Wednesday, 03 November 2021 06:43

Kiswahili Activities Questions and Answers - CBC Grade 2 End of Term 2 Exam 2021 Set 1

Share via Whatsapp

KISWAHILI
GREDI YA 2
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA 2

Soma sentensi hizi.

  1. Maziwa ya pakiti ni tamu.
  2. Pendo anapenda peremende.
  3. Roda anaruka kwa kamba
  4. Chatu na chui walikuwa marafiki.
  5. Hii ni risiti

Andika kwa maneno au nambari.

  1. 25 _________________________________
  2. 18. __________________________________
  3.  Arubaini na saba. ____________________________
  4. Themanini na nane _______________________________

Jaza pengo ukitumia kimilikishi sahihi.

  1. Pete_________________ ni nzuri. (wake, zake,lake)
  2. Vyoo _________________ vitaoshwa. (vyenu, vyenyu,chemu)
  3. Tumbo ___________ linauma. (-ake)
  4. Meno _________ yameoza. (-angu)

Andika maneno haya vizuri.

  1. Mueli ______________________________________
  2. Kiha ________________________________________
  3. kulacha _____________________________________

Eleza watoto hawa wanafanya nini.

  1.    
    KisG2et221q17
    ____________________

  2.    
    KisG2et221q18
    ______________________
       
  3.   
    KisG2et221q19
    _______________________

  4.    
    KisG2et221q20
    ______________________

Jaza nafasi ukitumia vizuri au vibaya.

  1. Alifukuzwa ____________________ na ndugu zake
  2. Mwalimu aliwafundisha ________________ wakafurahia.

Jibu maamkuzi haya.

  1. Shikamoo __________________________________
  2. Hujambo _____________________________________
  3. Hamjambo ___________________________________

Taja haki mbili za watoto.

  1. ___________________________________________________
  2. ____________________________________________________

Taja majina ya vifaa hivi vya usafiri.

  1.   
    KisG2et221q28
    ___________________________
  2.    
    KisG2et221q29
    ___________________________
  3.   
    KisG2et221q30
    ___________________________

Akifisha sentensi zifuatazo ukizingatia herufi kubwa na ndogo.

  1. mwalimu mkuu anaitwa bwana kamau. ____________________________________________
  2. sisi huenda kanisani jumatatu. _____________________________________________________
  3. kenya ni nchi yenye amani. __________________________________________________________

Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali.

Bwana Katama alikuwa tajiri sana. Alikuwa na shamba kubwa alilokuwa akipanda miti ya matunda kama vile miembe, michungwa na minanansi. Alikuwa akiyauza matunda hayo na kupata pesa. Siku moja maafisa wa polisi walimtambelea shambani.. Polisi hao walishangaa walipowaona watoto wadogo wa umri wa miaka kumi wakifanya kazi shambani mwake.

Maafisa hao walimkamata Bwana Katama na kumshtaki kwa kuwaajiri watoto wadogo ambo walifaa kuwa shuleni wakisoma. Watoto hao kumi na wawili, akiwemo Ndoro na Mbeyu walirudishwa shuleni na kuendelea na masomo yao.

Hivi leo Ndoro ni daktari wa meno, naye Mbeyu ni mwalimu mkuu wa shule ya upili ya Niache Nisome. Si haki ya watoto kuajiriwa hata kamwe.

Maswali.

  1. Ni nani aliyekuwa tajiri mkubwa? __________________________________
  2. Utajiri wa Bwana Katama ulitokana na ______________________________(biashara, ukulima)
  3. Watoto waliokuwa wakifanya kazi shambani walikuwa na umri gani? _____________________
  4. Ni nani aliyekuwa daktari ? _____________________________
  5. Ni akina nani waliomtembelea tajiri shambani? _______________________________
  6. Bwana Katama alikuwa akiuza nini? ________________________________
  7. Ni watoto wangapi waliokuwa wakifanya kazi huko shambani? _______________________

Taja watu watano wa familia.

  1. _________________________________
  2. ________________________________
  3. ________________________________
  4. ___________________________________
  5. __________________________________

Unda maneno ukitumia silabi ulizopewa.

  1. Ny _________________________________
  2. Pa. ________________________________
  3. Ki __________________________________
  4. Gh _______________________________
  5. Dh _________________________________

MAAKIZO

  1. , 2,3,4,5(Mwanafunzi anapaswa kusoma sentensi alizopewa kwa usahihi)

  1. Ishirini na tano
  2. kumi na nane
  3. 47
  4. 88
  5. yake
  6. vyenu
  7. lake
  8. yangu
  9. elimu
  10. haki
  11. chakula
  12. kukimbia/ anakimbia
  13. kusoma/anasoma
  14. kucheza mpira/wanacheza/ wanacheza mpira
  15. kuomba/ wanaomba
  16. vibaya
  17. vizuri
  18. marahaba
  19. sijambo
  20. hatujambo
  21. haki ya kusoma/ elimu
  22. haki ya kulishwa/ chakula/ ulinzi wa mwili
  23. gari moshi/ gari la moshi/ treni
  24. meli
  25. ndege
  26. Mwalimu mkuu anaitwa Bwana Kamau.
  27. Sisi huenda kanisani Jumatatu.
  28. Kenya ni nchi yenye amani.
  29. Bwana Katama
  30. ukulima
  31. kumi
  32. Ndoro
  33. Maafisa wa polisi
  34. matunda kama vile miembe, michungwa na minanasi
  35. kumi na wawili
  36. baba/ mama
  37. ndugu/dada
  38. babu/nyanya
  39. shangazi/mjomba
  40. binamu
  41. nyanya/nyumba/ nyoka/onya - sahihisha neno lolote lililo na silabi 'ny' mwanzo, mwisho au kati
  42. pa- papa/ panya/ paja/ lipa -sahihisha neno lolote lililo na silabi 'pa' mwanzo, mwisho au kati
  43. ki- kiti/kitanda/ haki -sahihisha neno lolote lililo na silabi 'ki' mwanzo, mwisho au kati
  44. Gh- ghorofa/ lugha/ ghafla - sahihisha neno lolote lililo na silabi 'gh' mwanzo, mwisho au kati
  45. Dh- dhana/ baadhi/ bidhaa/ nidhamu/ - sahihisha neno lolote lililo na silabi 'dh' mwanzo, mwisho au kati
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Activities Questions and Answers - CBC Grade 2 End of Term 2 Exam 2021 Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


.