Friday, 24 March 2023 11:03

Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 1 2023 Set 6

Share via Whatsapp

Jaza mapengo kwa kutumia jibu sahihi.

Kadala ni mwanafunzi ___1___. Badala ___2___ kuwasikiliza walimu ___3___, yeye hupendelea kufanya utukutu. Jana mwalimu mkuu alimpa onyo ___4___ mwisho. Alimwambia aende nyumbani akamlete baba ___5___.

   A   B   C   D 
 1.   mtukutu   kitukutu   litukutu   matukutu 
 2.  za  cha  la  ya
 3.  yake  wake  chake  lake
 4.  ya  za  cha  la
 5.  zake  chake  lake  yake

 

Andika sentensi zifuatazo kwa wingi.

  1. Mtu amenunua chungu kingine.
  2. Mkate utaliwa na mtoto.
  3. Kiatu cha mtoto kimeshonwa.

Andika kinyume cha maneno haya.

  1. Kijana
  2. Maskini
  3. Baba

Tunga sentensi ukitumia majina uliyopewa.

  1. kalamu yake __________________
  2. mbegu _________________

Jaza mapengo kwa usahihi.

  1. Yupi kati ya hawa si mnyama wa porini? _______________________________
    (Tembo, Ngedere, Punda)
  2. Chagua neno lisilo tunda.
    _________________________
    (Parachichi, Tikitimaji, Zabibu, Viazi)
  3. Tunatumia kinu na ___________________ kutwangia nafaka. (mchi, mafiga, mwiko)

UFAHAMU
Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali.

Hadija si tabia yake kufuatana na watu wenye tabia mbaya. Lakini siku moja alikata kauli kwenda katika sherehe za sikukuu ya Madaraka. Aliaandamana na watu vichwa maji. Watu hao walimcheka kila mahali. Wengine walisukumana hata na mama wajawazito waliwatisha watoto wadogo na kuwangurumia kama simba. Watoto walilia na kukimbia ovyo. Watu wengine walitoa sigara walizozificha mifukoni wakavuta. Hadija alichukia kile kitendo cha watu hao. Alichukia nywele zao chafu zilizosokotana kama manyoya ya kondoo. Aliyachukia mavazi yao yasiyo na adabu. Baada ya sherehe wanafunzi hao walirudi shuleni. Hadija alienda moja kwa moja hadi kwa mwalimu mkuu. Uchunguzi ulifanywa na ukweli wote ulipatikana, watukutu, wajeuri na vichwa maji waliadhibiwa.

  1. Hadija alipatana wapi na watu wenye tabia mbaya?
    1. Shuleni.
    2. Akjenda nyumbani.
    3. Sherehe za sikukuu.
    4. Nyumbani wakicheza.
  2. Hadija aliandamana na watu
    1. wazuri
    2. wenye bidii
    3. vichwa maji
    4. watiifu

Andika tabia mbili mbaya watu hawa walifanya.

  1. ____________________________
  2. ____________________________
  3. Watu wengine walitoa sigara walizoficha mifukoni na
    1. kuficha
    2. kuvuta
    3. kutupa
    4. kumpa Hadija.
  4. Kwa nini Hadija alienda kwa mwalimu mkuu? 
  5. Je, wafikiria maana ya vichwa maji ni gani?

UFAHAMU
Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali.

MUGUMO

Miti ina faida nyingi kwetu sisi wanadamu. Hutupatia matunda, mbao, kivuli na hata kuvuta mvua. Nchi isiyokuwa na miti hubadilika na kuwa jangwa. Hii ndiyo sababu ya kuwa na siku maalumu ya kupanda miti kila mwaka.

Babu zetu walikuwa na njia yao ya kuzuia ukataji wa miti. Watoto wadogo walitolewa hadithi za kuwafanya waogope kuikata miti fulani. Miti kama mugumo una hadithi nyingi kama hizo. Hii ni kwa sababu ulitumiwa na makabila mengi kutolea sadaka kwa Mungu.

Hadithi moja inahusu mtu mmoja aliyeishi katika kijiji kilichoitwa Makongo. Jina lake lilikuwa Tangawizi. Watu wa kijiji cha Makongo walimchukia Tangawizi kwa sababu ya kukata miti ovyo. Walijaribu kumzungumzia lakini aliendelea kuikata miti.

"Miti ni mali ya Mungu," aliwaambia. Siku moja, Tangawizi aliondoka nyumbani kulipopambazuka, shoka mkononi na kuuendea mugumo uliotumiwa na watu wa kijiji cha Makongo kutolea sadaka kwa Mungu.

"Watatafuta mahali pengine pa kutolea sadaka," alisema na kuanza kuukata. Lakini kabla ya kuendelea sana, damu ilianza kutoka katika sehemu aliyoikata. Mara aliisikia sauti kubwa kutoka kwa mugumo huo.
Tangawizi!.... Tangawizi!...... Tangawizi!
Kwa vile wataka kuniua, mimi nitakuadhibu.
Kutoka leo, utakuwa kipofu hadi kufa.
Macho ya Tangawizi yalijifunga na akawa kipofu hadi kufa kwake.

  1. Taja faida moja ya miti kama zilivyozungumziwa katika hadithi.
  2. Nchi isiyokuwa na miti hubadilika na kuwa nini?
  3. Muguro una hadithi nyingi kwa sababu gani?
    1. Ni mti mkubwa sana.
    2. Ni mti unaoweza kuongea.
    3. Ulitumiwa kutolewa sadaka kwa Mungu.
    4. Uliwapa watu matunda.
  4. Aliyekwenda kuukata Mugumo alikuwa na nini?
    Taja vitu viwili vilivyofanyika mti ulipoanza kukatwa.
  5. _________________________________
  6. _________________________________
  7. Tangawizi aliadhibiwa aje na mugumo?
    1. Alichapwa.
    2. Alikatwa mkono.
    3. Alikuwa zuzu.
    4. Alikuwa kipofu

INSHA  

Andika Insha kuhusu:

NYUMBANI KWETU   

MARKING SCHEME

  1. A
  2. D
  3. B
  4. D
  5. D
  6. Watu wamenunua vyungu vingine.
  7. Mikate italiwa na watoto.
  8. Viatu vya watoto vimeshonwa.
  9. mzee
  10. Tajiri
  11. mama
  12. Sentensi sahihi
  13. Sentensi sahihi
  14. punda
  15. viazi
  16. mchi
  17. C
  18. C
  19. Wato hao walimcheka kila mahali.
  20. Watu wengine walitoa sigara walizozificha mifukoni wakavuta
  21. B
  22. Kupiga ripoti
  23. Watu wenye tabia mbaya.
  24. Hutupatia matunda, mbao, kivuli na hata kuvuta mvua.
  25. jangwa
  26. C
  27. Tangawizi
  28. Damu ilianza kutoka
  29. Alisikia sauti kubwa
  30. D
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 Opener Exams Term 1 2023 Set 6.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students