Friday, 06 October 2023 08:29

Kiswahili Questions and Answers - Grade 5 Mid Term 3 Exam 2023 Set 1

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo haya kisha ujibu maswali 1 hadi 5: 

G5SwaMT3S12023Q1

Mwalimu Mkuu: Vicky! Vicky! Uko na shida gani?
Vicky:                  Asante ana Madam Lydia. Naomba niongee na wewe kidogo kama mamangu. Mimi nateseka sana ninapoishi.                              Nimepewa majukumu mengi sana nyumbani.
Mwalimu Mkuu: Pole sana. Wacha kulia ndio uniambie ukweli.
Vicky:                  Kazi nyingi ya jikoni, kufua na kupika. Kama jana nililala saa tano na nusu na sina hata saa ya kufanya kazi ya                              ziada. Kichapo na matusi nimezoea siku hizi. Shida kubwa tena, walimu pia kila asubuhi wanangoja kazi zao                                za ziada na sijafanya. Nakuomba unisaidie mwalimu. Nimeshindwa. Sijui kwa nini wazazi wangu waliniacha!                                  Kifo haina huruma!
Mwalimu Mkuu: Hayo yote ni ya Mungu. Nitakusaidia Vicky. Usiwe na wasiwasi. Nitamwita mlezi wako tukae chini tukomeshe                                ili jambo. Haifai kukufanyia mambo haya mabaya.
Vicky:                  Asante sana mwalimu. Ninamatumaini kama ya tai kuwa kila kitu kitakuwa vizuri. “Mola" akubariki sana.
Mwalimu Mkuu: Kuja hapa kwa ofisi uchukue barua umpeleke mlezi wako ukifika wakati wa kurudi nyumbani.

  1. Ni kwa nini Vicky alimtembelea Mwalimu Mkuu?
    1. Alikuwa mgonjwa
    2. Hakujua la kufanya
    3. Alitaka kumsalimia
    4. Alitaka kuripoti jambo fulani
  2. Neno "Mola" inamaana gani?
    1. Yatima
    2. Kazi ngumu
    3. Mateso
    4. Mungu
  3. Wazazi wa Vicky walikuwa wapi?
    1. Walikuwa nyumbani
    2. Walienda ng'ambo
    3. Hatujaambiwa
    4. Walifariki
  4. Vicky alikutana na Mwalimu Mkuu wapi?
    1. Darasani
    2. Njiani
    3. Ofisini
    4. Nyumbani
  5. Vicky angesaidiwa vipi na Mwalimu Mkuu?
    1. Kumwonya wazazi wake
    2. Kumwita mwalimu wake wa kanisa
    3. Kumwongelesha mlezi wake
    4. Kumripoti mlezi wake kwa polisi

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu swali la 6 hadi 9.

G5SwaMT3S12023Q2

Tura ni mkulima. Yeye ni mkulima shupavu sana. Ana shamba kubwa sana karibu na mto. Amepanda mimea na matunda ya aina tofautitofauti. Katika shamba lake, amepanda matunda kama vile mnazi, mbuni, mzabibu, mlimau, mparachichi na hata mpapai.

Bwana Tura pia hupanda mimea kama vile mhindi, mharagwe, mtama na hata mboga mbali mbali. Yeye hutumia maji kutoka mtoni kunyunyizia mimea na matunda. Ana mashini ya kunyunyizia maji. Yeye huuza mazao kutoka shamba lake na kupata fedha ya kuikimu familia yake.

  1. Kazi nyingi ya Tura inapatikana wapi? 
    1. sokoni
    2. shambani
    3. nyumbani
    4. mtoni
  2. Neno "fedha" iko na maana gani?
    1. pesa
    2. mazao
    3. hodari
    4. mvua
  3. Ni mimea gani haipatikani kwenye shamba la Tura?
    1. Mharagwe
    2. Mparachichi
    3. Mtama
    4. Pilipili hoho
  4. Mzabibu inatumika kutengeneza nini?
    1. chai tamu
    2. pombe
    3. mkate
    4. keki

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu swali 10 hadi 13

Saumu alikuwa msichana mrembo na mwerevu shuleni. Ndoto yake ilikuwa ni kusafiri nchi za ulaya. Siku moja wakati wa likizo, alikutana na kijana mmoja mwekezaji aliyekuwa tajiri. Alivutiwa sana na habari kuwa kijana huyo alipenda kusafiri nchi za ng'ambo katika biashara zake. Saumu alishawishika kuingia katika ndoa ya mapema ili kutimiza ndoto zake.

Jambo ambalo hakujua ni kuwa yote yang'aayo si dhahabu. "Msichana mwerevu kama wewe unatakiwa kuishi maisha ya starehe." Mapunda alimshawishi Saumu. "Unaweza kutengeneza pesa nyingi kwa muda mfupi."

Jumatatu moja wakati wa alasiri, Mapunda alifika kwa akina Saumu akiwa na tikiti ya kusafiri pamoja na pasipoti. Saumu alifurahi sana. Mapunda alijieleza kwa ufasaha kiasi cha mtu yeyote kushuku njama yake. Wazazi walilazimisha Saumu kufunga ndoa.

Saumu alivalia nguo kitalii. Rinda maridadi na kofia kubwa kichwani pake. Mrembo wa mtu alishuka ndege katika uwanja wa Uingereza. Upepo ulipeperusha rinda lake maridadi. Ilibidi watu washike marinda yao kujiepusha aibu. Hilo halikumgusa Saumu. Alishikilia kofia yake na kuacha upepo kupeperusha rinda lake kiasi cha kuonyesha uchini wake. Askari katika uwanja huo wa ndege walishangazwa na kitendo cha Saumu kushikilia kofia yake. Baada ya ukaguzi kwenye kofia yake ya thamani ya juu, mihadarati aina ya heroini ya thamani ya shilingi milioni tatu ilipatikana. Baada ya mabishano mafupi, Saumu alitiwa mbaroni na baadaye akapokezwa kufungo cha miaka kumi na miwili kwa ulanguzi wa dawa za kulevya.

Ndoa yake ya mapema haikumfaa kwa lolote wala chochote.

  1. Saumu alikuwa na ndoto gani?
    1. kupanda ndege
    2. Kuvaa kofia
    3. Kusafiri nchi za ng'ambo
    4. Kuuza dawa za kulevya
  2. Rinda huvaliwa na ________________________________
    1. Mwanaume
    2. Askari wa ndege
    3. Msichana
    4. Kasisi
  3. Kwa nini watu walishikilia marinda yao katika uwanja wa ndege?
    1. Ilikuwa baridi sana
    2. Askari alikuwa karibu
    3. Kulikuwa na upepo kali
    4. Walivaa nguo safi
  4. Dawa gani ilipatikana kwenye kofia ya Saumu?
    1. Heroini
    2. Bhangi
    3. Pombe
    4. Mandasi

Soma kifungu kifuatacho. Kina nafasi 14 had 18. Umepewa majibu manne hapo. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.

Siku moja, sungura na fisi ___14___ kuhudhuria harusi ya mwana wa simba. Marafiki ___15___ wawili walijipamba kwa ajili ya starehe.

Walijirashia __16___ na manukato ya kupendeza. Walionekana warembo sana. Mkononi sungura alibeba ___17___ uliokuwa na ___18___ kama vile mafuta ya kupakia, sukari na maziwa ya kupikia chai.

   A  B   C   D 
 14.  yalikuwa  mlikuwa   walikuwa  tulikuwa
 15.  hao  wao  huo  lao
 16.  marasi  marashi  malashi  marazi
 17.  mkopa  mukoba  mikopa  mkoba
 18.  zawadi  malipo  sawadi  mazuri

 

Kutoka swali 19 hadi 30, chagua jibu sahihi kulingana na maagizo uliyopewa

  1. Tegua kitendawili hiki: Mtoto umleavyo ndivyo
    1. akuavyo
    2. mpende
    3. njema
    4. ni mkorofi
  2. Umbo hili huitwa ______________________________
    Oval 2
    1. Duara
    2. Mraba
    3. Yai
    4. Duara dufu
  3. Tambua neno lililopigiwa mstari:
    Viti vizuri vimetengenezwa.
    1. Kielezi
    2. Kitenzi
    3. Kivumishi
    4. Kiwakilishi
  4. Je, neno "mwavuli" iko katika ngeli gani?
    1. U-YA
    2. LI-YA
    3. A - WA
    4. U - I
  5. Ni ndege yupi asiyekuwa wa porini?
    1. Mwewe
    2. Chiriku
    3. Bata
    4. Kanga
  6. Andika kwa wingi:
    Kitabu changu kimeraruka.
    1. Vitabu vyangu vimeraruka. 
    2. Vitabu vyetu vimeraruka.
    3. Vitabu vyao vimeraruka.
    4. Vitabu vyenu vimeraruka.
  7. Ni msamiati upi unapatikana hospitalini?
    1. Maabara, makaa
    2. Seredani, bendeji
    3. Machela, bendeji
    4. Meko, godoro
  8. Sabalkheri ni salamu za wakati gani?
    1. Asubuhi
    2. Jioni
    3. Usiku
    4. Mchana
  9. Kikombe kiko ____________________________________ya meza.
    G2EngMT3S12023Q6
    1. juu
    2. kando
    3. chini
    4. ndani
  10. Mtoto wa kuku huitwa? _________________________________
    1. kifaranga
    2. ndama
    3. mayai
    4. kiluilui
  11. Jaza pengo kwa neno mwafaka:
    Chakula ______________________________ hupendwa na watoto wadogo.
    1. tamu
    2. kitamu
    3. nzuri
    4. mtamu
  12. Kanusha sentensi hii: Nitatumia tarakilishi yangu.
    1. Sitatumia tarakilishi yangu.
    2. Sikukutumia tarakilishi yangu
    3. Situmii tarakilishi yangu.
    4. Nitatumia tarakilishi yangu.

INSHA

Andika insha ya kusisimua kuhusu;

UMUHIMU WA MAJI

MARKING SCHEME

  1. D
  2. D
  3. D
  4. C
  5. C
  6. B
  7. A
  8. D
  9. B
  10. C
  11. C
  12. C
  13. A
  14. C
  15. A
  16. B
  17. D
  18. A
  19. A
  20. D
  21. C
  22. B
  23. C
  24. B
  25. C
  26. A
  27. A
  28. B
  29. A
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Grade 5 Mid Term 3 Exam 2023 Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students