0 votes
1.6k views
in Chozi la Heri by

‘…familia yake bado inamiliki mashamba ya michai na mibuni pamoja na mashirika mengi…’

  1. Weka dondoo hili katika muktadha wake. 
  2. Kwa kurejelea mifano minane, eleza umuhimu wa msemaji katika kujenga riwaya hii. 
  3. Jadili kwa hoja nane suala la ukoloni mambo leo lilivyoshugulikiwa katika riwaya. 

1 Answer

0 votes
by
  1.   
    •  Maneno ya Chandachema
    • Akiwaambia Umu, Zohali na Mwanaheri.
    • Wakiwa katika bweni la wasichana ya Shule ya Tangamano.
    • Alikuwa akiwaeleza usuli wa uwepo wake katika shule hiyo.
  2.   
    • Mmoja kati ya wasimulizi wa hadithi ya Chozi la heri ndiye anayesimulia kuhusu maisha ya wahusika kama vile Fumba na Tenge.
    • Kupitia kwake, mwandishi anasisitiza umuhimu wa familia katika malezi.
    • Baba anamtelekezea kwa nyanyake baada ya kifo cha nyanya, anaishi katika familia ya jirani yao Satua, na hatimaye kwa Tenge. Hawa wote wana mchango katika malezi yake.
    • Mwandishi amemtumia kukashifu ukiukaji wa haki za kibinadamu. Baba yake anamtunga mwanafunzi wake mimba na baadaye kumtelekeza mtoto -Chandachema.
    • Chandachema anaendeleza ajira ya watoto. Anafanya kazi katika shamba la chai kwa malipo kidogo.
    • Anachimuza umuhimu wa mashirika ya kidini katika kutetea haki za kibinadamu. Makao ya Jeshi la wajane Wakristo yanawahifadhi watoto waliotupwa na wazazi pamoja na wale wazazi wahitaji.
    • Ni kielekezo cha vijana wasiokata tamaa. Anawaambia akina Umu kuwa atajitahidi masomoni ili ahitimu kuwa mwanasheria au afisa wa maslahi ya kijamii na kuweza kutetea haki za kibinadamu.
    • Anaendeleza maudhui ya elimu na kuonyesha jinsi elimu inachangia kuleta mustakabali mwema wa msomi siku za usoni. Chandachema angependa kuwa Mwanasheria au Afisa wa maslahi ya Kijamii na kuweza kutetea haki za binadamu
    • Kupitia kwake, dhiki zinazowapata wafanyikazi wa kima cha chini zinaangaziwa.
    • Anafunza mbinu-ishi ya uvumilivu. Anavumilia maisha ya taabu baadaya kifo cha nyanyake hadi anapopata ufadhili na kujiunga na shule yaTangamano.
    • Anajenga tabia za wahusika. Kupitia kwake, tunaona utu wa Waridi anayemsomesha, ukatili na ukosefu wa uwajibikaji wa Fumba ambaye anamuacha Chandachema kulelewa na nyanya yake, Fumba mwenyewe akihamia ng’ambo na familia nyingine.
    • Uzinifu wa Bwana Tenge kunakusababisha dhiki ya kisaikolojia kwa wanawe na Chandachema
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...