Thursday, 09 March 2023 13:54

KISWAHILI Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 1 2023 Set 4

Share via Whatsapp

 Soma kifungu kifuatacho na ujaze nafasi zilizoachwa.

Mama Rehema alienda sokoni kununua nyama na kusaga mahindi,         1         kwenye         2           aliuweka mkoba wake chini. Alijiunga na wanunuzi wengine, ili apimiwe nyama kwa         3          .Alilipa          4        kidogo na akaelekea kusaga mahindi

1. A.Walipofika    B. Watapofika    C. Alifika     D. Zilifika  
 2. A. buchari    B. hospitali    C. jikoni    D. shambani  
 3. A. kipimio   B. ratili     C.meza     D. kinu  
 4. A. vikombe    B. sarufi   C. pesa    D. mapeni  

Jaza kwa kutumia kihusishi sahihi.

  1. Paka yuko               mti
    GD4ST4KISW5
    1.  ndani ya 
    2. juu ya
    3.  kando ya
    4. chini ya . 
  2. GD4ST4KISW6
     kikombe kiko                 meza
    1. juu ya
    2. chini ya 
    3. mbele ya 
    4. ndani ya
  3. GD4ST4KISW7
    maji yamo                   bilauri
    1. mbele ya
    2. ndani ya 
    3. kati ya 
    4. juu ya 
  4. Rangi za bendera ni nyekundu, nyeusi, kijani kibichi na                  
    1. nyeupe 
    2. samawati 
    3. zambarau
    4. hudhurungi 

Chaqua jawabu sahihi kujaza nafasi

  1. Kiatu                    ni kizuri.
    1. hiki
    2. hili
    3. hizi
    4. huyu
  2. Nyumba                   inapendeza
    1. wao
    2.  lao
    3. yao
    4. hao
  3. Wazazi                   wameingia sasa.
    1. yenu
    2. zenu
    3.  lenu
    4. wenu
  4. Nguo                      zilifuliwa na mama.
    1. yao
    2. zao
    3. wao
    4. lao
  5. Matunda                   yameiva yote.
    1. hawa
    2.  huu
    3. hili
    4. haya
  6. Ni ndege yupi hapatikani mwituni?
    1. Kasuku
    2. Kuku
    3. Chiriku
    4. Mbayuwayu
  7. Kifaa hiki huitwa:-
    GD4ST4KISW15
    1. shoka
    2. plau
    3. bendera 
    4. jembe
  8. Kifaa ambacho hutumika kufyeka nyasi huitwa:-
    1. reki
    2. jembe
    3. kifyekeo
    4. plau

Andika kinyume cha neno lililopigwa mstari

  1. Wasichana walipanga viti vizuri.
    1.  watapanga
    2. walipangua
    3. walipenda
    4. watapangua
  2. Mtoto atalia baada ya kuachwa.
    1. atalala
    2. atacheza
    3. atasheka
    4. atacheka
  3. Mama ataingia.
    1. ataenda
    2. atatoka
    3.  atakimbia
    4. atakaa
  4. Yaya hutandika kitanda chake.
    1. hutanfua 
    2. hutenda
    3. hupanga
    4. hulala
  5. Kaka alianika nguo zake.
    1.  hutandua
    2. alianua
    3. alichukua
    4. alichezea

Andika jibu sahihi

  1.  Pahali ambapo pesa huhifadhiwa ni:-
    1. benki
    2. soko 
    3. kanisani
    4. dukani

Kanusha vitenzi vifuatavyo

  1. Alicheza
    1. atacheza
    2. hatacheza
    3. hakucheza
    4. halichezi
  2.  hutibu
    1. anatibu
    2.  hakutibu
    3. hatibi
    4. hatibu
  3. Alisoma
    1.  hakusoma
    2. anasoma
    3. atasoma
    4. anasoma
  4. Atakaa
    1.  halikaa
    2. hatakaa
    3. hakai
    4. hakukaa

Andika vifungu hivi kwa wingi.

  1.  Ua hili
    1. nyua hii
    2. maua hii
    3. maua haya
    4. ua haya
  2. Kiberiti hiki
    1. viberiti hivi
    2. viberiti hii
    3. kiberiti hivi
    4. viberiti hawa
  3. Nyumba hii
    1. nyumba hii
    2. nyumba hiyo
    3. nyumba hizi
    4. nyumba hiyo
  4. Kiota hiki
    1. viota hawa
    2. viota hivo
    3. viota hivi 
    4. viota hili

Soma hadithi kisha ujibu maswali yafuatayo.

Teknolojia ya kisasa imetuwezesha kuweka pesa kwenye simu. Huna haja ya kubeba pesa mfukoni unapoenda dukani. Unaweza kulipia bidhaa dukani kwa njia ya simu. Unaweza kufanya hivyo wakati wowote na mahali popote. Wanaotumia teknolojia hii hufanya mambo mengi zaidi kuliko walio na pesa taslimu. Kuna baadhi ya huduma zinazoweza kununuliwa kwa kutumia pesa kwenye simu.

  1. Je, teknolojia ya kisasa imetuwezesha kufanya nini kulingana na hadithi?
    1.  Kuweka pesa kwenye simu 
    2. Kuchora kwa simu
    3. Kupiga picha 
    4. Kufanya hesabu
  2. Ni njia gani inaweza tumika kulipia pesa?
    1. ya benki 
    2. ya kukopa 
    3. njia ya sim
    4. kubadilishana bidhaa
  3. Kuna faida gani kulipa pesa kwa kutumia simu?
    1. Mtu hafanyi jambo lolote 
    2. Mtu hufanya mambo mengi 
    3. Mtu hufanya mambo kidogo
    4. Mtu hasaidiki

Soma hadithi kisha ujibu maswali yafuatayo.

Nyanyiro alikuwa mvuvi aliyeishi karibu na soko la sokomoko. Alifanya kazi yake ya uvuvi kwa bidii. Asubuhi na mapema aliamka na kwenda mtoni. Pale mtoni palikuwa na aina mbalimbali ya samaki kama vile ngege na mkunga. Nyanyiro alivua samaki kila siku na mara nyingine alipenda kunadi samaki wake kwa kupaza sauti.

  1. Je, nyanyiro alikuwa anafanya kazi gani?
    1. Mpishi
    2. Mvuvi 
    3.  Msusi
    4. Mlevi
  2. Je, Nyanyiro alienda mtoni saa ngapi?
    1. Asubuhi na mapema
    2. Jioni
    3. Usiku
    4. Alasiri
  3. Samaki wale walipatikana mtoni ni kama:
    1. mbayuwayu
    2. njiwa
    3. mkunga
    4. kasuku
  4. Nyanyiro aliwauza samaki wake kwa:-
    1. kupeana
    2. kunadi
    3. kukopesha
    4. kimoyomoyo
  5. Kazi ya Nyanyiro ilikuwa ya:- 
    1. uvuvi 
    2. uvivu
    3. ualimu
    4. ukulima
  6. Ni mnyama yupi hapatikani nyumbani?
    1. Kondoo
    2. Ndovu
    3. Kima
    4.  Paka
  7. Samaki huishi:-
    1. ardhini
    2. mtini
    3. mwituni
    4. majini

KUSIKILIZA NA KUZUNGUMZA

Mwalimu amwamkue mwanafunzi, Habari yako?

(Mwanafunzi ajibu)

Mwalimu amtayarishe mwanafunzi kujibu maswali kuhusu vitendawili.

(Mwanafunzi azitegue)

  1. Huku ng'o kule ng'o
  2. Askari mlangoni
  3. Kisima changu hakitindiki maji
  4. Kamba yangu ndefu lakini haifungi kuni
  5. huku mwamba kule mwamba
  6. Nyumba yangu ina mlango mdogo
  7. Juu ya mlima kuna msitu mweusi

KUSOMA

Soma kifungu kifuatacho kwa sauti huku ukizingatia matamshi bora

Soko la mwembeni lililoko kwenye Kaunti ya Kwale lina bidhaa nyingi. Kuna sehemu zilizotengwa kulingana na bidhaa zinazouzwa. Kuna vibanda vya kuuzia matunda, nyama, nguo na mboga. Wafanyabiashara hupanga na kulinda bidhaa hizo kwa uangalifu mkubwa utafikiri ni kuku anayelinda kifaranga wake ndani ya kizimba. Wafanyabiashara hukata leseni na kupewa risiti. Bila leseni, huwezi kunadi au kuuza bidhaa zozote. Watu wa kila rika huja sokoni kwa sababu mbalimbali. Wengine huja kuuza na kununua bidhaa. Wengine huja kutazama bei za bidhaa. Wengine huja kwa matembezi na kujistarehesha tu. Wengine hawana sababu.

ANDIKA INSHA YA KUSISIMUA KUHUSU

RAFIKI NIMPENDAYE



MWONGOZO 

  1. C
  2. A
  3. B
  4. B
  5. C
  6. A
  7. B
  8. A
  9. A
  10. C
  11. D
  12. B
  13. D
  14. B
  15. A
  16. C
  17. B
  18. D
  19. B
  20. A
  21. B
  22. A
  23. C
  24. B
  25. A
  26. D
  27. C
  28. A
  29. C
  30. C
  31. A
  32. C
  33. B
  34. B
  35. A
  36. C
  37. B
  38. A
  39. B
  40. D
Join our whatsapp group for latest updates

Download KISWAHILI Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 1 2023 Set 4.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students