Tuesday, 28 March 2023 12:26

Shughuli za Kiswahili Ufahamu Questions and Answers - CBC Grade 2 Term 1 Midterm Exams 2023 SET 1

Share via Whatsapp

Maswali

Ufahamu (Alama 10) 
Soma hadithi kisha ujibu maswali yanayofuata. (Alama 5)

Imani akiamka asubuhi, ananawa uso. Anapiga meno mswaki kwa kutumia mswaki na dawa ya meno. Yeye huoga kabla ya kunywa kiamsha kinywa. Anatumia kikata kucha kukata kucha zake. Imani hutumia kichana kuchana nywele zake. Imani anapenda kuwa safi kila siku. Anajua usafi huleta afya bora.

  1. Taja mambo mawili anayofanya Imani anapoamka. (alama 2)
  2. Imani akitaka kukata kucha, atatumia nini?
  3. Kwa nini Imani anapenda kuwa safi kila siku?
  4. Tunatumia....................................kuchana nywele zetu.

Soma hadithi kisha ujibu maswali yanayofuata.(Alama 5)
Mama yangu ni mkulima. Yeye hupanda mimea tofauti kama vile mihindi, miharagwe, mboga na migomba. Yeye pia anafuga wanyama wa nyumbani kama vile ng'ombe, punda, mbuzi na sungura. Ng'ombe hutupa maziwa. Sisi hunywa maziwa kila siku. 
Pia tunatumia maziwa hayo kupika chai na kutengeneza sharubati. Kwa kweli mama yangu ni hodari.

  1. Taja mimea miwili ambayo mama amepanda. (alama 2)
  2. Ni mnyama yupi anatupa maziwa?
  3. Taja matumizi mawili ya maziwa. (alama 2)
    1. ................................................................
    2. ................................................................

2.. SARUFI (Alama 15)

  1. Unda maneno matatu ya sauti 'd' (Alama 3)
    1. ...........................................................
    2. ...........................................................
    3. ...........................................................
  2. Jaza pengo: (alama 2)
    1. g __ __ rid ___
    2. n__iz__
  3. Tumia 'huyu' au 'hawa' kukamilisha sentensi: (alama 5)
    1. Wavulana.................................wanacheza kandanda.
    2. Ng'ombe.................................wanakunywa maji.
    3. Mpishi.................................ana sufuria safi.
    4. Kuku.................................wametaga mayai mengi.
    5. Dereva.................................anaendesha basi kubwa.
  4. Kamilisha sentensi kwa kutumia -ang au -etu ipasavyo: (alama 5)
    1. Mipira.................................imepotea.
    2. Gari.................................limesimama.
    3. Ndugu.................................amelala.
    4. Kitabu.................................kimeraruka.
    5. Mti.................................umekauka.
  5. KUANDIKA
    Andika sentensi tano utakazosomewa na mwalimu. (Alama 10)
    1. ..................................................................
    2. ..................................................................
    3. ..................................................................
    4. ..................................................................
    5. ..................................................................

Majibu

  1.                      
    1. Ananawa uso 
      anapiga mswaki
      anaoga
      anakunywa kiamsha kinyua
      anakata kucha
      anachana nywele
    2. kikata kucha
    3. anajua usafi huleta afya bora
    4. kichana
  2.      
    1. mihindi, miharagwe, mboga, migomba
    2. ngombe, punda, mbuzi, sungura
    3. kupika chai, kutengeneza sharubati

Sarufi

  1.      
    1. dada
      damu
      dakika
      dunia
      dania
      etc
  2.     
    1. gwaride
    2. ndizi
  3.                
    1. hawa
    2. huyu
    3. huyu
    4. hawa
    5. huyu
  4.      
    1. yetu
    2. langu
    3. yangu
    4. chetu
    5. wangu

 

Join our whatsapp group for latest updates

Download Shughuli za Kiswahili Ufahamu Questions and Answers - CBC Grade 2 Term 1 Midterm Exams 2023 SET 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


.