Monday, 07 February 2022 06:36

Kiswahili Questions and Answers - Class 6 End of Term 3 Exams Set 2 2022

Share via Whatsapp

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya vale uliyopewa.

Sisi _ 1_ na mama_ 2__mkali sana. Mama_3_ hakuturuhusu_4_ sheria zozote kiamboni petu. Kila alipohisi kuwa 5_kuoga, alitulazimisha kuoga maji baridi lakini 6 kutumia sabuni mbayo 7__ vizuri sana. Au kila alipogundua ___8utovu kinidhamu, tulikaripiwa na kukumbushwa kuwa ulikuwa wajibu 9 _kuwalinda wavyele wetu kwa tabia.

  1.        
    1. tulilelewa
    2. tulielewa
    3. tulilelea
    4. tulilea
  2.        
    1. aliyokuwa
    2. aliyekuwa
    3. aliyekua
    4. aliokuwa
  3.        
    1. huo
    2. hio
    3. huyo
    4. hilo
  4.        
    1. kuvuja
    2. kufunja
    3. ufuja
    4. kuvunja
  5.        
    1. tuliogopa
    2. tumeogopa
    3. tutaogopa
    4. wanaogopa
  6.      
    1. ingawa
    2. na
    3. kwa
    4. kuwa
  7.          
    1. ilinukwa
    2. ilinukia
    3. inanukia
    4. ilinuka
  8.            
    1. tuna
    2. mna
    3. wana
    4. lima
  9.            
    1. wangu
    2. wetu
    3. wao
    4. yetu

Mawasiliano ni kitendo cha_10_ujumbe. Hii ni _ 11_. binadamu sanasana. Kuna njia 12 za mawasiliano. Kunazo zile za jadi kama vile kuwasha moto, kupiga uyoma au kutuma watu maalum_ 13 ujumbe mahali ulipohitajika, siku hizi, watu 14_ simu, magazeti, majarida na vifaa__15_ kuwasiliana.

  1.          
    1. kupishana
    2. kupashia
    3. kupashika
    4. kupashana
  2.          
    1. licha ya
    2. katikati ya
    3. baina ya
    4. mithili ya
  3.        
    1. ' mingi
    2. nyingi
    3. jingi
    4. mingi
  4.          
    1. kuupeleka
    2. kuzipeleka
    3. kulipeleka
    4. kukupeleka
  5.          
    1. walitumia
    2. hutumia
    3. wametumia
    4. wangetumia
  6.          
    1. nyinginezo
    2. zinginezo
    3. mengineyo
    4. vinginevyo

Kuanzia swali la 16-30. jibu kila swali kulingana na maagizo.

  1. Chagua orodha ambayo ni ya vielezi
    1. hivi, nyingi, yoyote, chake
    2. nyinyi, wewe, mimi, sisi
    3. sana, upesi, hakika, kabisa
    4. lini, gani, vipi mbona
  2. Chagua kiashiria takriri kilicho sahihi kujaza pengo:
    Vikombe              vilianguka hapa.
    1. Vivi hivyo 
    2. hivyo hivi 
    3. hivi vivi
    4. vivi hivi
  3. Jaza pengo kwa neno sahihi:
    Mama alienda shambani na alishinda kuko huko mchana -
    1. kutua 
    2. kutwa 
    3. kutwaa 
    4. kucha
  4. Ni yupi mpangilio uletao mfululizo ufaao wa wakati?
    1. Alfajiri, asubuhi, adhuhuri, alasiri magharibi
    2. Alasiri, asubuhi, alfajiri, magharibiadhuhuri
    3. Asubuhi, alfajiri, alasiri, adhuhuri,magharibi.
    4. Alfajiri, asubuhi, alasiri, adhuhuri,magharibi
  5. Umbo hili ni
    1
    1. duara
    2. mche
    3. mpira 
    4. duara dufu
  6. Mnyama ana manyoya mwilini, naye binadamu ana 
    1. nywele 
    2. malaika 
    3. ndewe 
    4. mashamba
  7. Tegua kitendawili hiki:
    Mava hapo mava pale
    1. kifo
    2. kioo
    3. kumetamcta
    4. kivuli
  8. Kutangaza kwa sauti kubwa ni
    1. kupiga maji
    2. kupiga mayowe
    3. kupiga mbiu
    4. kipiga domo
  9. Chagua kinyume cha sentensi ifuatayo:
    Kitindamimba alifurahi sana.
    1. Kifunguamimba alifurahi sana. 
    2. Kitindamimba alikasirika sana, 
    3. Mwanambee alifurahi sana. 
    4. Mwanambee alikasirika sana.
  10. Kanusha: Nimekula nikashiba
    1. Sijala nikashiba.
    2. Sijakula nikashiba.
    3. Sijala wala kushiba.
    4. Sikula wala kushiba.
  11. Jaza pengo kwa usahihi:
    Nyinyi               mli             tualika karamuni.
    1. ndinyi/o
    2. ndiwo/ wo
    3. ndio/o
    4. ndio/ ye
  12. Tunasema shungi la nywele                la kuni pia                 la mchanga.
    1. chane/ tita
    2. tita/ fungu
    3. shado/koja
    4. kicha/ bumba
  13. 3, 7, 17, 31 na 43 ni baadhi ya nambari
    1. tasa
    2. shufwa 
    3. chanya 
    4. witiri
  14. Kamilisha sentensi kwa usahihi:
    Mahali hapa palifyekwa
    1. pakafyekana
    2. pakafyekeshwa
    3. pakafyekela
    4. pakafyekewa
  15. Katika milioni sita kuna laki ngapi?
    1. Sita
    2. Sitini
    3. Elfu sita
    4. Mia sita

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31 mpaka 40.
Mlango ulibishwa. Bakari akachungulia kwenye tundu la mlangoni. Akaona mwanamke na mwanamume wamesimama wamebeba matunda. “Baba na mama wako?" waliuliza watu wale wawili. "La, hawapo, wameenda sokoni," Bakari alijibu,
“Basi watakapokuja wasalimie na uwape matunda haya na kuku huyu," wakamaliza. "Ngojeni niwapokee, insiende tafadhali." Bakari alisema huku akifungua mlango. Kufumba na kufumbua, Bakari alijikuta amewekewa bastola kichwani. “Funga mdono wako ukitaka usalama wako, ng'ombe wewe. Nyinyi mnashiba na watu wafa njaa!" Alisema mwanamume yule kwa ghadhabu. "Pesa, dhahabu na vyombo vya mama yako viko wapi?" Mwanamke aliuliza huku akizaba Bakari makofi mawili mazito. Bakari akamwonyesha kila kitu kwani roho yake ilikuwa mikononi, alikuwa hajijui hajitambui!
Wezi wale wawili wakaisafisha nyumba na kuifanya msikiti. Wakampulizia Bakari dawa ya usingizi. Papo hapo akaanguka na kulala fofofo!

  1. Bakari alikuwa na nani nyumbani?
    1. Pekee
    2. Bibiye
    3. Rafiki yake
    4. Mama  na baba
  2. Watu wale wawili waliuliza akina nani?
    1. Baba
    2. Wazee
    3. Baba na mama
    4. Mama
  3. Ni nini kilichomfanya Bakari afungue mlango?
    1. Alishurutishwa kufanya hivyo.
    2. Zawadi alizoambiwa ni za wazazi wake.
    3. Alitaka kuwaona wageni wale vizuri.
    4. Aliwaona mwanamume na mwanamke.
  4. Bakari alipigwa makofi na nani?
    1. Mamake
    2. Rafikiye 
    3. Mwanamume yule 
    4. Mwanamke yule
  5. "Kufumba na kufumbua' ina maana gani?
    1. Hapo hapo
    2. Mara kwa mara 
    3. Baadaye 
    4. Kwa haraka kabisa
  6. Kumpokea mtu ni kufanya nini?
    1. Kumchukia 
    2. Kumkaribisha 
    3. Kumwongelesha 
    4. Kumfungulia mlango
  7. Kuwa roho mkononi ni sawa na kusema
    1. kuwa karibu kufa. 
    2. kuwa na woga zaidi. 
    3. kwenda na roho kwenye mkono. 
    4. kubeba roho kwenye mkono.
  8. Wezi walilalamikia nini?
    1. Kutofunguliwa mlango. 
    2. Wao kushiba na watu kufa kwa njaa. 
    3. Kutokuweko na wazazi. 
    4. Kutopata dhahabu, vy'ombo na pesa.
  9. Wezi hawa wangeshikwa wakiiba tungewaambia methali gani? 
    1. Siku za mwizi ni arubaini.
    2. Mtaka yote hukosa yote.
    3. Bendera hufuata upepo.
    4. Mtegemea cha nduguye hufa masikini.
  10. Neno ghadhabu lina maana gani kuligana na ufahamu? 
    1. Elekeza 
    2. Haraka kabisa 
    3. Hofu kubwa 
    4. Kukasirika

Soma kifingu kifuatacho kisha ujibu maswali 41 mpaka 50.

Simu ni chombo cha watu cha kuwasiliana. Simu hutumia mawimbi ili kupokea sauti au picha. Kuna aina mbili za simu. Rununu na simu ya ofisi.
Stepford Press and Publishers, 2021
Simu ya ofisi au simu ya nyumbani mara nyingi hutumiwa ofisini ama nyumbani. Simu hii huwekwa mahali fulani maalum katika ofisi. Simu hii huwekwa katika mapokezi. Inapopigwa, huwezi kuona nambari ya anayepiga.
Rununu pia huitwa simu tamba, selula au rokono. Rununu ni simu ndogo ambayo unaweza kuibeba mahali popote unapoenda. Rumunu hutuinia simu kadi. Pia hutumia kadihela ili kupata muda wa maongezi. Manufaa ya rununu ni tumbi tumbi. Hata kama ni ndogo wahenga walisema usione wembamba wa reli, gari moshi hupita.
Manufaa ya rununu ni kuwa huweza kutuma arafa. Arafa ni ujumbe mfupi unaotumwa kwa njia ya kuandika. Pia, hutumika katika biashara kwa kutuma pesa za kununua bidhaa.
Simu pia hutumika kuwapa watu ajira kwa kuajiriwa katika duka la M-pesa, kuuza rununu na vifaa vyake. Watu wengine huzitengeneza simu zilizoharibika kwa malipo na wao hupata ajira.
Hakuna kizuri kisichokuwa na hila. Rununu ina hasara pia. Inaweza kutumiwa na waovu kuwaibia watu pesa. Aidha kutuma ujumbe wa chuki, matusi na picha chafu zisizofaa.
Daima, tutumie rununu kwa uangalifu mkubwa tusije tukajuta majuto ya mjukuu ambayo huja baadaye.

  1. Simu ndogo ambayo mtu anaweza akatembea nayo mahali popote inaitwa 
    1. simu tamba 
    2. simu ya nyumbani 
    3. simu ya ofisi 
    4. arafa
  2. Rununu ni kifaa cha
    1. maliasili 
    2. ajira 
    3. teknolojia 
    4. madini
  3. Rununu pia haiitwi
    1. ofisi 
    2. selula 
    3. rukono 
    4. simu tamba
  4. Kadi ambayo hununuliwa yenye nambari fulani za rununu ambazo mtu hutumia kwa kitambulisho chake pekee huitwa
    1. ajira 
    2. kadi 
    3. simu kadi 
    4. simu hela
  5. Ipi si manufaa ya rununu?
    1. Kutuma arafa.
    2. Kuwapa watu ajira.
    3. Kuwaibia watu pesa. 
    4. Kupata pesa kwa kutengeneza rununu zilizoharibika.
  6. Manufaa ya rununu ni tumbi tumbi.
    Maana ya tumbi tumbi ni
    1. si tele 
    2. chache 
    3. nyingi 
    4. haba
  7. Maana ya neno ‘ajira' ni
    1. Kazi 
    2. pesa 
    3. malipo 
    4. hela
  8. Ni methali gani inalingana na maelezo haya: Rununu, hata kama ni kifaa kidogo, kina faida nyingi? 
    1. Enga kabla ya kujenga. 
    2. Hakuna kizuri kisichokuwa na ila. 
    3. Majuto ni mjukuu huja kinyume. 
    4. Usione wembamba wa reli gari moshi hupita.
  9. Mojawapo ya hasara za rununu ni
    1. kuuza rununu na vifaa vyake kwa malipo kwenye duka la simu kama mfanyi kazi.
    2. kuwasiliana na marafiki.
    3. kutuma ujumbe wa chuki na matusi. 
    4. kuajiriwa katika duka la M-pesa.
  10. Kichwa mwafaka cha kifungu hiki ni
    1. Kadihela 
    2. Rununu 
    3. Mawasiliano 
    4. Arafa

INSHA
Umepewa dakika 40 kuandika insha yako.
HASARA ZA MMOMONYOKO WA UDONGO



MARKING SCHEME

  1. A
  2. B
  3. C
  4. D
  5. A
  6. C
  7. B
  8. A
  9. B
  10. D
  11. C
  12. B
  13. A
  14. B
  15. D
  16. C
  17. D
  18. B
  19. A
  20. B
  21. A
  22. D
  23. C
  24. D
  25. C
  26. C
  27. B
  28. A
  29. C
  30. B
  31. A
  32. C
  33. B
  34. D
  35. B
  36. B
  37. A
  38. B
  39. A
  40. D
  41. A
  42. C
  43. A
  44. C
  45. C
  46. C
  47. A
  48. D
  49. C
  50. B
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Class 6 End of Term 3 Exams Set 2 2022.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students