0 votes
6.8k views
in Fasihi by
Linganisha naulinganue vitendawili na methali.

1 Answer

0 votes
by
 

MFANANO

 
  • Zote ni tungo fupi za semi
  • Zote huwa na maana fiche
  • Zote hutumia lugha inayojenga taswira
  • Zote huwa na miundo maalum ya lugha
  • Zote hupata maana kulingana na jamii
 

TOFAUTI

 
  • Vitendawili vina fomyula ilhali methali hazina fomyula
  • Fumbo la kitendawili hufumbuliwa papo hapo fumbo si lazima kufumbuliwa papo katika methali.
  • Vitendawili hutumiwa na watoto sana, methali hutumiwa kuonyesha hekima miongoni mwa watu wazima na wazee
  • Vitendawili hutolewa katika vikao maalum, methali si lazima kutengewa vikao maalum.
  • Vitendawili hutumia lugha ya majibizano , methali aghalabu huwa kauli moja ya msemaji.

Related questions

0 votes
2 answers
0 votes
0 answers
asked Apr 16, 2022 in Fasihi by Aishanyambura
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...