Wednesday, 29 March 2023 12:55

Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Mid Term 1 Exams 2023 Set 4

Share via Whatsapp Written by
Rate this item
(0 votes)

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 1 hadi 5.

Kutoka: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.                                                       11/5/2021                                                                        10:00a.m
Kwa: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

MADA: NAFASI YA KUJIFUNZA

Hujambo rafiki mpendwa? Nataraji ujumbe huu utakupata ukiwa mzima. Habari ya huko kwenu? Nimekuandikia hii barua ili kuomba ruhusa ya kuja kukutembelea wakati wa likizo ya Agosti. Ningependa kujifunza mengi kuhusu intaneti katika duka lenu la "Kituo cha Kompyuta."

Mwalimu wetu ametuhimiza kuzuru mahali panapotoa huduma ya intaneti. Tafadhali nifahamishe tarehe na siku utakapopatikana. Tumia anwani yangu. Mola akubariki.

Wako mpendwa,
Njeri.

  1. Mwandishi wa barua pepe hii ni nani?
    1. Rafiki
    2. Njeri
    3. Mary
    4. Hatujui
  2. Nia kuu ya Njeri kuomba ualishi ni
    1. kwenda shereheni
    2. kuzuru kwao
    3. kujifunza kompyuta
    4. kuwasabahi
  3. Ni nani aliyetoa himizo la kuzuru palipo na huduma ya kompyuta?
    1. Mwalimu
    2. Mzazi
    3. Njeri
    4. Mary
  4. Ni duka la akina nani kuna huduma ya kompyuta na intaneti?
    1. Mary
    2. Mwalimu
    3. Njeri
    4. Mary
  5. Barua hii inahusu nini?
    1. Kujifunza mambo yanayohusu intaneti na kompyuta
    2. Marafiki
    3. Jumba la huduma ya kompyuta
    4. Hatujaelezwa

Soma shairi hili kisha ujibu maswali 6 - 10.  

Kioo!
Kioo!
Kuna mzuri
niambiye
Kuliko miye?

Aha!
Kwani una doa?
Labda una ila!
Au una dosari!
Pengine una walakini!
Kweli umejiangalia?

Hebu songea karibu
Uwe kama pua na madomo
Sasa jitazame!
Sasa jipekue!
Sasa jichunguze!

Umegundua nini?
Umeridhika na uloona?
Nakuasa mwandani;
Uzuri wa mkakasi
Ndani kipande cha mti!

  1. Mwandishi alitaka kujua iwapo
    1. kuna mzuri kuliko yeye
    2. wengi wabaya
    3. wengine
    4. ni mzuri
  2. Walakini na dosari ni maneno yenye maana sawa. Maneno yenye maana sawa huitwa
    1. vitawe
    2. vitate
    3. visawe
    4. nomino
  3. Uwe kama pua na domo ni mfano wa
    1. istiara
    2. tashbihi
    3. msemo
    4. kitenda
  4. Shairi hili linazungumzia nini?
    1. Sura
    2. Raha
    3. Kujitazama
    4. Kioo
  5. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti ni
    1. kitendawili
    2. msemo
    3. methali
    4. istiara

Soma kifungu hiki kisha ujibu maswali yafuatayo 11 - 15.

Ukulima ni mojawapo ya kazi muhimu katika nchi yetu. Faida za ukulima ni nyingi na hazina hesabu.

Faida ya kwanza ya ukulima ni kwa wananchi. Kila mwananchi anahitaji chakula ili aweze kupata afya ya kumwezesha kufanya kazi. Ili taifa kuendelea linahitaji wananchi wenye afya. Afya hii hutokana na chakula kinachotokana na ukulima.

Faida ya pili ya ukulima ni kwa mkulima. Mkulima anapouza mazao ya shamba hupata pesa. nyingi. Pesa hizi humwezesha kujifanyia shughuli zake kama vile kujijengea nyumba, kulipia watoto wake karo, kulipa bili ya umeme na kadhalika. Kwa jumla ukulima unaweza kumwezesha mkulima kuishi maisha ya raha na jamii yake.

Vilevile faida ya ukulima ni kwa serikali. Kuna mazao ya shambani ambayo huuzwa katika nchi za nje na kuletea nchi yetu pesa nyingi za kigeni. Serikali inapopata pesa za kigeni huzitumia kufanya maendeleo mbalimbali kama vile kujenga barabara, hospitali, shule na kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Viwanda mbalimbali vya kutengeneza bidhaa za kilimo pia hujengwa. Hii inamaanisha kuwa wananchi watapata ujira viwandani. Wananchi hupata mshahara wa kuwawezesha kuendelea na maisha yao nayo serikali itapata kodi kutoka kwa wafanyakazi na wenye viwanda.

  1. Ukulima ni
    1. kati ya kazi nyingine muhimu
    2. ambapo hakuna ya faida
    3. isiyohitajika taifani
    4. taifa litaendelea bila
  2. Ipi si faida ya ukulima?
    1. Kutoa kipato
    2. Kutoa chakula
    3. Kutoa uhasama
    4. Kutoa kazi
  3. Mshahara ni
    1. pesa nyingi
    2. pesa zinazolipwa baada ya kufanya kazi mwishoni mwa mwezi
    3. msamaha kazini
    4. pesa za kulipwa kila siku baada ya kazi
  4. Serikali hupata kodi kutokana na
    1. wafanyabiashara wanaolipa kodi
    2. kuiba
    3. huomba
    4. hupanda
  5. Ukulima humwezesha mkulima kuishi maisha ya
    1. shida
    2. raha
    3. taabu
    4. matatizo

Jaza pengo hizi nambari 16 hadi 20.

Madereva wanaokiuka sheria (16)_____________ barabara (17)____________kutiwa mbaroni na kufunguliwa mashtaka. Hata kama (18)_______________ ajali (19) _____________zinaweza (20)_______________.

   A   B   C   D 
 16.   ya   za   cha   kwa 
 17.  zafaa   yanafaa   wanafaa   inafaa 
 18.  mtu pweke ni uvundo    asiyekuja hakuthamini   asiyekuwepo na lake halipo   ajali haina kinga 
 19.  nyingine  nyingineyo   zingine   zingineyo 
 20.  kuzuia  kuzuilika   kuzuwika  kuzuilisha

 

Kuanzia swali la 21 hadi 30, chagua jibu sahihi.

Vivumishi vifutavyo ni vya aina gani?

  1. Mtoto yule ni mcheshi.
    1. viulizi
    2. viashiria
    3. visisitizi
    4. namna
  2. Mwanafunzi hodari ni yule.
    1. namna
    2. wingi
    3. sifa
    4. wakati
  3. Mkulima yupi alituzwa?
    1. Radidi
    2. Kisisitizi
    3. Kiulizi
    4. Sifa
  4. Nomino 'kucheka' lipo katika kundi lipi la nomino?
    1. Mahususi
    2. Pekee
    3. Wingi
    4. Kitenzi jina
  5. Barua rasmi huwa na anwani ngapi?
    1. 2
    2. 3
    3. 4
    4. 5
  6. Kipande cha pili katika ubeti wa shairi huwa
    1. utao
    2. ubeti
    3. kipande
    4. mshororo
  7. Ni kipi kiwakilishi cha nafsi kati ya haya uliyopewa?
    Yeye ni mpole sana.
    1. ni
    2. yeye
    3. mpole
    4. sana
  8. Neno lipi liko katika ngeli ya U-U?
    1. Ugali
    2. Uzi
    3. Nguo
    4. Ukuta
  9. Kanusha:-
    Mimi nilianika nguo.
    1. Mimi nilianua nguo.
    2. Mimi sikuanua nguo.
    3. Mimi sikuanika nguo.
    4. Mimi nilianika nguo.
  10. Kamilisha kwa kutumia 'amba':-
    Duka _________________lilifunguliwa ni langu
    1. ambaye
    2. ambayo
    3. ambacho
    4. ambalo

INSHA  

Andika insha kuhusu:-

"NCHI YANGU FAHARI YANGU"

MARKING SCHEME

  1. B
  2. C
  3. A
  4. D
  5. A
  6. A
  7. C
  8. B
  9. D
  10. C
  11. A
  12. C
  13. B
  14. A
  15. B
  16. B
  17. C
  18. D
  19. A
  20. B
  21. B
  22. C
  23. C
  24. D
  25. A
  26. A
  27. B
  28. A
  29. C
  30. D
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Mid Term 1 Exams 2023 Set 4.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Read 1783 times Last modified on Friday, 31 March 2023 11:27

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.