Kiongozi wa wafanyakazi kuwatetea wnzake licha ya pingamizi kutoka kwa mwajiri hatimaye hali yao ya kufanya kazi inaboreshwa.
    • Yeye akiwa mtoto aliyeajiriwa kuwasaidia ndugu zake na wazazi wakafaidika.Singatia hali nyingine zinazoafikiana na dondoo
      Tanbihi
    • Akikosa kumalizia kwa dondoo alilopewa lakini kisa kiafikiane nalo, amepungukiwa kimtindo
    • Akiongezea maneno baada ya dondoo au katikati achukuliwe kuwa ana upungufu wa kimtindo
    • Lazima kisa kimhusu yeye mwenyewe. Asipojihusisha amepotoka kimaudhui na atuzwe D – 03/20
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Momaliche Joint Pre Mock Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest