0 votes
1.7k views
in Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine by

Shibe inatumaliza : Salma Omar Hamad
“Hiyo ni dharau ndugu yangu. Kwa nini kila siku tunakula sisi kwa niaba ya wengine ?”

  1. Eleza muktadha wa dondoo hili. 
  2. Eleza sifa za msemaji. 
  3. Eleza jinsi viongozi wanavyokuwa wabadhirifu. 

1 Answer

0 votes
by
  1. Eleza muktadha wa dondoo hili.
    • Maneno haya yanasemwa na Mbura
    • alikuwa anazungumza na Sasa
    • walikuwa kwenye sherehe iliyoandaliwa na mzee Mambo
    • walikuwa wanazungumza kuhusu ‘kula kwao’ 
       
  2. Eleza sifa za msemaji. 
    • ni mzalendo - anafanya kazi kwa bidii katika wizara yake kama njia ya kuonyesha uzalendo
    • mwenye tamaa - anajaza sahani kwa chakula na kukila chote
    • mwenye utu - anataka wananchi wale kwa niaba ya viongozi kama vile wao wamekuwa wakila kwa niaba yao
    • ni fisadi - amepokea kazi kwa afisi ya serikali kwa njia isiyo halali
    • mzembe - baada ya kula sahani tatu za vyakula kwenye sherehe analala usingizi mzito badala ya kwenda kazini
    • mtetezi wa haki - mvumilivu-
       
  3. Eleza jinsi viongozi wanavyokuwa wabadhirifu. 
    • hulipwa mishahara mikubwa sana na serikali jambo linalochangia ubadhirifu wa mali ya umma
    • sherehe kubwa za viongozi wa kiserikali huchangia pakubwa ubadhirifu
    • viongozi hutumia raslimali za nchi kwa manufaa yao ya kibinafsi - magari ya serikali
    • raslimali zilizotumiwa katika kuvinunua vyakula na vinywaji vingetumika katika kuendeleza asasi tofauti za kijamii
    • DJ na wenzake wanapata mabilioni ya fedha kutokana na kuwatumbuiza wageni katikasherehe kama hizi
    • viongozi wanawachukua baadhi ya watu wao wa karibu na kufanya juu chini kuona kwamba wanajifaidi na mali na raslimali za wananchi pasipo kuzitolea jasho kamwe
    • upeperushaji wa matangazo katika vyombo vya habari ya sherehe za kiongozi binafsi ni njia ya kuendeleza ubadhirifu wa raslimali za umma
    • Mbura na Sasa wanaendeleza ubadhirifu pale wanapoamua kuchukua vyakula kupita kiasi katika sherehe za mzee Mambo
    • kuwaajiri viongozi wawili wenye nyadhifa sawa katika sekta tofauti za umma
    • vibaraka na vikaragosi kupewa mali ambayo ingewafaidi wananchi zozote

Related questions

Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...