0 votes
14.2k views
in Sarufi na Matumizi ya Lugha by
Fafanua nadharia zozote mbili zinazoeleza kuhusu chimbuko la lugha ya Kiswahili.

1 Answer

0 votes
by
  1. Kiswahili ni lugha ya Kiarabu- wageni wa mwanzo wa pwani ya Afrika Mashariki walikuwa ni waarabu ambao waliwaoa wanawake wenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki. Wazawa wa ndoa hii walizungumza lugha iliyokuwa na msamiati wa kiarabu na hivyo baadhi ya wachunguzi wa lugha wakahusisha asili ya Kiswahili na Uarabuni.
  2. Kiswahili ni lugha mseto- Kutokana na maingiliano ya wenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki waliozungumza Kiswahili na wageni kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni, lugha ya wenyeji iliweza kukopa msamiati wa wageni hao mbalimbali na hivyo baadhi ya wachunguzi wa lugha wakadai kuwa Kiswahili ni lugha mseto. 
  3. Kiswahili ni lugha ya kibantu- Hii ndiyo nadharia inayoelekea kuwa ya ukweli. Hii ni kwa sababu uchunguzi wa kiisimu uliofanywa na baadhi ya wanisimu umethibitisha kuwa upo mshabaha mkubwa baina ya majina ya lugha ya Kiswahili na yale ya lugha nyingi za kibantu. Aidha utaratibu wa kupanga nomino katika makundi ya ngeli zake hufafana na ule unaotumiwa na lugha nyingi za kibantu.
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...