Monday, 27 March 2023 12:28

Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 5 Mid Term 1 Exams 2023 Set 1

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1-5  

Asanyo: Hujambo Matoke? Naqna una haraka ama vipi?
Matoke:  Sijambo. Ndiyo nina haraka. Naelekea sokoni na kazi ya kuwalisha kuku yaningoja nyumbani
Asanyo: Ina maana kuwa unapata pesa nyingi sana.
Matoke:  Pesa zatoka wapi? Nimetumwa mboga sokoni na pia viungo vingine.
Asanyo: Nikifanya kazi yoyote nyumbani lazima nilipwe. Nikitumwa nalipwa. Kama silipwi naenda kurandaranda mtaani.
Matoke:  Huko ni kukosa busara na wavyele wako husemaje?
Asanyo: Hawana neno. Nikifanya kosa lolote hawawezi kuniadhibu.
Matoke:  Laiti wavyele wako wangalijua kuwa mchelea mwana kulia, hulia mwenyewe kwaheri.

  1. Matoke alikuwa anaelekea wapi?
    1. Dukani
    2. Nyumbani
    3. Sokoni
    4. Mtaani
  2. Kulingana na mazungumzo haya
    1. Asanyo ni mtoto mchafu
    2. wavyele wa Asanyo wanampenda
    3. matoke huwatii wavyele wake
    4. matoke hapendi kufanya kazi
  3. Neno wavyele limetumika kwenye kifungu lina maana gani?
    1. Wazazi
    2. Ndugu
    3. Marafiki
    4. Familia
  4. "Mchelea mwana kulia hulia mwenyewe" huu ni mfano wa?
    1. Msemo
    2. Kitendawili
    3. Fimbo
    4. Methali
  5. Ni sahihi kusema _______________________
    1. pesa hufanya mtoto afanye kazi nyumbani
    2. wavyele wanastahili kuwaadhibu wanao
    3. kurandaranda mitaani ni jambo muhimu
    4. kukosa busara ni jambo muhimu

Soma shairi hili kisha ujibu maswali

Nakupongeza mlezi, shuleni kunipeleka
Chakula nacho kanipa, karo pia kalipa
Mpendwa watapatapa, mimi hapa nikicheka
Pongezi mlezi wangu, kazi njema waifanya

Kanionya kaonyeka, za kulevya nikahepa,
Mbaya tabia nikaacha, masomoni, nikangara
Jukumu nilijitweka, ushauri ulionipa
Pongezi mlezi wangu, kazi njema waifanya

  1. Hili ni shairi la aina gani?
    1. Tarbia
    2. Tathlitha
    3. Tasdisa
    4. Takhmisa
  2. Shairi hili lina beti ngapi?
    1. Tatu
    2. Nane
    3. Nne
    4. Mbili
  3. Kila ubeti una mishororo mingapi?
    1. Miwili
    2. Mitatu
    3. Mmoja
    4. Minne
  4. Shairi hili linatufunza kuwa
    1. tuwalaani wazazi
    2. tupongeze wazazi
    3. tusome kwa bidii
    4. tupate mihadarati
  5. Kibwagizo cha shairi hili ni
    1. Nakupongeza mlezi, shuleni kanipeleka
    2. Kanionya kaonyeka, za kulevya nikahepa C
    3. Pongezi mlezi wangu, kazi njema waifanya
    4. Mbaya tabia nikaacha, masomoni nikangara.

Soma mtungo ufuatao kisha ujaze nafasi zilizoachwa 11-15.

Kaka ___11___ ni mzuri. Yeye ni ___12___.Anapenda kuvaa nguo ___13___ na viatu vyeusi. Kwake viatu vyote ni vizuri. Mimi huvaa viatu vikubwa ___14___ kuviweka pahali ___15___ hawezi kufikia viatu vikubwa vinaweza kuumiza vibaya.

   A   B   C   D 
 11.    yangu   zangu   wetu   wangu 
 12.  mupole   pole   mpole   mbole 
 13.  zeupe  nyeupe   eupe    mweupe 
 14.  na  pa   ya   za 
 15.  ambapo   ambao  ambazo   ambayo

 

Chagua jibu sahihi kujibu maswali 16-30.

  1. Kamilisha methali: Kinga na kinga __________________________
    1. hukingana
    2. ndio ujao
    3. ndipo moto uwakapo
    4. huona makuu
  2. Yeye ni mwenye maringo kama 
    1. samaki
    2. tausi
    3. kunguru
    4. malaika
  3. Wingi wa sentensi hii ni. Tunda hili ni tamu
    1. Tunda haya ni matamu
    2. Matunda haya ni yamu
    3. Matunda haya ni matamu
    4. Matunda hizi ni tamu
  4. Bibi harusi alikuwa amebeba __________________ la maua.
    1. shada
    2. kipeto
    3. shungi
    4. doti
  5. Kanusha. Mama atapika wali kesho
    1. Mama hakupika wali kesho
    2. Mama hatapika leo
    3. Mama hatapika wali kesho
    4. Mama hakupika wali kesho
  6. Tegua kitendawili: Huku ngo na huko ng'o
    1. Giza
    2. Uyoga
    3. Ndoto
    4. Fua
  7. Neno jino liko katika ngeli ya
    1. A - WA
    2. LI - YA
    3. U - ZI
    4. U - U
  8. Wao ________________ waliocheza na kutuzwa.
    1. ndio
    2. ndiye
    3. ndiyo
    4. ndizo
  9. Jibu la salamu 'Alamsiki' ni ____________________
    1. binuru
    2. tunayo
    3. nawe pia
    4. ya kuonana
  10. Ukubwa wa neno mlango ni
    1. jilango
    2. kilango
    3. lango
    4. kijilango
  11. Umbo lifuatalo huitwa ______________________________
    G4SWAT1SF23002Q25
    1. pia
    2. mche
    3. duara
    4. duaradufu
  12. Chagua nomino ambata
    1. Mweka hazina
    2. Mwanambee
    3. Sungura
    4. Mchezaji
  13. Tumia amba ipasavyo
    Mwanafunzi _________________ hufaulu huwa na bidii
    1. ambao
    2. ambaye
    3. ambayo
    4. ambazo
  14. Jua hutua wakati wa ______________________
    1. mashariki
    2. magharibi
    3. alasiri
    4. adhuhuri
  15. Mnene kama _____________________
    1. nyundo
    2. sindano
    3. nguruwe
    4. ndovu

SEHEMU YA B: INSHA   

Andika insha ya kusisimua kuhusu mada ifuatayo.

SAFARI ILIYOPENDEZA   

MARKING SCHEME

  1. C
  2. C
  3. A
  4. D
  5. B
  6. A
  7. D
  8. D
  9. B
  10. C
  11. A
  12. C
  13. B
  14. A
  15. A
  16. C
  17. B
  18. C
  19. A
  20. C
  21. A
  22. B
  23. A
  24. A
  25. C
  26. D
  27. A
  28. B
  29. B
  30. C
Join our whatsapp group for latest updates

Download Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 5 Mid Term 1 Exams 2023 Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students