Monday, 01 November 2021 11:04

Kiswahili Questions and Answers - Class 6 End of Term 2 Exams Set 1

Share via Whatsapp

KISWAHILI
DARASA LA SITA
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA 2 

Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kuchagua kitenzi kifaacho zaidi.

Hapo    1      za kale aliishi mzee       2           3       Falsafa. Hilo     4     jina la       5     kwa sababu alikuwa na hekima. Baada ya kazi zake mchana   6    aliwakusanya vijana jioni na kuanza    7   .Alikuwa na    8    ya kuwakuza vijana wakiwa na   9      kwani alifahamu kuwa vijana    10  kizazi cha kesho.

Mzee Falsafa hakutaka kulipwa kwa sababu alikuwa akiifanya kazi hiyo kwa     11     ulikuwa ni mchango wake kwa     12    . Katika kuwaelekeza, aliwahimiza   13      bila kujali kabila au tabaka kwani umoja ni nguvu. Suala    14     lilikuwa ni     15      ya wavulana ilikuwa ni daraja la utoto utu uzima.

  1. A. zamani                B. samani             C.kale                 D.juzi
  2. A.moja                     B.mmocha            C.mmoja             D.mocha
  3. A anayeitwa             B.aliyeitwa            C.anaitwa           D.ataitwa
  4. A.lilikuwa                 B.likuwa                C.lilikua               D.litakuwa
  5. A.msiba                   B.mzaha               C.msimbo            D.mtaa
  6. A.kesho                   B.usiku                  C.kucha              D.kutwa
  7. A.kuwafunza            B.kuwasoma        C.kuwajali            D.kuwazomea
  8. A.lengo                    B.nia                     C.mpango           D.ujuzi
  9. A.maadili                 B.maisha               C.maadili mema  D.furaha
  10. A.ndicho                  B.ndiyo                  C.ndio                  D.ndizo
  11. A.sharti                    B.lazima                C.hiari                  D.shurti
  12. A.umati                    B.uma                    C.walimu             D.umma
  13. A.kutengana            B.kutangamana     C.kuchukiana      D.kulaumiana
  14. A.lingine                  B.zingine                C.nyingine           D.jingine
  15. A.kutahiri                 B. tohara                C.funzo               D.somo

Kuanzia swali la 16-30. jibu swali kulingana na maagizo.

  1. Kiongozi wa sala msikitini ni
    1. imamu
    2. kuhani
    3. katkisti
    4. mchungaji
  2. Wanaume walioa dada wawili huitanaje? 
    1. Mwamu
    2. Shemeji
    3. Mwanyumba
    4. Wifi 
  3. Andika wingi wa sentensi hii
    Nenda naye akuonyeshe mali yangu.
    1. Nenda nao wakuonyeshe mali yangu.
    2. Nendeni nao wamuonyeshe mali yetu.
    3. Nenda nao wawaonyesghe mali yetu.
    4. Nendeni nao wawaonyeshe mali yetu.
  4. Kikembe cha samaki ni;
    1. dagaa
    2. kichengo
    3. kimatu
    4. kiluwiluwi
  5. Tegua kitendawili kifuatacho
    Hakionekani wala hakishikiki
    1. kisogo
    2. mafiga
    3. uga
    4. hewa
  6. Andika katika hali ya ukubwa
    Mtoto mzuri anasoma
    1. Toto zuri linasoma
    2. Toto mzuri anasoma
    3. Kitoto kizuri kinasoma
    4. Kitoto zuri kinasoma
  7. Kamilisha methali
    Mwenda tezi na omo marejeo
    1. nyumbani
    2. kazini
    3. inshallah
    4. ngamani
  8. Zana hii ya ujenzi inaitwaje
    kisst6et2q23
    1. timazi
    2. msasa
    3. tupa
    4. parafujo
  9. Kitanda cha kubebea wagonjwa hospitalini huitwaje
    1. kigoda
    2. wadi
    3. machela
    4. mkungu
  10. Kanusha sentensi hii
    Mzee aliniita kuniadhibu
    1. Mzee hakuniita wala kuniadhibu
    2. Mzee hajaniita na hajaniadhibu
    3. Mzee hakukuita ili akuadhibu
    4. Mzee hajaniita ili akuadhibu
  11. Makazi ya mfalme huitwa
    1. ikulu
    2. kasri
    3. kizimba
    4. wamamu
  12. Anayetibu wagonjwa ni tabibu
    Anayeendesha gari la moshi ni
    1. Rubani
    2. Mzegazega 
    3. Kandawala
    4. Hamali 
  13. Kemboi alijifunika
    1. chepechepe!
    2. Rovurovu!
    3. Ndi!
    4. Gubigubi!
  14. Andika akisami subui
    1. 1/5
    2. 1/7
    3. 1/6
    4. 1/9
  15. Nyama ya mgongo huitwa
    1. shahanu
    2. ndewe
    3. sarara
    4. . kidari

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali ya 31 - 40.

Kiprop alikuwa na mkewe aliyeitwa Lilia. Walibarikiwa kupata watoto watatu. Walikuwa wakiishi katika shamba lao kwenye kitongoji kilichoitwa Mwendakwao. Kijiji hiki kilikuwa mbali na mji wowote.

Jamaa hii haikuishi peke yake. Hapo nyumbani pao palikuwa naye mwanamume mzee kidogo aliyekuwa ameishi nao kwa siku nyingi kidogo. Mtu huyu aliitwa Matakia. Alikuwa mtu mwema. Aliisaidi. sila ya Kiprop kwa mengi. Walikwenda kulima shambani pamoja. Aliwasaidia kupalilia akiwaangalia na kuwatunza watoto wa jamaa ya Kiprop Matakia alikuwa ni rafiki wa dhati hapo nyumbani. Lakini nguvu zilianza kumwishia alipoanza kuwa mzee.

Nyumbani hapo pa Bwana Kiprop alikuwapo pia mbwa aliyeitwa Jeki. Mbwa huyo ndiye aliyekuwa mlinzi wa nyumbani wakati watu walipokwenda shambani. Akawa ni rafiki wa nyumba ile kwa muda mrefu.

Jeki alianza kuchoka kwa ajili ya uzee. Nguvu zake zikaanza kumalizika. Akawa analala ovyo ovyo tu. Kubweka na ukali wake, vyote vilikuwa vimemwishia. Meno yake yakaanza kung'oka moja mojamifupa kwake ikawa shida kutafuna. Akawa anapikiwa vyakula laini laini, rojorojo hivi kama uji. Akawa hawezi kuirarua mifupa migumu kama alivyozoea hapo awali akiwa na meno.

Naye Matakia alianza kuuguagua. Hakuweza kutenda kazi zake sawa kama hapo mwanzo. Badala ya kuamka saa thenashara za asubuhi kama kawaida yake, alichelewa kitandani kufikia hata saa tatu hivi.

  1. Kiprop alikuwa na aila ya watu wangapi?
    1. Watatu.
    2. Watano.
    3. Sita.
    4. Saba.
  2. Matakia alikuwa
    1. Ajuza
    2. Bawabu
    3. Mlinzi
    4. Msaidizi
  3. Pamoja na shughuli zake pale nyumbani,
    Matakia hakushiriki
    1. kuwalea watoto
    2. kufyeka konde C
    3. kuwaogesha watoto
    4. kuwanyanyasa watoto
  4. "Matakia alikuwa ni rafiki wa dhati hapo nyumbani" kwani
    1. Alisaidia kwa mapana na marefu
    2. Alisaidia kwa hali na mali
    3. Alisaidia kufa na kupona
    4. Alisaidia daima dawamu 
  5. "Jeki alihesabiwa kama rafiki wa nyumba ile, "kwa sababu
    1. Alibweka sana
    2. Aliyalinda maskani yale
    3. Aliwalinda watoto wa mifugo
    4. Aliishi muda mrefu
  6. Jeki alipoanza kuzeeka alikuwa
    1. Akichoka ovyo
    2. Akijilaza ovyo ovyo
    3. Akibweka kwa ukali
    4. Akitaka uji tu
  7. Matakia alianza kuugua na kuchelewa kuamka
    1. Alipoanza kuwa mzembe
    2. Alipoanza kuzeeka
    3. Alipochoka kufanya kazi
    4. Alipogombezwa
  8. Neno muhali limetumiwa kuinaanisha
    1. vigumu
    2. rahisi
    3. hataki
    4. mahali 
  9. Saa thenashara ni
    1. Saa kumi
    2. Alfajiri
    3. Saa kumi na mbili
    4. Asubuhi
  10. Kichwa mwafaka cha habari hii ni
    1. Matakia na Jeki
    2. Jamii ya Kiprop
    3. Kiprop na rafiki zake
    4. Jamii ya Kiprop na rafiki zake

Soma shairi hili kwa makini kisha wjibu maswali kutoka 41 hadi 50.

Moyo wanambia penda, mtu mjinga sipende,
Mjinga ukimpenda, hajui nini atende,
Moyo wanambia tenda, lisilotendwa sitende,
Fanya wanavyotenda, wenzio wasikushinde.

Moyo wanambia imba, wimbo mbaya siimbe,
Imba wimbo wa kupamba uwapumbaze wakembe
Moyo wanambia omba, ombi ovu usiombe,
Omba Mungu Muumba, dhiki azifanye chembe.

Moyo wanambia meza, kinachokwama simeze,
Kinachokwama kumeza, kinywani sielekeze,
Moyo wanambia uza, roho yako usluze,
Fanya unavyoweza, neno hili jikataze.

Moyo wanambia cheza, michezo mbi sicheze,
Cheza walcupendeza, wenzio wakuigize,
Moyo wanambia kaza, bidii usipunguze,
Usipunguze kuwaza, mawazonijiingize.

Moyo wanambia kopa, deni kubwa usikope,
Usiloweza kulipa, siku zote usiepe,
Moyo wanambia apa, kwa batili usiape,
Wala usifanye pupa, kiapo ukiogope.

Moyo wanambia kana, neno la kweli usikane,
Kweli unapiona, fanya bidii unene,
Moyo wanambia chuna, ngozi yako usichune,
Japo nyeusi sana, bora kuliko nyingine.

  1. Katika ubeti wa kwanza:
    1. Moyo wamkanya mtunzi kumpenda mjinga
    2. Moyo wamkanya mtunzi aismpende mjinga
    3. Moyo wamwambia mtunzi asitende kama wenzake
    4. Mtunzi asema ukimpenda mjinga, hujui unachotenda.
  2. Mtunzi anasema
    1. Wimbo mbaya unaweza kukupamba 
    2. Umwimbie Mungu Muumba
    3. Meza kitu kinachoweza kukusakama
    4. Uendeleze uwezo wa kufikiri na kutafakari .
  3. Mshairi asema kwamba 
    1. Ikibidi ukope deni dogo la kulipa
    2. siku zote uyaepe madeni ya aina yoyote 
    3. unaweza kuapa kwa ubatili
    4. fanya bidii uwe mnene lakini usichune ngozi
  4. Shairi lenye muundo huu huitwa
    1. tathlitha
    2. taklimisa
    3. tarbia
    4. tathnia
  5. Kifungu kimoja cha shairi huitwa
    1. mshororo
    2. mizani
    3. kibwagizo
    4. ubeti
  6. Kibwagizo cha ubeti wa tatu kina mizani mingapi?
    1. 15
    2. 16
    3. 4
    4. 8
  7. Upini mpangilio sahihi wa vina vya kati na vya mwisho katika ubeti wa sita (mwisho)
    1. na-ne
    2. ne - na
    3. .za - ze
    4. .a-e
  8. Badala ya kutumia neno wakembe; mtunzi angetumia neno jingine sawa na hilo ambalo
    1. wazembe
    2. watu
    3. wapumbavu
    4. watoto
  9. Bingwa wa kutunga nyimbo huitwa manju, naye bingwa wa kutunga mashairi huitwa?
    1. Sogora
    2. Malenga
    3. Manju
    4. Hatibu
  10. Kichwa mwafaka kwa shairi hili ni
    1. Moyo
    2. Wakembe
    3. Shule yangu
    4. Ajali

MAAKIZO

  1. A
  2. C
  3. B
  4. A
  5. C
  6. D
  7. A
  8. B
  9. A
  10. C
  11. C
  12. D
  13. B
  14. D
  15. B
  16. A
  17. C
  18. D
  19. B
  20. D
  21. A
  22. D
  23. A
  24. C
  25. A
  26. B
  27. C
  28. D
  29. B
  30. C
  31. B
  32. D
  33. D
  34. A
  35. B
  36. C
  37. B
  38. A
  39. C
  40. D
  41. A
  42. A
  43. A
  44. C
  45. D
  46. B
  47. D
  48. C
  49. B
  50. A
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Class 6 End of Term 2 Exams Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students