0 votes
4.5k views
in Chozi la Heri by
  1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
  2. Eleza namna msemaji alivyoukata mkono aliostahili kuubusu. (alama 6)
  3. Eleza tamathali ya usemi unaojitokeza katika dondoo hili. (alama 2)
  4. Fafanua sifa nne za msemaji wa kauli hii. (alama 8)

2 Answers

0 votes
by
edited by
  1. Kuukata mkono uk 70-71
  2. Anapokuwa mkurugenzi katika shirika la uzalishaji nafaka, Lunga anapinga kuagizwa kwa nafaka ambayo yalihofiwa kuharibika na hayangefaa kwa matumizi ya binadamu.
  3. Jazanda - Kuukata mkono aliostahili kuubusu - kuwapinga wakubwa wake.
0 votes
by
edited by

4.  

  • Mwenye Msimamo Dhabiti: anakataa kushawishika na wakubwa wake kukubali uuzaji wa mahindi yaliyohofiwa kuharibika Mwenye bidii: asifika kwa uhodari wake wa ukulima. Amepandikwa jina mkulima namba wani Uk 70
  • Mwajibikaji: anawajibika kutetea umma dhidhi ya kuuziwa mahindi yaliyokuwa yameharibika na mabayo ni sumu kwa Binadamu
  • Mwenye tamaa: anapooana zao la mahindi katika msitu wa mamba, anaghairi nia ya kuhamisha babake asishiriki uharibivu wa mstitu na kuanza ukulima katika msitu wenyewe.
  • Jasiri:anaamua kutetea umma japo anafahamu fika kuwa ni sawia na kuukata mkono aliostahili kuubusu na kuwa angefutwa kazi wakati wowote
  • Mpenda haki: anatoa mhanga kutetea maslahi ya wanyonge jambo linalosababisha afutwe kazi.
  • Mwenye busara:anatoa ushauri kuwa raia wanastahili kufunzwa jinsi ya kutuia ardhi kwa njia endelevu (uk.71)
  • Mwanaharakati wa mazingira: aawali anapofika katika msitu wa mamba,anataka kuhamisha babake kwani anaona ni Edeni pa wanyamapori na si vizuri kuuharibu
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...