Friday, 06 October 2023 13:03

Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Mid Term 3 Exam 2023 Set 1

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo haya kisha ujibu swali 1 hadi 5

                                                                          EngmidtermQ2

Tumbo: Ami siku ___1____  sana sijakuona! Nimefurahi sana kukuona leo. U hali gani?
Ami Tambo: Njema Tumbo. Mpwa wangu Tumbo, nimefurahi sana kukuona. Karibu sana hapa nyumbani.
Tumbo: Pole ami naona umelifunga goti __2____ kwa bendeji. Kuna nini?
Ami Tumbo: Nilikuwa nikiteremka ___3___ uwanjani. Niliteguka ___4____ kuanguka. Palikuwa na jiwe pale nikaliangukia likagusa goti langu. Damu ilitiririka ___5___. Nilihisi uchungu.

      A    B    C    D 
 1.  mingi  kingi  nyingi  mengi
 2.  lako  yako  chako  pako
 3.  kule  pale  uko  yake
 4.  kwa  la  badala  na
 5.  kidogo  mdogo  ndogo  midogo


Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 9

Mjomba wangu na aila yake wanaishi karibu na msikiti. Wakati mwingi hunialika kwake, Mimi hufurahi kukutana na wakoi wangu. Wakoi wangu pia wananipenda mno. Sisi huhusiana kama ndugu wa toka nitoke. Nyumbani kwa mjomba kuna sebule, jiko, vyumba vya kulala na msala. Msalani hutumika kwenda haja ndogo na haja kubwa.

Mara yangu ya kwanza kumuona shehe ilikuwa nikiwa kwa mjomba. Shehe alikuwa anaelekea msikitini. Shehe huyo alimsalimu mjomba, "salaam aleikum!" "Aleikum salaam," mjomba alimjibu. Mwadhini alikuwa anaendelea na kutangaza kuwa wakati wa kusali ulikuwa umefika. Wengi wa waumini walioelekea msikitini walikuwa wanaume na wavulana.

Kanzu walizovaa waumini hao ziliwasitiri vyema.

  1. Mjomba na familia yake wanaishi karibu na nini?
    1. shuleni
    2. kanisani
    3. msikitini
    4. barabarani
  2. Nyumba ya mjomba ilikuwa:-
    1. kubwa
    2. ndogo
    3. mbali
    4. ya nyasi
  3. Eleza maana ya shehe
    1. Immam
    2. Kiongozi chini ya Imam
    3. Mola
    4. madrasa
      ya imam
  4. Kinyume cha neno "mjomba" ni:-
    1. Shangazi
    2. Ami
    3. Babu
    4. Nyanya

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu swali 10 hadi 13
                                                                                        EngmidtermQ4

Ugonjwa hatari wa Korona ni ugonjwa wa kuambukizwa ambao ni hatari. Ugonjwa huu umeleta maafa mengi na kusababisha wengi kuipungia dunia mkono wa buriani. Kuna njia mbalimbali za kujikinga kutokana na ugonjwa wa Korona. Njia mojawapo ni kuvaa maksi. Tunashauriwa kuvaa maksi safi na inavyostahili. Pia, maksi ivuliwe kwa njia inayofaa na kuanikwa. Ni bora pia kupigwa pasi inapokauka.

Mtu anaweza kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Korona kwa kunawa mikono kwa sabuni na maji safi mara kwa mara. Sabuni huua virusi kutokana na maradhi ya Korona. Wataalamu wanahimiza watu kila uchao kukaa umbali wa mita moja na nusu au zaidi hasa wakati wa
mkurupuko wa ugonjwa huu.

  1. Ni kweli kusema kuwa:-
    1. Korona huambukizwa
    2. Korona haiui
    3. Korona huleta mema
    4. Korona si ugonjwa
  2. Ni jukumu la nani kuangamiza Korona?
    1. kila mtu
    2. madaktari
    3. walezi
    4. serikali
  3. Ukitaka kuzuia ugonjwa wa Korona si lazima:-
    1. Kuvaa maksi
    2. Kupata chanjo
    3. Kukaa mbali
    4. Kuhamia kwingine
  4. Ugonjwa wa Korona unapatikana kupitia:-
    1. maji
    2. vumbi
    3. hewa
    4. mbu

Soma kifungu kifuatacho. Kina nafasi 14 hadi 18. Umepewa majibu manne hapo.
Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.

Watoto majirani walikuwa na urafiki ___14___ dhati. Urafiki __15___uliwafanya kushiriki ___16__ mbalimbali kila walipopata nafasi.
Siku moja walimwona mtu wasiyemjua. Mtu __17___ alitabasamu alipowakaribia. Aliwaita ati awape ___18___. Werevu wao uliwaepusha kutekwa nyara. Mtu huyo hakuwa na nia njema.

               A           B            C             D 
 14.  wa  ya  cha  la
 15.  yao  wao   lao   yanu 
 16.  micheso  mchezo  michezo  machezo
 17.  huyu  hawa  yule  huyo
 18.  sawadi  peremende  zawadi  kipindi


Kutoka swali 19 hadi 30, chagua jibu sahihi kulingana na maagizo uliyopewa.

  1. Tambua neno lililopigiwa mstari.
    Kamene na zawadi walitembea haraka.
    1. kitenzi
    2. kielezi
    3. kiulizi
    4. kiwakilishi
    5. </ol start=20>
  2. Umbo hili ni:-
                                                           EngmidtermQ3
    1. Duara
    2. Kopa
    3. Mche
    4. Hiram
  3. Chagua sentensi sahihi.
    1. Vipepeo sita wamepaa.
    2. Vipepeo wasita wamepaa.
    3. Vipepeo visita vimepaa.
    4. Vipepeo sita vimepaa.
  4. Jibu la Sabalkheri ni:-
    1. masalkheri
    2. Buriani
    3. Aherii
    4. Asante
  5. "Kifaru" ni mnyama wa pori. Neno "kifaru" liko katika ngeli gani?
    1. KI - VI
    2. A - WA
    3. LI - YA
    4. U - U
  6. Andika sentensi hii kwa hali ya wingi
    Taa inawaka vizuri
    1. Taa zinawaka vizuri
    2. Mataa zinawaka vizuri.
    3. Taa yamewaka vizuri.
    4. Taa inawaka vizuri.
  7. Maana ya Istiari ''yeye ni njiwa'' ni:-
    1. Yeye ni mdogo.
    2. Yeye ni ndege.
    3. Yeye ni mpole.
    4. Yeye ni mkorofi.
  8. Nguo _____ ilianikwa baada ya kufuliwa.
    1. mzuri
    2. zuri
    3. nzuri
    4. mazuri

Chagua jibu sahihi ili kukamilisha sentensi.

  1. ______ amevali viatu vilivyopigwa rangi
    1. Kile
    2. Wale
    3. Huyu
    4. Mle
  2. Andika kinyume cha sentensi ifuatayo.
    Dobi alianika nguo alizofua.
    1. Dobi alianua nguo alizofua.
    2. Dobi alianikwa nguo alizofua.
    3. Dobi hakuanika nguo alizofua.
    4. Dobi alianua nguo
  3. Kamiilisha methali ifwatayo
    Bidii ni _____
    1. nguvu
    2. upepo
    3. jua
    4. mawingu
  4. Tumia -pi kwa ufasaha
    Chungu ______ kilinunuliwa sokoni jana?
    1. yupi
    2. kipi
    3. vipi
    4. lipi

INSHA

Andika insha murwa kuhusu;

SIKU YA KANDANDA SHULE YETU

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. C
  2. D
  3. B
  4. A
  5. C
  6. C
  7. B
  8. D
  9. C
  10. C
  11. A
  12. B
  13. A
  14. B
  15. C
  16. A
  17. A
  18. C
  19. D
  20. D
  21. B
  22. A
  23. B
  24. C
  25. C
  26. D
  27. C
  28. C
  29. D
  30. B
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Mid Term 3 Exam 2023 Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students