- SWALI LA LAZIMA
- Eleza miviiga katika fasihi simulizi. (alama2)
- Fafanua sifa tano za miviga. (alama 5)
- Wewe ni mwigizaji wa michezo ya jukwaani, eleza mambo matano ambayo utazingatia ili kufanikisha uigizaji wako. (alama 5)
- Unaniuia kutumia mbinu ya maandishi kukusanya na kuhifathi habari kuhusu miviga ya tohara,
- Eleze manufaa ya kutumia mbinu hii? (alama 4)
- Eleza udhaifu wa kutumia mbinu hii? (alam4)
SEHEMU YA B
(MAPAMBAZUKO YA MACHWEO NA HADITHI ZINGINEZO
HADITHI YA FADHILA ZA PUNDA – ALAMA 20
- ''Nitapata wapi mwandani kama mkee wangu marehemu?“
- Eleza mukthatha wa dondoo hiili ? (alama 4)
- Fafanua sifa tatu za msemaji. (alama 6)
- Tambua na ufafanue maudhui mawili yanayojitokeza katika dondoo hili. (alama 4)
- Fafanua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa kwenye dondo hili. (alama 2)
- Eleza masaibu yanayomkumba Lilia katika hadithi hii. (alama 4)
AU
- Kwa kuzingatia hadithi zifuatazo eleza namna maudhui ya unyanyasaji yanavyojitokeza (alama 20)
- Fadhila za Punda
- Sabina
- Nipe Nafasi
- Pupa
- Toba ya Kalia
SEHEMU YA C
TAMTHILIA YA BEMBEA YA MAISHA
- Ni mshtuko wa namna Fulani unaotokana na mtu kukabiliwa na hali ya maisha ya watu wengine ambayo inapingana na ile yake.
- Eleza muktadha wa dondoo hili? (alama 4)
- Eleza namna ambavyo msemewa wa dondoo hili anavyojenga maudhui ya nafasi ya mwanamke. (alama 6)
- Onyesha namna maudhui ya ubabe dume yanavyodhihirika katika tamthilia hii. (alama 10)
AU
- Kwa kurejelea tamthilia hii eleza namna mila na destruri zinavyoweza kuzua migogoro katika jamii. (alama 20)
SEHEMU YA D
RIWAYA YA CHOZI LA HERI
- Eleza namna wahusika mbali mbali walivyokabiliana na changamoto zilizowakumba riwayani. (alama 20)
AU - Binadamu aliumbwa kupambana na ulimwengu na kutumia rasilimali za Mungu kuyaboresha maisha yake.
- Eleza muktadha wa dondoo hili? (alama 4)
- Eleza umuhimu ya msemaji kwa kuijenga riwaya ya Chozi la Heri. (alama 4)
- Eleza ukitoa mifano riwayani namna binadamu anavyotumia rasimali anayopewa na Mungu kuyaboresha maisha yake. (alama 6)
- Kwa kutoa mifano riwayani, eleza namna ukiukaji wa haki za watoto ulivyojitokeza. (alama 6)
SEHEMU YA E
USHAIRI (ALAMA 20)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
SABUNI YA ROHO
- Ewe tunu ya mtima kwa nini wanikimbia?
Ndiwe suluhu za zama, waja wakumbilia,
Waja wanakutazama, madeni wakalipia,
Ndiwe sabuni ya roho,ndiwe mvunja mlima. - Ndiwe mafuta ya roho,walisema wa zamani,
Utanunua majoho, majumba na nyumbani,
Umezitakasa roho, umekuwa mhisani,
Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima. - Matajiri wanakujua, wema wako wameonja,
Nguo zao umefua, wakupata kwa ujanja,
Sura zao mefufua, wanazuru kila Nyanja,
Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima. - Ndiwe mvunja mlima, onana na maskini,
Watazame mayatima, kwao kumekuwa duni,
Wabebe waliokuwa wainue walio chini,
Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima. - Ndiwe mvunja mlima, wapi kapata uwezo,
Umezua uhasama waja kupata mizozo,
Ndiwe chanzo cha zahama, umewatia vikwazo,
Ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima. - Umevunja usuhuba, familia zazozana,
Walokuwa mahabuba kila mara magombana,
Roko zao umekaba, manyumbani wachinjana,
Ndiwe sabuni ya roho ndive mvunja mlima. - Nakutafuta kwa hamu sabuni unirehemu,
Sinilipue ja bomu, sije kawa marehemu,
Niondoe jehanamu, ya ufukara wa simu,
Ndiwe sabuni ya roho ndiwe mvunja mlima - Naondoka wangu moyo, nikwitapo itika,
Fulusi wacha uchoyo, tatua walonifika
Nichekeshe kibogoyo, nami nipate kuwika
Ndiwe sabuni ya roho ndiwe mvunja mlima.
MASWALI- Tambua na udhibitishe nafsi neni katika shairi hili? (alama 2)
- Kwa hoja nne eleza muundo wa shairi hili. (alama 4)
- Tambua uhuru wa kishairi unaojitokeza katika shairi hili. (alama 2)
- Mshairi atatumia mbinu gani za lugha katika shairi lake. (alama 3)
- Tambua bahari zozote tatu zinazojitokeza katika shairi. (alama 3)
- Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
- Andika ubeti wa tatu kwa lugha nathari. (alama 4)
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
- FASIHI SIMULIZI
- Ni sherehe za kitamaduni zinazofanywa na jamii mbalimbali katika kipindi maalum xha mwaka. (Al 2)
-
- Huandamana na matendo au kanuni flani.
- Huongozwa na watu mahususi ambao huiendeleza.
- Huandamana na utoaji mawaidha.
- Maleba maalum huvaliwa na wanahusika ili kuwatofautisha.
- Shugli za miviga hufanywa m,ahali sherehe inapofanyiwa.
- Huambatana na utamaduni wa jamii husika. ( zozote 5 x 1 = 5)
-
- Kuwa mchangamfu na mcheshi.
- Kuhakikisha umefahamu utamaduni wa jamii husika.
- Kufahamu hadhira na mahitaji yake.
- Kutumia ufaraguzi.
- Kuwa na kumbukumbu nzuri.
- Kubadilisha kiimbo kulingana na mahitaji
- Kutumia viziada lugha k.v ishara za uso.
- Kushirikisha hadhira .
- Kutumia lugha kwa uhodari ili kuipa mvuto.
- Kuvalia maleba yanayooana na maigizo.
- Kujenga mlahaka mwema na hadhira. ( zozote 5 x 1 = 5)
-
- Si rahisi kwa data kusahaulika.
- Huweza kufikia vizazi vingi.
- Si ghali kama mbinu zingine.
- Si rahisi kufisidiwa au kupotea. ( zozote 4 x 1 = 4)
-
- Hayaonyeshi baadhi ya mambo kama kiimbo, toni na ishara.
- Si hai, hayawezi kwenda wala kusoma.
- Baadhi ya waandishi wanayohitaji kwa wakati mahususi.
- Huikwezesha fasihi simulizi taadhira asili (huondoa utangamano kati ya hadhira na fanani).
- MAPAMBAZUKO YA MACHWEO NA HADITHI ZINGINEZO
- Muktadha: Pastor Lee Imani
- Akijiwazia mwenyewe baada ya kupata shinikizo la mke mwingine baada ya kifo cha mkewe. Anaeleza kuwa kwa kuwa hayupo anayelingana na marehemu mkewe. (1x4)
-
- Mcha Mungu - anaanzisha na kuendeleza kanisa
- Mkarimu - anampa mamake Luka jira
- Mdasisi - anamwita Luka na kumuuliza nia yake kwa bintiye
- Mwenye mapenzi - alimpenda marehemu mkewe pia bintiye (Za kwanza 3 x 2 = 6)
Tanbihi- Kadiria majibu mengine ya mwanafunzi, maelezo ya sifa yao na sifa yenyewe.
- Akikosea msemaji katika (2a) asituzwe sehemu hii
-
- Ndoa na mapenzi
- Kifo/mauti (Za kwanza 2 x 2 = 4)
- alama 1 kutaja, 1 ufafanuzi wa kweli
-
- Swali balagha
- Tashibihi (Za kwanza 2)
- Atolee maelezo ya kila mbinu, asipoeleza asitozwe chochote
- Muktadha: Pastor Lee Imani
-
- FADHILA ZA PUNDA
- Lilia kushurutishwa kuacha kazi
- Lilia kupigwa na Luka kwa kosa la kutokeleza chumvi kwemnye chakula
- Lilia kukosa usingizi kwa kumgoja Luka ambaye haji
- Luka kumpiga Lilia kwa kosa la kumtembelea ofisini
- Luka kumyanyasa Lilia kwa kuwa na mpenzi mwingine
- Luka kumlazimisha Lilia kuanadmana naye kwenye kamepeni licha ya kuwa mjamzito ( zozote 4 x 1 = 4)
- SABINA
- Yunuke anamyanyasa Sabina kwa mumwachia kazi ya kuwachukua ng'ombe malishoni na kuwakama
- Yunuke kumlazimisha Sabina kupeleka kisonzo shambani kabla ya kwenda shuleni
- Sabina analazimika kuuza maziwa kwa soko la Itumbe kabla ya kwenda shuleni
- Babake kumakana baada ya kuzaliwa kwake Sabina
- Mjomba wake Ombati kutaka kumuoza mapema
- Yunuke kumyima Sabina fursa ya kudurusu akiwa nyumbani
- Yunuke kumyima Sabina ushirikiano na wanawe
- Yunuke kumtusi Sabina k.m anapomweleza kuwa amepokea barua ( zozote 4 x 1 = 4)
Kadira majibu mengine ya mwanafunzi
- NIPE NAFASI
- Mamake msimulizi ananyanyaswa kwa kutotumia pesa za mumewe
- Wazazi wa mumewe mamake msimulizi wananyanyasa mamake msimulizi kwa kuto sikiliza malalamishi yake kuhusu mumewe kuwa na mke mwingine
- Babake msimulizi kutumia pesa mkewe kupitia kwa nyanyake ambaye angeamua kumpa au kutompa
- Mamake msimulizi kulaimiwa kwa kifo cha mwanawe na ukoo wa bwanake ( zozote 4 x 1 = 4)
- PUPA
- Bi mtego anamyanyasa Mwakuona kwa kumdanganya kuwa angefadhiliwa kwa kukubali kufanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja.
- Wamiliki wa Chengaways wanawanyanasa wasichana kwa kuwaingiza katika ukahaba
- Mwakuona ananyayaswa kimapenzi na mwanamme mke kwenye chumba alichopelekwa kule Changeways.
- Wamiliki na walinzi wanawanyanyasa wasichana kwa kuwanyima uhuru wa kutembe. (Wanafungiwa baada ya kutoweka kwa Mwakuina. ( zozote 4 x 1 = 4)
Tanbihi: Mtahini akadilie hoja zingine.
- TOBA YA KALIA
- Bwana Kalia anamyanyasa Jack kwa kubadilisha ushindi wake kweny mashindano ya Sayansi na kumpa mwanawe Siri
- Wazazi wa Siri wanamyanyasa Jack kwa kutotimiza ahadi yao ya kumsomesha baada ya kifo cha wazazi wake
- Wazazi wa Siri wanamyanyasa Jack kwa kutaka awape nusu ya faida aliyopata katika biashara ya kuuza viatu.
- Jack ananyanyasawa kwa kupokonywa nafasi ya kupata ufadhili wa kupata masomo na familia ya Bi. Kalia na Bi. Mshewa
( zozote 4 x 1 = 4) Kadiria hoja zingine
- FADHILA ZA PUNDA
- TAMTHILIA YA BEMBEA YA MAISHA
- Msemaji - Asna
Msemewa - Sarah
Mahali - Hospitalini- Kiini - Alirejelea slivyoshangaa namna ambavyo Bunju alizingatia kushugulikia na familia yake, yeye mke na watoto bila kujali wengine/Alikuwa akitafsiri ujumbe wa '' culture shock'' kwa mamaye. ( zozote 4 x 1 = 4)
- Msemwa ni Sarah
- Anajenga maudhui ya uvumilivu
- Anaendeleza mila mna tamaduni
- Mwanamke ameajibika kulilinda jamii k.v kuwafunza wanawe
- Anashauri vyema k.v kwa wanawe
- Mwanamke anaonekana ndiye wa kudhulumiwa katika ndoa.
- Nafasi ya mwanamke ni jikoni na kumhudumia mumewe ( zozote 6 x 1 = 6)
Tanbihi- Kaadiria majibu mengine ya mwanafunzi
- Akikosea msemewa kwenye swali la (4b) asituzwe hapa
- Maudhui ya ubabedume
- Kazi za nyumbani ni za mama
- Mtoto wa kike kutoaminiwa k.v wananwe Sara kuonekana si muhimu
- Panapotokea tatizo la uzazi mama ndiye wa kulaumiwa k.v Sarah
- Mwanamke kumjuza mmewe kila kitu akifanyacho
- Maomo ya mtoto wa kiume kuthaminiwa ( zozote 5 x 2 = 10)
Tanbihi akadirie majibu ya mwanafunz9i
- Msemaji - Asna
- MILA NA DESTURI KUZUA MIGOGORO
- Mwanamke kutoruhusiwa kulala nyumbani kwa mwanawe wa kike aliyeolewa ; Mgogoro ni Bunju na Neema kutofautiana
- Mila ya kuwaamini watoto wa kiume kushinda wa kike - Yona anakuzwa na mgogoro wa nafsi na kuzama katika ulevi
- Kutothamini mtoto wa kike - Mgogor kati ya Yona na Sarah
- Mila inayomruhusu mwanamke kuwa ndiye wa kutekeleza majukumu ya nyumbani - Mgogoro kati ya Yona na Sarah, hasa Sarah anapokuwa mgonjwa.
- Mila inayomlazimisha mwanamke kumtegemea, kumheshimu na kuwa mnyenyekevu kwa mmewe - Neema nakubali pendekezo la Bunju katika kila hali jambo linalomkosesha amani.
- Mila inayopendekeza mtoto wa kike kuolewa anpoifika umri flani - Asha na mamake wanakosa kuelewana kwa hilo
- Mila ya kuhalalisha ulevi ( Luka anapozungumza na Beni na Yona - inaleta mgogoro baina ya Yona na Sarah (katika ndoa)
- Mila ya kumfunza mtoto wa kike kwa kuwa hana umuhimu (maelezo ya Luka) - Yona anakosa kujukumika kuwafunza wanawe.
- Mila kuwa mtoto mkubwa katika familia wa kiume ndiye anayestahili kumtunza mamake - Neema na Bunju wanazozana wakati Neema alipopendekeza kumhifadhi mamake. ( zozote 10 x 2 = 10)
Tanbihi- Mtahini akadirie majibu mengine
- Mtahiniwa lazima lenge pande zote mbili nkatika maelezo yake la sivyo, asituzwe chochote.
- CHOZI LA HERI
- Langa kiriri anapata dhiki ya kupoteza kazi katika Shirika la Maghala ya nafaka anaamua kufanya kazi ya ukulima
- Baada ya Umu kuwapoteza ndugu zake Dick na Mwaliko anaamua kwenda kupiga ripoti katika kituo cha polisi ili kupata usaidizi
- Petu alipopata hedhi yake ya kwanza aliamua kumjulisha bibiye ambaye anamtafutia tambara la blanketi kama sodo.
- Baada ya Sauna kuhujiwa kimapenzi na Bw. Moya, anaamua kutoka nyumbani kwao na kutamba katika ulimwengu.
- Kutokana na adhabu ambayo Dick angepewa na mwajiri wake, Buda anaamua kuingilia ulanguzi wa dawa za kulevya
- Chandachema anaamua kuwasimulia kina Zohali, Umu na Mwanaheri ili kupunguza mlemeo wa matazio yake.
- Chandachema anaondoka kwa jirani katini baada ya Satua mke wa jirani wake kuanza kumwona mzigo.
- Zohali anapigana na majitu yaliyotaka kumhujumu utu wake na kumyanyasa kimapenzi
- Baada ya mkewe Mwangeka, Lily kuaga dunia, Mwangeka anaamua kumuua Apondi ambaye amziba pengo hilo.
- Neema na Mwangeka kw akukosa mtoto wanaamua kumpanga Mwaliko
- Mzee Mwimo Msubili baada ya ardhi yake kuwa ndogo kustahimili familia yake kubwa anaamua kuwahamish awake zake wawili wa mwisho katika msitu wa Heri.
- Mamake Sauna anaamua kuavya mimba ili kujieupusha na aibu ambayo ingewakumba katika familia.
- Sauna aliamua kuingilia ulanguzi wa watoto ili apate pato la kujikimu kimaisha.
- Shomsi baada ya yote aliyoyapitia anaamua kuingilia unywaji wa pombe ili kupunguza mawazo
- Baada ya mwanawe Mwangeka, Becky kuaga anaamua kumpanga Umu ili kuziba pengo.
- Kutokana na upweke ambao Umu alikua nao katika mlima wa Simba anaamua kuondoka nyumbani kwano na kwenda kuanza maisha upya
- Baada ya Neema kukuiokota kitoto ambacho hakijui anachukua anachukua hatua moja kwa moja mpaka kituo cha polisi na kisha kituo cha Benefactor.
- Baada ya Ridhaa Kurejea nyumbani kwa kuitwa mfwata mvua, mamake anamrudisha shuleni na kuzungumza na mwalimu.
- Kutokana na yale amabayo Zohali alifanyiwa na wazizi wake k.v. Kusimwaga anaamua kumdanganya mtawa Packa kwamba ni yatima
- Kutokana na msongo wa mawazo wa Umu kwa kukosa wazazi anaamua kumwelekeza mwalimu ambaye anamtafutia wafadhili
- Kutokana na ukosefu wa karo mamaye mamaye Kairu anaamya kuongea na mwalimu mkuu ili kumlipia karo kidogo kidogo
- Kutokana na mawazo yake kuwa biashara yake ni uovu, Dick anaamua kuanzisha bisahra ya kuuza electroniki.
- Pete anapoona kuwa anaenda kuwa na watoto watatu kwa umri wake mdogo, anaamua kujitoa uhai yeye pamoja na katoto chake.
- Kutokana na hali duni ya maisha vyuoni, wanafunzi wanaamua kujihusisha katika unywaji wa pombe haramu.
- Tuama aliamua kupashwa tohara ili asitengwe na wenzake (zozote 20, 1x 1)
Tanbihi- Lazima mtahiniwa azungumzie kuhusu tatizo kisha mbinu aliyotumia kujinasu, la sivyo asituzwe chochote.
-
-
- Maneno ya Chandachema
- Akisimulia wenzake - Umu, Mwanaheri na Zohali
- Wako aktika shule ya upili ya Tangamano
- Chandachema anawasimulia wenzake dhiki alizopitia maishani mwake tangu utotoni
- Msemaji; Chandachema
- Anawanjenga wahusika wengine; sifa ya Fumba (babake)
- Swala la ukiukaji wa haki za watoto limejitokeza
- Anaendeleza ploti ya riwaya
- Anaibua swala la umaskini, anaajiriwa akiwa umri mdogo (1x1 = 4)
Akikosea msemaji katika (7a), asitozwe chochote katika sehemu hii.
-
- Watoto wanatafuta kazi wakiwa umri mdogo ili kuyakidhi mahitaji yao - Chandachema
- Watoto wanatumia kidogo walichonacho kuyanusuru maisha yao - Dick kuanzisha biashara ya electroniki
- Kutia bidii katika biashara waliyonayo ili kukidhi mahitaji - Mamake Kairu
- Kutia bidii masomoni ili kuyaboresha maisha - Umu
- Ridhaa kujenga kituo cha afya cha Mwazno mpya ili kuendeleza huduma za matibabu
- Pete kaujiriwa kwenye kiwanda cha sare licha ya kupata mshahara duni anaita bidii awalishe watoto wake (zozote 6)
-
- Watoto wanaajiriwa wakiwa umri mdogo - Chandachema
- Watoto wanatumiwa vibaya na watu kuendelesha biashara zao - Dick
- Watoto kuibiwa na kutekwa na kuuzwa. Sauna kuiba Dick na Mwaliko
- Watoto wanaachiwa maleiz na wazazi wao - Naomi anawaachia wanawe malezi anapowatoroka na mumewe
- Watoto wanaingizwa bishara haramu - Sauna na Bi. Knagara
- Watoto wanatishiwa na watuw wakubwa - Dick anatishiwa na Buda.
- Watoto wanaozaliwa kutupwa - kitoto kilichookotwa na Neema
- Watoto kuuwawa bila hatia - Lemi kusingiziwa wizi.
- Watoto kubakwa - Lemi na Mwanaheri (zozote 6 1 x 1)
Kadiria majibu mengine ya mtahiniwa
-
- USHAIRI
- Makini/Mhitaji - ubet 7, msh. 3 (1 x 2)
-
- Lina beti nane
- Kila beti una mishororo 4
- Kila mshororo umegwawa viapnde viwili
- Kila pande kina mziani 8
- Shairi lina kibwagizo ( zozote 4 x 1 = 4)
-
- Kuboronya sarufi/kubananga - mfano, madeni wakalipa, naondoka wangu moyo n.k
- Inkisari - sura za mefufua
- Vikule - mtima (zozote 2 x 1)
-
- Swali la balagha - Kwa nini wanikimbia?
- Tashbihi - Sinilipue ja bomu
- Tashhisi/uhuishi - Fuusi wacha uchoyo (zozote 3 x1)
-
- Tarbia - mishororo minee katika kila ubeti
- Ukaraguni - Vina tofauti kwa kila ubeti
- Pindu - Mshororo wa mwisho ubeti wa nne, kiande cha mwisho kinatumiwa kaunzia mshororo wa kwanza ubeti wa tano
- Sakarani - Lina bahari zaidi ya moja (za kwanza 3 x 1)
- Toni ya kushawishi/kusihi
(ataje kuthibitisha) - Wakwasi wanakutambua kwa sababu wameona uzuri wako. Umewangarisha na waatumia njia nyingi za kupata. Wanafurahia kutembea kila sehemu. Unapendeza roho na kufanikisha chochote.
Download Kiswahili Paper 3 Questions and Answers - Lugari Constituency Joint Pre Mock Exams 2023.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students