Thursday, 31 August 2023 12:41

Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 3 2023 Set 1

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo haya kisha ujibu maswali 1 hadi 5.

G4SwaT3OS12023Q1

Halima: Hamjambo wanangu?
Wendy na Lucy: ___1___ mama u hali gani?
Halima: Wendy nenda utayarishe meza ili tuandae kiamsha ___2___.
Wendy: Aya mama.
Halima: Lucy peleka chungu ___3___ kwa moto.
Lucy: Mama chungu kizito, sikiwezi.
Halima: Najua wewe ni ___4___ basi nenda ukasaidie dada ___5___ kuandaa meza.
Lucy: Sawa mama.

   A   B   C   D 
 1.   Sijambo   Hujambo   Hatujambo   Jambo 
 2.  Kimya  Kinywa   Kinyua   Kunywa 
 3.   hiki  hii    hili   huu 
 4.   msembe   mzebe   mzembe   mizembe 
 5.  lako  wako  zako  yako


Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 9.

Kazungu ana tabia ya wizi. Siku moja alikata kauli kwenda katika sherehe za kuanzia mwaka. Aliandamana na watoto wenzake waliomcheka kwa sababu hakuwa na hata shilingi moja mfukoni ya matumizi madogo. Kazungu alikasirika sana. Alisukumana nao na kuwatisha wampe pesa walizo nazo.

Watoto hao waliogopa na kuanza kukimbia ovyo. Kazungu alifanikiwa kuiba pesa za sarafu pekee. Watoto hao walienda moja kwa moja hadi kituo cha polisi. Walimshtaki Kazungu. Uchunguzi ulipofanyika na ukweli wote kupatikana na Kazungu aliadhibiwa.

  1. Jina jingine la pesa ni:-
    1. hela
    2. karibu
    3. kituo cha polisi
    4. aibu
  2. Ni kweli kusema:-
    1. Kazungu ni mtoto mzuri.
    2. Kazungu alizembea.
    3. Kazungu alikuwa na hela zake.
    4. Kazungu aliiba pesa za watoto wenzake.
  3. Kazungu aliiba pesa gani?
    1. Pesa za sarafu.
    2. Pesa za nauli.
    3. Pesa za karo.
    4. Pesa za noti.
  4. Nani aliyeadhibu Kazungu?
    1. watoto wenzake
    2. kituo cha polisi
    3. afisa wa polisi
    4. mwalimu mkuu

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 10 - 13.

Ni muhimu sana mzazi kutunza mtoto wake. Malezi ya wazazi si kama ya mtu yeyote yule. Si haki kumnyima mtoto nafasi ya kupata malezi bora. Ni jukumu la mzazi kumpa mtoto chakula, makaazi, matibabu yaliyo bora na elimu.

Pia inapaswa mtoto apate mavazi safi. Inasikitisha kuona wazazi wengine wakiwatoa watoto wao shule. Pengine watoto hao huamriwa kufanya kazi kwa majumba au mashamba ya watu.

Tuwape watoto wetu mapenzi na tukatae malezi duni. Malezi duni hufanya watoto kwenda kuzurura mtaani. Tujitahidi kutunza watoto wetu inavyotakikana.

  1. Ni kazi gani ambazo hufanywa shambani? 
    1. kupalilia
    2. kusoma
    3. kushika nyoka
    4. kuwinda
  2. Tusipo watunza watoto, nini kitatokea?
    1. viakula
    2. machakula
    3. vyakula
    4. vyaakula
  3. Tusipo watunza watoto, nini kitatokea?
    1. watoto watakuwa werevu.
    2. watakuwa matajiri
    3. watalipwa pesa zao.
    4. watoto wataanza kuzurura mtaani.
  4. Gani si mambo muhimu mzazi anatakiwa ayatekeleza kwa mtoto wake?
    1. kuajiri mtoto
    2. kuelimisha mtoto
    3. kupatia mtoto chakula
    4. kununulia mtoto vazi.

Tumia maneno haya kwa kujaza mapengo 14 hadi 18.

Nyumba ni makazi ___14___ wanadamu. Vitu ___15___ hupatikana katika nyumba. Sebuleni kuna viti na ___16___ pia kuna rafu ya kuweka vitabu. Jiko huwa na mboga mbalimbali kama ___17___ nyanya, vitunguu, limau na ___18___.

   A   B   C   D 
 14.   cha   ya   la   mwa 
 15.  kingi   nyingi   kwingi   vingi 
 16.  sofa  randa   kitanda   jiko 
 17.  kile  lile   vile   mle 
 18.  viasi  vyazi   viazi   viaazi 

 

Kutoka swali 19 hadi 30, jibu kulingana na maagizo.

  1. Majina kama mayai, maembe, malori yako katika umbo gani?
    1. Pembe tatu
    2. Mraba
    3. Mstatili
    4. Duara
  2. Ni vazi lipi kati ya haya huvaliwa na mwanaume?
    1. kanchiri
    2. kaptura
    3. rinda
    4. kitambaa
  3. Tegua kitendawili hiki.
    Nifungue nikufunike, _____________________________________
    1. mwavuli
    2. nyumba
    3. viatu
    4. nguo
  4. Kamilisha sentensi.
    Kikombe ___________________________ kiko jikoni.
    1. cherefu
    2. virefu
    3. mrefu
    4. kirefu
  5. Kitambaa cha kusafisha sakafu kwa maji na sabuni huitwa _________________________________.
    1. nguo
    2. pazia
    3. dodoki
    4. hankachifu
  6. Chagua kitenzi ilichonyambuliwa katika kauli ya kutendwa.
    1. ruka
    2. uliwa
    3. oshwa
    4. mshororo
  7. Mstari moja katika shairi huitwa?
    1. beti
    2. tarbia
    3. sentensi
    4. mshororo
  8. Udogo wa neno “mtu" ni _________________________________
    1. kitu
    2. jijitu
    3. kijitu
    4. jitu
  9. Andika kwa wingi.
    Giza limetanda angani.
    1. Angani kuna giza mingi.
    2. kiko jikoni.
    3. Giza mingi zimetanda angani.
    4. Giza zimetanda angani.
  10. Tunasema nzito kama _________________________________
    1. vitabu
    2. meza
    3. nanga
    4. pamba
  11. Sehemu ya dira R ni:-
    G4SwaT3OS12023Q29
    1. Kusini
    2. Magharibi
    3. Mashariki 
    4. Kaskazini mashariki
  12. Vazi hii huitwaje?
    G4SwaT3OS12023Q30
    1. Suruali
    2. Rinda
    3. Kaptura
    4. Chupi

INSHA

Andika insha murwa kuhusu.

UMUHIMU WA MAJI:

MARKING SCHEME

  1. C
  2. B
  3. A
  4. C
  5. D
  6. A
  7. D
  8. A
  9. C
  10. A
  11. C
  12. D
  13. A
  14. B
  15. D
  16. A
  17. C
  18. C
  19. D
  20. B
  21. D
  22. D
  23. C
  24. B
  25. B
  26. C
  27. D
  28. B
  29. C
  30. D
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 3 2023 Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students