Friday, 28 October 2022 12:13

Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 End of Term 3 November 2022 Exams Set 1

Share via Whatsapp

QUESTIONS

SEHEMU 3: Ufahamu
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
Vazi ni kitu kilichotengenezwa kwa kitambaa au ngozi ili kuvaliwa na binadamu. Kuna mavazi ya kiasili na mavazi ya kisasa. Mavazi ya kiasili ni kama vile shuka, kanzu na leso. Mavazi ya kisasa ni kama vile; suruali, tai, shati, rinda na koti.
Watu huvaa mavazi wakati wa baridi na joto. Joho huvaliwa wakati wa baridi. Fulana huvaliwa wakati wa joto.
Mavazi ni muhimu kwa binadamu. Mavazi kama vile chupi na fulana huficha uchi. Mavazi kama vile ovaroli huzuia uchafu mtu anapofanya kazi. Vilevile, mavazi huzuia baridi shadidi. Pia mavazi husaidia mtu kujikinga wakati wa hatari. Binadamu huvaa tai na suti ili kuonekana nadhifu. Mavazi ni muhimu katika maisha ya binadamu.

  1. Kati ya mavazi yafuatayo ni lipi si vazi la kisasa? 
    1. Leso
    2. Shati
    3. Shuka
    4. Kanzu
  2. Ni vazi lipi huvaliwa wakati wa baridi?
    1. Joho
    2. Fulana
    3. Chupi
    4. Tai
  3. Ni ipi si sababu ya kuvaa mavazi? 
    1. Kujikinga baridi
    2. Kuwa nadhifu
    3. Kujificha 
    4. Kujikinga kutokana na hatari
  4. Makanika anapotengeneza gari huwa amevalia vazi lipi kati ya yafuatayo? 
    1. Aproni
    2. Joho
    3. Fulana
    4. Ovaroli
  5. Chagua vazi ambalo huvaliwa ndani ya mavazi mengine.
    1. kanzu
    2. shuka
    3. chupi
    4. joho
  6. Mavazi yanayovaliwa na wanafunzi huitwa; 
    1. magwando 
    2. sare
    3. ovaroli
    4. surupwenye
  7. Neno vazi liko katika ngeli gani? 
    1. LI-YA
    2. I-ZI
    3. I-I
    4. YA-YA
  8. Ni vazi gani huvaliwa wakati wa joto? 
    1. Joho
    2. Fulana
    3. Ovaroli
    4. Chupi

Soma barua kituatacho kisha ujibu maswali
Wanariadha hupeperusha bendera ya Kenya. Bendera ya Kenya ina rangi nne. Kila rangi husimamia jambo fulani. Rangi nyeusi huashiria raia wa Kenya. Raia wa Kenya ni Waafrika.
Rangi nyekundu ni ishara ya damu iliyomwagika wakati wa kupigania uhuru wa nchi yetu. Wapiganiaji uhuru waliteseka na kupigwa. Walimwaga damu nyingi.
Kijani kibichi inaonyesha utajiri wa maliasili ya wakenya. Rangi hii inaashiria mimea ya shambani. Pia hii ni rangi ya misitu yetu. Rangi nyeupe huonyesha upendo na amani ya Wakenya. Bendera ya Kenya pia ina ngao na mikuki miwili. Vitu hivi huonyesha kuwa wakenya wako tayari kuitetea na kuilinda nchi yao.
Bendera ya Kenya hutumika katika shughuli mbalimbali. Mbali na kupeperushwa shuleni, hupatikana kwenye ofisi za serikali, magari ya viongozi wa taifa na katika makao makuu ya ofisi za kibalozi. Bendera inapopandishwa watu wote husimama wima. Kusimama wima ni ishara ya kuonyesha heshima kwa bendera ya Kenya. Bendera ya Kenya hupandishwa na kushushwa wakati wa sherehe za kitaifa kama vile: sherehe za siku Mashujaa Bendera ya Kenya ni fahari yetu. Bendera ya Kenya ni kitambulisho cha Wakenya. Ninaipenda bendera ya nchi yetu.

  1. Mtu anayeipenda nchi yake huitwa;
    1. mzalendo 
    2. msaliti
    3. mkwasi
    4. mkenya
  2. Katika bendera ya Kenya ni nini huonyesha kuwa wakenya wako tayari kuipigania nchi yao: 
    1. rangi nyeupe 
    2. rangi nyeusi 
    3. ngao na mkuki 
    4. rangi ya kijani
  3. Ni maelezo yapi si sahihi? 
    1. Bendera hupeperushwa shuleni 
    2. Bendera huwa kwenye ofisi za serikali 
    3. Bendera huwekwa kwenye magari ya viongozi 
    4. Bendera huvaliwa na mabalozi
  4. Ni rangi ipi huonyesha utajiri wa nchi yetu? 
    1. Nyeusi
    2. Kijani kibichi
    3. Nyeupe
    4. Nyekundu
  5. Ni yupi si mnyamapori?
    1. Nguruwe
    2. Ngiri
    3. Kifaru
    4. Swara
  6. Tunafaa kufanya nini ili kuonyesha heshima kwa bendera ya taifa letu? 
    1. Kupigana
    2. Kuimba 
    3. Kusimama wima bendera inapopandishwa 
    4. Kukimbia wakati bendera inapopandishwa
  7. Ni nani hupeperusha bendera yetu ya Kenya?
    1. Wakenya
    2. Wanariadha
    3. Mashujaa
    4. Wazalendo
  8. Mashujaa wetu waliteswa na nani kabla nchi yetu haijapata uhuru?
    1. Wanariadha
    2. Wakoloni
    3. Raia
    4.  Wakenya
  9. Mashujaa waliopigania uhuru wa nchi yetu husherehekewa katika sikukuu gani?
    1. Krismasi
    2. Siku ya wafanyikazi
    3. Siku ya Mashujaa
    4. Siku ya wanariadha
  10. Jibu maswali kulingana na maagizo
    Tambua nomino katika sentensi ifuatayo. Kochi ambalo limenunuliwa ni kubwa,
    1. kubwa
    2. kochi
    3. limenunuliwa 
    4. ambalo
  11. Chagua kitenzi katika sentensi
    Mtoto analilia chumbani mwake.
    1. analilia
    2. chumbani
    3. mwake
    4. mtoto
  12. Chagua jibu la salamu 'mwambaje
    1. sina la kuamba 
    2. vyema 
    3. salama
    4. hatuna la kuamha
  13. Ni neno lipi si maagane katika orodha ifuatayo
    1. U hali gani? 
    2. Kwaheri 
    3. alamsiki
    4. Buriani
  14. Kanusha sentensi ifuatayo
    Mama ameenda sokoni asubuhi. 
    1. Mama ameenda sokoni asubuhi 
    2. Mama hajaenda sokoni asubuhi 
    3. Baba alikuja nyumbani jioni 
    4. Mama alienda sokoni asubuhi
  15. Chagua sentensi ambayo ina kielezi 
    1. Ndizi zimeiva vizuri 
    2. Kalamu yake imevunjika 
    3. Juma amevunja kalamu yangu
    4. Huyu ni kimbiaji bora
  16. Kifungu kimoja cha shairi huitwaje?
    1. Mshororo
    2. Mizani
    3. Silabi
    4. Ubeti
  17. Tegua kitendawili kifuatacho Pitia huku nami kule tukutane mbele.
    1. ugali
    2. mshipi 
    3. jiwe
    4. nazi
  18. Chagua methali ambayo inahimiza bidii 
    1. Mtaka cha mvunguni sharti ainame
    2. Asiyesikia la mkuu huvunjika guu 
    3. Mwana hutazama kisogo cha nina 
    4. Majuto ni mjukuu huja baadaye
  19. Ni upi si msamiati wa sebuleni.
    1. kabati
    2. makochi
    3. meza
    4. jokofu
  20. Chagua kivumishi katika sentensi
    Mwanamume huuyu anamkongojo mkubwa.
    1. mwanamume
    2. mkongojo
    3. mkubwa
    4. ana
  21. Ni nafsi ipi imetumika sawasawa.
    1. sisi wote tuutaenda mjini
    2. wao wataenda kanisani kesho
    3. mimi ndiye nitakayetuzwa
    4. wewe ndiye utaibuka mshindi
  22. Ni kipi si kifaa cha tarakilishi
    1. zulia
    2. kipanya 
    3. kiwambo 
    4. kibodi 

INSHA
Andika insha ukizingatia mada ifuatayo:
SOKO LETU

KUSOMA

SEHEMU YA  A : Kusikiliza na Kuzungumza

Mwalimu amkaribishe mwanafunzi kwa mazungumzo kwa maamkizi mwafaka kisha amweleze j=kuwa , : Leo tunajadiliana kuhusu wanyamapori."

  1. Ni nini maana ya wanyamapori?
    (Mwanafunzi ajibu)
  2. Ni mnyama yupi anajulikana kama mfalme wa porini?
    (Mwanafunzi ajibu)
  3. Taja mnyama mmoja mabaye hukimbia kwa kasi zaidi?
    (Mwanafunzi ajibu)
  4. Ni mnyama yupi huwindwa sana na majangili kwa sababu ya pembe zake?
    (Mwanafunzi ajibu)
  5. Jina lingine la ndovu ni ?
    (Mwanafunzi ajibu)

SEHEMU YA B: Kusoma kwa sauti
Soma kifungu kifuatacho kwa sauti

Mchezo wa kuigiza ni mchezo ambao umeandikwa kulingana na vitendo vya wahusika. Mchezo wa kuigiza vitendo fulani kuhusu jambo fulani. Mchezo wa kuigiza ni mtungo wa kisanii na unapaswa kuigizwa kwenye jukwaa. Mawazo ya mchezo wa kuigiza hupitishwa na mhusika. Mhusika ni mtu anayetumiwa kupitisha ujumbe wa mtunzi wa mchezo wa kuigiza. Mchezo wa kuigiza huwa na maelekezo na maelezo yanayomwonyesha mhusika namna ya kutenda. Maelekezo hueleza mazingira ya kuigiza. Maelezo haya huandikwa kwenye mabano.

MARKING SCHEME

swa ms 1

Join our whatsapp group for latest updates

Download Shughuli za Kiswahili Questions and Answers - Grade 4 End of Term 3 November 2022 Exams Set 1.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students