Monday, 06 March 2023 09:43

School Based Assessment 2023 Grade 6 Kiswahili Lugha - Grade 6 Opener Exams Term 1 2023 Set 3

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1 hadi 5.     

G6SwaT1SB23P1
Rozina:   Shikamoo Lawi?
Lawi:       Marahaba Rozina. U hali gani?
Rozina:    Njema. Nashuru "Mola" kwa kila hali ya leo. Habari za utokako?
Lawi:        Nzuri. Lakini nimechoka sana. Nimekuwa shambani kutwa nzima niking'oa magugu.
Rozina:    Pole sana kwa uchovu. Mwakani utalia kivulini.
Lawi:       Umegonga ndipo. Uzohali ni nyumba ya njaa. Bidii zangu zitanifaidi sana.
Rozina:    Hakika mimi nilimaliza kazi zote za shambani jana. Leo nikaamua kumtembelea bibi. Si unajua amekula chumvinyingi.
Lawi:        Naam, pia kazi hiyo ni nzuri.
Rozina:    Nimemsaidia kupiga deki na kuosha nguo zake. Amefurahi sana.
Lawi:        Umefanya vyema. Heko!
Rozina:    Tutaonana kesho kikaoni.
Lawi:        Inshallah! Asante Rozina.

  1. Kati ya Rozina na Lawi nani ako na umri nyingi?
    1. Rozina
    2. Lawi
    3. Hakuna
    4. Wote
  2. Nani alisaidiwa kulingana na mazungumzo haya?
    1. Ajuja
    2. Mke
    3. Nyanya
    4. Shaibo
  3. Kulingana na mazungumzo haya ni kweli kusema kuwa:--
    1. Lawi alimsaidia bibi
    2. Rozina alipenda kazi tofauti.
    3. Lawi na Rozina ni wakulima
    4. Lawi aling'oa kwekwe shambani
  4. Ni neno gani la adabu alitumia Rozina kwa Lawi?
    1. pole
    2. samahani
    3. karibu
    4. asante
  5. Neno "Mola" imetumika kwa mazungumzo. Maana yake ni:-
    1. Mazao
    2. Bidii
    3. Mungu
    4. Shamba

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 15.        

G6SwaT1SB23P2

Hapo jadi na jadudi paliishi mhunzi alikuwa na taaluma ya ufinyazi. Aliitwa Zuma. Alitegeneza sime, visu na hamadi kwa mhanga mwarara. Zilikuwa zana za hali ya juu. Aidha, vilimezewa mate na wengi. Kutokana na kipaji chake alizidi kutokuwa na jasho jekejeke kutokana na zaburi alizopokea kutoka kwa wateja wake. Kwa udi na uvumba alijifunga kibwekibwe kutimiza ahadi zake. Mchanga aliotumia Zuma ulikuwa wa kipekee. Ulipatikana tu katika nchi ya mbali.

Siku moja aliumaliza mchanga wake. Alimuaga mkewe aliyekuwa na jukumu la kumtunza mwana mtarajiwa. Nyathira hakutaka kuachwa peke yake. Zuma alimuuliza ninaye kumtunza akiondoka.

Ingawa mamaye Zuma alikuwa ajuza alikuwa mhariri na mwenye nguvu. Alimsaidia mkazamwana wake kwa kazi za nyumba kisha akawapeleka kondoo malishoni. Nyathira alipika na kuosha vyombo pasi kufanya kazi ngumu. Aliacha kuchota maji, kutafuta kuni na kupalilia mimea.

Jioni moja Bi. kizee yule hakurudi kutoka malishoni. Mwangaza ulipoondoka, Nyathira hakujua la kufanya kwani hakuwa na kurunzi nao mwangaza ulikuwa adimu. Alishikwa ma woga na akakata tamaa. Alijiloza katika kitanda kungoja kuche
akamtafute.

  1. Zuma alifanya kazi gani? Kazi ya:-
    1. kufinyanga
    2. uashi
    3. kuwinda
    4. usonaha
  2. Vifaa alivyotengeneza ni:-
    1. Ala za vita
    2. Vifaa vya upishi
    3. Vifaa vya usafiri
    4. Vifaa vya muziki
  3. Kutokana na habari hii ni kweli kusema:-
    1. Zuma alikuwa na wateja wengi.
    2. Zuma alikuwa kapera
    3. Zuma alikuwa na watoto wawili
    4. Zuma alikuwa mzembe.
  4. Si kweli kusema kwamba:-
    1. Zuma alitengeneza vitu vizuri.
    2. Mamake Zuma alimsaidia mkazamwanawe.
    3. Zuma alitumia mchanga wowote kufinyanga.
    4. Mamake Zuma alikuwa na nguvu.
  5. Kifungu "vilimezewa mate na wengi" ni kumaanisha kwamba:-
    1. watu walivitemea mate.
    2.  watu walitokwa na mate.
    3. walividharau
    4. watu walivitamani
  6. Mama Zuma alifanya kazi gani?
    1. Kuchunga kondoo
    2. Kuteka maji
    3. Kuvunja kuni
    4. Kufanya biashara
  7. Mkewe Zuma aliitwa nani?
    1. Mumbi
    2. Mfinyazi
    3. Nyathira
    4. Ajuza
  8. Nyathira angeenda kumtafuta mama yake lini?
    1. jioni
    2. usiku
    3. asubuhi
    4. hatujui
  9. Neno "taaluma" linamaanisha nini?
    1. ujuzi
    2. kutojua
    3. daktari
    4. kasoro
  10. Mke wa Zuma aliachiwa kazi zifuatazo isipokuwa:-
    1. kupalilia
    2. kuchota maji
    3. kutafuta kuni
    4. kufua nguo

Kutoka swali 16 hadi 20, jaza pengo na maneno chini.

Karai___16___hununuliwa dukakuu na dobi. Huwekwa maji___17___ ya___18___ nguo chafu. Dobi hutumia sabuni ___19___ katika duka la reja reja. Baada ya nguo kuwa safi, huanikwa na baadaye kupigwa ___20___.

   A   B   C   D  
 16.   ile   lile   yale   kile 
 17.  mingi   chache   mengi   ndogo 
 18.  kuvulia   kuvua   kufua   kufulia 
 19.  kinachonunuliwa   inunuliwayo   yanayonunuliwa   inayonunua 
 20.  bao  jeki    kitutu  pasi 


Kutoka nambari 21 hadi 30, jibu kulingana na maagizo.

  1. Tulienda kanisani kuimba kwaya. Neno kanisani ni:-
    1. Nomino
    2. Kivumishi
    3. Kiwakilishi
    4. Kielezi
  2. Gari ___________________________________liliharibika njiani.
    1. nzuri
    2. langu
    3. moja
    4. lile
  3. Wingi wa sentensi hii ni:-
    Msichana yule ni mgonjwa.
    1. Wasichana wale ni wagonjwa.
    2. Wasichana yule ni mgonjwa.
    3. Wasichana hao ni wagonjwa.
    4. Wasichana hawa ni wagonjwa.
  4. Umbo hili huitwa?
    G6SwaT1SB23P3
    1. Duara
    2. Mraba
    3. Mche
    4. Duara dufu
  5. Neno "ufahamu" lina irabu ngapi?
    1. mbili
    2. tatu
    3. nne
    4. saba
  6. Neno "ua" liko katika ngeli gani?
    1. I-ZI
    2. I-I
    3. LI-YA
    4. A-WA
  7. Jibu wa waambaje ni nini?
    1. vizuri
    2. vyema
    3. vibaya
    4. sina la kuamba
  8. Mtoto wa mjomba au shangazi ni:-
    1. kuzo
    2. mkoi
    3. shemeji
    4. wifi
  9. Tumia -enyewe kwa ufasaha.
    Shati __________________________ ni safi.
    1. lenyewe
    2. yenyewe
    3. enyewe
    4. mwenyewe
  10. Wageni walikula wali ______________________________________ nyama
    1. na
    2. pia
    3. kwa
    4. tena

INSHA  

Andika insha ya kusisimua kuhusu:

UMUHIMU WA MITI



MARKING SCHEME

  1. B
  2. C
  3. C
  4. A
  5. C
  6. A
  7. A
  8. A
  9. C
  10. D
  11. A
  12. C
  13. C
  14. A
  15. A
  16. B
  17. C
  18. D
  19. D
  20. D
  21. A
  22. B
  23. A
  24. D
  25. C
  26. C
  27. D
  28. B
  29. A
  30. C

 

Join our whatsapp group for latest updates

Download School Based Assessment 2023 Grade 6 Kiswahili Lugha - Grade 6 Opener Exams Term 1 2023 Set 3.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students