Tuesday, 07 March 2023 11:31

Kiswahili Lugha Questions and Answers - Grade 5 School Based Assessment Opener Exams Term 1 2023 Set 4

Share via Whatsapp

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1 hadi 5.    

G5SwaT1SB23P1

Polisi:      Usijaribu! Unaendesha gari bila taa zote za mbele?
Utingo:    Niko hapa Afande. Hujambo mzee?
Polisi:      Nimemwita dereva. Sikukuita wewe. Kwa nini anaendesha gari barabara i ilhali halina taa zote za mbele? Tena mnabeba                          abiria wawili wanaosimama.
Utingo:     Lakini afande, hapa pana chui kidogo!
Polisi:      Usijaribu! Wewe huna aibu? Unajaribu kumhonga afisa wa polisi!
Dereva:    Lakini Afande ....................
Polisi:       Sitaki hizo lakini zenu. Nimewakamata wewe na dereva wa gari hil. Twende kwenye kituo cha polisi. Nyinyi mtamweleza                          hakimu hizo lakini zenu. Ala! Njia ya mwongo ni fupi!
Utingo:     Tafadhali ............
Polisi:       Abiria wengine shukeni mngojee gari jingine.
Dereva:    Tafathali. Tusamehe................
Polisi:       Hapana cha tafadhali. Nyinyi abiria wawili mliosimama pia twendeni kwenye kituo cha polisi.

  1. Utingo ni mtu gani?
    1. Afisa wa polisi
    2. Msaidizi wa dereva.
    3. Abiria.
    4. Mtu ambaye anachukua nauli
  2. Watu wangapi walishikwa na Afisa wa polisi?
    1. Wanne
    2. Wawili
    3. Watatu
    4. Watano
  3. Hakimu anapatikana wapi kazini?
    1. Kwenye kituo cha polisi
    2. Kortini
    3. Barabarani
    4. Kwa jela
  4. Utingo alisema, "hapa pana chai kidogo." maana yake ni:-
    1. Chai kwa kikombe
    2. Nauli
    3. Pesa
    4. Hongo
  5. Dereva wa gari alipatikana na hatia ngapi?
    1. moja
    2. mitatu
    3. hakuna
    4. mawili

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 11.            

G5SwaT1SB23P2

Hapo zamani za kale paliishi wazee watatu waliokuw marafiki. Wote walikuwa maskini. Siku moja waliamua kwenda mahali panapoitwa Kaunguni kutafuta mali. Kufika huko ilikuwa ni tabu kwa sababu iliwabidi kupita vijiji vingi na kuvuka jito kubwa sana.

Kwa vile safari ilikuwa ndefu, waliamua kutafuta farasi ili waweze kufika upesi. Kwa bahati mbaya, kila
walikokwenda kutafuta farasi hawakufanikiwa kwa sababu
farasi walikuwa safarini. Basi wazee hao waliendelea na safari mpaka wakafika kwenye kijiji kilichokuwa karibu na lile jito.

Hapa walibahatika kupata farasi watatu ingawa farasi hawa hawakuwa wa kawaida. Farasi hawa wakiwa wakila vyakula tofauti. Wa kwanza alikula nguo za binadamu, wa pili alikula nyama ya binadamu, na wa tatu alikula nyama ya farasi. Kwa hivyo wazee walikuwa na tatizo la kutafuta vyakula vya farasi hawa.

  1. Wazee hawa watatu walikuwa na uhusiano upi?
    1. walikuwa matajiri
    2. Walikuwa wajinga
    3. Walikuwa wajanja
    4. Walikuwa maskini
  2. Safari ya wazee hawa ilikuwa na nia gani?
    1. Kutafuta farasi
    2. Kwenda kutafuta utajiri
    3. Kuvuka jito
    4. Kuenda Kaunguni
  3. Farasi wa mwisho alikuwa yupi?
    1. Aliyekula nguo
    2. Aliyekula farasi
    3. Aliyeluka binadamu
    4. Aliyekuwa mzembe
  4. Ni farasi yupi alikuwa katikati?
    1. Alaye watoto
    2. Mlafarasi
    3. Mlanguo
    4. Mlawatu
  5. Ni kitu gani kilichofanyikia farasi hawa walipovuka mto?
    1. Waligeuka kuwa wa kawaida
    2. Walimea pembe
    3. Walipata mali nyingi
    4. Walitajirika
  6. Kichwa kifaacho taarifa hii ni:-
    1. Juhudi sio pato
    2. Mchagua jembe si mkulima
    3. Akili nyingi huondoa maarifa
    4. Baada ya dhiki ni faraja

Jaza mapengo kwa kutumia jibu bora zaidi kutoka nambari 12 hadi 16.

Dawa___12___ kulevya hutumiwa na baadhi ya watu na kufanya kuonekana kama 13. Miongoni ___14___dawa hizi ni kama vile bangi, aina fulani ya ___15___ za kumeza na dawa fulani za ___16___kwa sindano.

   A   B   C   D 
 12.   ya   la  za   cha 
 13.  welevu   warefu   waolevi   walevi 
 14.  kwa  ya  mwa  pa
 15.  tembe  tembo  mawe  muitingoi 
 16.  kutunga   kuchoma   kuweko   kujidunga 

 

Kutoka nambari 17 hadi 30, jibu kulingana na maagizo.

  1. Neno "kifaru" iko katika ngeli ipi?
    1. I - ZI
    2. KI - VI
    3. U - ZI
    4. A - WA
  2. Umbo hili huitwa?
    G5SwaT1SB23P3
    1. Mraba
    2. Mstatili
    3. Duara
    4. Mche
  3. Rafiki _____________________________ amefika.
    1. wangu
    2. yangu
    3. langu
    4. changua
  4. Anayejenga kwa mawe huitwa _______________________________
    1. mwashi
    2. sonara
    3. seremala
    4. mhunzi
  5. Humusi huandikwaje?
    1. 1/5
    2. 1/6
    3. ¼
    4. 1/8
  6. Andika wingi wa:-
    "Uso mfupi"
    1. Macha mafupi
    2. Mauso fupi
    3. Nyuso fupi
    4. Nyuso mfupi
  7. Msimu wa baridi kali bila mvua huitwa:-
    1. Kiangazi
    2. Vuli
    3. Masika
    4. Kipupwe
  8. Samaki ___________________________ ni wakubwa sana.
    1. hizo
    2. hao
    3. zile
    4. hio
  9. Aliandika barua ____________________________ kalamu ya wino.
    1. na
    2. kwa
    3. la
    4. cha
  10. Kitenzi "cheka" katika hali ya kutendewa ni:-
    1. Chekwa
    2. Chekelewa
    3. Chekea
    4. Chekewa
  11. _________________________________ niazime kalamu yako, yangu imepotea.
    1. Pole
    2. Tafadhali
    3. Samahani
    4. Niwie radhi
  12. Pesa anazolipa abiria yeyote ni:-
    1. faini
    2. karo
    3. nauli
    4. kiingilio
  13. Tunapita mtihani _______________________ tulifanya bidii.
    1. na
    2. pia
    3. lakini
    4. kwa sababu
  14. Simu ya mkono huitwa? ____________________________
    1. Runinga
    2. Rununu
    3. Sare
    4. Kompyuta

INSHA

Andika insha ya kusisimua kuhusu

SHULE YETU



MARKING SCHEME

  1. D
  2. A
  3. B
  4. D
  5. D
  6. D
  7. B
  8. B
  9. D
  10. A
  11. D
  12. C
  13. D
  14. C
  15. A
  16. D
  17. D
  18. B
  19. B
  20. A
  21. A
  22. C
  23. D
  24. C
  25. B
  26. B
  27. B
  28. C
  29. D
  30. B
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Lugha Questions and Answers - Grade 5 School Based Assessment Opener Exams Term 1 2023 Set 4.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students