Wednesday, 05 July 2023 08:01

Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Opener Exams Term 2 2023 Set 3

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo haya kisha ujibu maswali 1-5.

Zara:   Kakai ulielewa somo la leo la kufunga na kufungua faili?
Kakai: Ndio, sasa ninafanya mazoezi ya kusakura matini kwenye tovuti. Natafuta vifungu vya kusoma vyenye mada ya dira.
Zara:   Kumbuka mwalimu alivyotueleza. Tunapaswa kuzingatia hatua za kiusalama katika matumizi ya vifaa vya kidijitali, pia
            tutambue mitandao salama kwa sababu kuna watu hatari mtandaoni
Kakai: Ni kweli kuna hatari nyingi mtandaoni mtu anaweza kutekwa nyara kwa kutoa maelezo yake mtandaoni.
Zora:   Pia kuna mitandao iliyo na habari zisizo nzuri. Kuna hata watu wanaosambaza video zisizo nzuri : Mimi nitakuwa makini                        ninapokuzwa mtandaoni. Nikuona mtu au jambo ambalo nadhani ni hatari nitamwambia mwalimu
Zora:   Mimi pia nitakuwa mwangalifu sana. Napenda sana kutumia kompyuta. Ninapata maarifa mengi sana mtandaoni
Kakai: Tumalize kazi ili twende nyumbani

  1. Ni kweli kusema kuwa
    1. mtandaoni hamna hatia yoyote
    2. mtu anaweza kutekwa nyara kwa kutumia mitandao
    3. ni watu wazuri tu hutumia mitandao
    4. kompyuta ni mbaya
  2. Neno lenye maana sawa na kompyuta ni
    1. rununu
    2. simu tamba
    3. tarakilishi
    4. faksi
  3. Kakai alikuwa anatafuta nini mtandaoni?
    1. Hatari zilizomo mtandaoni
    2. Jinsi ya kutekwa nyara
    3. Mada kuhusu dira
    4. Video zilizo mtandaoni
  4. Neno kompyuta lina silabi ngapi
    1. tatu
    2. nane
    3. saba
    4. tano
  5. Kichwa mwafaka cha mazungumzo haya ni\
    1. video mtandaoni
    2. umuhimu wa kompyuta
    3. mtandao
    4. hatari za kompyuta

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu swali 6-10.

Siku moja mimi na sahibu yangu Baraka tulikuwa tukipalilia mimea kwenye mradi wetu shuleni. Tulipiga soga huku tukiipinda migongo yetu. Ghafla kama mauti sahibu yangu alipiga mayowe. Alikuwa amejikata muundi kwa jembe baada ya kugonga jiwe. Bila kupoteza wakati nilienda shoti hadi kwenye ofisi ya mwalimu wa zamu na kumuarifu kilichokuwa kimetokea.

Bi. Sara, aliyekuwa mwalimu wa zamu alichukua hatua mara moja. Aliwaita maskauti wapatao wanne tukaandamana nao. Tulipofika alipokuwa ameketi baraka, Bi Sara aliwaelekeza maskauti jinsi ya kumpatia majeruhi huduma ya kwanza. Walichukua kitambaa safi na kufuga jeraha. Damu iliposita kutoka waliosha lile eneo kwa maji safi yaliyotiwa chumvi. Kisha walifunga kidonda bendeji na kumpeleka kwenye zahanati iliyokuwa karibu. Tangu siku hiyo niliamua kujiunga na maskauti.

  1. Maana ya kupiga soga ni
    1. kufanya mazungumzo
    2. kucheza soka
    3. kufanya uzembe
    4. kulima shambani
  2. Ni nini hakuonyeshi kuwa B.Sara anawajibika?
    1. Alikuwa zamu
    2. Alichukua hatua mara moja
    3. Aliwaelekeza maskauti kumpa baraka huduma ya kwanza
    4. Alikuwa ameketi ofisini
  3. Kupiga soga, kupinda migongo, kuenda shoti yote ni mifano ya tamathali gani ya lugha?
    1. Methali
    2. Misemo
    3. Nahau
    4. Tashbihi
  4. Je majeruhi ni nani?
    1. Jeraha
    2. Mitu au watu waliojeruhiwa
    3. Maumivu
    4. Maiti
  5. Kisawe cha neno sahibu ni
    1. ndugu
    2. rafiki
    3. adui
    4. baba mzee

Soma kifungu kifuatacho kwa kujaza nafasi wazi 11-15.

__11__ ya mjomba kuwasili nyumbani tulimkaribisha __12__. Mama alimpa maji baridi ili akate kiu __13__. Aliketi kwenye kochi huku
__14__ na baba. Alikuwa amekawia __15__.

   A   B   C   D 
 11.   Kabla   Kando   Sababu   Baada 
 12.  chumbani   sebuleni   jikoni   hamamuni 
 13.  yake  chake   yao   zake 
 14.  wakipiga kamsa   wakipiga miayo   wakipiga gumzo   wakapiga hoihoi 
 15.  kutembea  kutembezwa   kutembelewa   kututembelea 

 

Kuanzia swali la 16-30. Jibu kulingana na maagizo.

  1. Chagua kundi la nomino pekee
    1. kuimba, hasira, maji
    2. Shuleni, polepole, jana
    3. Safi, yoyote, wale
    4. Ilhali, maandamo, bora
  2. Maneno yapi yaliyo katika ngeli ya U-ZI pekee?
    1. Mkate, ukuta, unga
    2. Uzi, ufagio, wino
    3. Ubinda, wenzo, ulimi
    4. Ukucha, uwanja, ugali
  3. Chagua sentensi sahihi kisarufi 
    1. Kiprop ni mrefu kumliko kirui
    2. Asingeimba vyema asingalituzwa 
    3. Vazi zuri hupendeza
    4. Panya ameingia shimoni pale
  4. Kinyume cha kutabasamu ni
    1. kucheka
    2. kununa
    3. kulia
    4. kukasirika 
  5. Kati ya viungo hivi vya mwili ni kipi si cha  ndani?
    1. Wengu
    2. Utosi
    3. Nyongo
    4. Maju 
  6. Kanusha: Aliamka na kuenda sokoni
    1. Aliamka na kuelekea kwa soko
    2. Hakuamka wala hakuenda sokoni
    3. Haamki kuenda sokoni
    4. Hataamka na kuenda sokoni
  7. Chagua jibu lenye tashbihi
    1. yeye ni wembe masomoni
    2. alikata kiu baada ya mbio zake
    3. wana bidii kama mchwa
    4. mwizi alilewa chakari
  8. Chagua sentensi iliyo katika hali ya ukubwa
    1. Jiko hilo litawashwa baadaye
    2. Kabati lake limefungwa vizuri
    3. Jina lake lina herufi chache
    4. Kono hilo lina nguvu nyingi
  9. Tegua kitendawili
    Huku ng'o huko ng'o
    1. Kaburi
    2. shamba
    3. giza
    4. kamasi
  10. Mchoro huu unaonyesha saa ngapi?
    G6SwaT2OS22023Q25
    1. saa nane kamili
    2. saa mbili kamili
    3. saa sita na dakika kumi
    4. saa sita kamili
  11. Nahau gani yenye maana ya kukamatwa na askari
    1. Shika sikio
    2. Tia mbaroni
    3. Kula kalenda
    4. Mkono mrefu
  12. Bunda ni kwa punda kama vile zaa ni kwa
    1. saa
    2. zao
    3. zana
    4. sana
  13. Maneno yaliyopigiwa kistari ni mfano kwa
    Gari safi lilioshwa vizuri
    1. nomino, kivumishi
    2. kielezi, kivumishi
    3. kivumishi, kitenzi
    4. kivumishi, kielezi
  14. Mavazi rasmi ya wachezaji huitwa
    1. jozi
    2. sare
    3. daluga
    4. fulana
  15. Jibu la makiwa ni
    1. sijambo 
    2. tunayo
    3. pole
    4. nishapoa

INSHA

Andika insha kuhusu

MCHEZO NIUPENDAO

MARKING SCHEME

  1. B
  2. C
  3. C
  4. A
  5. B
  6. A
  7. D
  8. C
  9. B
  10. B
  11. D
  12. B
  13. B
  14. C
  15. D
  16. A
  17. C
  18. C
  19. B
  20. B
  21. B
  22. C
  23. D
  24. C
  25. A
  26. B
  27. A
  28. D
  29. B
  30. B
Join our whatsapp group for latest updates

Download Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 6 Opener Exams Term 2 2023 Set 3.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students