0 votes
1.2k views
in Chozi la Heri by

“ Kwa kweli ni hali ngumu hii”

  1. Weka dondoo katika muktadha wake. 
  2. Ni hali gani yamsemewa inayorejelewa kwenye dondoo.

1 Answer

0 votes
by
  1. Weka dondoo katika muktadha wake. 
    • Mzungumzaji ni Ridhaa
    • Anayezungumziwa ni Kaizari
    • Ni katika kambi/mabanda- Kwenye Msitu wa Mamba
    • Ni baada ya Kaizari kumsimulia Ridhaa magumu aliyoyapitia kutoka kwake nyumbani hadi kujipata kweye hali nyingine ngumu katika kambi.
       
  2. Ni hali gani yamsemewa inayorejelewa kwenye dondoo. 
    • Mke wa Kaizari, Subira ananyakwa kofi kubwa
    • Anarejelewa kama kidume kijoga-kudharauliwa
    • Mke wake anakatwa kwa sime na kuzirai kwa uchungu
    • Bintize –Lime na Mwanaheri- wanafanyiwa unyama na mabarobaro
    • Jirani yake Tulia anamfukuza anapojaribu kuwapa mke wake na watoto huduma za kwanza
    • Wanawe wanazirai ubavuni mwake
    • Anaabiri gari bila kujua waendako na jamaa zake
    • Walitazama mabasi yakichomwa kwenye safari iliyokuwa ndefu
    • Gari linaisha petroli- wanajitoma msituni
    • Wanakula mate usiku wa kwanza kutokana na ugeni/ukosefu wa chakula
    • Kuna hali mbaya ya baridi na umande wa asubuhi
    • Wanakosa maji safi ya kunywa kwenye msitu
    • Kunywa maji ya Mto wa Mamba kunawasababishia homa ya tumbo.
    • Vijumba vichache havikutosha kuhimili idadi ya wakimbizi
    • Huduma za kijamii zinaadimika –ukosefu wa misala na misala ya kupeperushwa
    • Sandarusi za kutumiwa kama misala zilitafutwa mbali kwenye milima ya taka.
    • Roho za watoto zilibwakurwa na magarimoshi kwenye reli walipoenda haja kule
    • Kuna hali ya njaa na vilio vya watoto wenye njaa
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...