Monday, 13 March 2023 09:52

Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 School Based Assessment Term 1 Exams 2023 Set 5

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo haya kisha ujibu maswali 1 hadi 5

Mwalimu: Hamjambo wanafunzi?
Wanafunzi: Hatujambo sana mwalimu Lydia! Shikamoo?
Mwalimu? Marahaba watoto wangu! ketini.
Wanafunzi: Asante sana mwalimu!
walimu: Leo nataka kwanza kuangalia kucha ya kila mtu. Sasa kila mtu aende mbele kisha nikague kama kucha ni safi na fupi. Nitaanza na wasichana kwanza.
Mwanafunzi. 1: Tafadhali mwalimu, mama hana pesa ya kununua wembe. Nitakata kesho unisamehe!
Mwalimu: Ngoja pale kwa mlango ungoje kiboko.
Mwanafunzi 2: Mwalimu makucha zangu ni fupi na safi sana. Ebu angalia.
Mwalimu: Ni vizuri Angela. Rudi kwenye kiti chako.
Mwanafunzi 3: Mwalimu makucha zangu ni refu lakini safi sana.
Mwalimu: Nitakusamehe leo lakini uikate kesho.
Mwanafunzi 3: Asante mwalimu.

  1. Lydia alikuwa             
    1. Mwanafunzi
    2. Mwalimu mkuu
    3. Mwalimu wa darasa
    4. Mpishi
  2. Kinyume cha neno "wasichana" ni
    1. wavulana 
    2. msichana 
    3. walimu 
    4. watoto
  3. Ni neno lipi la adabu aliotumia mwanafunzi wa tatu katika mazungumzo haya?
    1. Tafadhali 
    2. Pole
    3. Labda
    4. Asante
  4. Watoto wangapi waliokaguliwa na mwalimu?
    1. wanne
    2. watatu 
    3. wawili 
    4. mmoja
  5. Mtoto yupi alikuwa na kucha fupi na safi?
    1. Angela
    2. Lydia
    3. Mwanafunzi 3 
    4. Mwanafunzi 1

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 13.
KSWSQN6

Mama Jamila alimaliza kupika chamcha, yaani chakula cha mchana. Alikuwa amewapikia wanawe ugali na kuku. Aliwapakulia watoto wake. Kila mmoja akapata kipande kimoja kikubwa cha kuku na ugali wake. Aliwaita wakae chumbani wale chakula chao. Jamila alipopewa chakula chake alikataa kukaa na nje na chakula chake. wengine na kutoka alisimama kwa mshangao. Mamake alipogundua kilichofanyika, alimwuliza, "Jamila nyama iko Mara alipotoka nje akaja mwewe na kuchukua nyama yake kutoka sahanini. Jamila wapi?" Jamila akakosa la kusema. Alilia na kujuta kwa nini hakumtii mamake kwa kuketi chumbani kula chakula na wengine.

  1. Mwewe alichukua nini?              
    1. Jamila
    2. Sahani
    3. Nyama
    4. Ugali
  2. Mwewe ni aina ya
    1.  ndege
    2. simba
    3. mwizi
    4. nyoka
  3. Chamcha ni chakula cha saa kama 
    1.  asubuhi 
    2. saa saba
    3.  jioni
    4. usiku
  4. Tunasema: Mama Jamila alikula ugali               kuku.
    1. na
    2. kando na
    3.  kwa
    4. pamoja na
  5. Wingi wa neno "chakula" ni
    1. chakula
    2. viakula
    3. vyakula
    4. mavyakula
  6. Kuku hutaga
    1. nyama
    2. ugali
    3. maziwa
    4. mayai
  7. Kwa nini Jamila alisimama kwa mshangao? Kwa sababu
    1. alipewa chakula kidogo. 
    2. alipigwa na Mwewe
    3. chakula chake kilichukuliwa na Mwewe 
    4. hakushiba
  8. Ni nani aliyekuwa amepika chakula?
    1. Jamila
    2. Mwewe
    3. Hatujaambiwa
    4. Mama Jamila

Kutoka nambari 14 hadi 18, jaza mapengo ukitumia maneno uliopewa chini.

Wanyama wa nyumbani wana faida        14         kwetu. Ng'ombe na mbuzi        15        nyama na maziwa.          16        wanyama hao wanatupatia ngozi           17        hutumika        18            kutengeneza ngoma. Punda na farasi hutubebea mizigo. Kuku na bata hutupa mayai

  A      B      C      D   
 14.  mingi    nyingi    kingi    wengi  
  15. hutupatia       hutupitia      hutupatiwa      hutupata   
  16.halafu      kisha      ndio      baadaye   
 17. ambayo       ambaye      ambao      ambacho  
 18. zigo      mizigo      mizigo      mazigo   

Kutoka swali 19 hadi 30, jibu kulingana na maagizo.

  1. Tambua akisami hii kwa maneno.
    KSWSQN19
    1. Robo 
    2. Thuluthi
    3. Nusu
    4. Sudusi
  2. Kamilisha methali
    Bendera                 
    1. ni baraka 
    2. hufuata upepo
    3.  ina rangi nne
    4. ni maridadi
  3. Umbo hili huitwa?
    KSWSQN21
    1. mraba
    2. mstatili
    3. duara
    4. duara dufu
  4. Mpira iko                 ya meza.
    1. chini ya
    2. ndani ya
    3. juu ya
    4. kando ya
  5. Andika sentensi kwa wingi.
    Mtoto huyu ni mgonjwa.
    1. Watoto hawa ni wagonjwa.
    2. Watoto hao ni wagonjwa.
    3. Watoto hawa ni mgonjwa.
    4. Matoto hawa ni wagonjwa.
  6.  "Kikapu" iko katika ngeli gani?
    1. LI-YA
    2. U-ZI 
    3. M-WA
    4. KI-VI
  7. Sentensi hii iko katika wakati gani?
    Mgeni atakuja kwetu.
    1. uliopo
    2. ujao
    3. uliopita
    4. wowote
  8. Nyasi mbichi zina rangi ya
    1. nyeusi
    2. nyekundu
    3. samawati
    4. kijani.
  9. Nikiwa na njaa nitaenda kwa
    1. mpishi
    2.  mkulima
    3. mwalimu
    4. nahodha
  10. Kanusha sentensi ifuatayo.
    Unywe maji safi                     maji chafu.
    1. usikunywe 
    2. ukunywe 
    3. usinywe
    4. usimeze
  11. Kinyume cha neno "cheka" ni
    1.  chekea
    2. chekelea 
    3. lia
    4. furahia
  12. Sehemu ya dira imeandikwa Q ni
    KSWSQN30
    1. magharibi 
    2. kusini
    3. mashariki
    4. kaskazini 

Andika insha murwa kuhusu 

DARASA  LETU MPYA

MWONGOZO 

  1. C
  2. A
  3. D
  4. B
  5. A
  6. C
  7. A
  8. B
  9. C
  10. C
  11. D
  12. C
  13. D
  14. B
  15. A
  16. C
  17. A
  18. C
  19. A
  20. B
  21. C
  22. C
  23. A
  24. D
  25. B
  26. D
  27. A
  28. C
  29. C
  30. C
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 School Based Assessment Term 1 Exams 2023 Set 5.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students