Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Bunamfan Cluster Pre Mock Exam 2022

Share via Whatsapp

Maagizo

  • Andika insha mbili.
  • Insha ya kwanza ni ya lazima
  • Kisha chagua insha nyingine kutoka tatu zilizobakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400
  • Kila insha ina alama 20


Maswali 

  1. Wewe ni chifu wa Kata ya Mwangaza. Umeandaa mkutano wa wanakata wako. Andika hotuba utakayo toa kuhusu mambo yanayoathiri utangamano wa kitaifa na hatua zinazoweza kuchukuliwa.
  2. Fafanua hatua ambazo zimechukuliwa nchini ili kukabiliana na tatizo la unyanyasaji wa jinsia ya kike.
  3. Andika insha itakayo dhihirisha maana ya methali hii.
    Ukicheza ujanani utalipa uzeeni
  4. Andika kisa kitakacho malizikia kwa maneno yafuatayo.
    ...sasa ninaelewa maneno yake kuhusu kufanya maamuzi ya busara. Sasa nimepata baraka za wazazi na ridhaa yakuishi pamoja.


Mwongozo wa Kusahihisha

  1. Wewe ni chifu wa kata ya Mwangaza. Umeandaa mkutano wa wanakata wako. Andika hotuba utakayotoa kuhusu mambo yanayoathiri utangamano wa kitaifa na hatua zinazoweza kuchukuliwa.
    • JIBU
      • Hii ni insha ya kiuamilifu
      • kichwa kionyeshe; mada na hadhira lengwa
        Neno hotuba sharti liwepo
    • UTANGULIZI
      1. Huanza kwa kutaja watu kwa vyeo vyao na majina yao rasmi.
      2. Aliye na cheo cha juu zaidi hutambuliwa kwanza ukielekea chini/itifaki izingatiwe.
      3. Hufuatiwa na maamkuzi
      4. Baadaye lengo la hotuba yenyewe.
    • MWILI
      1. Ndicho kiina cha hotuba
      2. Huanza katika aya ya pili
      3. Kila hoja hufafanuliwa katika aya yake.
      4. Ili hoja ya mtahiniwa ikamilike lazima mwanafunzi azingatie hatua zifuatazo:
      5. Ataje hoja,aieleze na ataje hatua zinazoweza kuchukuliwa kusuluhisha mambo yanayoathiri utangamano wa taifa(katika aya moja).
    • HOJA
      MAMBO YANAYOATHIRI UTANGAMANO WA KITAIFA
      1. Ufisadi kama vile kuajiri watu kwa mapendeleo
      2. Ukabila
      3. Viongozi kueneza chuki/uchochezi
      4. Mafunzo hasi ya kidini/
      5. Ukosefu wa ajira/utabaka
      6. Kubagua maeneo Fulani kimaendeleo.
      7. Ukimbizi wa ndani kwa ndani
      8. Mashambulizi ya kigaidi/kikoo/kijamii
      9. Migogoro ya ardhi/mipaka ya kijamii
    • Hatua zinazofaa kuchukuliwa
      1. Lugha ya taifa kuhimizwa
      2. Kukabiliana na ufisadi
      3. Usawa katika ugawaji wa raslimali
      4. Kuelimisha kuhusu umoja wa kitaifa/hamasisho
      5. Tamasha za kitamaduni
      6. Kutalii sehemu zingine za nchi
      7. Ndoa za makabila tofauti/ndoa za mseto
      8. Serikali ya muungano
      9. Viongozi wachochezi kuchukuliwa hatua kisheria
    • HITIMISHO
      Hatibu kuwashukuru wote waliohudhuria kwa muda wao na utulivu wao wakati wa kumsikiliza.
    • TANBIHI
      1. Alama za mtajo hazitumiki
      2. Hoja zisipungue nane
  2. Fafanua hatua ambazo zimechukuliwa nchini ili kukabiliana na tatizo la unyanyasaji wa jinsia ya kike.
    • HOJA
      1. Hatua kali za kisheria kwa wanaowapiga na kuwabaka, na wanaotekeleza mila ya kuketa na ndoa za mapema
      2. Kufanya kampeni dhidi ya mila zinazochangia udunishaji wa wanawake
      3. Kuwashauri watoto wa kike waende shuleni
      4. Kuanzisha makao ya watoto wa kike wanaotishiwa na mila mbaya
      5. Kuelimisha mwanamke kuhusu haki zake
      6. Kuhimiza wanawake kupigania haki zao
      7. Serikali kutenga pesa za kuelimisha watoto wa kike
      8. Kuwepo kwa mashirika ya kutetea haki za wanawake kama FIDA na maendeleo ya wanawake.
      9. Hazina ya kutoa mikopo kwa wanawake kama K.W.F.T
      10. Kuwapa wanawake nafasi sawa za ajira
      11. Kutekelezwa kwa kipengele cha thuluthi mbili ya wanawake katika uongozi
      12. Kupunguza alama ambazo wasichana wanapaswa kufikisha ili kujiunga na vyuo vya elimu ya juu
      13. Kubuni sheria za kuwawezesha kumiliki mali
    • TANBIHI
      1. Kadiria hoja za mwanafunzi
      2. Ili hoja iwe kamili, mtahiniwa ataje hoja na aitolee maelezo katika aya moja.
  3. Andika insha itakayodhihirisha maana ya methali hii
    Ukicheza ujanani utalipa uzeeni.
    • MATUMIZI
      1. Hutumiwa kuwahimiza watu wajitahidi kujitengenezea maisha yao ya kesho/mustakabali wao wakiwa wangali na uwezo wa kufanya hivyo.
    • TANBIHI
      1. Mtahiniwa sharti aandike kisa kitakachodhihirisha maana ya methali
      2. Kichwa kionyeshe pande mbili za methali:
        • kucheza ujanani
        • kulipa uzeeni
      3. Mtahiniwa atakayerejelea upande mmoja atakuwa amepungukiwa kimaudhui. Insha yake isizidi alama 10
      4. Atakayeandika kisa kisichohusiana na methali hii atakuwa amepotoka kimaudhui. Atuzwe alama 03.
      5. Atakayejitungia swali na kulijibu atuzwe BK 01
      6. Dhana ya kulipa uzeeni ijitokeze hata kama ni kwa aya chache/sentensi chache.
      7. Andika kisa kitakachomalizikia kwa maneno yafuatayo. ...sasa ninaelewa maneno yake kuhusu kufanya maamuzi ya hekima au busara.Sasa nimepata baraka za wazazi na ridhaa ya kuishi pamoja.
    • MAJIBU
      1. Hii ni insha ya mdokezo
      2. Mtahiniwa ajihusishe na kisa (nafsi ya kwanza)
      3. mtahiniwa amhusishe pia aliyempa wosia(nafsi ya tatu)
      4. Ruwaza ya kisa idhihirike kwamba mhusika alikuwa amepotoka na kuvuruga uhusiano na wazazi wake LAKINI akapata mawaidha/mwelekeo/wosia kutoka kwa mhusika mwingine na uhusiano mwema ukarejeshwa baina yake na wazazi wake.
    • Baadhi ya visa ni;
      1. Mhusika anayetoroka nyumbani kwa kukosana na wazazi ,apewe ushauri kisha aamue kurudi kuomba msamaha na kuendeleza maisha pamoja na wazazi wake.
      2. Mhusika anayetamauka kimasomo kwa sababu fulani .Jambo hili livuruge uhusiano na wazazi wake ,apewe ushauri na mwalimu au mwanafunzi mwenzake, asome afaulu na kufurahisha wazazi wake.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Bunamfan Cluster Pre Mock Exam 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest